UWEZO WA MUNGU KUKUTOA KATIKA MABAYA

BWANA HAJAZUIA MABAYA KUTUPATA BALI ATATUTOA KATIKA MABAYA YOTE:

Mungu wetu anatupenda sana. Wapo watu wanateseka kwa majarbu mengi matokeo wanalalamika km BW amewaacha wkt wanamtumikia BW kwa mal zao,muda wao,zaka zao n.k lkn hayo ni mawazo ya watu kuwa BW AMETUACHA hapana BW hakzuia tatzo kukupata bali YUPO TAYARI NA ANA NGUVU YAKUKUTOA KATIKA TATZO HILO BILA KUJALI UKUBWA WA TATZO. ona BW hakuzuia magum kmkuta YUSUPH lkn akamponya na yote. MWNZO37:1….MWNZ39 NA MWNZ41 BW Hakuzuia tatzo kumpata DANIEL. MESHACK na Shedrack n.k bali aliwatoa ktk tatzo DANIEL3:13-30 DAN6:1-28 YEREMIA38:2-3,4-13 MATENDO9:36-42 Bw hajazuia matatizo kuja Duniani lakini kwa wewe unaemtumikia Bw kwa uaminifu hutakufa kwa colona Amini tu kwakua Mungu hajabadirika aliye waokoa wana waisrael atatuokoa na matatizo kama unaamini Mungu anauwezo hata sasa na atakuponya na magonjwa na matatizo yote yaliyoingia kwako unayoyafahamu na hata usiyoyafahamu….

Ubarikiwe Sana na uwabariki wengine pia. MUNGU NI MWEMA WAKATI WOTE.

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI. https://nenolamungutz.blogspot.com/2018/11/kazi-kuu-tano-5-za-imani-katika-maombi_69.html

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

11 months ago

Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu.
Karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Uhusiano ni upendo unaozaa ushirikiano na mawasiliano kati ya pande mbili tofauti.
Kama tuna upendo kwa MUNGU inatupasa sana kushirikiana na MUNGU na kuwasiliana na MUNGU Mara kwa Mara.
Mawasiliano hayo ni maombi . Lakini maombi tu hayawezi kuzaa matunda kama sio maombi ya imani.
Kama kuna mambo matano(5) muhimu katika maombi yako basi ni hivi:
=Jina la YESU KRISTO(Yohana 14:14),
=Damu ya YESU KRISTO(Ufunuo 12:11),
= Neno la MUNGU la ufunuo wa ROHO MTAKATIFU(Zaburi 107:20),
=Nguvu za ROHO MTAKATIFU(Luka 1:35a)
=Na Kuomba kwa imani(Waebrania 11:6)
Kama imani ni kitu muhimu kiasi hicho, je imani ni nini?
Biblia inajibu ikisema Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.-Waebrania 11:1′
Imani ni kuwa na uhakika na mambo yajayo.
Imani katika maombi ni kuwa na uhakika na ulichokiomba kwa MUNGU kwamba utakipata.
Kwa sababu imani ni kitu muhimu sana katika maombi, basi tuangalie kwa sehemu kazi za imani katika maombi.
Kazi Tano(5) za imani katika maombi.
1. Inakuondolea hofu, Woga na mashaka ndani yako.
Isaya 54:14 ” Utathibitika katika haki; utakuwa mbali na kuonewa, kwa maana hutaogopa; na mbali na hofu, kwa maana haitakukaribia.”
Hofu haitakukaribia maana utakuwa na imani kubwa ya ushindi.
2. Inakufanya umwamini MUNGU.
Waebrania 11:8-11 ”

Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni MUNGU. Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba; alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu.
Biblia inaanza kwa kusema ”kwa imani” maana yake imani ilifanya kazi kubwa sana hata wakafanikiwa hawa katika mahitaji yao, imani yao iliwafanya wamwamini MUNGU.
Kazi mojawapo ya imani ni kukufanya umwamwini MUNGU.

3. Inakupa kushinda
Mathayo 9:22 ”

YESU akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.”
Imani ya Mwanamke huyu ilikuwa inaamini uponyaji wa Bwana YESU na hakika akapona saa ile ile.
Hata wewe kama unamwendea YESU kwa maombi ili akuponye au akutendee muujiza hakika imani yako inaweza kukupa kushinda kama kweli una imani kubwa ya kupokea ushindi kutoka kwa Bwana YESU.
Imani humpa muombaji kushinda
4. Inakupa kuwa mwenye haki.
Habakuki 2:4 ”

Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.”
Imani yako kwa Bwana YESU imekufanya umwamini na kumpokea na hivyo kufanyika mwenye haki, kuwa mwenye haki ni kibali cha kupokea pia ushindi kupitia maombi.Imani katika YESU KRISTO inakufanya uwe mwenye haki.
5. Imani inakupa Ulinzi.
1 Petro 1:5 ”

Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho. ”
Tunalindwa na nguvu za MUNGU kwa imani, hivyo imani inakupa ulinzi wa MUNGU maana unamwamini katika KRISTO.
Labda ngoja niseme pia neno hili.
Katika Agano la kale Neno ‘‘Imani’‘ Linapatikana katika maandiko mawili tu yaani Kumb 32:20 na Habakuki 2:4 lakini matukio ya kumwamini MUNGU ni mengi sana sana na hayo yanaonyesha Imani hata kama Hakuna Neno Imani.

Unatakiwa sana kuomba kwa imani lakini pia licha ya jambo hilo muhimu sana unatakiwa pia kutunza maisha yako ya ndani ili kwa njia hiyo umruhusu MUNGU kukutetea katika maisha yako ya nje.
Tunza utakatifu,Tunza utu wako wa ndani ulio mzuri,Tunza utauwa.
Tunza ucha MUNGU wako ,Kwa hayo hakika utamruhusu MUNGU kukutetea pindi unapomuomba akutetee.

Kumbuka pia kwamba MUNGU ni mkamilifu, Kazi yake ni kamilifu, Ametuumba kwa ukamilifu.
Akianzisha kazi huwa anaikamilisha.

Kumb 32:4 “Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; Maana, njia zake zote ni haki. MUNGU wa uaminifu, asiye na uovu, Yeye ndiye mwenye haki na adili.”
MUNGU ni mwenye haki,Kazi zake ni kamilifu.
Ahadi zake ni ndio na kweli,Yeye ni mwaminifu na mkamilifu.

Ndugu yangu, kutokumwamini MUNGU ni dhambi na ni kosa kubwa sana.
Ndugu usikubali dhambi ya kutokumwamini MUNGU muumba wako ikawa na wewe.
Nakuomba mwamini na mtii yeye na neno lake Biblia.

Isaya 40:28-31 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye MUNGU wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki. Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”
Neno hilo naomba nikusaidie kumwamini MUNGU na kumtegemea.
Imani hiyo ya kumwamini MUNGU katika KRISTO YESU itakupa ushindi Mkuu sana.

Neema ya MUNGU iko pamoja wenye Imani watakatifu.
MUNGU ampe kila mmoja wetu roho ya kutubu na kuacha uovu, aliyepotelewa na ufahamu, ufahamu wake mzuri umrudie sasa.

Kuomba maombi ya imani ni jambo la muhimu sana ila zingatia pia na utakatifu sana katika maisha yako ya wokovu na maombi.
Baraka yako ni ya kwako tu hivyo ing’ang’anie.
Ngoja nikushauri pia kuhusu malengo yako.
Ukiweka malengo mazuri kwenye maisha yako hakikisha.
1. Unayaombea malengo hayo.
2. Unamhusisha ROHO MTAKATIFU akusaidie katika kutimiza malengo hayo.
Kumbuka bila MUNGU wewe huwezi lolote hata unalodhani unaliweza, ndivyo Biblia inasema.
Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.”

3. Tafuta kusudi la MUNGU na kibali cha MUNGU ili kutimia kwa malengo hayo.
4. Anza kufanyia kazi malengo hayo, huku ukimshirikisha MUNGU kwa kila hatua.
5. Unaweza kumtolea MUNGU sadaka ya shukrani au sadaka ya nadhiri ili msaada wa MUNGU uambatane na wewe katika kukamilika kwa malengo hayo.
Kumbuka ndani ya sadaka sahihi kwa MUNGU kuna agano na MUNGU (Zaburi 50:5) hivyo kufanikiwa inakuwa rahisi maana MUNGU analiangalia agano lake kupitia sadaka yako.

6. Ishi maisha matakatifu ya Wokovu daima, ili dhambi isikupate na kukuzuia kufanikiwa katika malengo yako.
7. Hakikisha malengo yako yanampa MUNGU utukufu wote.

Maombi ya Leo kwa imani.

1. Amuru nguvu za Giza ziachie afya yako, uchumi wako, uzao wako , ndoa yako na kibali chako.
Simama na Matendo 16:18

2. Omba kwa MUNGU kwamba ukae salama chini ya ulinzi wake.
Omba ndoa yako ikae salama.
Omba kazi yako ikae salama.
Omba uchumi wako ukae salama na omba uzao wako ukae salama.
Simama na Mithali 18:10

3. Muite MUNGU akuokoe katika kila eneo la maisha yako.
Simama na Zaburi 18:3

4. Fungua malango yako ya baraka zako yaliyokuwa yamefungwa.
Simama na Isaya 60:11
Kumbuka maana ya lango au malango ni mlango mkubwa wa kuingia katika mji au uwanja.
Kuna baraka zingine ziko karibu sana kukufikia kutokana na maombi yako na uaminifu wako kwa MUNGU ila ukifungua lango la kiroho utapata baraka yako ambayo inawezekana huwa unaiona tu kwenye ndoto kwamba unaipokea.
Leo omba na utamuona Bwana YESU akikushindia.

Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.

Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu. Ukiweza pia toa copy na kuwasambazia watu wengi zaidi.

Mungu atubariki….

Umeifikiaje furaha YAKO?

Siri ya Kuwa na Furaha Katika Maisha

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitafunga ndoa na kuwa na watoto.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitakuwa na nyumba yangu.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati nitapata kazi.”

“Nitakuwa mwenye furaha wakati . . .”

UMEKWISHA kuwa na mawazo kama hayo? Wakati ulifikia muradi wako ao wakati ulipata kitu ulichotamani, je, furaha yako iliendelea? Ao ilianza kupunguka? Ni kweli kwamba, kufikia muradi fulani ao kupata kitu tulichotamani kunaweza kutuletea furaha, lakini furaha hiyo ni ya muda mufupi. Furaha ya kudumu haitegemee tu kufikia miradi ao kupata vitu fulani. Inaomba mambo mengi ili kuwa na afya nzuri, vilevile furaha ya kweli inategemea mambo mengi.

Kila mutu iko tofauti na mwengine. Pengine mambo ambayo inakufurahisha haitamufurahisha mwengine. Tena, kadiri tunaendelea kukomaa, tunabadilika. Hata hivyo, ushuhuda unaonyesha kwamba kuna mambo fulani yanayoleta furaha. Kwa mufano, ili kuwa na furaha ya kweli inaomba kutosheka, kuepuka tamaa, kuwapenda wengine, na kuwa na uwezo wa kupambana na matatizo. Tuone sababu gani.

1. TOSHEKA

Kisha kuchunguza maisha ya watu, mutu mwenye hekima alisema hivi: “Pesa ni ulinzi.” Lakini aliongeza hivi: ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato. Hilo pia ni ubatili.’ (Mhubiri 5:10; 7:12) Alitaka kusema nini? Hata kama tunahitaji feza ili tuishi, tunapaswa kuepuka tamaa, sababu hatuwezi kushiba feza! Muandikaji Sulemani aliyekuwa Mufalme katika Israeli, alitafuta kujua ikiwa maisha ya utajiri na vitu vya kimwili yanaweza kuleta furaha ya kweli. Aliandika hivi: “Wala sikuyanyima macho yangu chochote ambacho yaliomba. Sikuunyima moyo wangu shangwe ya aina yoyote.”—Mhubiri 1:13; 2:10.

Kisha kupata mali mingi, Sulemani alijenga manyumba makubwa, alijifanyia mabustani mazuri na mahali pa kuogelea na alikuwa na wafanyakazi wengi. Kila kitu alitamani, alikipata. Alijifunza nini? Alipata furaha kwa kiasi fulani, lakini furaha ya muda tu. Alisema hivi: “Nilitazama kila kitu kilikuwa ubatili, na hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.” Alifikia hata kuchukia maisha! (Mhubiri 2:11, 17, 18) Sulemani alijifunza kwamba kufuatia tu raha mwishowe kunamufanya mutu akose furaha na kutosheka. *

Uchunguzi wa leo unakubaliana na hekima hiyo ya zamani? Kitabu kimoja kinaonyesha kwamba “kisha kutimiza mahitaji ya lazima, kupata feza za zaidi hakuongezee mutu furaha kabisa.” (Journal of Happiness Studies) Pia, ushuhuda unaonyesha kwamba kufuatia sana vitu vya kimwili, zaidi sana ikiwa kunatufanya tuzarau mambo ya kiroho, kunaweza kumaliza furaha ya mutu.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mukirizika na vitu vya sasa.’Waebrania 13:5.

2. EPUKA WIVU

Wivu ni “kujisikia mubaya ao kuwa na kinyongo kwa sababu ya vitu vya mutu mwengine, na hivyo, kutamani kuwa na vitu hivyo.” Kama vile ugonjwa wa kansa unaua chembe za mwili pole pole, wivu unamaliza pole pole furaha ya mutu. Wivu unaweza kuanza namna gani? Tunaweza kujua namna gani kwamba tuna wivu? Na tutapambana nao namna gani?

Kitabu fulani kinaonyesha kwamba watu wana mwelekeo wa kusikilia wivu watu walio kama wao, pengine, wana miaka moja ya kuzaliwa, uzoefu mumoja, ao hali moja ya maisha. Kwa mufano, mufanya biashara hawezi kusikilia wivu muchezaji mwenye kujulikana sana wa filme. Lakini atamusikilia wivu mufanya biashara mwenzake kwa sababu biashara yake inavuma. (Encyclopedia of Social Psychology)

Tuchukue mufano: Maofisa wakubwa katika utawala wa Uajemi ya zamani walimusikilia wivu ofisa mwenzao mwenye akili nyingi anayeitwa Danieli; hawakumusikilia wivu mufalme. Ili kuonyesha kama walimusikilia wivu sana, walipanga hata kumuua Danieli! Lakini hawakuweza. (Danieli 6:1-24) Kitabu tulichozungumuzia kinasema hivi: “Ni jambo la lazima kujua kwamba wivu utakuchochea uwatendee wengine mambo mabaya. Hilo linaonyesha sababu gani katika historia watu wengi ambao walihusika katika jeuri walichochewa na wivu.” *

Wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha

Unaweza kutambua namna gani kwamba una wivu? Jiulize: ‘Ikiwa mwenzangu anapata faida fulani, ninafurahi ao ninajiona wa bure? Ikiwa kaka ao dada yangu, mwanafunzi mwenzangu mwenye akili, ao mufanya kazi mwenzangu anashindwa, ninahuzunika ao ninafurahi?’ Ikiwa “unajiona wa bure” na “unafurahi,” hilo linaonyesha kwamba pengine wivu umekuwa na mizizi katika moyo wako. (Mwanzo 26:12-14) Kitabu kimoja kinasema “wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha na kumufanya mutu asiwe mwenye shukrani kwa zawadi nyingi tunazopata katika maisha. . . . Muelekeo huo unamukosesha mutu furaha.” (Encyclopedia of Social Psychology)

Ili kuondoa wivu katika mioyo yetu inaomba tuonyeshe unyenyekevu wa kweli na kiasi. Sifa hizo zinatusaidia tupendezwe kabisa na uwezo mbalimbali na sifa nzuri za wengine. Biblia inasema hivi: ‘Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora kuliko ninyi.’—Wafilipi 2:3

KANUNI YA BIBLIA: ‘Na tusiwe wenye kujisifu, wenye kuchochea mashindano juu ya mutu na mwenzake, tukioneana wivu.’Wagalatia 5:26.

3. PENDA WENGINE

Kitabu kimoja kinasema: “Namna watu wanaona uhusiano wao na wengine inaweza kuwasaidia sana wawe wenye kutosheka katika maisha kuliko kazi yao, feza, jamii, ao hata afya yao.” (Social Psychology) Kwa kifupi, ili mutu awe na furaha ya kweli, ni lazima apende na kupendwa na wengine. Mwandikaji fulani wa Biblia alisema hivi: “Ikiwa . . . sina upendo, mimi si kitu.”—1 Wakorintho 13:2.

Ukitaka kujifunza kuwapenda wengine, haujachelewa. Kwa mufano, baba wa Vanessa alikuwa mukali na mulevi. Wakati alikuwa na miaka 14, alitoka nyumbani kwao ili kuishi katika familia fulani zilizokubali kumukaribisha, na pia, katika nyumba moja ya watu wasio na makao ambako anakumbuka kwamba alianza kumuomba Mungu amusaidie. Kisha, aliwekwa katika familia ambayo ilitumikisha kanuni ya Biblia inayosema kwamba ‘upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili.’ Pengine hiyo ilikuwa jibu kwa sala yake. (1 Wakorintho 13:4) Hali ya familia hiyo, na yale alikuwa anajifunza kupitia funzo lake la Biblia, yalimusaidia Vanessa apate kitulizo katika moyo na akili. Alisema hivi: “Nilianza kuweza masomo.”

Vanessa angali anaumia katika moyo wake. Hata hivyo, kwa sasa yeye ni mama mwenye furaha, na ana mabinti wawili.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mujivike upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.’—Wakolosai 3:14.

4. JIFUNZE KUPAMBANA NA MATATIZO

Kuna mutu asiye na magumu katika maisha? Kama vile Biblia inasema, kuna “wakati wa kulia” na “wakati wa kuomboleza.” (Mhubiri 3:4) Uwezo wa kupambana na matatizo unatusaidia tuendelee mbele ijapokuwa magumu. Fikiria mufano wa Carol na Mildred.

Carol ana ugonjwa wa uti wa mugongo, diabete ao ugonjwa wa sukari, kushindwa kupumua anapolala, na ugonjwa ambao umefanya jicho lake la kushoto lisione tena. Lakini anasema: “Ninajikaza ili nisiwe mwenye kuvunjika moyo kwa wakati murefu sana. Wakati fulani ninajisikilia huruma. Lakini kisha ninasahau magumu yangu na kumushukuru Mungu kwa yale ninaweza kufanya, zaidi sana kwa ajili ya wengine.”

Mildred naye ana magonjwa mengi, kama vile maumivu ya sehemu zinazounganisha viungo, kansa ya maziba, na diabete. Lakini kama Carol, anajikaza ili asiwaze mingi juu ya magumu yake. Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwapenda watu na kuwafariji wengine wakati wanagonjwa, kufanya hivyo kunanisaidia mimi pia. Tena, ninatambua kwamba wakati ninafariji wengine, ninasahau magumu yangu.”

Carol na Mildred wanahubiria habari njema mutu aliyekuja kufanya matembezi katika bustani

Carol na Mildred walipata furaha kwa kuwafariji wengine

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.



1. TOSHEKA

Kisha kuchunguza maisha ya watu, mutu mwenye hekima alisema hivi: “Pesa ni ulinzi.” Lakini aliongeza hivi: ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato. Hilo pia ni ubatili.’ (Mhubiri 5:10; 7:12) Alitaka kusema nini? Hata kama tunahitaji feza ili tuishi, tunapaswa kuepuka tamaa, sababu hatuwezi kushiba feza! Muandikaji Sulemani aliyekuwa Mufalme katika Israeli, alitafuta kujua ikiwa maisha ya utajiri na vitu vya kimwili yanaweza kuleta furaha ya kweli. Aliandika hivi: “Wala sikuyanyima macho yangu chochote ambacho yaliomba. Sikuunyima moyo wangu shangwe ya aina yoyote.”—Mhubiri 1:13; 2:10.

Kisha kupata mali mingi, Sulemani alijenga manyumba makubwa, alijifanyia mabustani mazuri na mahali pa kuogelea na alikuwa na wafanyakazi wengi. Kila kitu alitamani, alikipata. Alijifunza nini? Alipata furaha kwa kiasi fulani, lakini furaha ya muda tu. Alisema hivi: “Nilitazama kila kitu kilikuwa ubatili, na hapakuwa na lolote lenye faida chini ya jua.” Alifikia hata kuchukia maisha! (Mhubiri 2:11, 17, 18) Sulemani alijifunza kwamba kufuatia tu raha mwishowe kunamufanya mutu akose furaha na kutosheka. *

Uchunguzi wa leo unakubaliana na hekima hiyo ya zamani? Kitabu kimoja kinaonyesha kwamba “kisha kutimiza mahitaji ya lazima, kupata feza za zaidi hakuongezee mutu furaha kabisa.” (Journal of Happiness Studies) Pia, ushuhuda unaonyesha kwamba kufuatia sana vitu vya kimwili, zaidi sana ikiwa kunatufanya tuzarau mambo ya kiroho, kunaweza kumaliza furaha ya mutu.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mukirizika na vitu vya sasa.’Waebrania 13:5.

2. EPUKA WIVU

Wivu ni “kujisikia mubaya ao kuwa na kinyongo kwa sababu ya vitu vya mutu mwengine, na hivyo, kutamani kuwa na vitu hivyo.” Kama vile ugonjwa wa kansa unaua chembe za mwili pole pole, wivu unamaliza pole pole furaha ya mutu. Wivu unaweza kuanza namna gani? Tunaweza kujua namna gani kwamba tuna wivu? Na tutapambana nao namna gani?

Kitabu fulani kinaonyesha kwamba watu wana mwelekeo wa kusikilia wivu watu walio kama wao, pengine, wana miaka moja ya kuzaliwa, uzoefu mumoja, ao hali moja ya maisha. Kwa mufano, mufanya biashara hawezi kusikilia wivu muchezaji mwenye kujulikana sana wa filme. Lakini atamusikilia wivu mufanya biashara mwenzake kwa sababu biashara yake inavuma. (Encyclopedia of Social Psychology)

Tuchukue mufano: Maofisa wakubwa katika utawala wa Uajemi ya zamani walimusikilia wivu ofisa mwenzao mwenye akili nyingi anayeitwa Danieli; hawakumusikilia wivu mufalme. Ili kuonyesha kama walimusikilia wivu sana, walipanga hata kumuua Danieli! Lakini hawakuweza. (Danieli 6:1-24) Kitabu tulichozungumuzia kinasema hivi: “Ni jambo la lazima kujua kwamba wivu utakuchochea uwatendee wengine mambo mabaya. Hilo linaonyesha sababu gani katika historia watu wengi ambao walihusika katika jeuri walichochewa na wivu.” *

Wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha

Unaweza kutambua namna gani kwamba una wivu? Jiulize: ‘Ikiwa mwenzangu anapata faida fulani, ninafurahi ao ninajiona wa bure? Ikiwa kaka ao dada yangu, mwanafunzi mwenzangu mwenye akili, ao mufanya kazi mwenzangu anashindwa, ninahuzunika ao ninafurahi?’ Ikiwa “unajiona wa bure” na “unafurahi,” hilo linaonyesha kwamba pengine wivu umekuwa na mizizi katika moyo wako. (Mwanzo 26:12-14) Kitabu kimoja kinasema “wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha na kumufanya mutu asiwe mwenye shukrani kwa zawadi nyingi tunazopata katika maisha. . . . Muelekeo huo unamukosesha mutu furaha.” (Encyclopedia of Social Psychology)

Ili kuondoa wivu katika mioyo yetu inaomba tuonyeshe unyenyekevu wa kweli na kiasi. Sifa hizo zinatusaidia tupendezwe kabisa na uwezo mbalimbali na sifa nzuri za wengine. Biblia inasema hivi: ‘Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora kuliko ninyi.’—Wafilipi 2:3

KANUNI YA BIBLIA: ‘Na tusiwe wenye kujisifu, wenye kuchochea mashindano juu ya mutu na mwenzake, tukioneana wivu.’Wagalatia 5:26.

3. PENDA WENGINE

Kitabu kimoja kinasema: “Namna watu wanaona uhusiano wao na wengine inaweza kuwasaidia sana wawe wenye kutosheka katika maisha kuliko kazi yao, feza, jamii, ao hata afya yao.” (Social Psychology) Kwa kifupi, ili mutu awe na furaha ya kweli, ni lazima apende na kupendwa na wengine. Mwandikaji fulani wa Biblia alisema hivi: “Ikiwa . . . sina upendo, mimi si kitu.”—1 Wakorintho 13:2.

Ukitaka kujifunza kuwapenda wengine, haujachelewa. Kwa mufano, baba wa Vanessa alikuwa mukali na mulevi. Wakati alikuwa na miaka 14, alitoka nyumbani kwao ili kuishi katika familia fulani zilizokubali kumukaribisha, na pia, katika nyumba moja ya watu wasio na makao ambako anakumbuka kwamba alianza kumuomba Mungu amusaidie. Kisha, aliwekwa katika familia ambayo ilitumikisha kanuni ya Biblia inayosema kwamba ‘upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili.’ Pengine hiyo ilikuwa jibu kwa sala yake. (1 Wakorintho 13:4) Hali ya familia hiyo, na yale alikuwa anajifunza kupitia funzo lake la Biblia, yalimusaidia Vanessa apate kitulizo katika moyo na akili. Alisema hivi: “Nilianza kuweza masomo.”

Vanessa angali anaumia katika moyo wake. Hata hivyo, kwa sasa yeye ni mama mwenye furaha, na ana mabinti wawili.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mujivike upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.’—Wakolosai 3:14.

4. JIFUNZE KUPAMBANA NA MATATIZO

Kuna mutu asiye na magumu katika maisha? Kama vile Biblia inasema, kuna “wakati wa kulia” na “wakati wa kuomboleza.” (Mhubiri 3:4) Uwezo wa kupambana na matatizo unatusaidia tuendelee mbele ijapokuwa magumu. Fikiria mufano wa Carol na Mildred.

Carol ana ugonjwa wa uti wa mugongo, diabete ao ugonjwa wa sukari, kushindwa kupumua anapolala, na ugonjwa ambao umefanya jicho lake la kushoto lisione tena. Lakini anasema: “Ninajikaza ili nisiwe mwenye kuvunjika moyo kwa wakati murefu sana. Wakati fulani ninajisikilia huruma. Lakini kisha ninasahau magumu yangu na kumushukuru Mungu kwa yale ninaweza kufanya, zaidi sana kwa ajili ya wengine.”

Mildred naye ana magonjwa mengi, kama vile maumivu ya sehemu zinazounganisha viungo, kansa ya maziba, na diabete. Lakini kama Carol, anajikaza ili asiwaze mingi juu ya magumu yake. Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwapenda watu na kuwafariji wengine wakati wanagonjwa, kufanya hivyo kunanisaidia mimi pia. Tena, ninatambua kwamba wakati ninafariji wengine, ninasahau magumu yangu.”

Carol na Mildred wanahubiria habari njema mutu aliyekuja kufanya matembezi katika bustani

Carol na Mildred walipata furaha kwa kuwafariji wengine

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.



2. EPUKA WIVU

Wivu ni “kujisikia mubaya ao kuwa na kinyongo kwa sababu ya vitu vya mutu mwengine, na hivyo, kutamani kuwa na vitu hivyo.” Kama vile ugonjwa wa kansa unaua chembe za mwili pole pole, wivu unamaliza pole pole furaha ya mutu. Wivu unaweza kuanza namna gani? Tunaweza kujua namna gani kwamba tuna wivu? Na tutapambana nao namna gani?

Kitabu fulani kinaonyesha kwamba watu wana mwelekeo wa kusikilia wivu watu walio kama wao, pengine, wana miaka moja ya kuzaliwa, uzoefu mumoja, ao hali moja ya maisha. Kwa mufano, mufanya biashara hawezi kusikilia wivu muchezaji mwenye kujulikana sana wa filme. Lakini atamusikilia wivu mufanya biashara mwenzake kwa sababu biashara yake inavuma. (Encyclopedia of Social Psychology)

Tuchukue mufano: Maofisa wakubwa katika utawala wa Uajemi ya zamani walimusikilia wivu ofisa mwenzao mwenye akili nyingi anayeitwa Danieli; hawakumusikilia wivu mufalme. Ili kuonyesha kama walimusikilia wivu sana, walipanga hata kumuua Danieli! Lakini hawakuweza. (Danieli 6:1-24) Kitabu tulichozungumuzia kinasema hivi: “Ni jambo la lazima kujua kwamba wivu utakuchochea uwatendee wengine mambo mabaya. Hilo linaonyesha sababu gani katika historia watu wengi ambao walihusika katika jeuri walichochewa na wivu.” *

Wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha

Unaweza kutambua namna gani kwamba una wivu? Jiulize: ‘Ikiwa mwenzangu anapata faida fulani, ninafurahi ao ninajiona wa bure? Ikiwa kaka ao dada yangu, mwanafunzi mwenzangu mwenye akili, ao mufanya kazi mwenzangu anashindwa, ninahuzunika ao ninafurahi?’ Ikiwa “unajiona wa bure” na “unafurahi,” hilo linaonyesha kwamba pengine wivu umekuwa na mizizi katika moyo wako. (Mwanzo 26:12-14) Kitabu kimoja kinasema “wivu unaweza kuharibu uwezo wa mutu wa kufurahia mambo mazuri katika maisha na kumufanya mutu asiwe mwenye shukrani kwa zawadi nyingi tunazopata katika maisha. . . . Muelekeo huo unamukosesha mutu furaha.” (Encyclopedia of Social Psychology)

Ili kuondoa wivu katika mioyo yetu inaomba tuonyeshe unyenyekevu wa kweli na kiasi. Sifa hizo zinatusaidia tupendezwe kabisa na uwezo mbalimbali na sifa nzuri za wengine. Biblia inasema hivi: ‘Bila kufanya jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kujisifu, bali kwa unyenyekevu wa akili mukiwaona wengine kuwa ni bora kuliko ninyi.’—Wafilipi 2:3

KANUNI YA BIBLIA: ‘Na tusiwe wenye kujisifu, wenye kuchochea mashindano juu ya mutu na mwenzake, tukioneana wivu.’Wagalatia 5:26.

3. PENDA WENGINE

Kitabu kimoja kinasema: “Namna watu wanaona uhusiano wao na wengine inaweza kuwasaidia sana wawe wenye kutosheka katika maisha kuliko kazi yao, feza, jamii, ao hata afya yao.” (Social Psychology) Kwa kifupi, ili mutu awe na furaha ya kweli, ni lazima apende na kupendwa na wengine. Mwandikaji fulani wa Biblia alisema hivi: “Ikiwa . . . sina upendo, mimi si kitu.”—1 Wakorintho 13:2.

Ukitaka kujifunza kuwapenda wengine, haujachelewa. Kwa mufano, baba wa Vanessa alikuwa mukali na mulevi. Wakati alikuwa na miaka 14, alitoka nyumbani kwao ili kuishi katika familia fulani zilizokubali kumukaribisha, na pia, katika nyumba moja ya watu wasio na makao ambako anakumbuka kwamba alianza kumuomba Mungu amusaidie. Kisha, aliwekwa katika familia ambayo ilitumikisha kanuni ya Biblia inayosema kwamba ‘upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fazili.’ Pengine hiyo ilikuwa jibu kwa sala yake. (1 Wakorintho 13:4) Hali ya familia hiyo, na yale alikuwa anajifunza kupitia funzo lake la Biblia, yalimusaidia Vanessa apate kitulizo katika moyo na akili. Alisema hivi: “Nilianza kuweza masomo.”

Vanessa angali anaumia katika moyo wake. Hata hivyo, kwa sasa yeye ni mama mwenye furaha, na ana mabinti wawili.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mujivike upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.’—Wakolosai 3:14.

4. JIFUNZE KUPAMBANA NA MATATIZO

Kuna mutu asiye na magumu katika maisha? Kama vile Biblia inasema, kuna “wakati wa kulia” na “wakati wa kuomboleza.” (Mhubiri 3:4) Uwezo wa kupambana na matatizo unatusaidia tuendelee mbele ijapokuwa magumu. Fikiria mufano wa Carol na Mildred.

Carol ana ugonjwa wa uti wa mugongo, diabete ao ugonjwa wa sukari, kushindwa kupumua anapolala, na ugonjwa ambao umefanya jicho lake la kushoto lisione tena. Lakini anasema: “Ninajikaza ili nisiwe mwenye kuvunjika moyo kwa wakati murefu sana. Wakati fulani ninajisikilia huruma. Lakini kisha ninasahau magumu yangu na kumushukuru Mungu kwa yale ninaweza kufanya, zaidi sana kwa ajili ya wengine.”

Mildred naye ana magonjwa mengi, kama vile maumivu ya sehemu zinazounganisha viungo, kansa ya maziba, na diabete. Lakini kama Carol, anajikaza ili asiwaze mingi juu ya magumu yake. Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwapenda watu na kuwafariji wengine wakati wanagonjwa, kufanya hivyo kunanisaidia mimi pia. Tena, ninatambua kwamba wakati ninafariji wengine, ninasahau magumu yangu.”

Carol na Mildred wanahubiria habari njema mutu aliyekuja kufanya matembezi katika bustani

Carol na Mildred walipata furaha kwa kuwafariji wengine

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.



4. JIFUNZE KUPAMBANA NA MATATIZO

Kuna mutu asiye na magumu katika maisha? Kama vile Biblia inasema, kuna “wakati wa kulia” na “wakati wa kuomboleza.” (Mhubiri 3:4) Uwezo wa kupambana na matatizo unatusaidia tuendelee mbele ijapokuwa magumu. Fikiria mufano wa Carol na Mildred.

Carol ana ugonjwa wa uti wa mugongo, diabete ao ugonjwa wa sukari, kushindwa kupumua anapolala, na ugonjwa ambao umefanya jicho lake la kushoto lisione tena. Lakini anasema: “Ninajikaza ili nisiwe mwenye kuvunjika moyo kwa wakati murefu sana. Wakati fulani ninajisikilia huruma. Lakini kisha ninasahau magumu yangu na kumushukuru Mungu kwa yale ninaweza kufanya, zaidi sana kwa ajili ya wengine.”

Mildred naye ana magonjwa mengi, kama vile maumivu ya sehemu zinazounganisha viungo, kansa ya maziba, na diabete. Lakini kama Carol, anajikaza ili asiwaze mingi juu ya magumu yake. Aliandika hivi: “Nimejifunza kuwapenda watu na kuwafariji wengine wakati wanagonjwa, kufanya hivyo kunanisaidia mimi pia. Tena, ninatambua kwamba wakati ninafariji wengine, ninasahau magumu yangu.”

Carol na Mildred wanahubiria habari njema mutu aliyekuja kufanya matembezi katika bustani

Carol na Mildred walipata furaha kwa kuwafariji wengine

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.

Hata kama wanawake hao wawili wanapenda kupata matunzo mazuri, hawahangaikie tu afya yao ya kimwili, lakini wanajikaza kuwa na maoni yanayofaa juu ya matatizo yao na wanatumia vizuri wakati wao. Kwa hiyo, wanapata furaha ya moyoni ambayo hakuna mutu anaweza kuwanyanganya. Tena, wanapendwa na wengine na wanakuwa mufano muzuri kwa watu walio na magumu.KANUNI YA BIBLIA: ‘Mwenye furaha ni mutu anayeendelea kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uzima.’Yakobo 1:12.Shauri hilo lenye hekima la Biblia linapotumikishwa ni ‘muti wa uzima kwa wale wanaoishika, na wale wanaoishika sana wataitwa wenye furaha.’ (Methali 3:13-18) Unaweza kutambua kweli hiyo wewe mwenyewe kwa kutumikisha hekima inayopatikana katika Biblia. Kwa vyovyote, Mutungaji wa kitabu hicho kitakatifu, anayeitwa “Mungu mwenye furaha” anataka wewe pia uwe mwenye furaha. —1 Timotheo 1:11.




*THINGS ARE IN CONTROL, IF YOU TAKE CONTROL OF THEM*(LECTURE 6).

LESSON: *THINGS ARE IN CONTROL, IF YOU TAKE CONTROL OF THEM*(LECTURE 6).

LECTURER: *JOHN WEREMA*.

*Genesis 1:26″ God said ” Now we will make humans,and they will be like us. We will let them rule the fish,the birds,and all other living creatures. “*

➡When God created a man,He gave him all authorities to rule/ to have dominion over the sea,air and over all the earth!!

➡Ruling means controlling!!! i.e, to do whatever you wish to something!!!!

➡Everything has Spiritual ears,if you talk to it, it will hear and obey you!!!

➡👇👇👇👇
*Mark 4:35-39 And the same day, when the even was come, he saith unto them, Let us pass over unto the other side.*
*And when they had sent away the multitude, they took him even as he was in the ship. And there were also with him other little ships.*
*And there arose a great storm of wind, and the waves beat into the ship, so that it was now full.*
*And he was in the hinder part of the ship, asleep on a pillow: and they awake him, and say unto him, Master, carest thou not that we perish?*
*And he arose, and rebuked the wind, and said unto the sea, Peace, be still. And the wind ceased, and there was a great calm.*

➡👆👆👆we have seen that Jesus Spoke to the Sea and it obeyed him!!!

➡Even you now,you can speak with the sea! And the sea will obey you!!

The sea may be diseases, problems, affliction e.t.c.

➡👇👇

*Mark 11:12-14,20 And on the morrow, when they were come from Bethany, he was hungry:*
*And seeing a fig tree afar off having leaves, he came, if haply he might find any thing thereon: and when he came to it, he found nothing but leaves; for the time of figs was not yet.*
*And Jesus answered and said unto it, No man eat fruit of thee hereafter for ever. And his disciples heard it.*
*And in the morning, as they passed by, they saw the fig tree dried up from the roots.*

➡Also Jesus spoke to the Fig tree and it withered!!!!

➡👇👇👇

*Joshua 10:12-13 Then spake Joshua to the LORD in the day when the LORD delivered up the Amorites before the children of Israel, and he said in the sight of Israel, Sun, stand thou still upon Gibeon; and thou, Moon, in the valley of Ajalon.*
*And the sun stood still, and the moon stayed, until the people had avenged themselves upon their enemies. Is not this written in the book of Jasher? So the sun stood still in the midst of heaven, and hasted not to go down about a whole day.*

➡also we have seen that Joshua spoke to the sun,and it obeyed him!!!!

🔵The spirit that was in Jesus, is the same Spirit that is in I and You!!!!

*2 Corinthians 4:13 We having the same spirit of faith, according as it is written, I believed, and therefore have I spoken; we also believe, and therefore speak;*

➡Therefore today you can speak to everything in every conditions, and it will obey you!!!!!

➡Now, start to speak to your condition( sickness,affliction etc,),by knowing that when you speak, it hears you!!!! Command it to leave you in Jesus name!!!!!

Pray…..pray……

*GOD BLESS YOU*

Aina 2 za NAFASI ZA MKRISTO

SOMO: *AINA 2 ZA NAFASI ALIZOPEWA MKRISTO.*(LECTURE 5).

NA *JOHN WEREMA*(0763 441172).

➡Mtu yeyote punde anapookoka,lazima atambue kuwa nafasi mbili zimo ndani yake:-

*1) NAFASI AMBAYO MUNGU AMEMWITIA/AMEMWEKA MTU( WITO)*

➡Angalia 👇👇👇

*Yohana 15:16 imeandikwa ” Si ninyi mlionichagua Mimi, Bali ni Mimi niliyewachagua ninyi; _NIKAWAWEKA_ mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa…”*

*Yeremia 1:10 imeandikwa “Angalia, _NIMEKUWEKA_ leo juu ya Mataifa na juu ya Falme ili Kung’oa na kubomoa na kuharibu,na kuangamiza;ili kujenga na kupanda.*

*Mwanzo 2:15 imeandikwa” BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, _AKAMWEKA_ katika bustani ya Edeni,ailime na aitunze.*

➡Kulingana na misitari hiyo👆👆👆 tunajifunza mambo yafuatayo:-

*a) Hauwezi kuzaa matunda,kama nafasi uliyokaa si sahihi!!*

*b) Hata kama ukizaa matunda kwenye nafasi ambayo sio yako matunda hayo hayawezi kukaa(kudumu)!!!*

*c)Mungu huwa anasema na nafasi;*

– Mara nyingi tumeshindwa kumsikia Mungu kwa sababu tumehama kwenye nafasi zetu

*c)Mungu huwa anaitembelea nafasi*

~Mungu anapotaka kumtembelea mtu huwa anamfuata kwenye ile nafasi aliyomweka!!!!!!

Kwa mfano tunaona Mungu alipomkosa Adam kwenye nafasi aliyimweka,angalia swali ambalo Mungu alimuuliza Adam;
*Adam uko wapi?*
-Maana MUNGU alitegemea kwamba akienda kwenye nafasi angemkuta Adam! Lakini cha kushangaza Adam akawa amehamia kwenye nafasi nyingine tu!!

~Wakristo wengi wamekuwa wakikaa kwenye nafasi ambazo sio za kwao na ndio maana hata kuzaa kwao kumekuwa ni kwa shida sana!!!!

*c)Mungu huwa anaachilia jibu kwenye nafasi*

*d) Mungu huwa anamhesabu mtu kuwa kafanya kazi pale anapofanya kazi akiwa kwenye nafasi yake,hivyo Hata taji ya mtu itategemea mtu huyo aliwajibika vipi kwenye nafasi yake*

➡saa naomba ungalia huu mfano ili uweze kuelewa vizuri kipengele c na d 👇👇

Kwa mfano; *Werema* ameajiriwa na Magufuli na kuwa mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari inayoitwa *Kilimani Secondary school.*
Pia Werema anajihusisha na Kazi ya ukulima!!!

Swali!!!!

1)Je siku vifaa vya Shule vikiisha,Najua werema ni lazima atamtaarifu Mwajiri wake ili amletee vingine! Sasa je,siku Magufuli akiagiza hivyo vifaa, atavileta shuleni unapofanyia kazi ama atavipeleka shambani unakolimia?

~Najua hapo jibu ni kwamba; atavipeleka shuleni!!!!

2)Je werema siku akiishiwa mbolea ya kupandia kwenye shamba lake; Je atampa Mwajiri wake taarifa ili amletee mbolea?

~Najua jibu ni hapana kwasababu mwajiri wake hakumwajiri ili alime,Bali alimwajiri ali Afundishe!!!!

~Kadharika na Mungu ndivyo alivyo!!!! Huwa anaachilia majibu kwenye nafasi aliyomweka mtumishi wake na sio vinginevyo!!

*KUMBUKA*

~Wepesi wa kuifanya kazi fulani,unategemea na eneo sahihi ulilowekwa!!!!!

Kwa mfano!!!ukitaka kushika kitu kwa mikono utafanikiwa haraka sana kwa sababu mikono ipo katika nafasi sahihi!!! Tofauti na ukishika kitu kwa kutumia miguu!

➡watumishi wengi kazi ya Mungu imekuwa ngumu kwao kwa sababu wanatumika eneo ambalo sio sahihi!!!

Omba usiku na mchana ili Mungu akuonyeshe eneo alilokuweka!!!!

*Kipindi kijacho tutaangalia nafasi ya pili anayopewa mtu baada ya kuokoka!!!*

*HII NDO PASAKA YA LEO,KULA UONDOKE*

KUPEVUKA KIIMANI NI KUCHUKUA HATUA NA KWENDA KWENYE TOBA YA KWELI

*KUPEVUKA KIIMANI NI KUCHUKUA HATUA NA KWENDA KWENYE TOBA YA KWELI*
By Pastor Oscar Mkopoka✍✍✍
*LUKA 15:18.*
_Nitaondoka,nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia:Baba nimekosa juu ya mbingu na mbele yako._

*Dhambi ndiyo inayo kutenga na Uso wa Mungu,*
Uchafu wako umekutenga mbali na Neema ya Mungu
*Lakini wewe Mungu, Bwana wangu wewe Umwema mwenye upendo mwingu sana✍✍✍*
*Umesema kwamba kwamba kamwe hutagawana upendo wako na miungu, nahitaji msaada wako*
Hebu Mwambie Mungu siku ya leo Niokoe sasa sababu kwa uovu wangu Jina lako Mungu linatukanwa
*Ndugu yangu mpendwa kupevuka katika imani yaani ni mtu aliyefundishwa kweli na akaijua kweli*
_Ni mtu anayeondoka na kwenda kwa baba mara pale anapopata fahamu kwamba amekosea._
*Swala sio kusikitika na kulia swala ni kuondoka dhambini* Mpendwa,Dhambi ni mbaya
*Tena dhambi sio tasa*

Mtu wa Mungu dhambi ikikomaa huzaa mauti
inakusafirisha hadi kwenye moyo wa jehanam
*dhambi inakupeleka ukachomwe motoni.*

Mtu aliyetambua kosa lake,huondoka na kwenda kutubu mbele ya Mungu wake,
Ushauri wangu
*Ondoka dhambini Upesi*
Unajua kweli ni mkosaji usibaki dhambini
*Ukikosea usitake urudie dhambi acha dhambi ni mbaya*
Kuondoka ni maamuzi yenye afya kuondoka na kwenda kwa Kwa BABA
*Kwanini ukaehivyo mpaka ufe rudi kwa baba yako*
Usibaki dhambini usiseme nitafanya nini sasa mbona kila nikiacha narudia tena dhambi ileile natubu kesho natenda tena
Sikiliza ndugu
*Amua sasa kuachana na dhambi na tubu bila aibu yeyote*
*Usiseme dhambi imekushinda sababu ya aibu zako*
Leo Umeacha hata kuabudu umejitenga mbali na uso wa Mungu ulikuwa unahofu ya dhambi ila sasa huna hofu kabisa

*unashangaa imekuwaje Unafanya dhambi bila woga wowote unatembea na dhambi unalala na dhambini,*
*Unacheka unazungumza na dhambi sababu hiyoo mwonekano wako unaashiria dhambi dhambi dhambi tu*💉💊💊
Leo jibu ni hili hapa,
*Unatakiwa uondoke dhambini na uende kwa Mungu Mungu anakuita Urudi* Achana na dhambi
_Mungu yutayari kukupokea_
Na kukupa wewe nafasi ya wewe kuanza upya

*LUKA 15:18.*
Nitaondoka,nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia:
Baba nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.
barikiwa sana
By Pastor Oscar Mkopoka🙏🙏🙏🙏

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MAOMBI

💫 MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MAOMBI 🛐

Mwl.Peter Francis Masanja

0679392829

SAUTI YA MUNGU MINISTRY

💻 11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

Waefeso 6:11

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 6:12

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

Waefeso 6:13

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

Waefeso 6:14

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

Waefeso 6:15

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

Waefeso 6:16

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

Waefeso 6:17

💫 Kama askari aendavyo vitani , vivyo hivyo na mtu aingiapo katika maombi anatakiwa kujua kuwa maombi ni vita.

💫 Ili mtu aingie kwenye maombi anatakiwa ajipange kwanza , maana anakwenda vitani kupambana na shetani na jeshi lake .

💫 Mtu aendapo vitani huchukua silaha yake na kuiweka tayari kwa kuanza vita .

Mfano , ataandaa bunduki na risasi nyingi kwaajili ya kumpiga adui.

💫 Kwa mtu mwombaji , anapomwendea Mungu anatakiwa ajipange na kuhakikisha kuwa moyo wake wote upo kwa BWA

💫 Baada ya kujipanga anatakiwa kujua kwamba kutangaza vita na shetani vita kwelikweli .

💫 Unatakiwa kufahamu kwamba silaha kuu ya kumshinda shetani ni neno la Kristo pekee.

💫 Shetani hupingwa kwa neno , bila neno huwezi kumshinda shetani na hila zake.

💫 Neno la Kristo linamfanya shetani akimbie .

💻 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Yakobo 4:7

💫Shetani anapingwa kwa neno

💫 Unasisitizwa sana kabla ya kuanza maombi hakikisha unaomba ulinzi.

💫 Tubu pale uponkosea Mungu

💫 Mkaribishe roho Mtakatifu awe mwalimu wako katika maombi yako .

💻 26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Warumi 8:26

💫 Lialike jeshi kutoka mbinguni likulinde

Pia jifunike na damu ya Yesu .

💻 Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama Bwana asingaliwatoa?

Kumbukumbu la Torati 32:30

💫 Ni kazi ngumu kumfanya shetani akukimbie , mpaka uite msaada kutoka mbinguni.

🖊 Ualike jeshi la malaika kutoka mbinguni liwe pamoja na wewe katika maombi .

💫 Vita ya kiroho unayopigana siyo yako ni vita ya Mungu na adui zako

💫 Mungu ni adui wa adui zako wanaokusumbua katika ulimwengu wa roho na ulimwengu wa macho .

💫 Ili Mungu aingilie hiyo vita lazima umwite yeye maana ukinyamaza hawezi kuwaondosha adui zako.

💻 6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;

Isaya 62:6

💫Hutakiwi kunyamaza kimya wewe mwana wa Mungu maana Mungu mwenyewe anasisitiza usinyamaze mkumbushe mahitaji yako .

💫 Maombi yako yatafaa zaidi ukianza na kumsifu Mungu .

💫 Kumwimbia Mungu sifa na kuabudu kunamfanya Mungu aachilie nguvu ya ajabu ndani yako .

💫 Maombi ya mtu anayeanza na kumsifu Mungu yana nguvu sana kuliko maombi makavu yaani maombi bila kumsifu Mungu .

✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻

Mungu akubariki sana nahitimisha kwa kuaema hivi.

💫 Katika maombi zingatia

1⃣ Sifa na kuabudu ili maombi yako yawe ya ushindi .

2⃣ Hakikisha unamwalika Roho Mtakatifu akufundishe vita .

3⃣ Alika jeshi la malaika kutoka mbinguni likuzingire ili shetani asipate nafasi ya kukudhuru.

4⃣ Jifunike na damu ya YESU wewe na vitu vyote ulivyonavyo ili shetani asipate nafasi ya kukudhuru wewe na vitu vyako.

5⃣ Hakikisha unatumia neno la Mungu katika maombi yako maana neno ndyo silaha kuu ya kumharibu shetani .

https://peterfrancismasanja.blogspot.com

Visit website

JINSI YA KUPATA NGUVU YA MUNGU KUTOKA KWENYE NENO LA MUNGU

SOMO LA 3: *JINSI YA KUPATA NGUVU YA MUNGU KUTOKA KWENYE NENO LA MUNGU*

NA *JOHN WEREMA*(0763 441172)

Kabla hatujaendelea Naomba nikuulize kwanza hili swali!!!!
*Swali*
Hivi mtu akikwambia kwamba Chakula hiki kina wanga,ama kina protini,ama kina kabohydrate!! Je ukitaka kupata kile kichomo ndani ya kile chakula ,unatakiwa ufanye nini?

Au ngoja nirahisishe swali:-

kwa mfano,huwa nasikia watu wanasema kwamba ugali wa Dona una nguvu sana! Je,ukitaka kuipata ile nguvu iliyomo ndani ya Ugali wa dona; unapaswa kufanya nini??

Hapo bila shaka najua ni lazima ule huo ugali wa dona,kisha ugali huo usharabiwe!! Hapo ndipo mtu atakuwa amepata nguvu zilizomo kwenye ugali wa Dona!!!

➡Haya tuendelee sasa👇👇👇👇
*Waebrania 4:12 imeandikwa “Maana Neno la Mungu li hai,tena lina NGUVU…….……….*

➡Sikiliza,Hatua zile zile zinazochukuliwa kupata nguvu iliyomo ndani ya ugali wa Dona,ndo hatua hizo hizo zinazochukuliwa kupata nguvu iliyomo ndani ya Neno la Mungu!!!!

➡Sikiliza tena; Neno la Mungu ni chakula cha roho!

ndo maana sasa katika *Mathayo 4:4 imeandikwa” Mtu hataishi kwa mkate tu,bali kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu*

➡Sikiliza tena;Mwanadamu ni mtu,katika watu wawili yaani mtu wa nje(mwili,ambaye ametokea duniani) na mtu wa ndani(roho),ambaye ametokea Mbinguni!!!!

*1 wakorintho 15:47 imeandikwa ” Mtu wa kwanza atoka katika nchi,ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.*

➡Mtu wa nje huwa anajengwa kwa vyakula vya duniani mfano,nyama,ugali,wali n.k
Lakini mtu wa ndani huwa anajengwa na vyakula vya Mbinguni!

*Yohana 6:51 imeandikwa ” Mimi ndimi chakula chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka MBINGUNI;mtu akila chakula hiki,ataishi milele.*

➡Chakula cha Mbinguni alichokuwa anakizungumzia Yesu lilikuwa ni neno lake! na hapo aliyekuwa anapaswa kula chakula hicho ni mtu wa ndani!!!!

➡sasa kama tunavyofahamu kwamba,kuna vyakula aina ya protini,wanga,kabohydrate,mafuta! N.k

Kadharika hata katika Neno la Mungu ni hivyo hivyo; yaani kuna neno la kutia joto,kutia nguvu,kuimarisha roho n.k!!!!

*Swali*
Je nifanye nini ili niweze kupata nguvu iliyomo ndani ya Neno la Mungu?

*Jibu*

*Yoshua 1:8 imeandikwa ” Kitabu hiki cha torati kisiondoke Kinywani mwako,Bali uyatafakari maneno yake mchana na usiku,upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo;maana ndipo utakapoifanikisha njia yako,kisha ndipo utakapositawi sana.*

📩ukiangalia huo msitari utagundua vitu kama vinne, ambavyo vimebeba majibu kamili! Navyo ni:-

*1)Kulisoma Neno.(Kuingiza neno kwenye tumbo la roho)*
Hii ni hatua ya mwanzo kabisa ambayo imefananishwa na mtu pale anapokuwa anaingiza matonge ya ugali tumboni!!!!!

-Kumbe cha kwanza Ni lazima tuliingize neno la Mungu ndani yetu kwa wingi kama tunavyoingiza matonge ya ugali!!!!

*Wakolosai 3:16a imeandikwa ” Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu*

➡Kama vile Mwili ulivyo na tumbo la chakula,kadharika na roho ina tumbo la kuhifadhia neno la Mungu,na kama mwili ulivyo na kinywa cha kupokelea chakula; kadharika na roho nayo ina kinywa cha kupokelea neno la Mungu!

*Ezekieli 3:3 imeandikwa “akaniambia mwanadamu lisha TUMBO lako,ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila,nalo KINYWANI mwangu lilikuwa tamu,kama utamu wa sukari.*

➡hivyo tunapaswa kuhakikisha kila siku matumbo yetu ya rohoni yanapata chakula cha kutosha!!!!

*2)Kulimeng’enya Neno(kulitafakari neno)*

➡Kama vile baada ya chakula kuingia tumboni,hatua inayofuata huwa ni hatua ya umeng’enyaji; kadharika Neno la Mungu linapoingizwa ndani ya tumbo la roho,hatua inayoyfuata inabidi iwe hatua ya kumeng’enywa!

➡Neno la Mungu huwa tunalimeng’enya kwa kulitafakari muda wote muda tuhakikishe nguvu iliyokuwa ndani ya neno imeingia ndani ya roho na kuzalisha nguvu.

*N.B:Kuna tofauti kubwa sana kati ya kushiba chakula; na kupata nguvu ya chakula!!!!kama hauamini kawaulize wale wanaoendesha(wanaoharisha) wakishamaliza kula watakwambia Ukweli huu*

*Mithali 16:20 imeandikwa” Atakayelitafakari Neno,atapata mema*

➡Hili ndilo eneo ambalo huwa huwa linahamisha virutubisho vilivyomo kwenye Neno na kiviingiza rohoni!!!
➡Pia hili ni eneo ambalo watu Mara nyingi huwa wanamsikia Mungu!!!

➡hili ndio eneo ambalo watu huwa wanapata sana nguvu za Mungu!!!

➡Ukiwa ni msomaji tu halafu hutaki kutafakari neno,hakika huwezi kupiga hatua ya kiroho!

➡Kusoma Neno sio issue,issue ni kwamba,Je unakipata kile kilichomo ndani ya Neno?

*USHAURI*

Kama vile unavyotenga muda wa kusoma neno,muda wa kuomba; kadharika Tenga na muda wa kulitafakari Neno ulilolisoma!!!!!!!

Mwambie Roho Mtakatifu akupe NGUVU ya kulitafakari neno lake usiku na mchana!!!

Namalizia kwa kusema kwamba ;

*Mafanikio hayaji kwa kulisoma neno tu,Bali kwa kulisoma na kulitafakari.*

*Hii ndo pasaka ya leo,kula UONDOKE*

Chakula chenye NGUVU NA USHINDI WAKE

SOMO LA 1: *UWEZO WA KULIFIKIA KUSUDI INATEGEMEA NA NGUVU YA CHAKULA UNACHOKULA*

NA *JOHN WEREMA*(0763 441172).
Tunaanza hivi:-

*1 wafalme 19:4-8 imeandikwa “Lakini Yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja,akaenda akaketi chini ya mretemu………Naye akajinyosha akalala chini ya mretemu;tazama Malaika akamgusa,akamwambia,INUKA,ULE. Akatazama, kumbe!pana MKATE umeokwa juu ya makaa,na gudulia la maji,kichwani pake. Akala,akanywa,akaenda KATIKA NGUVU ZA CHAKULA HICHO SIKU AROBAINI MCHANA NA USIKU hata akafika Horebu,Mlima wa Mungu*

➡Katika hiyo mistari tunajifunza vitu vifuatavyo:-

1) Usipotembea kwa nguvu zitokanazo na chakula cha Mungu,safari yako itakuwa fupi sana!!!

Angalia👇👇👇
Kwenye ule msitari wa 4 Biblia inatuambia kwamba *lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa Siku moja,akaedelea akaketi chini ya mretemu. Akajiombea roho yake afe.*

Mtumishi yeyote anayeifanya kazi ya Mungu pasipo kuwa na nguvu za Mungu za kutosha,itamwia vigumu sana kufanya kazi hiyo! Na ndo maana wengi Wao huwa wanaishia njiani katika utumishi!!!!

*Mithali 24:10 imeandikwa” UKUZIMIA SIKU YA TAABU,NGUVU ZAKO NI CHACHE*

2) Kilichomfanya Elia atembee siku arobaini jangwani usiku na mchana; ni ile nguvu iliyozalishwa na kiwango cha chakula alichokula!

➡Sikiliza,Kinachomfanya mtu atembee,aongee,aruke ruke,sio ujanja wake! La hasha! Bali ni ile nguvu inayozalishwa na chakula anachokula siku zote!!

Kama hauamini haya niyasemayo, kamuulize mtu aliyefunga siku tano kavu kama anaweza hata kukimbia mchaka mchaka!

➡Kadharika katika utumishi,Neno la Mungu ndo Chakula cha Mtumishi wa Mungu!

➡kiwango cha Neno anachokula mtumishi wa Mungu,ndo kiwango cha Nguvu inayozalishwa!

Biblia inasema *Elia akaenda kwa Nguvu ya Chakula hicho muda wa Siku arobaini*

Angalia tena👇👇👇

*waefeso 3:20 imeandikwa “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo,KWA KADRI YA NGUVU ITENDAYO KAZI NDANI YETU*

➡Sikiliza,Mungu huwa anatumia kiasi cha Nguvu cha neno lake kilichomo ndani ya mtu katika kutenda kazi !!!

➡Ndo maana sasa usije ukashangaa wewe unakemea pepo linashindwa kutoka,lakini anakuja mwenzako anakemea pepo linatoka!!

Kama haumini Kawaulize wanafunzi wa Yesu kama ukibahatika kukutana nao hapo mtaani kwenu,kwamba ni kwanini walishindwa kumtoa yule pepo lakini Yesu akaweza!!!!

Hapo issue ni nguvu zao zilikuwa chache kuliondoa Pepo!

*N.B; Kiwango cha nguvu za Mungu ndani ya mtu ni proportion na kiwango cha imani iliyomo ndani ya mtu*

3) Eliya alifika Mungu alipotaka afike baada ya kula mkate!!!

Angalia:-

Biblia inasema,baada ya Elia kula ule mkate na kuyanywa yale maji,alitembea siku arobaini mchana na usiku mpaka kufika kwenye mlima wa Mungu!!!!

➡Sikiliza mpendwa,kuna kiwango cha neno la Mungu unapaswa kula ili kikupatie nguvu ya kufika Mungu alipokukusudia ufike!

Sikiliza,Chakula anachotakiwa kula *Kazimoto* ili apate nguvu ya kulitimiza kusudi la Mungu alilomwitia,ni tofauti na Chakula anachotakiwa kula *Werema*maana kila mtu ameitiwa kusudi tofauti tofauti!!!

➡Elia asingekula mkate,asingepata nguvu ya kufika horebu!
Ukifatilia vizuri,utaona kabisa Elia alitembea Siku moja tu ghafla akajiombea kufa! Mpaka Mungu alipoingilia kati!!

➡Ndo maana watumishi wengi huwa wanakufa haya kabla ya kutimiza kusudi!

Kabla sijamaliza Hii sehemu ya kwanza,naomba nikuachie maswali haya:-
1) Je unalijua kusudi alilokuitia Mungu?

2)unafahamu kusudi hilo lina urefu kiasi gani?

3) unafahamu kiwango cha chakula unachotakiwa kula ili kikupe nguvu ya kuimaliza safari?

*HII NDO PASAKA YA LEO,KULA UONDOKE*

Uhusiano kati ya KUONA,KUAMINI na UHAKIKA

SOMO: *MAHUSIANO KATI YA UHAKIKA, KUONA NA KUAMINI* (LECTURE 2).

NA *JOHN WEREMA*(0763 441172).

Angalia👇👇
*Marko 15:31-32 imeandikwa “Kadharika na wakuu wa makuhani wakamdhihaki wao kwa wao,pamoja waandishi,wakisema,aliponya wengine; hawezi kujiponya mwenyewe. Kristo,mfalme wa Israeli,na ashuke sasa msalabani tupate _KUONA NA KUAMINI._*

➡Sikiliza,watu wale walikuwa walichokuwa wanakitafuta ni kitu kilichokuwa kinaitwa *UHAKIKA*.

➡Sikiliza,Kinacholeta *UHAKIKA*ni *KUONA*, na kinacholeta *KUAMINI* ni *UHAKIKA.*
➡huwezi kuwa na Uhakika na kitu fulani,kama haujakiona bado! na huwezi kukiamini kitu kama haujapata uhakika!

➡Ndio maana sasa katika kitabu cha Waebrania tunaambiwa kwamba Imani ni kuwa na Uhakika…

*Waebrania 11:1 imeandikwa” Basi imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo.,……..*

➡hakuna mtu awezae kuamini kama hana Uhakika na anachotaka kukiamini!!!

➡Angalia alichokizungumza Tomaso alipotaka kuaminishwa pasipo kuona 👇👇👇

*Yohana 20:24-29 imeandikwa “Walakini mmoja wa wale Thenashara,Tomaso,aitwaye Pacha,hakuwa pamoja nao alipokuja Yesu. Basi wanafunzi wakamwambia,TUMEMWONA Bwana. Akawaambia, Mimi NISIPOZIONA mikononi mwake kovu za misumari,na KUTIA KIDOLE CHANGU katika mahali pa misumari,na kutia mkono wangu katika ubavu wake,mimi SISADIKI hata kidogo. Basi baada ya siku nane,wanafunzi wake walikuwamo ndani tena,na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu,na milango imefungwa,akasimama katikati,akasema,Amani iwe Kwenu. Kisha akamwambia Tomaso,lete hapa kidole chako;uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu,wala usiwe asiyeamini bali aaminiye. Tomaso akajibu,Bwana wangu na Mungu wangu! Yesu akamwambia,Wewe ,kwa kuwa UMENIONA,UMESADIKI; wa heri wale wasioona,wakasadiki.*

➡Ukiangalia hiyo mistari vizuri utagundua vitu vifuatavyo:-

1)Kilichowafanya wale wanafunzi wamwamini Yesu,ni pale walipomwona!!!

Hapa utaona pale walipomwambia Tomaso kwamba *tumemwona Bwana*

2)Kilichomfanya Tomaso ashindwe kuamini kwamba Yesu amewatokea wenzake ni kwa sababu hakumwona Yesu; hivyo ndani yake yalibaki mashaka!!!

3)Kilichoondoa mashaka na wasiwasi ni pale alipoona kile alichotaka kukiona!!!

4)Kilichomfanya Yesu amkemee Tomaso ni pale Tomaso alipotaka kuona kwa kutumia macho ya mwilini badala ya kutumia macho ya Imani.

*AINA MBILI ZA KUONA*
1) Kuona kwa jinsi ya mwili(kuona kwa macho ya kimwili
2) kuona kwa jinsi ya rohoni(kwa kutumia macho ya Imani)

➡Kipindi hiki cha Agano jipya, ni kipindi ambacho Mungu anataka tutembee na kuishi katika roho,hivyo kila kitu tunapaswa kukifanya katika roho.

Kama ni kuona,basi tutumie macho ya Imani katika kuona!

➡Narudia tena, hakuna mtu awezaye kuamini pasipo kukiona kile kitu kwa macho ya Imani.

➡tunapolisikia neno la Mungu,tunapaswa kulitafakari lile Neno mpaka picha ijengeke,then tuione hiyo picha kwa jinsi ya imani!! Na hapo ndipo tutakapoweza kuwa na Imani isiyo na mashaka!!!

*warumi 4:19-20 imeandikwa “lakini yeye asiyekuwa dhaifu wa Imani,alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa………Lakini AKIIONA ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini bali alitiwa nguvu kwa imani,akimtukuza Mungu; huku akijua HAKIKA Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.*

Angalia mambo haya:-
1)Kilichomfanya Ibrahimu aache kuuangalia mwili wake ni *IMANI*

2)Kilichomfanya Ibrahimu awe na Imani ni *UHAKIKA* alioupata juu ya Ahadi za Mungu.

3)Kilichompatia Ibrahimu Uhakika ni *KUONA*
Tumesoma kwamba Ibrahimu *alipoiona*ahadi hakusita kwa kutokuamini!

➡Ndani ya Neno la Mungu,imo picha ambayo kazi yake ni kukuonesha kile kilichobebwa na Neno!!!!!!

*Waebrania 11:13 imeandikwa” Hawa wote wakafa katika IMANI,wasijazipokea zile ahadi,bali WAKAZIONA tokea mbali na kuzishangilia na kukiri kwamba walikuwa wageni,na wasafiri juu ya nchi.*

➡hivyo tunapolisoma neno la Mungu,ili tuweze kuipata Imani isiyo ya unafiki,ni lazima tulitafakari neno hilo mpaka tukione kwa macho ya imani kile tunachotakiwa kukipata!!!!

🔵Karibu kama kuna mwenye kuongezea katika haya!! Mungu akubariki!!

*HII NDO PASAKA YA LEO,KULA UONDOKE*

KUKAA KIROHO

_Kila Mwenda mbinguni ‘sipite hapa_

*MFASIRI WA MAMBO MAGUMU YA MUNGU*

Na
*Ev.Kazabao Edson*
*+255763575550*

Mpendwa ,kati ya mambo yanayoleta changamoto kubwa kwa Kanisa la Leo ni *uduni Wa kuisikia sauti ya Mungu*…katika nyakati hizi za ukingoni tunapotegemea Bwana na Mwokozi wetu kurudi ,zimekuwapo sauti nyingi nyingine hata za udanganyifu.

*1 Tim.4:1 1* Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, *wakisikiliza roho zidanganyazo,😈 na mafundisho ya mashetani👹;*

NB:
Ni rahisi mno kuelewa ninachoongea katika mazungumzo ya kawaida na ngumu sana kuelewa ninachomaanisha ,bila kuujua moyo wangu.

*Maana yake*
Ni rahisi mno kuhisi “kuelewa” kile Neno/sauti ya Mungu imesema bila kujua *original intention* ya Mungu katika neno au sauti hiyo.Katika Biblia zetu hizi zinazobadilika tafsiri kila kukicha tunamwitaji sana “mfasiri Wa kale asiyebadili neno wala maana ,achukuaye katika moyo Wa Msemaji Wa kwanza *( A translator of primary speaker)*

Kanisa lipo hapa lilipo leo,kwa sababu kila mmoja anakuja na ujuzi wake *,tena wengine mkienda zaidi na kuiga kila afanyacho au asemacho “so called a mentor au baba Wa kiroho*…I tell you Mungu apendi na haya maneno nayaandika nikiambiwa hivyo na Roho.

*Moses heard an original voice,David saw real vision like Daniel and Isaiah.. Why not me and you?????*…Tatizo linakuja hapo Tukubaliane na kurekebisha *”TUMEKUWA WAVIVU WA KUOMBA NA KUJENGA USHIRIKA MZURI NA ROHO MTAKATIFU”*

unapoomba (hasa kwa Roho/lugha mpya) na kutafakari katika Roho unapata kitu kinaitwa *Divine ntelligence* yaani mbinu ya kiroho ya *kupeleleza na kufahamu mambo ya Rohoni katika uhalisia wake*(inahusisha kulata majibu ya maombi yako ,moja kwa moja,Na *akili mpya za kufanya mambo katika ubora ikiwemo Huduma,wokovu,biashara n.k*)

Ni rahisi mno Leo ,kukuta Mtumishi Wa Mungu mwenye *mafunuo* mengi (ya ajabu na kuaibisha) akidai ni sauti ya Mungu huku akiwa na akili timamu *( Achana na zile Delusions za Nabii Tito😄)*

Njia nyepesi ya kutambua aina ya sauti inayonena masikioni mwake inategemea *Kama alipokea kipawa cha “mfasiri” yaani Roho Mtakatifu kabla ya kuitwa katika Huduma Fulani*

Hakuna mtume hata mmoja,aliyeanza Huduma bila kipawa cha Roho Mtakatifu,Unaona hata Petro anaanza kuhubiri Mara tu baada ya *kubatizwa kwa moto*🔥🔥🔥 wa Roho Mtakatifu pale Jerusalem 33A.D.Kwa wewe unayeweza kusimama madhabahuni in the name of “shule”/uzoefu/Vitabu ingi/na theology sikukatishi tamaa …ila nakukumbusha …lazima utenge muda Wa kutosha kuhakikisha *”Mfasiri”* anakufundisha “unavyoweza kuzinena Siri za Mungu waziwazi na watu wakafunguliwa vifungo,mizigo ,dhambi n.k Isaya 60:1 *Jesus original mission* entrusted*)

Mambo ya Mungu ni magumu sana kueleweka kwa jinsi ya mwili,yanamuhitaji “mfasiri mkuu atokaye katika moyo Wa Mungu”yaani Roho wake.Hata Yesu alifahamu kuwa wanafunzi wake waingeweza bila huyo Roho *”mfasiri mkuu Wa mambo ya Mungu”*

Roho mtakatifu ni muungwana sana *(He is very Gentleman)*…Yaani kama hujajitenga ukapanda ghorofani Pale Jerusalem na Kusema *karibu*. Yeye huwa hajipendekezi. Kwahiyo unakuwa unaishi bila Yeye (na ikumbukwe Yeye ndiye nafsi pekee ya Mungu anayekaa kati kati yetu…bila Huyo unakuwa ni *Yatima*(Yesuvakasema sitowaacha yatima kwahiyo bila Roho unakuwa in ….malizia basi☺) yaani huna Mungu zaidi ya Dini na dhehebu (Carnal man)

Mtu ambaye hana Roho wa Mungu *hawezi kupokea mambo yanayotoka kwa Roho wa Mungu kwa sababu mambo hayo ni upuuzi kwake;*(Yaani hapa anaona kama naandika upuuzi,non applicable skills na kujifanya kiroho zaidi🤣🤣🤣kazi ya Mungu yahitaji moyo dah) na hawezi kuyaelewa kwa kuwa hayo yanaeleweka tu kwa msaada wa Roho. (Muhubiri aliyejizoesha kufundishwa na Roho akihubiri ,in Mara chache mno MTU Wa mwilini kuelewa kuwa kweli hajakusudia kumsema Yeye na huenda ana *spy* matokeo huwa ni Toba,kiu mpya yakumjua Mungu au Chuki kwa mhubiri kulingana na kiwango cha neema kilicho juu take…Lako lipi hapo?)

Imeandikwa katika *….1wakorinto2:13-15*

*13.Basi mwanadamu wa tabia ya asili (ambaye hajabatizwa kwa Roho Mtakatifu/MTU Wa Dini) hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.*

14 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.

*15 Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.*

*Ni kitu kigumu sana kupendeza Mungu pasipo kujua mapenzi yake,Ni vigumu kuyajua mapenzi yake pasipo kuelezwa ,ni vigumu kuelezwa pasipo kuwa na ushirika naye na pasipo kusikiliza ,ni ngumu kusikia ,Ni ngumu pia kuelewa pasipo kujizoeza katika kuomba,kusoma neno na kutafakari*

*Yohana:16.13-14*
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, *lakini yote atakayoyasikia atayanena*, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

14.Yeye atanitukuza mimi, *kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.*

*Tusiombe tena ,kuhubiri wala kusikiliza ama kusoma neno la Mungu kwa akili na mazoea yetu,Leo*

*Kanisa na watu mmoja mmoja Leo wanatofautisna na kunyosheana vidole sababu hii*

*Katika utafiti mfupi niliofanya nimejikuta nikiwa na siri moja na MTU mwingine aliyefunuliwa neno Fulani bila kutofautiana hata nukta(Mfasiri mkuu kazini)

#Nimefasiri kama alivyonifasiria mfasiri mkuu Wa mambo ya Mungu

#Mahubiri yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe huwabadili watu sana kwani Mungu mwenyewe hunena kupitia mhubiri embu angalia hapa

_Kila Mwenda mbinguni ‘sipite hapa_

*MFASIRI WA MAMBO MAGUMU YA MUNGU*

Na
*Ev.Kazabao Edson*
*+255763575550*

Mpendwa ,kati ya mambo yanayoleta changamoto kubwa kwa Kanisa la Leo ni *uduni Wa kuisikia sauti ya Mungu*…katika nyakati hizi za ukingoni tunapotegemea Bwana na Mwokozi wetu kurudi ,zimekuwapo sauti nyingi nyingine hata za udanganyifu.

*1 Tim.4:1 1* Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, *wakisikiliza roho zidanganyazo,😈 na mafundisho ya mashetani👹;*

NB:
Ni rahisi mno kuelewa ninachoongea katika mazungumzo ya kawaida na ngumu sana kuelewa ninachomaanisha ,bila kuujua moyo wangu.

*Maana yake*
Ni rahisi mno kuhisi “kuelewa” kile Neno/sauti ya Mungu imesema bila kujua *original intention* ya Mungu katika neno au sauti hiyo.Katika Biblia zetu hizi zinazobadilika tafsiri kila kukicha tunamwitaji sana “mfasiri Wa kale asiyebadili neno wala maana ,achukuaye katika moyo Wa Msemaji Wa kwanza *( A translator of primary speaker)*

Kanisa lipo hapa lilipo leo,kwa sababu kila mmoja anakuja na ujuzi wake *,tena wengine mkienda zaidi na kuiga kila afanyacho au asemacho “so called a mentor au baba Wa kiroho*…I tell you Mungu apendi na haya maneno nayaandika nikiambiwa hivyo na Roho.

*Moses heard an original voice,David saw real vision like Daniel and Isaiah.. Why not me and you?????*…Tatizo linakuja hapo Tukubaliane na kurekebisha *”TUMEKUWA WAVIVU WA KUOMBA NA KUJENGA USHIRIKA MZURI NA ROHO MTAKATIFU”*

unapoomba (hasa kwa Roho/lugha mpya) na kutafakari katika Roho unapata kitu kinaitwa *Divine ntelligence* yaani mbinu ya kiroho ya *kupeleleza na kufahamu mambo ya Rohoni katika uhalisia wake*(inahusisha kulata majibu ya maombi yako ,moja kwa moja,Na *akili mpya za kufanya mambo katika ubora ikiwemo Huduma,wokovu,biashara n.k*)

Ni rahisi mno Leo ,kukuta Mtumishi Wa Mungu mwenye *mafunuo* mengi (ya ajabu na kuaibisha) akidai ni sauti ya Mungu huku akiwa na akili timamu *( Achana na zile Delusions za Nabii Tito😄)*

Njia nyepesi ya kutambua aina ya sauti inayonena masikioni mwake inategemea *Kama alipokea kipawa cha “mfasiri” yaani Roho Mtakatifu kabla ya kuitwa katika Huduma Fulani*

Hakuna mtume hata mmoja,aliyeanza Huduma bila kipawa cha Roho Mtakatifu,Unaona hata Petro anaanza kuhubiri Mara tu baada ya *kubatizwa kwa moto*🔥🔥🔥 wa Roho Mtakatifu pale Jerusalem 33A.D.Kwa wewe unayeweza kusimama madhabahuni in the name of “shule”/uzoefu/Vitabu ingi/na theology sikukatishi tamaa …ila nakukumbusha …lazima utenge muda Wa kutosha kuhakikisha *”Mfasiri”* anakufundisha “unavyoweza kuzinena Siri za Mungu waziwazi na watu wakafunguliwa vifungo,mizigo ,dhambi n.k Isaya 60:1 *Jesus original mission* entrusted*)

Mambo ya Mungu ni magumu sana kueleweka kwa jinsi ya mwili,yanamuhitaji “mfasiri mkuu atokaye katika moyo Wa Mungu”yaani Roho wake.Hata Yesu alifahamu kuwa wanafunzi wake waingeweza bila huyo Roho *”mfasiri mkuu Wa mambo ya Mungu”*

Roho mtakatifu ni muungwana sana *(He is very Gentleman)*…Yaani kama hujajitenga ukapanda ghorofani Pale Jerusalem na Kusema *karibu*. Yeye huwa hajipendekezi. Kwahiyo unakuwa unaishi bila Yeye (na ikumbukwe Yeye ndiye nafsi pekee ya Mungu anayekaa kati kati yetu…bila Huyo unakuwa ni *Yatima*(Yesuvakasema sitowaacha yatima kwahiyo bila Roho unakuwa in ….malizia basi☺) yaani huna Mungu zaidi ya Dini na dhehebu (Carnal man)

Mtu ambaye hana Roho wa Mungu *hawezi kupokea mambo yanayotoka kwa Roho wa Mungu kwa sababu mambo hayo ni upuuzi kwake;*(Yaani hapa anaona kama naandika upuuzi,non applicable skills na kujifanya kiroho zaidi🤣🤣🤣kazi ya Mungu yahitaji moyo dah) na hawezi kuyaelewa kwa kuwa hayo yanaeleweka tu kwa msaada wa Roho. (Muhubiri aliyejizoesha kufundishwa na Roho akihubiri ,in Mara chache mno MTU Wa mwilini kuelewa kuwa kweli hajakusudia kumsema Yeye na huenda ana *spy* matokeo huwa ni Toba,kiu mpya yakumjua Mungu au Chuki kwa mhubiri kulingana na kiwango cha neema kilicho juu take…Lako lipi hapo?)

Imeandikwa katika *….1wakorinto2:13-15*

*13.Basi mwanadamu wa tabia ya asili (ambaye hajabatizwa kwa Roho Mtakatifu/MTU Wa Dini) hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.*

14 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.

*15 Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.*

*Ni kitu kigumu sana kupendeza Mungu pasipo kujua mapenzi yake,Ni vigumu kuyajua mapenzi yake pasipo kuelezwa ,ni vigumu kuelezwa pasipo kuwa na ushirika naye na pasipo kusikiliza ,ni ngumu kusikia ,Ni ngumu pia kuelewa pasipo kujizoeza katika kuomba,kusoma neno na kutafakari*

*Yohana:16.13-14*
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, *lakini yote atakayoyasikia atayanena*, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

14.Yeye atanitukuza mimi, *kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.*

*Tusiombe tena ,kuhubiri wala kusikiliza ama kusoma neno la Mungu kwa akili na mazoea yetu,Leo*

*Kanisa na watu mmoja mmoja Leo wanatofautisna na kunyosheana vidole sababu hii*

*Katika utafiti mfupi niliofanya nimejikuta nikiwa na siri moja na MTU mwingine aliyefunuliwa neno Fulani bila kutofautiana hata nukta(Mfasiri mkuu kazini)

#Nimefasiri kama alivyonifasiria mfasiri mkuu Wa mambo ya Mungu

#Mahubiri yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe huwabadili watu sana kwani Mungu mwenyewe hunena kupitia mhubiri embu angalia hapa
type *”boring preaching”*

*Asomaye na afahamu na kufurahi*

https://m.facebook.com/kazabao.edson?ref=bookmarks
*Kazabao Edson*
*+255763575550*
What’s app

(MtumwaKwaAjiliYaBwana)

*Asomaye na afahamu na kufurahi*

https://m.facebook.com/kazabao.edson?ref=bookmarks
*Kazabao Edson*
*+255763575550*
What’s app

(MtumwaKwaAjiliYaBwana)

Mahusiano kati ya dhambi na magonjwa

SOMO: *MAHUSIANO KATI YA MAGONJWA NA DHAMBI* ( LECTURE 1)

NA *JOHN WEREMA*(0763 441172)

📩Magonjwa mengi yanayowapata wanadamu chanzo chake huwa ni dhambi!!! Lakini sio kwamba kila aliye mgonjwa ametenda dhambi!!!

Angalia👇

*Zaburi 103:3 imeandikwa “Akusamehe MAOVU yako yote,AKUPONYA MAGONJWA yako yote.*

➡Umeona sasa,kumbe tunaona kwamba punde msamaha unapotolewa,na uponyaji unaachiliwa!!!!

➡kifungo kikubwa kinachozuia watu wengi kupokea uponyaji huwa ni dhambi.

➡hivyo,palipo na msamaha,kuna uponyaji wa kweli.

*Marko 2:3,5 imeandikwa” Wakaja watu wakimletea mtu mwenye KUPOOZA,anachukuliwa na watu wanne. Naye Yesu, alipoiona imani yao,akamwambia yule mwenye KUPOOZA, mwanangu,UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.*

➡katika hiyo misitari, tunaona kwamba kilichokuwa kimemfunga yule ndugu aliyekuwa amepooza ilikuwa ni dhambi! Lakini punde dhambi ilipoondolewa ndani yake,mara akawa mzima!!

➡Mara nyingi unaweza ukawa unamuombea mgonjwa,halafu unashangaa hapokei uponyaji!! Ukiona jambo kama hilo usianze kujilaumu kwamba labda hauna nguvu za Mungu; NO!!! bali fuatilia siri iliyo nyuma ya yule mgonjwa! Inaweza kuwa kuna vitu fulani fulani anavificha hataki kuvisema hadharani!!! Kwa hiyo mtu kama huyo usitegemee kama atafunguliwa asipojiweka wazi!!

*Mithali 28:13 imeandikwa “Afichaye dhambi zake HATAFANIKIWA;bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”*

➡hilo neno *HATAFANIKIWA* maana yake hawezi kupata kile anachokihitaji. Sasa kama anahitaji uzima hawezi kuupata maana bado hajatubu!

➡Sio kila aliye Kanisani amesamehewa dhambi!! NO!! Kuna watu wanasali lakini bado kuna vitu vya kishetani wamevishikilia hawataki kuviachilia!!!

➡Biblia inasema kwamba,kila akaaye kwenye ufalme wa Yesu,hatapatwa na magonjwa maana atakuwa ameshasamehewa dhambi!

*Isaya 33:24 imeandikwa” Wala hapana mwenyeji atakayesema,Mimi MGONJWA;watu wakaao humo watasamehewa UOVU wao.*

➡Sikiliza,ni kweli Yesu aliyatwaa magonjwa yote ya mwanadamu na kuyaweka msalabani!ili sisi wanadamu tusiwe na magonjwa! Lakini mwanadamu atahesabiwa kuwa hastahili kupata magonjwa punde anapotubu dhambi zake na kumpokea Yesu moyoni mwake!!!

*SWALI*
*_Mbona kuna watu wengine wameokoka vizuri sana na wengine ni wachungaji, maaskofu,wainjilisti; lakini bado wanasumbuliwa na magonjwa kama kisukari,pressure,kansa,moyo n.k!! Je watu hao wanakuwa wametenda dhambi?_*

*JIBU*
Watu hao wanakuwa hawajatenda dhambi! Lakini ukiona hivyo,tambua kati ya haya mawili moja linaweza likawa ni la kwake!!!

*1)PITO*
-muda mwingine Mungu huwa anaamua kumpitisha mtumishi wake,ili kumtengeneza kujitwalia utukufu!!

-Mungu anapoachilia pito kama hili huwa pia anaachilia amani ndani ya mtu huyo!!!na mlango wa kutokea!!

*1Wakorintho 10:13 imeandikwa ” Jaribu halikuwapata ninyi,isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu;ila Mungu ni Mwaminifu;ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo;lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea,ili mweze kustahimili.*

Kwa hiyo,sio kila anayepitia magonjwa,ametenda dhambi!!!!!!

*2) KUTOTAMBUA MAMLAKA ALIYONAYO JUU YA MAGONJWA*

*1 Petro 2:24 imeandikwa ” Yeye Mwenyewe(Yesu),alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti,tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi,tuwe hao kwa mambo ya haki; NA KWA KUPIGWA KWAKE MLIPONYWA.*

➡Yesu aliyachukua magonjwa yote ya mwanadamu katika mwili wake!

Kila ugonjwa unaoufahamu,Yesu aliuchukua!!

*Isaya 53:4 imeandikwa ” Hakika ameyachukua masikitiko yetu,AMEJITWIKA huzuni zetu.*

➡Sikiliza, Huzuni unayoipata punde unapokuwa mgonjwa,Biblia inasema kwamba Yesu aliichukua! Ili wewe usiwe mwenye huzuni tena!!

Lakini Shetani amewafanya watu wengi wameshindwa kuutambua ukweli huu!!!!!

Sikiliza,Adui hataacha kukuingizia magonjwa eti kisa unasali kanisa fulani au una cheo fulabi kanisani! NO! Bali ataacha kwa sababu unaujua Ukweli kuhusu jambo fulani!!

➡Ukitaka kufanikiwa katika mambo ya Mungu,usiangalie mazingira yanavyosema,bali liangalie Neno la Mungu linavyosema!!!!!

*HII NDO PASAKA YA LEO,KULA UONDOKE*

Kipofu wa kiroho

KESHO YA KIPOFU WA KIROHO IMEFICHWA GIZANI

mapundagustaph

Imeandikwa na: LUKUTA

Kipofu wa kiroho huwa hajui kesho yake kutokana na vidanganyifu mbali mbali vinavyozunguka machoni pake Kipofu wa kiroho atazamapo vinavyozunguka hufikiri kwamba na kesho yake ipo hivyo

Atazamapo mapaja yake makubwa anafikiri na kesho yake ipo kwenye hayo mapaja atazamapo weupe au macho yake anafikiri na kesho yake ipo kwenye vitu hivyo atazamapo uzuri wake anafikiri kuwa na kesho yake pia itakuwa nzuri atazamapo mali zake au umaarufu wake anafikiri kwamba kesho yake ipo humo, masikini kipofu hajui kabisa kwamba kesho yake imo mikononi mwa Mungu na Mungu ndiye pekee wa kutumainiwa katika maisha na wala si uzuri wala umaarufu wala cheo kwa kuwa hayo yote ni ubatili tu
👇🏼
“Nimeziona kazi zote zifanywazo chini ya jua; na, tazama, mambo yote ni ubatili na kujilisha upepo.”
MHUBIRI 1:14.
🖕🏼
Sulemani anena kwa roho ya kuwa yote ni ubatili laiti watu wangemwelewa kamwe wasingebakia na kiburi cha uzima cha kujiona ni bora na hata kufikia hatua za kumdharau Mungu kudharau Ibada na kuishi maisha ya kupost picha za kuonyesha makalio yao makubwa na mali zao pamoja na picha za kunyonyona ulimi wakifikiri kwamba wako Salama lakini kumbe yote ni ubatili tu kwa sababu kesho ya kipofu wa kiroho ipo ndani ya kiza kinene imefichwa naye hawezi kuiona hadi akubali kuacha dhambi kwanza

*MAUTI AKIJA HAZUILIWI NA UZURI*

Siku ya mauti kumfikia kipofu wa kiroho ni siku moja mbaya sana iliyojaa mafumbo na itakayoacha maswali mengi kwa wengi kwa sababu hatoamini kama ni kweli kwa sababu itamkuta hajajiandaa kiroho yani hajatubu na kuokoka kwa kuwa maisha yake yote Alitaraji kwamba ataendelea kuwepo na moyoni mwake hudhani kwamba atakufa miaka miingi ijayo na akiumwa ataenda kutibiwa nje ya nchi lakini kumbe hajui kuwa mauti akija wala hatazuiliwa na Doctor yoyote yule, tena mauti alivyo mbabe na asivyopenda kupoteza muda anaweza kumchukua mtu akiwa mapokezi kabla hata ya kuingia kwa Doctor kwa hii inatokea ili kudhihirisha kwamba kesho ya kipofu wa kiroho imefichwa gizani

*UJANJA NI KUOKOKA TU*

Ujanja ni kuokoka maana ukiokoka hutokuwa gizani tena maana utajua wazi kwamba ipo siku utatakiwa kwenda kuishi mbinguni hivyo utajiandaa kila wakati kwa kuishi maisha yaliyojaa hofu ya Mungu maisha matakatifu ili siku ile ikufukiapo basi uweza heri kama ilivyoandikwa Heri wafu wafao katika Bwana, Hii ina maana ya kwamba wamebarikiwa wale wanaokufa katika Kristo Yesu hii inaonesha kwa mtu aliyeokoka kwake kufa ni baraka tena Roho anena kwa kinywa cha Paulo kuwa kufa ni faida kuishi ni Kristo lakini kwa upande wa pili hiyo ina maana ya kwamba Ole kwa wafu wafao katika shetani maana yake wamelaaniwa wale wafu wanaokufa ndani ya shetani. hapa inaweka wazi ya kwamba kufa ukiwa na Dhambi yaani mfuasi wa shetani kwake kifo ni laana hivyo ndugu yangu unayesoma ujumbe huu usijidanganye kuwa eti una umbile la kuvutia kingono na kiuasherati ukafikiri kuwa utakuwa Salama no sio kweli Mimi nakuhakikishia kwamba hautokuwa Salama kabisa siku ya mauti kuja kwako Itakuwa siku moja mbaya Sana.

Siku ambapo wale waliokuhonga magari ya kifahari na ukayumbisha ndoa zao kwa sababu ya mapaja yako watakapokuona umelala kwenye sanduku na huwezi kuwapiga busu tena wala kuwakumbatia maana upo kwenye sanduku na imejaa pamba mdomoni na puani watalia sana hasa wakikumbuka vile vitanda vya gharama kubwa mlivyotumia kule hotelini lakini leo ndiyo wewe umelala tena umekuwa mzoga usiotamanika tena kwa sababu hapo ndani ya sanduku mapaja hayana thamani bali yanasubiri kwenda kuliwa na funza wa kaburini kisha baadae kuliwa na wale funza wa kwenye ziwa liwakalo ule moto wa Milele

Achana na tamaa za dunia hii achana na ujinga upuuzi njoo uokoke wewe binti wewe kijana usipokubali kutii injili hii basi siku chache tu zijazo Utayakumbuka meneno haya Ninao Ushahidi Wa Hili

Kwa Mkono Wangu Mimi Lukuta NimekuandikiaNIFUATE KWA MWAMBA YESU

SIMAMA KISHUJAA AMINI UNAWEZA FANYA UTASHINDA.

Published by mapundagustaph

(I love Jesus Christ View all posts by mapundagustaph )

MZALIE MUNGU MATUNDA YAFAAYO

_UJUMBE WA LEO_

*” MZALIE MUNGU MATUNDA YAFAAYO”*

*Zaburi 11: 3*

3 Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
7 Kwa kuwa BWANA ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.

*2Falme 2: 19 – 22*

19 Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza.

20 Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea.

21 Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, BWANA asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza.

22 Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.

KUHUSU UBATIZO  KWA MAJI MENGI AU MACHACHE

*SOMO:*  
*UBATIZO WA KWELI NI UPI KI-BIBLIA*
             *KATI*
               *YA*
*MAJI MENGI AU MACHACHE*❓
⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪

Biblia inasema katika *WAEBRANIA 6:1-3:-“Kwa sababu hiyo , tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikie utimilifu; tusiweke misingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, na wa MAFUNDISHO YA MABATIZO, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. Na hayo tutayafanya Mungu akitujalia*”
Kama waalimu wengine wa uongo watalitumia andiko hilo kupotosha watu na kusema , suala la ubatizo halina umuhimu sana kuhangaika nalo , kikubwa wewe ukishaokoka , basi ! Haijalishi kwamba umepatiza kwa ubatizo upi maji mengi au machache. 
Watu wanaofundisha hivyo hao ni wapotoshaji wakubwa wa kweli ya neno la Mungu. Wanakudanganya hao !!
Ni muhimu kuelewa *UBATIZO NI SUALA LA LAZIMA NA LENYE UMUHIMU MKUBWA KATIKA IMANI YETU YA WOKOVU”*
Bwana Yesu mwenyewe alisema MARKO 16:16:-

*” Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”*.
Maana yake ni kwamba kama ni mtu uliyeishia kumwamini tu Bwana Yesu , lakini hujabatizwa kwa *ubatizo ulio wa kweli wa Ki-biblia* ingawa ulikuwa nayo nafasi hiyo, lakini ukabeza kufanya hivyo.

Nakuambia pamoja na kudai kwako umemwamini tu Yesu, kama usipotafuta kubatizwa kwa ubatizo ulio wa kweli kibiblia, *UTAHUKUMIWA KWENDA MOTONI*. Na utashangaa, imekuaje !!
Kwa kuonyesha ulazima na umuhimu wa kubatizwa kwa ubatizo ulio sahihi . Yesu mwenyewe alimwambia , *MATHAYO 3:13-16:-“Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitajwi kubatizwa nawe, nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, KUBALI HIVI SASA (KUNIBATIZA);KWA KUWA NDIVYO ITUPASAVYO KUITIMIZA HAKI YOTE. Basi akamkubali. Naye Yesu alipokwisha kubatizwa Mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu take*
Ndugu yangu UBATIZO WA MAJI CHACHE NI UBATIZO FAKE , HAUPO KI-BIBLIA.
Ndugu yangu mpendwa ukileta kiburi na ubishi, usipokubali *kuitimiza haki yote kwa kubatizwa kwenye maji mengi kama alivyobatizwa Yesu* . Utahukumiwa kwenda Jehanamu ya moto. Sikuhukumu , ila nakwambia ukweli mtupu kabisa.
WAEBRANIA6:1-3.Kulingana na neno hilo, linatufundisha kwamba nyakati za kanisa la kwanza , moja ya mafundisho ya kwanza ya wokovu yaliyozingatiwa kufundishwa kwa watoto wachanga kiroho, ilikuwa ni suala la ubatizo.
Ikiwa mtu leo ambaye ni mkristo bado ni kama hajui , anachangakiwa kutokuelewa ubatizo upi ni sahihi wa maji mengi au machache ki-biblia!! Mkristo wa namna hiyo hata kama anajiita mwalimu, bado ni mtoto mchanga kiroho anahitaji kufundishwa.
Katika pale tuliposoma inasema *WAEBRANIA 6:3-4:-“……na wa mafundisho ya MABATIZO ….Na hayo tutayafanya Mungu akitujalia*.
Neno hilo MABATIZO , maana yake linatufundisha kuna aina nyingi za ubatizo katika Biblia .
*SWALI:-“JE! NA UBATIZO WA MAJI MACHACHE UMO KWENYE BIBLIA AU ?*
Katika utangulizi wa somo letu , labda itakuwa ni muhimu kufaham kwanza kuna aina ngapi za ubatizo uliotajwa katika Biblia nzima, neno la Mungu.
Hakuna ubatizo wa maji machache katika Biblia, Asikudanganye mtu .
Kuna aina kuu nne tu za ubatizo uliotajwa katika Biblia. Ambao ni:-
(1) UBATIZO WA MAJI

(2) UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU.

(3) UBATIZO WA MOTO
[ MATHAYO 3:11-12; UFUNUO 20:11-15 ]

(4) UBATIZO WA DHIKI NA MATESO.
[ LUKA 12:49-50; 2 WAKORINTO 4:8-17; 1 PETRO 5:10 ]

 

Wakristo tuliokoka tunabatizwa kwa aina zote za ubatizo ambao ni *1, 2, 4*.
Lakini ubatizo wa aina ya tatu *(3)*, unawahusu hasa watu wote wenye dhambi waliokataa kumkiri na kumwamini Yesu kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha, wakaokolewa.

*⛪UBATIZO WA MAJI MENGI NDIO UBATIZO SAHIHI , UTOKAO KWA MUNGU*
Ubatizo wa maji machache huo ni ubatizo wa kipagani , ambao hautokanani na Mungu aliye hai, kwa sababu haupo kwenye maelekezo ya Mungu ki-biblia.
Biblia inasema hivi katika *LUKA 20:2-6:-“Wakamwambia, wakisema, tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii ? Akajibu akawaambia, Nami nitawauliza neno moja; NIAMBIENI, UBATIZO WA YOHANA, JE! ULITOKA MBINGUNI AU KWA WANADAMU? Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, kama tukisema ulitoka mbinguni, atasema, basi, mbona hamkumwamini? Na tukisema ulitoka kwa wanadamu watu wote watatupiga kwa mawe, kwa kuwa wamemkubali Yohana kuwa ni nabii*”
Kuna ubatizo utokao kwa Mungu na kuna ubatizo mwingine unatokana tu na mapokeo ya wanadamu wenyewe na sio Mungu.
Sasa basi, tukitaka kujua *Ubatizo wa maji mengi au machache, ni upi ulio wa kweli utokao kwa Mungu mbinguni ?*
Jibu ni rahisi tu. Tazama ubatizo wa Yonana ambao pia Yesu alibatizwa nao. Ulikuwa ni wa maji Mengi au machache ?
Ni muhimu kufahamu kuwa Yohana mbatizaji alimbatiza Yesu katika maji tele (MATHAYO 3:13-17). Yesu Kristo alibatizwa katika mto Yordani kwasababu huko kulikuwa na maji tele. Yohana mbatizaji alikuwa akibatiza sehemu zenye maji tele ili watu waweze kuzamishwa katika maji kama tutakavyoona maana ya ubatizo na kwa nini kuzamisha katika maji tele. Yohana mbatizaji hakubatiza Yordani tu, alibatiza Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. 

*YOHANA 3:23 “Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, KWA SABABU HUKO KULIKUWA NA MAJI TELE (MENGI), watu wakamwendea wakabatizwa”*. 
Kwa maana hiyo, kumbe tunagundua kwamba *UBATIZO WA MAJI MENGI NDIO UBATIZO WA KWELI UTOKAO MBINGUNI KWA MUNGU. Haleluya!!*
Ubatizo wa maji machache huo ni ubatizo wa kipagani tu ulioanzishwa na kanisa la Roman Catholic. Na mtu wa kwanza kubatizwa kwa kunyuniziwa maji usoni, alikuwa ni mfalme Constantino. Alipongoka na kuwa mkristo. Kwa heshima yake ya juu ya kifalme, kanisa la Roman wakaona kumbatiza mfalme kwa kumzamisha kwenye maji mengi, itaonekana kama ni tendo la kumshushia hadhi yake. Wakabuni ubatizo mpya wa kumnyunyuzia maji .
Hapo ndipo ikawa ni mwanzo rasmi wa ubatizo wa maji kidogo ulipojitokeza na kusambaa mpaka Leo hata kwenye makanisa mengi yalipokea upotofu huo.
*MARKO 7:6-8:-” Akawaambia, Isaya alitabiri vyema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, watu hawa huniheshimu kwa midomo ila mioyo yao iko mbali nami; NAO WANIABUDU BURE, WAKIFUNDISHA MAFUNDISHO YALIYO MAAGIZO WANADAMU. Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadam. Akawaambia, vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu*.
Ndivyo ilivyokuwa, Kanisa la Roman Catholic liliamua kuupotosha msingi ulio wa ubatizo wa kweli kinyume na Biblia isemavyo.
UBATIZO WA KWELI KI-BIBLIA. lazima ufanye kwenye maji tele ya kumtosha mtu kuzamishwa majini.

*⛪MAANA YA NENO KUBATIZWA AU UBATIZO*
Watu wanaotetea ubatizo wa maji machache, hawajui hata nini maana ya neno ubatizo. Na kama wanajua , basi shetani anawatumia watu kama hao kufanya upotoshaji wa makusudi kinyume na Kweli. *2 PETRO 2:1-3:-“Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale, kama vile kwenu kutakavyokuwako WAALIMU WA UONGO, WATAKAOINGIZA KWA WEREVU UZUSHI WAKUPOTEZA, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usio kawia. Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. Na katika kutamani WATAJIPATIA FAIDA KWENU KWA MANENO YALIYOTUNGWA TU; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii*”
Ubatizo wa maji machache umetungwa tu wanadamu na sio elekezo sahihi la Mungu kwenye Biblia. Na watu wanaotetea au kufundisha ubatizo maji machache kwamba hakuna shida, ni sahihi tu.

*HAO NI WAPOTOSHAJI TU WA KWELI YA MAANDIKO. AMBAO WANALAZIMISHA KUINGIZA VYA KWAO, AMBAVYO WALA HATA HAVIKO KIBIBLIA* 
Kwa sababu Neno lenye tu ubatizo linamainisha kuwa ni maji mengi na sio machache.
Lugha za asili za biblia kabla ya tafsiri mbalambali ni kiebrania na kiyunani. Agano la kala iliandikwa kwa lugha ya kiebrania na agano jipya iliandikwa kwa kiyunani. Katika kuifasiri biblia kwa lugha zetu kuna baadhi ya maneno machache ambayo misamiati yake ilipoteza maana halisi iliyopo katika biblia. Kwasababu lugha zingine zunakuwa na mapungufu.
Katika biblia ya lugha ya kiebrania kuna neno *“BAPTIZO”* lenye maana ya UBATIZO kwa Kiswahili na kwa kiingereza BAPTIZM,
Katika biblia ya lugha ya kiyunani kuna neno *“BAPTO” lenye maana ‘kuzamisha au kuchovya”*.
Mifano katika biblia kuhusiana na neno” *BAPTO’ kuzamisha au kuchovya*.
 ( 1 ). Tonge la ugali linavyotowelewa katika ugali kisha linazamishwa lote. Tendo hilo la kuzamishwa ni kubapto *“bapto”*(kubatiza) katika kiyunani (YOHANA 13:26).

 ( 2 ). Kuchovya ncha ya kidole. Neno kuchovya hapo (LUKA 16:24) lina katika lugha ya kiyunani ni *‘BAPTO” bapto likiwa na maana kuchovya au kuzamisha*.

 ( 3 ) Tendo la kuchovya vazi katika damu lina maana ya kubapto *“ BAPTO”* kubatiza katika biblia ya ya lugha ya asili kwa kiyunani.
Kwahiyo biblia inapozungumzia juu ya ubatizo inazungumzia ubatizo wa maji tele na sio machache.
*WATU WOTE WALIOBATIZWA KATIKA BIBLIA, ILIKUWA NI MAJI MENGI TU*
(1) Nabii Yohana aliwabatiza watu wa Ainoni kwa sababu huko nako kulikuwa na maji tele (YOHANA 3:23). 

(2)Pia tunamuona mtumishi wa Mungu Filipo na towashi *wakitelemkia majini* ili abatizwe katika maji tele (MATENDO 8:34-39). Walitelemka majini akambatiza kisha wakapanda kutoka majini (MATENDO 8:36-39).

(3) Wana wa Israeli katika Agano la kale, waliotoka utumwani misri wanatajwa kuwa walibatizwa ili wawe wa musa . Na ubatizo huo ulikuwa ni wa maji mengi.
Biblia inasema katika *1WAKORINTO 10:1-2:-Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufaham ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; WOTE WAKABATIZWA wawe wa Musa KATIKA WINGU NA KATIKA BAHARI*”.
 

(4) MAJI YA UBATIZO NI KABURI. Kimsingi kubatizwa ni kuzikwa na kufufuliwa pamoja na Kristo katika ulimwengu wa roho.
*WARUMI 6:4-5:-“Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Kwa maana kama tulivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika tutaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake*.”

*WAKOLOSAI 2:12:-“MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu*.
Sasa basi mtu anapozikwa, maana yake anafunikizwa na udongo pande zote, anazazimishwa na kufukiwa chini ya udongo. Hakuna mtu anayezikwa kwa kunyunyuziwa udongo. 
Na kwa msingi huo, ubatizo kama tendo la ishara ya kuzikwa pamoja na Kristo, ndiomana ni *LAZIMA UFANYIKE KWA MAJI MENGI, ILI MTU AZAMISHWE kama ishara ya kuzikwa kiroho*. Na sio vinginevyo. 
Lakini Nje na hapo kwa ubatizo maji machache , tutakuwa tumedanganywa na kudanyika kwa kujifariji bure eti tumebatizwa, kumbe hamna kitu !!

*WAGALATIA 6:3:-“Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake*”.
*ACHANA NA UBATIZO WAKO HUO FAKE WA KUNYUNYUZIWA MAJI, sijui uliobatizwa nao tangu utoto*. Lakini Kubali hivi sasa, nenda kabatizwe upya kwenye maji mengi. Huu ndio ubatizo wa kweli kibiblia, utokao kwa Mungu. Amina.

*⛪ WATU WANAOFUNDISHA JUU YA UBATIZO WA KUNYUNYIZIA MAJI KICHWANI AU USONI NAO PIA WANA MAANDIKO. Ambayo watayatumia maandiko haya kwa maana isiyo kweli halisi, kwa kuyapotosha kitafsiri*.
Hoja potofu za wapotoshaji wanaojaribu kuhalalisha ubatizo wa maji machache. Watatumia maandiko yafuatayo yafuatayo:-
*EZEKIELI 36:25:- “Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafuwenu wote, na vinyago vyenu vyote”*.
*HESABU 8:5-7:- “Kisha Bwana akanena na Musa. Na kumwambia, watwae walawi na kuwaondoa kati ya wana wa Israeli, kasha uwatakase. Nawe utawafanyia mambo haya ili kuwatakasa, nyunyiza juu yao maji yatakasayo dhambi, nao wajinyoe kwa wembe mwili wote, kasha wazifue nguo zao na kujitakasa”*.    
Upotofu ni rahisi kuingia kama tutayatafsiri maandiko isivyo kama tupendavyo. (2 PETRO 1:20; 2TIMOTHEO 2;15).
Maana ya maandiko hayo yanayotumiwa kimakosa kuharalisha ubatizo wa kunyunyiza maji kichwani au usoni. *KWA SABABU WAKATI WA TORATI YA MUSA KULIKUWA HAKUNA SUALA LA UBATIZO. Desturi ya Ubatizo umeanzia rasmi wakati wa Agano jipya*.
Kwa maana hiyo hatuwezi kuyahusianisha Maandiko hayo na suala la nzima la ubatizo. kunyunyuziwa maji hapo , yana maana nyingine iliyo mbali na suala suala la ubatizo.

*TUSICHANGANYE TAFSRI YA MANDIKO, Bali tulitafsiri andiko kwa tafsiri yake iliyo halali*.
*HESABU 19:13 “Mtuawaye yote agusaye maiti ya mtualiyekufa, asijitakase, yuatia unajisi maskani ya Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na Israeli; maana, hayo MAJI YA FARAKANO hayakunyunyizwa juu yake, atakuwa najisi, unajisi wake ungali juu yake bado”*. 
Kwahiyo tunaona kuwa wakati wa agano la kale mtu aliyekuwa akiigusa maiti ya mtu aliyekufa, alihesabika kuwa amenajisika kwa kuigusa tu. Alihesabika kuwa ni mwenye dhambi (unajisi) na angeweza kulinajisi hekalu la Bwana (maskani ya Mungu). Mtu aliyenajisika alihesabika kuwa safi baada ya kunyunyiziwa kichwani maji ya utakaso yaitwayo *FARAKANO*. 
WAEBRANIA 9:10 “kwa kuwa ni sharia za jinsi ya mwili tu……..

*ZILIZOAMRIWA HATA WAKATI WA MATENGENEZO MAPYA*”
Hayo maandiko wakati wake ulishapita, maana sisi Leo tunaongozwa na Agano jipya, Agano la rohoni; Agano la kale lilikuwa na mapungufu (WAEBRANIA 8:7-9).
*LEO KATIKA AGANO JIPYA HATUITAJI TENA KUNYUZIWA HAYO MAJI ILI TUTAKASIKE*. Badala yake dhambi au uchafu unaondoka kwa damu ya Yesu kwa njia ya imani ( WAEBRANIA 12:24 ;1PETRO 1:2). Hatunyunyuziwa maji kichwani Leo kama wakati wa Agano la kale, bali *damu ya Yesu Kristo Leo ndiyo inayonyunyizwa juu yetu na kuondoa dhambi*
Tendo la kunyunyuziwa damu ya Yesu ndilo linaitwa kuzaliwa kwa kwa roho au kuzaliwa Mara ya pili ( YOHANA 3:3-10). Mtu asipozaliwa Mara ya pili, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu ( YOHANA 3:5; 1:12). Maji yanayotajwa katika Yohana 3:-3-10, *Ni neno la Mungu*, siyo ubatizo wa maji kama waalimu wengine wanavyopotosha. Neno la Mungu linamsafisha mtu kama vile maji yasafishavyo (YOHANA 15: 3; 1PETRO 1:23).

*ITAENDELEA SEHEMU YA PILI…..

*INAENDELEA SEHEMU YA PILI……..*

Wapotoshaji hawa watalitumia tena hili andiko kujaribu kuhalalisha ubatizo wao wa maji machache.
Watanukuu katika *MATENDO 9:17-18:-” Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia ulioijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu. Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, AKASIMAMA, AKABATIZWA*”.

Watasema Paulo mtume alikuwa ndani ya nyumba hapo, akasimama akabatizwa. Kwahiyo watafikiri hapo kulikuwa na ubatizo wa maji machache. Jambo ambalo siyo sahihi.
MATENDO 9:18, Biblia zetu za kiswahili zinasemama akasimama , akabatizwa lakini hazielewei vzuri kitafsiri.
Tafsiri nzuri ya mstari huo tunaipata katika Biblia ya kingereza ya King James vision, *ACTS 9:18;-“Immediately there fell from his eyes something like scales, and he received his sight at once; And HE AROSE AND WAS BAPTIZED**.
MATENDO 10:20:-” Basi ondoka ushuke ufuatene nao….. *( Arise therefore, go down and go with them….)*
Kwahiyo hapo Paulo mtume alioondoka (mahali hapo ndani ya nyumbani) na kwenda kubatizwa. Na ubatizo alibatizwa nao huko, ulikuwa ni maji mengi.

*🔷JE, ASKARI WA GEREZANI NA WATU WA NYUMBANI MWAKE WALIBATIZWA KWA MAJI MENGI ?*
[ MATENDO 16:30-34] 
 *Jibu ni Ndiyo*.
Bila shaka watumishi hawa waliwapeleka mahali penye maji mengi kwa wakati huo na kuwabatiza kwa kuwazamisha ili washiriki mauti ya Yesu kwa kuzikwa na kufufuka kwake

( WAKOLOSAI 2:12; WARUMI 6:4).

*🔷 JE UBATIZO , WA NYUMBA YOTE UNAOTAJWA KATIKA BIBLIA SI PAMOJA NA WATOTO WADOGO ?*
[ MATENDO 18:8; MATENDO 16:31-33].
*Jibu ni Hapana*.
Ni muhimu kufaham katika tamuduni za wakati wa Biblia, watoto wadogo hawakuruhusiwa kuwepo eneo lenye watu wazima, ndiyo maana wanafunzi wa Yesu waliwafukuza (KUMBUKUMBU 3:5-6). Hata katika hesabu za watu watoto hawakuhusishwa katika hesabu ( 1SANWELI 22:19; EZRA 10:1; YEREMIA 40:7). Watoto hawakubatizwa katika familia zao (1 KORINTO 1:10-11; MATENDO 10:1-2), mtoto Mdogo/mchanga hawezi kumcha Mungu, hivyo Biblia inaposema nyumba nzima wakabatizwa, *ina maana ya watu wazima*.

*⛪ UBATIZO HAUFANYWI KWA WATOTO WADOGO/ WACHANGA*
Kwa kawaida katika makanisa hayo, watoto wadogo wanapobatizwa eti huwa anakuwepo mtu mzima anayempakata na kujibu maswali badala ya mtoto huyo. *Hiyo siyo sahihi kibiblia*
*EZEKILI 18:20:-” Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; MWANA HATAUCHUKUA UOVU WA BABAYE, WALA BABA HATAUCHUKUA UOVU WA MWANAWE; haki ya mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake*”.
Tena Biblia inasema

*Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe ( WAGALATIA 6:5)*.
Kwa. Msingi huo , mtu hawezi kutubu dhambi kwa niaba ya mtu mwingine.
Ni muhimu kufaham kuwa watoto wadogo ufalme wa mbingu ni wao hata bila ya kutubu dhambi (MARKO 10:13-14). Sisi sote tumezaliwa tukiwa na asili ya dhambi. Tumezaliwa kwa mfano wa Adamu na si kwa mfano wa Mungu ( ZABURI 51:5; 58:3). Pasipo sheria hakuna dhambi, dhambi inahesabiwa kwa sheria (WARUMI 4:15; 5:12-13).
Mtoto Mdogo anaweza kutenda dhambi kama vile kusema uongo, kucheza dansi, kuzira, uchoyo n.k. Lakini watoto wadogo hawahesabiwi dhambi, kwa kuwa hawajui vizuri mema na mabaya. Watoto wadogo hawana uwezo wa Kujua kupambanua au kutofautisha mema na mabaya. Wanafanya bila Kujua ni dhambi, ndiomaana Yesu alisema ufalme wa mbinguni ni wao.

*WAEBRANIA 5:13-13-14*. Mwenye uwezo wa kupambanua mema na mabaya ni mtu mzima *ndiyo mwenye sifa ya kubatizwa*; lakini mtoto Mdogo hata kama akifa anakwenda mbinguni moja kwa moja bila kizuizi chochote.

*🔷 Kabla ya kubatizwa sharti mtu huyo atubu dhambi zake zote kwa kumwamini Yesu baada ya kuhubiriwa au kufundishwa*
Ili mtu awe na sifa ya kubatizwa kibiblia lazima atubu dhambi zake kwanza kwa kumwamini kwa moyo wake, Mwana wa Mungu Yesu Kristo.
BIBLIA INASEMA katika
*MATENDO 2:37-38, 41:-Waliposikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akamwambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA kwa jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu*
*Nao waliolipokea lile neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu elfu tatu*”.

*MATENDO 8:12-13;-” Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, WAKABATIZWA, WANAUME NA WANAWAKE. Na yeye simoni mwenyewe ALIAMINI AKABATIZWA, akashikamana na filipo: akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa iliyotendeka*”.

*MARKO 16:15-16:-” Akawaambia, Enendeni ulimwenguni kote, mkahubiri injili kwa kila kiumbe. AAMINIYE NA KUBATIZWA ATAOKOKA; asiyeamini atahukumiwa*”.
Pia katika MATENDO 8:35-38, Towashi aliamini kwanza kabla ya kubatizwa na Filipo. Mtu baada ya kujifunza neno la Mungu na kuliamini kwa moyo wake wote na kusafishwa kwa damu ya Yesu kwa njia ya imani, baada ya kutubu kwake; ndipo aweza kubatizwa.

( MATENDO 16:31-33; MATENDO 18:8).
Sasa basi kwa mtu ambaye ni mtoto sana Mdogo/mchanga hawezi akahubiriwa, akaamini na kutubu, kisha akaokolewa. Kwa maana hiyo mtoto mdogo asiyejua kupambanua mema na mabaya, HANA SIFA YA KUBATIZWA KI-BIBLIA.

*⛪ WATOTO WADOGO WANABARIKIWA TU, HAWABATIZWI*.
Biblia inasema katika MARKO 10:13-16;-” Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao. Amin, nawaambieni, Ye yoyote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa. *AKAWAKUMBATIA, AKAWEKA MIKONO JUU YAO , AKAWABARIKIA*”.
Yesu mwenyewe alilokuwa mtoto mdogo, alibarikiwa tu, hakubatizwa. *Simeoni akawabariki*(LUKA 2:27-34).
Yesu alibatizwa katika maji tele alipokuwa mtu mzima (LUKA 3:21-23; MATHAYO 3:13-17). Ametuachia kielelezo; tufuate nyayo zake ili MUNGU apendezwe nasi. 
Ubatizo wa kweli kibiblia ni wa maji mengi tena kwa watu wazima, na sio watoto wadogo.
Biblia inasema katika
*WAEBRANIA 12:2:-” TUKIMTAZAMA YESU, mwenye kuanzisha na mwenye kuitimiza imani yetu……..*”.

*1 YOHANA 2:6*:-” Yeye asemaje ya kuwa anakaa ndani yake,

*IMEMPASA MWENYEWE KUENENDA VILE VILE KAMA YEYE (YESU) ALIVYOENENDA*”.
(1) Je, Yesu alibatizwa kwenye maji mengj au machache ❓

(2) Yesu alibatizwa akiwamtoto mdogo au mtu mzima ❓
Kama kweli tunataka kwenda mbinguni ni muhimu tumtazme Yesu na kuenenda sisi wenyewe vilevile kama Yesu alivyoenenda. *TUBATIZWE NA SISI KWENYE MAJI MENGIIIII*!! Maana Yesu alituachia kielelezo ili tufuate nyayo zake (1 PETRO 2:21).

 MUNGU AWABARIKI wote kwa ujumbe wa neno hili.

🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺
Mtumishi wa Mungu aliye hai,
*MWL:- ODRICK BRYSON* 
(0759 386 988; 0717 591 466).
Whatsap.

*KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA*
[ 2 WAKORINTO 2:17 ]
🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺

MAOMBI YANAWEZA KUIMARISHA IMANI YAKO.

*SOMO:JINSI MAOMBI YANAVYOWEZA KUIMARISHA IMANI*(A FULL DIET).
*NA JOHN WEREMA*

*1 WATHESALONIKE 3:10 imeandikwa” Usiku na mchana tunapoomba kwa juhudi tupate kuwaona nyuso zenu na kuyatengeneza mapungufu ya Imani yenu?*
Biblia ya Kiingereza inasema hivi ” *Night and Day praying exceedingly that we may see your face and perfect what is LACKING in your Faith?*
~Ukiutafsiri huo msitari wa Kiingereza kwa kiswahili utakuta unasema hivi ” *Usiku na Mchana tunapoomba kwa juhudi ili tuzione nyuso zenu na kuyaimarisha yanayopungua katika Imani.*
✍🏻Biblia ya Kiswahili imetumia neno *Mapungufu* lakini Biblia ya Kiingereza imetumia neno *Lacking*
~Kiuhalisia neno Mapungufu kwa Kiingereza linaitwa *Shortage* likimaanisha kwamba,kitu kipo lakini hakikidhi mahitaji( hakitoshelezi)
~Lakini neno *Lacking* linamaanisha *Ukosefu* yaani kutokuwepo kwa kitu kabisa hata chembe!
✍🏻Kwa hiyo tofauti kati ya *Shortage* na *Lacking* ni kwamba, katika Shortage maana yake vitu vipo lakini havitoshi! Ambapo *Lacking*maana yake vitu havipo kabisa!!
~Unapoona kwenye Biblia neno *Upungufu* limetajwa,ukienda kwenye Biblia ya Kiingereza utakuta wamelitaja kama *Lacking*na sio *Shortage*
~Hasahasa hili neno huwa linatajwa kwenye kipengele cha Imani
Kwa mfano:-
*Mahayo 17:19-20 imeandikwa ” Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa Faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu Akawaambia, kwa sababu ya _UPUNGUFU WA IMANI YENU_.*
~Hilo Neno 👆

AINA ZA MATENDO

*SOMO:AINA MBILI ZA MATENDO*(A FULL DIET)
*NA JOHN WEREMA*(rafiki wa Mungu)
*Yakobo 2:14 imeandikwa ” Ndugu zangu,yafaa nini,mtu akisema ya kwamba anayo imani,lakini hana matendo?*
~Angalia tena na huu msitari
*Wagalatia 2:16 imeandikwa “Hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa MATENDO YA SHERIA,bali kwa Imani ya Kristo Yesu*
✍🏻kwa mistari hiyo hapo juu 👆

LEARN ABOUT “OLDCOVENAN”

*OLD COVENANT VS. NEW COVENANT*
–Old covenant replaced by New covenant Heb8:7

In Greek (the language of the New Testament) there are 2 words for ”NEW”: ”neos” it means ‘new’ as ‘another to add to previous one’, and ‘kainos’ which means ‘new/fresh that replaces the old’. In Luke22:20 ”new covenant” uses the word *’KAINOS’* , meaning that the new covenant in the blood of Jesus fulfills and replaces the old covenant made through the blood of animals; the old covenant included:

-the 10 commandments as the heart of the Old Covenant: Ex34:28; Deut4:13

– 680 ceremonial commandments – Leviticus

-sacrifices
*Word ”COVENANT” in Greek is ”DIATHEKE”* which means also ‘testament, will”. In the Old Covenant man had his part of responsibility which made the covenant weak as man could not fulfill perfectly his part and the way of forgiveness and thus salvation was faith in the blood of animals which pointed to the blood of Jesus; in the new covenant man through faith is the beneficiary of the testament or will of Jesus inheriting freely heaven and all God’s promises.
Many adventists, masowe and others believe the 10 commandments were not part of the old covenant and therefore we are to keep the 10 commandments, including Sabbath, in order to please God; however, the 10 commandments were given to prove to each of us that we are sinners and we need a Savior Gal3:24; you will not please God by trying to keep the 10 commandments since you do break them anyway: keeping them 95% is not better than keeping them 5%, you still deserve hell, James2:10. You please God by believing in Jesus Jn6:28,29 (thus being born again) and then walking in the Spirit Gal5:16 (spiritual growth), which results in not walking in the lusts of the flesh (flesh which breaks the 10 commandments).

See some verses that prove that Christians are not under the law: 2Cor3:6-13; Eph2:15; Rom10:4; 2Cor3:7; Heb10:5-9; Col2:14-16; Rom6:14; 7:4,6; Gal3:19,24-25; Acts15:1-24; Gal5:4; Rom3:21-22; 1Tim1:7-10. Ask me for our lessons “We are not under the law of Moses”.
*Here are some contrasts between the 2 covenants:*
1. OLD COVENANT: *Moses and levites as Ministers* 2Cor3:13-15; Jn1:17; Heb3:5 – NEW COVENANT: *Jesus and His Disciples as Ministers* Jn1:17; 2Cor3:6; Jn16:12-15, Heb1:1
2. A Covenant of the *Letter* 2Cor3:6 – A Covenant of the *Spirit* 2Cor3:6-8
3.A Cov. which *Kills* 2Cor3:6 – A Cov. which *Gives Life* 2Cor3:6 – literally “makes alive”
4. A Ministry of *Death* 2Cor3:7 – A Ministry of *Life* 2Cor3:6
5.A Ministry of *Condemnation* 2Cor3:9 – A Ministry of *Reconciliation and Righteousness* 2Cor3:9
6. *Written with Ink* – the 680 ceremonial commandments 2Cor3:3 – *Written with the Spirit of the Living God* 2Cor3:3
7. *Written on Stone* (the 10 commandments 2Cor3:3-7) – *Written on the Heart of Man* (2Cor3:3;Jer31:33; Ez11:19,20;36:26)
8. *Came with fading Glory* 2Cor3:7; Ex34:29-35 – came with the Greatest Glory 2Cor3:8-11
9. *Glory was Passing/Fading* 2Cor3:7 – *Glory Continues to Shine* 2Cor3:18
10. *A Veiled* or Covered Glory 2Cor3:12-16 – An *Unveiled* Ever-Increasing Glory 2Cor3:18
11.Destined *to be Done Away* 2Cor3:11; Heb7:12,8:13, 10:9 – Destined *to Last Forever* 2Cor3:11; Heb13:20
12. *Blood of animals* Heb9:19 – *blood of Christ* Heb9:14
13. *Shadow, image, symbol* Col2:17, Heb8:5,10:1– *Substance or real object* Col2:17
14. *Law of Moses* Acts13:39 – *law of Messiah* Rom8:2, Gal6:2
15.Law of works Rom.3:27,11:6 – *law of faith* Rom3:27
16. *Many Sacrifices* Heb9:7 – *one sacrifice* Heb9:12
17.Sprinkled with *blood of animals* Heb.9 – washed in the *blood of Jesus* Rev1:5, 1Jn1:7
18. *Provision for failure:* sacrifice of animals – Provision for failure: Christ’s sacrifice
19. *Earthly* tabernacle – *heavenly* tabernacle
20. *Outer* form, *flesh* – *inner reality, spirit*
21. *Righteousness of law* Rom10:5, Gal2:21– *righteousness of Christ* Phil3:9
22. *Imperfect* Heb8:7 – *perfect* Heb8:13
23. *Glorious* – *more glorious*
24. *Yoke of bondage* Gal5:1, Acts15:10 – *law of liberty* Gal2:4, Jam1:25
25. *Law of sin* Heb10:3 – *law of life* Rom8:2
26. *Remembers sins* Heb10:3 – *forgets sins* Heb8:12, 10:17
27. *Ineffective to save* Heb9:9,10:4 – *eternal redemption* Heb7:25
28. *Priests have sin* Heb5:1-4 – *Sinless priest* Heb7:26
29. *Aaronic priesthood* Heb.7:11 – *Melchizedek priesthood* (first mentioned priest in the Bible) Heb5:5-10
30.Priests *on the earth* – priest *in heaven* Heb8:4
31.Priests *made by law* Heb7:12,28 – Priest *through God’s oath*
32. *Unavailing* ministers Heb7:18 – *Able* ministers 2Cor3:6
33. *Perfected nothing* Heb7:19 – *Perfected believers* Heb7:19
34. *A good* covenant Rom7:12 – *A better* covenant Heb7:22, 8:6
35. *Earthly* things Heb9:1-5,24 – *Heavenly* things Heb9:24
36.Tent *built by man* – tent *built by God* Heb8:2
37.An *old way* Heb8:13 – *New and living way* Heb10:19,20
38.Brings *bondage* Gal4:24,25 – Brings *liberty* 2Cor3:17
39. *Cannot* justify Gal2:16 – *Does* justify Acts13:38,39
40.Brings a *curse* Gal3:10 – *Redeems from the curse* Gal3:13
41. *Life by works* Gal3:10 – *Life by trust or faith* Gal3:11
42. *I obey, therefore I am accepted* – *I am accepted, therefore I obey*
43.Life as a *merit* through works Rom10:5 – Life as a *gift* through faith Rom6:23
44. *Exposes sin* Gal3:19 – *Covers sin* Rom4:1-8 and removes sin 1Jn1:7-9
45. *Under law* Rom6:14-15 – *Under grace* Gal3:22-25
46. *Done away* 2Cor3:7-14 – *Eternal* 2Cor3:11
47. *Abolished* 2Cor3:13 – *Continues* glorious 2Cor3:11
48. *Faulty* Heb.8:7 – *Perfect* Jam1:25
49. *Needs* reform Heb9:10-14 – *Perfect* 2Cor3:6,18
50. *If you do* (focused on self) Lev18:5 – *it is done* (focused on God) Jn19:30
51. *Slave* Deut34:5, Heb.3:5– *Son* Jn1:12, Gal4:7
52. *Unregenerated* – *new creation* 2Cor5:17
53. *Under a curse* Gal3:10, Jam2:10 – *Under blessing* Eph1:3
54. *Under works* Gal2:16 – *Under rest* in the work of Christ Mat11:28, Jn17:4, Heb4:10, Tit3:5
55. *You must bring* Lev2:4 – *Jesus brought himself* Heb7:27
56. *If you follow* you will be righteous Lev26:3 – *Through faith* Jesus is your righteousness 1Cor1:30
57. *If you make* Deut23:21 – *You are made* Eph2:10
58. *If you obey* Deut28:2 – *Jesus obeyed* in your place Rom5:19
59. *Harsh punishment* Heb10:28 – *Forgiveness and/or loving parental chastisement* Heb8:10;12:6-11
60.God *requires* a sacrifice Lev.1:10 – God *provides* the sacrifice Jn1:29, 3:16; Gen22:8,13
61. *Animal* sacrifices – *Christ’s* sacrifice Heb10:10
62. *Ten commandments plus 680 ritual rules* – *One commandment: to believe* in the Son Jn6:29,3:16,6:47
63. *Under the law* – *Under grace* Rom6:14
64.*Fear* Heb2:15 – *no fear* 1Jn4:18
65. *Fearsome mountain* Sinai Heb12:18 – Zion where Jesus died, also *heavenly Jerusalem* Heb12:22-24
66. *A good country* Canaan Ex.3:8 – *a better country*, heaven Heb11:16, Phil3:20
67.Promises *impossible to reach* Heb8:7 – *Better promises* Heb8:6, 2Cor1:20, 2Pet1:3,4
68.Written with *ink* – written *with the Holy Spirit*
69.Letter which *kills* – Spirit which *gives life*

70. *Bondwoman* – *free woman* Gal4:22
71.Born *according to the flesh* Gal4:23 – Born *through promise*
72. *Persecutes* the one born according to the Spirit Gal4:29 – *Loves* the lost
73. *Is not heir* – *Is heir* together with Jesus Gal4:7
74. *Can’t come near* God Heb12:20 – *Draws near* with confidence
75. *Works* – *faith* Rom11:6
76. *Circumcision of the flesh* as sign of old covenant Lev.12:1-13 – *circumcision of the heart* Rom2:25
77.Sabbath keeping offered *physical rest* only – *spiritual rest* in Christ through faith not by keeping sabbath Mat11:28, Gal4:10, Col2:16,17, Heb4:3
78.Holy Spirit came *on the mountain* Ex24:16 – Holy Spirit *is in the believer* 1Cor3:16,6:19
79.God *spoke on the earth* – God *speaks from heaven* Heb12:25
80. *Earthly altar* Lev6:26 – *heavenly altar* (the cross) Jn6:54
81. *Animal sacrifice* – *sacrifice of praise* Heb13:15,16
82. *Behavior* (do not kill, do not steal, do not commit adultery…) – *thinking* (do not hate, do not lust) Col3:1-3
83. *Old heart* Jer19:9, Mat15:19 – *new heart* Ez36:26
84. *Works of the flesh* Gal5:19 – *Fruit of the Spirit* Gal5:22
85. *Friend of the Bridegroom* Jn3:29 – *Bride* of the Bridegroom Eph5:25-32, 2Cor11:2, Rev19:7-9
…please consider sharing this message with friends;
…send ”add me” to +263734022204 to be added to our daily broadcast list (also save number as ”pastor Daniel”)
by Pastor Daniel Timofte; http://www.ggzim.org

KUMTII MUNGU

* *🙏KUMTII MUNGU NA KUMHESHIMU🙏* Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. 1 Wakorinto:10.10

Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. 

1 Wakorinto:10.11

Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. 

1 Wakorinto:10.12

Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke. 

1 Wakorinto:10.13

Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. 

            *✍🏽YESU asifiwe sana mpendwa: katika maisha haya ya wokovu,tunahitaji neema ya MUNGU,ili tuweze kushinda vikwazo na majaribu iliyo mbele yetu. Sana wa israeli Waliangamia kwa kutomheshimuu MUNGU. Hata walipotundikiwa nyoka ili iwe msaada kwao,walishindwa kumtazama. SHIDA ILIYOPO LEO: watu wamemsahau MUNGU. 👉wanalalamika. 👉wananug’unika. 👉na kumtukana MUNGU kwa matendo yao. ✍🏽Usitazame tatizo uliyonayo mtazame YESU atakusaidia. Anayejifahamu kuwa amesimama na awe macho asije akashidwa kuendelea na YESU. Majaribu yapo iliyokawaida ya wanadamu,lakini simama na YESU. 🙏UBARIKIWE🙏*

HAKI NA JINSI INAVYOPATIKANA (DIET 1)

*SOMO:HAKI NA JINSI INAVYOPATIKANA* ( DIET 01)
*_NA, JOHN WEREMA_*

Kabla sijatoa maana ya Neno haki hebu tuangalie huu mfano!
*Mfano 01*

Wewe ni mwanafunzi unayesoma ktk shule fulani na ndani ya hiyo shule kuna Mwalimu anafundisha tuition,ikatokea umehitaji kusoma tuition, Ukamlipa Mwalimu huyo hela ya Topic 20, halafu Mwalimu akakufundisha topic 5 za mwanzo then zilizobaki akawa ameacha kukufundisha! swali, Je unaweza ukawa na ujasiri wa kumfuata Mwalimu huyo na kumtaka akumalizie topic zilizobaki?
*Mfano 02*

wewe ni Mwanafunzi,halafu kuna Mwalimu kakuahidi kuwa atakufundisha Topic 4 za Physics bure bila kumlipa pesa yoyote! Alipokufundisha,punde alipofika topic ya 2 mara akaamua aache!!! Je wewe kama mwanafunzi utaenda kumdai Mwalimu zile topic zilizobaki na ukizingatia alikuwa anakufundisha bure?
*MAJIBU*

Katika mfano wa 1,najua ni lazima udai kufundishwa topic zilizobaki maana ulilipia!!!
Lakini ktk mfano wa 2 huwezi kudai maana hukulipia chochote!!!!
✍🏻Haki maana yake kuwa na uhalali wa kutenda au kutendewa jambo fulani kwa sababu unastahili!!
✍🏻Ili uitwe kwamba unastahili ni Lazima kuna kitu unakuwa umekifanya kitakachoweza kukupa ujasiri wa kufanyiwa jambo Fulani!!
✍🏻Kadharika Yesu alipokufa Msalabani alilipa deni lote tulilokuwa tunadaiwa na dhambi ili wale wote watakaomwamini Yesu wahesabiwe haki mbali na dhambi!
*Warumi 6:10 imeandikwa” Maana kwa kule kufa kwake,aliifia dhambi mara moja tu,lakini kwa kule kuishi kwake,amwishia Mungu*
✍🏻kwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti,hivyo dhambi imeshalipwa mshahara wake kupitia kujiunganisha na Yesu!!
✍🏻Ili tuhesabiwe kwamba tuna haki ya kutotawaliwa na dhambi ni lazima tuliamini jina la Yesu!
*Yohana 3:16 imeandikwa ” Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ILI KILA MTU AMWAMINIYE ASIPOTEE*
➡Sikiliza,unapookoka tu,wewe unaitwa *MWENYE HAKI* kivipi?

Hiyo haki uliipata kupitia *KULIAMINI JINA LA YESU* na kama tunavyojua,hakuna mtu awezaye kuokoka pasipo kuamini!!!!
✍🏻Yesu alikufa msalabani then akatuuzia haki kwa njia ya Imani! Kwa maana hiyo Kila aliyenunua haki kwa njia ya imani(aliyeokoka),inabidi Dhambi,laana,mikosi,magonjwa,kukataliwa,utasa,n.k visiwe na uhalali wa kumtawala!
✍🏻Dhambi,Magonjwa,laana,mikosi,utasa,na mabaya yote yana uhalali ya kumtawala yule tu ambaye hajaokoka(maana bado mtu huyo hajavilipa vitu hivyo madai yao) 
✍🏻ila aliyeokoka vitu hivyo havina nguvu juu yake maana alishavilipa madai yao kwa njia ya Imani!
*Wagalatia 3:13 imeandikwa ” Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu*
✍🏻Hivyo wewe uliyeokoka,tambua kabisa umehesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo!!!
Haki tulizohesabiwa ni haki ya:-

Kutokuugua,kutolaaniwa,kutotawaliwa na dhambi,kutoabishwa,kutokuwa tasa n.k!!!!

*Kumbuka*Mtu aliyeokoka,ana haki ya kutotawaliwa na Dhambi!! Lakini mtu ambaye hakaokoka hana haki ya kutotawaliwa na dhambi( dhambi lazima imwendeshe).

✍🏻hivyo kama hujaokoka,unapaswa kumwamini Yesu ili ufanywe MWENYE Haki kwa njia ya Imani!!!!!
*Kama hujaokoka na unataka kuokoka,wasiliana nami katika 0763 441172*

Ubarikiwe.

TOBA YA KWELI …

Swali: “Toba ni nini na ni muhimu kwa ajili ya wokovu?”
Jibu: Wengi huelewa neno toba kuwa na maana ya “kugeuka kutoka dhambi” Hii si tafsiri ya Biblia ya toba. Katika Biblia, neno toba lina maana ya “kubadili mawazo ya mtu.” Biblia pia inatuambia kwamba toba ya kweli itasababisha mabadiliko ya vitendo (Luka 3:8-14; Matendo 3:19). Matendo 26:20 inasema, “bali kwanza niliwahubiri wale wa Dameski na Yerusalemu, na katika nchi yote ya Uyahudi, na watu wa Mataifa kwamba watubu na kumwelekea Mungu, wakiyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao.” Ufafanuzi kamili wa Biblia wa toba ni badiliko la nia akilini ambayo matokeo yake yamo katika matendo yaliyobadilika.
Basi, kuna uhusiano gani kati ya toba na wokovu? Kitabu cha Matendo kinaonekana kuzingatia toba hasa inayo husu wokovu (Matendo 2:38; 3:19; 11:18; 17:30; 20:21; 26:20). Kutubu, kuhusiana na wokovu, ni kubadili akili yako katika suala la Yesu Kristo. Katika mahubiri ya Petro siku ya Pentekoste (Matendo 2), anamalizia na wito kwa watu watubu (Matendo 2:38). Tubu kutokana na nini? Petro anawaita watu walio mkataa Yesu (Matendo 2:36 ) wabadili mawazo yao kumhusu, kutambua kwamba hakika Yeye ni “Bwana na Kristo” (Matendo 2:36 ). Petro anawaita watu wabadili mawazo yao kutoka kumkataa Kristo kama Masihi na kuwa na imani kwake kama Masihi na mwokozi wetu.
Toba na imani inaweza kueleweka kama vile “pande mbili za sarafu moja.” Haiwezekani kuiweka imani yako katika Yesu Kristo kama mwokozi bila kwanza kubadilisha mawazo yako kumhusu yeye na chenye amefanya. Hata kama ni toba ya katao ya makusudi au toba ya kutojua au kutokua na haja, ni badiliko la akili. Toba ya kibiblia, uhusiana na wokovu, ni kubadilisha mawazo yako kutoka kwa kumkataa Kristo hadi kuwa na imani katika Kristo.
Ni muhimu sana tuelewe kuwa toba si kazi sisi huifanya ili tupate wokovu. Hakuna mtu anayeweza kutubu na kuja kwa Mungu, isipokuwa Mungu amvute huyo mtu kwake (Yohana 6:44). Matendo 5:31 na 11:18 zinaonyesha kwamba toba ni kitu ambacho Mungu anatoa – inawezekana tu kwa sababu ya neema yake. Hakuna mtu anaweza kutubu, isipokuwa Mungu ampe toba. Wokovu wote, ikiwa ni pamoja na toba na imani, ni matokeo ya Mungu kutuvuta kwake, kuyafungua macho yetu, na kubadilisha mioyo yetu. Uvumilivu wa Mungu hutuongoza sisi kutubu (2 Petro 3:9), kama ilivyo wema wake (Warumi 2:4).

1. TOBA YA KWELI HUAMBATANA NA KUBADILIKA NIA..
Warumi 12:2 ” Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya MUNGU yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. ” 

-Baada ya kutubu dhambi lazima ubadilishe nia yako kutoka nia ya dhambi na kuingia katika nia ya utakatifu. kuna mtu kila siku hufanya uzinzi na kila siku hutubu, hiyo sio toba ya kweli maana nia yake haijabadilika. Nia ikibadilika hutaruhusu tena dhambi ambazo zilikutesa kabla hujatubu. kama nia yako imekuwa nia safi hakika huwezi hata kukaa katika bar ambayo kila siku ulikuwa unashinda pale kabla hujatubu kwa BWANA YESU. Kama nia yako isipobadilika hakika kila siku utakuwa unajikwaa katika lilelile unalolitubia na hapo unakuwa hujatubu toba ambayo inampendeza MUNGU. 
Mathayo 15:19 ”Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano; ”

-Ukibadilika nia kutoka nia kuwaza uzinzi na uasherati hakika utafanikiwa kuingia katika toba ya kweli. kama mabaya hayo bado yako moyoni mwako hakika utajikuta tu unayatenda tena maana bado wewe ni mtumwa wa dhambi hizo.

-Ukitubia dhambi fulani hakikisha unabadilika nia ya kufuata dhambi hiyo tena.
Waebrania 8:10b ” Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa MUNGU kwao, Nao watakuwa watu wangu. ” 
-Katika nia yako MUNGU huweka sheria yake yaani huweka kila jambo ambalo unatakiwa uliendee au uliishi baada ya hapo. Sheria hiyo MUNGU huitoa kupitia watumishi wake na neno lake Biblia takatifu . baada ya kutubu unatakiwa usitende dhambi tena hiyo ndio sheria ya MUNGU kwako.

       2. TOBA YA KWELI HUAMBATANA NA KUBADILIKA MTAZAMO.
 Yohana 15:4 ” Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.”.

-BWANA YESU hapo anaposema kwamba tukae ndani yake maana yake tusiondoke ndani yake kimtazamo na kimatendo.

-Huwezi kusema umetubu halafu mtazamo wako ukabaki kwamba hakuna haja ya kwenda kanisani wala kujifunza Neno la MUNGU. Ndugu ukifanya hivyo hutafika popote utajikwaa tu na kuirudia dhambi ambayo ilikufanya utubu. toba ya kweli ni pamoja na kubadilika mtazamo kutoka mitazamo mibaya na kuingia katika mtazamo mzuri ambao ni kukaa ndani ya YESU.
Kukaa ndani ya YESU ni;
-Kukaa katika Fundisho lake.

-Kukaa katika Wokovu wake.

-Kukaa katika Neno la MUNGU na maombi.

-Kukaa katika mapenzi yake.

-Kukaa katika utakatifu.

-Kukaa katika upenndo wa wake.

-Kukaa katika Imani pasipo kuondoka wala kuhama.
1 Kor 15:33-34 ” Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.” 
-Kama bado mtazamo wako uko katika kujumuika na marafiki zako watenda dhambi katika eneo lile lile lililokuwa linasababisha kutenda dhambi basi utajikuta tu unaanguka tena na tena katika dhambi.

-Kama mtazamo wako ni kwamba unatubu kisha unajitenga na kanisa hakika hutafika popote bali utaanguka tu dhambini.

Toba halisi ni pamoja na kubadilika mtazamo. kuna watu mtazamo wao ni kwamba kwenda disko kujirusha na kucheza ni jambo jema wakati mtazamo huo ni wa shetani maana ukiwa katika maeneo hayo utajikuta una ”onja ila usilewe” kumbe ni usanii tu wa shetani. disko utajikuta unatamani watu wasiokuhusu maana upo katika uwepo wa shetani. Mtazamo kama huo lazima ubadilike ndipo toba yako itakaa maana adui hatapeleka mashitaki yeyote kuhusu wewe.
3. TOBA YA KWELI HUAMBATANA NA KUFANYA MABADILIKO KATIKA JINSI YA KUISHI.
2 Thesalonike 1:9-10 ” Kwa kuwa wao wenyewe wanatangaza habari zetu, jinsi kulivyokuwa kuingia kwetu kwenu; na jinsi mlivyomgeukia MUNGU mkaziacha sanamu, ili kumtumikia MUNGU aliye hai, wa kweli; na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni YESU, mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja. ”.
-Huu ni mfano wa yule aliyebadilika baada ya toba na kuacha na maisha ya kuabudu sana au kusujudia. Kama alikuwa na sanamu nyumbani mwake ambayo kila siku alikuwa anaibussu na kuisujudia baada ya toba ya kweli anachoma moto sanamu hizo, hayo ndio matokeo halisi ya toba ya kweli.

-Kama ulikuwa mganga wa kienyenyi baada ya toba unabadilika na kuchoma moto zana zote za uganga na kuanza kuishi maisha mapya matakatifu mbele za MUNGU BABA, Hiyo ndio toba ya kweli.

-Kama ulikuwa unaroga watu au kuwatapeli, baada ya kumpokea YESU na kutubu unaamua kuharibu zana zote za uchawi ulizokuwa nazo, hayo ndio matokeo ya toba ya kweli.

-Haiwezekani mfano kijana mzinzi anaamua kumpokea YESU na kutubu kisha kuacha uzinzi lakini nyumbani kwake ana pakti 3 za kondomu na kila siku huvaa moja kwa kijifurahisha na pia ana kitabu cha picha za x na katika laptop yake amejaza filamu za ngono. mtu wa hivyo kama anajishughulisha na vitu hivyo vitamnajisi tu na kujikuta akirudi tena dhambi.
Mathayo 3:8 ” Basi zaeni matunda yapasayo toba;”
-Ndugu, ni matunda gani au ni mambo gani yanazaliwa baada ya wewe kutubu? je unazaliwa utakatifu wa kudumu au utakatifu wa muda tu?

Ndugu nakushauri zaa matunda/matendo mazuri baada ya kutubu.

 

Ukweli hakuna Andiko lolote lenye pumzi ya Mungu mahali popote linasomeka kuwakumbuka marehemu, iwe kwa dakika moja au kwa dakika mbili. Lakini lipo Andiko linasomeka, “wafu hawana Ijara tena katika nchi ya walio hai”. Kwa hiyo kwa mujibu wa andiko hilo, hata misa za wafu HAZIRUHUSIWI, ikimaanisha arobaini za marehemu wote hazina nafasi ndani ya Neno la Mungu.

WAFU/MFU NI NANI?

Utangulizi:-Neno wafu ndani ya Biblia limetumika likiwa na Maana zaidi ya moja, Linaweza kutumika kama

i. Ni hali ya Roho kutengana na mwili yaani Kifo cha mwili.(Luka 8:55, Muhubiri 9:5)

ii. Ni hali ya Mtu kutengana na Mungu au kuvunja uhusiano mwema na Mungu (Kutenda dhambi) yaani Kifo cha Kiroho (Ayubu 21:25)

Kifo cha kiroho. Kuna aina tatu ya wafu katika eneo hili ambayo mtu anaweza kufa kiroho lakini bado anaendelea kuwa hai kimwili. Huyu anaweza akatubu na kufufuka katika wafu akawa hai tena .Pia mtu anaweza kufa kiroho na kimwili maana yake Roho imekufa na mwili umekufa hana nafasi ya kutubu tena. (Ufunuo 20:5). Kifo hiki ni kibaya zaidi na kinatisha. Ambacho Bwana Yesu alisema msiwaogope wawezao kuuwa mwili bali Mungu mwenye uwezo wa kuuwa mwili na Roho, (Soma Matayo 10:28). Kifo cha tatu ni Mtu kufa kimwili lakini bado anaendelea kuishi Kiroho. Hapa Yesu alisema mtu akiniamini mimi na kutimiza neno langu ataishi hata kama akifa.

MAOMBI KWA AJILI YA WAFU

Viongozi wengi hufundisha kwamba hakuna kuokoka duniani na hao hao mtu akifa wanamwombea kwamba alazwe pema peponi kana kwamba kuna wokovu baada ya kufa. Biblia inasema baada ya kifo ni hukumu.(Waebrania 9:27).

Kanisa au Mchungaji au Padri, au Mtume haliwezi kuomba mfu kupumzika kwa amani pema peponi, Ndugu zangu wakati wa wokovu ni sasa hivyo baada ya kufa ni hukumu (Waebrania 9:27). Watakie kupumzika kwa amani wafu ila tambua kwamba huwezi kuwabadilishia makao yao ya milele, kama ni mbinguni ni mbinguni tu na kama ni motoni ni motoni tu.

Kuombea wafu huwafanya wenye dhambi kuendelea kutenda dhambi wakiamini kwamba baada ya kufa kanisa litaomba ili wao waingie mbinguni. Ndugu nakuambia tena WOKOVU NI SASA. Katika Luka 16:26…Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.” Biblia inatuonyesha watu waliokufa wengine wako pema peponi na wengine wako kuzimu,’’ ’’ MUNGU humpokea mwenye dhambi ambaye hutubu kwa woyo na kujitakasa kwa msingi wa imani peke yake katika damu ya YESU KRISTO. Hivyo humpa uzima wa milele. 2 WaKorintho 6:2’’(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)‘’ Wakati wa wokovu ni sasa Wakati wa kuokolewa/kuokoka ni sasa Wakati huu ndio unatakiwa kuokolewa sio baada ya kufa.

Ndugu zanguni, ningependa kuwakumbusha kuwa, wakati wa Wokovu ni sasa na sio utakapo kufa. Mafundisho ya kuombea wafu hayapo kwenye Biblia na hatuoni Yesu akiombea wafu bali akifufua wafu. (Yohana 11:43-44; Luka 7:11 -15; Marko 5:35).

Mungu awabariki sana

KUHUSU TOBA YA KWELI

Swali: “Toba ni nini na ni muhimu kwa ajili ya wokovu?”
Jibu: Wengi huelewa neno toba kuwa na maana ya “kugeuka kutoka dhambi” Hii si tafsiri ya Biblia ya toba. Katika Biblia, neno toba lina maana ya “kubadili mawazo ya mtu.” Biblia pia inatuambia kwamba toba ya kweli itasababisha mabadiliko ya vitendo (Luka 3:8-14; Matendo 3:19). Matendo 26:20 inasema, “bali kwanza niliwahubiri wale wa Dameski na Yerusalemu, na katika nchi yote ya Uyahudi, na watu wa Mataifa kwamba watubu na kumwelekea Mungu, wakiyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao.” Ufafanuzi kamili wa Biblia wa toba ni badiliko la nia akilini ambayo matokeo yake yamo katika matendo yaliyobadilika.
Basi, kuna uhusiano gani kati ya toba na wokovu? Kitabu cha Matendo kinaonekana kuzingatia toba hasa inayo husu wokovu (Matendo 2:38; 3:19; 11:18; 17:30; 20:21; 26:20). Kutubu, kuhusiana na wokovu, ni kubadili akili yako katika suala la Yesu Kristo. Katika mahubiri ya Petro siku ya Pentekoste (Matendo 2), anamalizia na wito kwa watu watubu (Matendo 2:38). Tubu kutokana na nini? Petro anawaita watu walio mkataa Yesu (Matendo 2:36 ) wabadili mawazo yao kumhusu, kutambua kwamba hakika Yeye ni “Bwana na Kristo” (Matendo 2:36 ). Petro anawaita watu wabadili mawazo yao kutoka kumkataa Kristo kama Masihi na kuwa na imani kwake kama Masihi na mwokozi wetu.
Toba na imani inaweza kueleweka kama vile “pande mbili za sarafu moja.” Haiwezekani kuiweka imani yako katika Yesu Kristo kama mwokozi bila kwanza kubadilisha mawazo yako kumhusu yeye na chenye amefanya. Hata kama ni toba ya katao ya makusudi au toba ya kutojua au kutokua na haja, ni badiliko la akili. Toba ya kibiblia, uhusiana na wokovu, ni kubadilisha mawazo yako kutoka kwa kumkataa Kristo hadi kuwa na imani katika Kristo.
Ni muhimu sana tuelewe kuwa toba si kazi sisi huifanya ili tupate wokovu. Hakuna mtu anayeweza kutubu na kuja kwa Mungu, isipokuwa Mungu amvute huyo mtu kwake (Yohana 6:44). Matendo 5:31 na 11:18 zinaonyesha kwamba toba ni kitu ambacho Mungu anatoa – inawezekana tu kwa sababu ya neema yake. Hakuna mtu anaweza kutubu, isipokuwa Mungu ampe toba. Wokovu wote, ikiwa ni pamoja na toba na imani, ni matokeo ya Mungu kutuvuta kwake, kuyafungua macho yetu, na kubadilisha mioyo yetu. Uvumilivu wa Mungu hutuongoza sisi kutubu (2 Petro 3:9), kama ilivyo wema wake (Warumi 2:4).

MAHUSIANO KATI YA YESU,NENO NA IMANI.

SOMO: *MAHUSIANO KATI YA YESU, NENO NA IMANI*(DAY 19)
NA *JOHN WEREMA*

*Waefeso 3:17a imeandikwa ” Kristo akae mioyoni mwenu kwa Imani*
~The Bible English states that ” *Christ may dwell in your Heart through faith*
~Ukiutafsiri huo msitari wa Kiingereza kwa kiswahili,unasema hivi:-
*Kristo akae mioyoni mwenu kwa kupitia Imani*
~Ahaaa,Kumbe njia pekee inayomruhusu Yesu aingiena kukaa ndani yetu ni IMANI.
~Ili Imani iweze kutengenezwa,ni lazima yawepo material ya kuitengeneza! Na Material hayo yanaitwa ” *Neno la Mungu*
~Angalia 👇🏿👇👇🏿
*Warumi 10:17 imeandikwa ” Basi Imani,chanzo chake ni kusikia;na kusikia huja kwa neno la Kristo*
~Mmmmh! Kumbe ili mtu ahesabike kuwa ana Imani ni lazima ndani yake liwemo Neno la Kristo!
~Imani ina tabia ya kuongezeka! 
~Ili Imani iwe kubwa ni lazima kile kinachoitengeneza nacho kiwe kingi/kikubwa.
~Angalia tena 👇🏿👇👇🏿

*Wakolosai 3:16 imeandikwa “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu…..*
~ kumbe mahusiano kati ya Neno na Imani ni kwamba, Neno likiwa jingi,na imani inakuwa kubwa!
~Kumbe sasa, kiwango cha Imani ndani ya mtu,ndo kiwango cha ukaaji wa Yesu ndani ya mtu huyo!
~Kwa Lugha nyingine, Yesi huwa *Anaumbika*ndani yetu kupitia imani!
*Wagalatia 4:19 imeandikwa” Vitoto vyangu,ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo AUMBIKE ndani yenu*
~Kumbe,mahusiano kati ya Imani na Yesu ni kwamba,Imani ikiongezeka na Utendaji kazi wa Yesu unaongezeka!
~Yesu aliye ndani ya kila mtu aliyeokoka ni wa kiwango kimoja! Tofauti ni utendaji kazi!
~Yesu huwa anatenda kazi kwa kadri ya kiwango cha Imani iliyomo ndani yetu!
~Biblia inaposema kwamba *Imani chanzo chake ni Neno la Kristo*
Na pia inasema *Kristo akae mioyoni mwenu kwa Imani*
~Kwa maana hiyo kiwango kile unacholiweka neno la Mungu ndani yako,ndo kiwango hicho hicho Kristo anajengeka ndani yetu!
~Nguvu inayotiririka kutoka kwenye Jina la Yesu ina kiwango sawa na kiasi cha Neno la Mungu lililomo ndani yako!
~Kiwango cha nguvu inayotoka ktk kuachilia uponyaji iko sawa kabisa na kiwango cha Neno la Mungu kilichomo ndani yako!!!!!
~Hebu jiulize,Neno la Mungu ndani yako limo kwa kiasi gani????
~Mungu akusaidie na kukupa nguvu ktk kuliweka neno la Mungu moyoni mwako!!!
*Hii ndo Pasaka ya Leo,kula uondoke!*

MASWALI 

*SOMO:MASWALI*(DAY 17)
NA *JOHN WEREMA*
~Kiwango mojawapo kinachoonesha kuwa wewe umekua kiroho au unamuelewa Mungu,ni ufahamu wako juu ya Neno la Mungu.
~jibu swali mojawapo au yote Kati ya yafuatayo! *Hakikisha majibu yako yanakuwa na references kutoka kwenye Biblia*
*SWALI 1*
Katika Yohana 15:7 imeandikwa ” *Ninyi mkikaa ndani yangu ,na maneno yangu yakikaa ndani yenu,Ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.*
  a) Je,kuna utofauti wowote kati ya YESU na NENO LAKE? kama ni ndio au hapana! Thibitisha!!!
b)Je ni kipi kinatangulia kuingia ndani ya mtu kati ya Neno la Mungu na Yesu? Thibitisha!!!
*Swali 2*
~Je ni vitu gani vinavyomtofautisha Yesu kabla hajafa na baada ya kufufuka?

Au, 

Kuna utofauti wowote unaouona kwa Yesu kipindi hajafa Msalabani na baada ya kufufuka?( vitaje vitu hivyo).

*Swali 3*

Kuna Mahusiano gani kati ya Imani na Neno la Mungu? na jinsi gani vinavyotegemeana?
” *NAOMBA UJARIBU KUJIBU NA MUNGU ATAKUBARIKI*

 “And, ye fathers, provoke not your children to wrath: but bring them up in the nurture and admonition of the Lord. Ephesians 6:4”

CHUNGA ULIMI WAKO UAIKUTIE ILI KITANZI.

NGUVU YA MANENO YA KINYWA CHAKO 
“ Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;…” Mithali 18:21a
“ Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako,Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,” Mithali 6:2.
“ Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache. ” Muhubiri 5:2
“ Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum .” Yakobo 3:5-6
“ Uuzuie ulimi wako na mabaya,Na midomo yako na kusema hila.” Zab.34:13
MAOMBI 
1.Muombe MUNGU TOBA KWA KILA NENO BAYA ULILO LISEMA KWA AJILI YAKO AU KWA AJILI YA MWINGINE 
2 Futa kila Neno baya ulilosemewa au ulilo jisemea mwenyewe kwa kujua au kutokujua (TUMIA DAMU YA YESU,UFUNUO 12:11a)
3.Omba MSAADA WA ROHO MTAKATIFU AKAMATE NA KUTAWALA KINYWA CHAKO 
4.Omba KIBALI CHA MUNGU KATIKA KINYWA CHAKO, UNAPOKUWA UNAONGEA NA WATU 
USIKU MWEMA 

KABLA HUJAINGIA KUOMBA NI MUHIMU KUANZA NA TOBA, YAANI KUJITAKASA 

0753391634

(Whatsapp)

KUJIUNGA NA KUNDI LETU
*RUKSA KUSHARE NA GROUPS ZINGINE*
*Mwalimu Conrad C*

TUMIA MUUJIZA WA KWANZA KUTATUA TATIZO LINALOKUKABILI.

*SOMO:TUMIA MUUJIZA WA KWANZA KUTATUA TATIZO LINALOKUKABILI* (DAY 16).
NA *JOHN WEREMA*
~Imani yenye nguvu na ya kweli ni pale mtu anapokiri ushindi mbele za watu hata kabla tukio halijatokea.
~Hebu mwangalie alichokifanya Daudi👇👇🏿👇

*1Samwel 17:36-37 imeandikwa ” Mtumishi wako alimwua Simba na dubu pia;na huyu mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao,kwa sababu amewatukana Majeshi ya Mungu aliye hai.Daudi akasema,Bwana aliyeniokoa na makucha ya Simba,na makucha ya dubu,ataniokoa na mkono wa mfilisti huyu.*
~Kumbuka,Daudi aliyasema maneno hayo hata kabla hajaingia kupigana na mtu aliyekuwa anaogopwa na watu wote!
~Hakika Imani ya namna hii,huwa inamfanya Mungu aingie kutenda kazi hata kama hakukusudia kutenda!
~Kwa maana nyingine, tunapaswa kukiri ushindi hata kabla hatujafanya kitu.
~Angalia jinsi Daudi alivyomwambia Goliath 👇🏿👇👇🏿
*1Samwel 17:46 imeandikwa ” Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu,nami nitakupiga,na kukuondolea kichwa chako,nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya wafilisti.*
~Ujasiri huwa unakuja pale mtu anapokuwa na uhakika na Mungu anayemtumikia! 
~Daudi alijua kabisa,Mungu aliyemshindia kule porini ndiye huyo huyo atakayemshindia katika mjini!
~Mungu anapokutendea muujiza,huwa anataka uutumie muujiza huo kumwamini ili akutendee mwingine pale unapokutana na tatizo, Maana Mungu huwa habadiliki!
~Mungu anapomwokoa mtu huwa kuna muujiza wa kipekee huwa anamtendea ili muujiza huo umpe mtu ujasiri wakati wa kukabiliana na tatizo!
~Jiulize,je kuna muujiza Mungu alishakutendea? Kama jibu ni ndio,tumia huo huo ili kukabiliana na tatizo linalokukabili!!!
~Mwangalie mtu mwingine tena ambaye ni Yesu! Tunamwona Yesu anawaambia watu waliondoe jiwe ili amfufue Lazaro! Yesu alikuwa na Uhakika kuwa Lazaro ni lazima afufuke kwa sababu kabla Yesu hajamfufua Lazaro,alikuwa ameshafufua watu wengi kwa hiyo ndo maana alikuwa na ujasiri wa kuwaambia watu waliondoe jiwe!
*Yohana 11:39a imeandikwa “Yesu Akasema,liondoeni jiwe.*
~Sikia hii point aliyoisema Yesu mbele za Baba yake kabla ya kumfufua Lazaro. 👇🏿👇🏿👇🏿

*Yohana 11:41-42 imeandikwa” Basi wakaliondoa lile jiwe.Yesu akainua macho yake juu,akasema Baba nakushukuru kwa kuwa umenisikia.Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote……….;*
~Hapo aliposema, *Nami najua wanisikia siku zote* hii ina Maana kuna kitu Yesu alishawahi kuomba kuhusu kumfufua yule maiti aliyekuwa kwenye Lango la Naini,Hivyo Yesu alipata ujasiri maana alijua kabisa kwamba Mungu yule aliyemsaidia kufufua maiti wa Lango la Naini,ndiye huyo huyo atakayemsaidia kumfufua Lazaro!! Ndo maana Yesu akasema *Najua wanisikia siku zote*
~Ahaaaa,Mungu yule aliyekusaidia kutatua tatizo la kwanza jua kabisa ni Mungu huyo huyo atakayekuwezesha kutatua tatizo la pili!
~Watu wengi huwa tunashindwa kumuamini Mungu katika mambo yajayo kwa sababu huwa tunasahau alichotutendea nyuma!!!!! 
~OK,hebu mwangalie Petro ujasiri aliokuwa nao katika ule mlango wa mzuri katika kumwinua kiwete!
~Biblia inasema baada ya Petro kumwombea yule kiwete,hatua iliyofuata ni kumshika yule kiwete mkono na kumwinua!
*Swali*

ni nini kilichomfanya Petro awe na ujasiri mpaka wa kumshika mkono kiwete na kumwinua? 

~Jibu ni kwamba,Petro kuna miujiza mingi alishatendewa na Mungu hivyo hakuona shaka yoyote kuhusu kiwete kuinuka!
*Matendo 3:6-7 imeandikwa ” Petro akasema Mimi sina Fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho.Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,simama uende.Akamshika mkono wa kuume,akamwinua,na nyayo zake na vifundo vya miguu vikatiwa nguvu.*
~Hebu tumia Muujiza uliotendewa na Mungu kutatua tatizo la kazi,ndoa,afya linalokukabili!, na Mungu atakuwa pamoja nawe!
*Hii ndo pasaka ya Leo, kula uhame kiroho*

USIWE ASIYEAMINI BALI AAMINIYE.

*SOMO: USIWE ASIYEAMINI,BALI AAMINIYE.*(DAY 15)
NA *JOHN WEREMA*
~Naomba radhi kwa kutokutuma somo la DAY 13 na DAY 14 kwa sababu Wassap yangu ilikuwa inasumbua.Ninamshukuru Mungu kwa sasa iko vizuri.
Sasa tunaweza kuendelea na somo la DAY 15.
*Yohana 20:27 imeandikwa “Kisha akamwambia Tomaso,lete hapa kidole chako;uitazame mikono yangu;ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu,WALA USIWE ASIYEAMINI,BALI AAMINIYE.*
~Jambo kubwa linalomfanya Mwanadamu ashindwe kupokea vitu kutoka kwa Mungu ni tatizo la *KUTOKUAMINI*
~Kichowafanya Wakristo wengi tushindwe kufanya aliyoyafanya Yesu ni tatizo la *KUTOKUAMINI*
~Unajua,kumiliki na kuisoma Biblia na kujua kilichoandikwa sio tatizo! tatizo lipo kwenye kuamini ulichokisoma!
~Sikiliza,Katika Agano la Kale; watu walikuwa wanapata haki kwa njia ya matendo Lakini katika Agano jipya Haki inapatikana kwa njia ya Imani.
~Sikiliza,Katika Agano jipya mtendaji mkuu ni Yesu Kristo; sisi kazi yetu ni kuamini tu!
*Swali*
~Kama Ahadi za Mungu zimehakikiwa na kuthibitishwa na kila anayezitumia lazima apate majibu! Sasa kwanini tukizitumia muda mwingine hatupati majibu?
*Jawabu*

~Naomba nikupe jibu kwa kutumia huu mfano:

Mfano:Wewe umeenda bank kuchukua pesa kwenye ATM,umeingiza kadi kwenye machine vizuri,ukakomandi na kiasi,then Pesa ikatoka! Swali,je ile pesa inapotoka huwa inaruka moja kwa moja mpaka mfukoni au huwa inatoka na kubaki pale kwenye ATM mpaka uichukue kwa mkono? Najua ili pesa iwe ya kwako ni lazima unyoshe mkono na kuiweka mkononi mwako! hapo ndipo itahesabika kuwa umepata ulichokitaka!

~kadharika ATM Kadi imefananishwa na ahadi za Mungu,Pesa imefananishwa na kile unachokitaka kutoka kwa Mungu; Imani imefananishwa na Mkono wa kuchukulia Pesa iliyotoka kwenye ATM machine!!!!!
~Kumbe watu wengi tunashindwa kupokea kwa sababu hatuna mkono wa kupokelea tulichokiomba!
*Swali*

Katika Luka 9:1-2,tunaona Yesu aliwapa Wanafunzi wake amri ya Kuponya kila aina udhaifu,Magonjwa na kutoa pepo! Je,ni kwanini Wanafunzi hao hao walishindwa kutoa Pepo la Kifafa?(rejea Mathayo 17:15-16).
*Jawabu*
~Sikiliza,Kuna tofauti kubwa kati ya kuwa na Mamlaka na kuwa na Imani!
~Kila aliye na Imani anayo mamlaka; lakini sio kila mwenye Mamlaka ana Imani.
~Imani itaitwa imefanya kazi pale itakapokuwa imekupa kile unachohitaji!
~OK,sikiliza tena,kabla Imani haijatenda kazi kuna baadhi ya vitu ambavyo inapaswa ivishinde! Vitu hivyo ni 

*1)Mashaka/hofu/kusita-sita/wasiwasi*
*2)Woga*
~Maana yake,unapotaka kufanya jambo fulani la kiroho,ni Lazima degree ya Imani ya kutaka kufanya jambo hilo,iwe kubwa kuliko degree ya Mashaka na Woga!
~Wanafunzi wa Yesu walishindwa kutoa Pepo la Kifafa kwa Sababu degree ya Mashaka iliyokuwa ndani yao ilikuwa kubwa kuliko degree ya Imani waliyoiachilia!
~Sikiliza tena,Daima matatizo huwa hayana uzito unaolingana,hivyo kila tatizo ili liweze kutoka,ni lazima iachiliwe Imani yenye uzito sawa na tatizo hilo!
~Kwa mfano,huwezi kutumia Fimbo kumuua nyati lakini unaweza ukatumia Bunduki kumuua nyati!
~Wanafunzi walipomuuliza Yesu ni kwanini walishindwa kumtoa Yule Pepo,Akawaambia ni kwa sababu ya *Upungufu wa Imani hao*
~Kwa Lugha nyingine,ni kama Yesu aliwaambia hivi *degree ya Imani mliyoitumia kutoa pepo ni ndogo kuliko degree ya lile tatizo lililomfunga*
~sikiliza,ukitaka kujua kuwa lile unalotaka kulikabiri ni lina ukubwa kuliko Imani unayotaka kuachilia,hata kabla hujaachilia Imani,ni lazima hofu ikuingie! Ukiona hivyo,tambua kabisa degree ya tatizo lina ukubwa kuliko Imani uliyonayo!
~Sikiliza tena,Imani haiwezi kukopwa!!!
Kivipi? 

Kwa mfano,wewe ukiwa na Imani ya kuponya magonjwa haina maana kwamba Imani hiyo inaweza kukusaidia kutoa pepo la Umaskini!

~Ukitaka kuamini,angalia watumishi wengi wenye uwezo wa kuponya Magonjwa, haya kawaangalie watumishi hao hao kwenye upande wa Uchumi! ni maskini kweli!
~Sikiliza,kila tatizo unaloliona hapa duniani,Mungu ameweka na Ahadi ya kulipangua!!! 
~Ndio Maana kuna umuhimu sana wa kuzifahamu ahadi za Mungu!
~wanafunzi wa Yesu hawakuwa na Imani ya Kutoa Pepo la Kifafa! ila walikuwa na imani ya kuponya Magonjwa ya kawaida!
Ndo maana Yesu Akawaambia hivi *Mkiwa na Imani kiasi cha punje ya Haradali mtauambia mlima huu,Ondoka hapa uende kule;nao utaondoka.*
~Yesu akaamua kuwapa suhulisho la kukuza Imani/kuondokana na mashaka.
~Akawaambia hivi👇🏿👇👇🏿

*Mathayo 17:21 imeandikwa ” Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na Kufunga*
~Kwa Lugha nyingine, Yesu angewaambia hivi *Tatizo la KUTOKUAMINI kwenu ili litoke mioyoni mwenu,ni lazima mfanye maombi ya kufunga na kuomba.*
~kumbe ili tupate MPENYO katika Imani,ni lazima tufunge na kuomba ili kuliondoa tatizo hili.
*Hii ndo Pasaka ya Leo,kula uondoke*

NITATUMAINI WALA SITAOGOPA.

*SOMO: NITATUMAINI WALA SITAOGOPA*

ISAYA 12:2

*“Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; NITAMTUMAINI WALA SITAOGOPA; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; naye amekuwa wokovu wangu.”*
Tangu katika kitabu cha MWANZO mpaka katika kitabu cha mwisho cha Biblia, UFUNUO, mara nyingi mno Mungu amekuwa akiwaambia watu wake wasiogope.
 Katika MWANZO 15:1, Mungu alimwambia Abramu, *“USIOGOPE, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana”*. Katika UFUNUO WA YOHANA 1:17, Yesu Kristo alimwambia Yohana, *“USIOGOPE, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho”.* Nyakati zote, Mungu amerudia mara nyingi akiwaambia watu wake wasiogope. Hata leo, ujumbe wa Mungu ni huohuo kwa kila mtu aliyeokoka. Hupaswi kuogopa katika mazingira yoyote. 
Roho ya woga, haitokani na Mungu bali ni ya shetani. Biblia inasema katika 2 TIMOTHEO 1:7, *“Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi”*. Biblia inasema katika UFUNUO 21:8, kwamba waoga watatupwa katika ziwa la moto sawasawa na waabudu sanamu, waongo, wachawi, wauaji na wazinzi. 
Mtu aliyeokoka hapaswi kamwe kuogopa katika mazingira yoyote yanayomkabili. 
✍🏻BEBA SILAHA HIZI, KUWA MKAKAMAVU

ZABURI 91:2:

*“Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini”.*

KUTOKA 14:13-14:

*“Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele, Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.”*
ZABURI 20:7:
*“Hawa wanataja magari na hawa farasi, bali sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.”*
Je! kuna jambo lililo gumu linalokukabili katika maisha yako? Je, ni ugonjwa ulioshindikana? Je ni vitisho vya Uchawi au kuachiwa “laana” na wazazi kwa ajili ya kuokoka? Je ni kutishwa kufukuzwa na mumeo au nduguzo sababu ya wokovu? Je ni masomo magumu? Je ni kukosa mtoto? Je ni vitisho vya kufukuzwa kazi? Je ni vitisho kwamba hutafanikiwa katika biashara yako? Ni nini? USIOGOPE, SIMAMA TU UKAUONE WOKOVU WA BWANA. Iambie nafsi yako na jirani yako pia, *“NITAMTUMAINI, SITAOGOPA.”*
NAKUTAKIA JUMAPILI YENYE BARAKA

YESU ALIONJA MAUTI KWA NIABA YETU.

*SOMO:YESU ALIONJA MAUTI KWA NIABA YETU*(DAY 12).
NA *JOHN WEREMA*
*Waebrania 2:9b imeandikwa “Kwa Sababu ya maumivu ya Mauti,amevikwa taji ya utukufu na heshima,ili Kwa NEEMA YA MUNGU AIONJE MAUTI KWA AJILI YA KILA MTU.*
~Neno *Kwa ajili ya kila mtu* kwa maana nyingine tunaweza kusema hivi *Kwa niaba ya kila mtu* 

~Hii ina maana kwamba,kila mwanadamu alipaswa aionje mauti(afe),lakini akachaguliwa mmoja ambaye atatuwakilisha katika kuionja mauti.
~Mtu huyo alikuwa ni Yesu Kristo, Maana yake Yesu alionja mauti kwa niaba ya Waafrika wote,Wazungu wote,Wahindi wote,Wachaga wote,wabena wote,n.k
~Yeye aliyetuwakilisha,yaani Yesu; hakuishia kuionja mauti tu,bali alimharibu haribu kabisa yule aliyekuwa na nguvu za mauti ili mauti isiwe na nguvu kwetu tena.
Angalia👇🏿👇🏿
*Waebrania 2:14 imeandikwa” Basi kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili,yeye naye(Yesu)vivyo hivyo alishiriki yayo hayo,ili kwa njia ya MAUTI AMHARIBU YEYE ALIYEKUWA NA NGUVU ZA MAUTI,YAANI,IBILISI.”*
~Ahaa,Kumbe nyuma ya Mauti yupo Shetani! Na kinachomtia nguvu mauti ni Shetani!!! Sasa je; kama Mtia nguvu ameharibiwa; mtiwa nguvu atakuwa na hali gani?( jibu ni kwamba,hana nguvu tena).
~Kwa Maana hiyo,Mauti hauna nguvu juu yetu tena!
*Swali:Je ni kweli Mauti haina nguvu juu ya watu wote?*
~Jibu ni hapana! Mauti ina nguvu juu ya baadhi ya watu,na tena mauti haina nguvu juu ya baadhi ya watu!!!!!
*Swali:Mbona imeandikwa kwamba Yesu alionja mauti kwa ajili ya watu wote,sasa inakuwaje tena mauti iwe na nguvu juu ya baadhi ya watu?*
*Jibu*

Kwa mfano, wewe umejiunga kwenye group fulani la Wasapu,halafu ukawa umezima data! Je,zile SMS zinazotumwa kwenye group zitakufikia ukiwa umezima data? Jibu ni hapana! mpaka uwashe data!

Kadharika Yesu alionja Mauti ili kila atakayejiunganisha naye,Mauti isiwe na nguvu juu yake!
~Kwa maana nyingine ni kwamba,Yesu atakuwa Shirika na wewe pale utakapojiunganisha naye!!!(Utakapookoka)!!!maana imeandikwa ” *Kila amwaniniye Yesu ana uzima wa milele*
*Swali: Je ambao hawajaokoka mauti ina nguvu juu yao?*
*Jawabu*

~Ndio,ambao hawajaokoka Shetani ana nguvu juu yao na mauti ina nguvu juu yao.
*Je ni wote waliookoka mauti haina nguvu juu yao?*
*Jibu*

Kwa mfano, watu wawili(baba na mtoto) wamepanda kwenye gari! baba amekaa siti ya mbele na mtoto amekaa siti ya nyuma! Kondakta alipoanza kudai nauli,baba alilipa yake na ya mtoto! Kondakta alipofika kudai kwa mtoto,mtoto akawa hana nauli,konda akamshusha huyo mtoto maana hakuwa na nauli! Lakini kumbuka konda alipewa kabisa nauli ya yule mtoto!

~Je unafikiri kama mtoto angefahamu kwamba amelipiwa nauli angekubali kushuka? Jibu ni hapana! Unafikiri ni kwanini alishuka? Jibu ni kwa sababu alikuwa hajui kuwa amelipiwa nauli!!
~Kadharika ndivyo ilivyo na hata kwa waliookoka! 
~Shetani anaweza akaja akamwingizia roho ya Mauti mtu aliyeokoka,naye akaipokea! Inaweza ukawa ni Mauti ya tumbo( yaani mtu ni wa kuugua tumbo Mara kwa Mara,),mauti ya moyo,mauti ya kifua( yeye ni wa kifua kubana siku zote)

~Tatizo la mtu huyu lipo kwenye kutambua kwamba Yesu aliiharibu mauti na mauti haina nguvu tena!!!!
~Ndio Maana tunapookoka,tunapaswa kukaa kwenye kweli(Neno)ili tuweze kuwa huru!
~sasa Kwa kuwa umetambua kwamba Yesu alionja mauti kwa niaba yako,hivyo sasa anza kuamuru vile vilivyokufa maishani mwako vianze kufufuka! iwe ni huduma,ndoa,uchumi,Afya,n.k!!!!!
~Iambie Mauti kwamba ilishashindwa!!!!!
*Neema ya Kristo iwe juu yako katika kufanya hivi;Amina*.

ADUI MKUBWA WA MTU NI MWILI WAKE.

*SOMO:ADUI MKUBWA WA MTU NI MWILI WAKE*(DAY 11).
NA *JOHN WEREMA*

*Warumi 8:6 imeandikwa ” Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.*

Biblia ya Kiingereza inasema *For the mind of Flesh is death, but the mind of spirit is Life and peace*
~Neno Mauti lina maana ya Kifo au “kutengwa mbali na.”

~Mwanadamu yupo katika sehemu tatu,yaani:-

*Mwili* *Nafsi* na *roho*

~Kazi za Nafsi ni kupokea maamuzi kutoka kwenye Mwili au kwenye roho( inategemea) ni kipi kina nguvu kuliko kingine.
~Mwili na roho huwa vinashindana kila siku kuhusu kupeleka maamuzi kwenye Nafsi!
*Wagalatia 5:17 imeandikwa ” Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho,na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana hata hamwezi kufanya mnayotaka.*
~Kutembea kimwili maana yake ni kutembea kama Dunia inavyotaka,ni kutembea sawasawa na mapenzi ya Mwili.
~Mtu anapokuwa chini ya mwili/ anapoongozwa na mwili,akiyafanya ya Kimwili,matunda yanayozaliwa ni haya:-
*Wagalatia 5:19 imeandikwa ” Basi matendo ya Mwili ni dhahiri,ndiyo haya, Uasherati,ufisadi,Uchawi,uadui,ugomvi,wivu,hasira,fitina,n.k*

~Kila anayeyafanya hayo👆

JINSI YA KUNYOOSHA MAPITO YALIYOKWAMISHWA.

*SOMO: JINSI YA KUYANYOSHA MAPITO YALIYOKWAMISHWA*(DAY 10)
NA *JOHN WEREMA*
~Jamani lengo la Maombi haya ni kutafuta MPENYO katika ulimwengu wa roho! Na ili upate MPENYO ni lazima ufanye Maombi ya vita(Maombi ya kushindana).
~Fuatana nami katika masomo ninayokuletea kila siku asubuhi!!!!!
~Leo tutaangalia jinsi mapito yaliyokwamishwa.
*Ayubu 19:8 imeandikwa ” Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita,Na kutia giza katika mapito yangu.”*
~Katika huo msitari👆

KUVUNJA TABIA ZA KURITHI.

SUB-TOPIC *02*: *KUVUNJA TABIA ZA KURITHI*(DAY 09).
NA *JOHN WEREMA*
~Somo lililopita tuliangalia jinsi ya kung’oa Magonjwa unayoweza ukayarithi katika familia! tukasema mtu anaweza akawa ameokoka lakini bado ana yale Magonjwa ya kurithi mfano,Sicklecell,kisukari,Asthma n.k!
~tukasema Mtu unapookoka inabidi uvunje laana zote zinazokufuatilia! Na laana hizo tunazishinda kwa kutumia damu ya Yesu pekee.
~Leo;tutaingia kipengele kingine cha JINSI ya Kuvunja Tabia za Kifamilia!!!!
~Sio Magonjwa tu ndo yanayorithiwa,hata Tabia zinaweza kurithiwa! mfano 
~kwenye Biblia tunaona uongo ule ule Ibrahimu aliomdanganya Abimeleki ndo uongo huo huo Isaka( mtoto wa Ibrahimu) aliowadanganya watu wa kijiji cha Gerari.
*Mwanzo 20:1-2 imeandikwa ” Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini,akakaa kati ya Kadeshi ya shuri,naye akatembea katika Gerari.Ibrahimu akamnena Sara mkewe,Huyu ni ndugu yangu.Basi Abimeleki Mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.*
*Mwanzo 26:6-7 imeandikwa “Isaka akakaa katika Gerari. Watu wa mahali hapo wakamwuliza habari za mkewe.Akadema ni ndugu yangu huyu maana aliogopa kusema ni mke wangu,watu wa nchi wasije wakamwua kwa ajili ya Rebeka; kwa maana alikuwa mzuri wa uso.*
~Haitoshi,uongo huu ulienda mpaka kwa Mjukuu wa Ibrahimu yaani Yakobo 
*Mwanzo 27:19 imeandikwa” Yakobo akamwambia babaye,Mimi ni Esau,Mzaliwa wako wa kwanza,nimefanya kama ulivyoniambia.Ondoka tafadhari,ukae kitako,ule mawindo yangu ili roho yako inibariki.*
~Umeona sasa roho ya uongo inavyoweza kutembea!!!
~Kadharika unaweza kumkuta mtu kaokoka lakini ni mwongo kweli kweli, maana yake hiyo roho kairithi mahali kwenye familia yao!
~Kuna wengine tabia zao ni kuoa wake wawili wawili! Kwa hiyo hiyo roho inakuwa inafuatilia mpaka kizazi na kizazi,sasa kwa kuwa mtu kaokoka yeye atashindwa kuoa mke wa PILI kwa sababu kaokoka; sasa unajua atakachofanya;roho ya Uzinzi itamuandama kweli!!! Ndo maana utakuta makanisani mazinzi mengi kweli!( sio wanawake sio wanaume). Kwa hiyo ukiona jambo kama hilo tambua kabisa mtu huyo kwenye familia yao kuna tabia hizo.
~Wengine wanakuwa na tabia ya kuachika wanapoolewa! Utasikia,bibi yake aliachika,shangazi yake aliachika n.k kwa hiyo ukiona hivyo usishangae,jua kabisa karithi.
~wengine tabia zao ni kung’oa meno! Utashangaa mtoto wa miaka kumi sasa hivi eti naye anang’oa jino,ukiulizia utasikia linauma! Kwa hiyo hizo ni tabia za kurithi!
~Wengine Tabia zao ni kutokuoa au kuolewa na hata kama wakioa au kuolewa,wataolewa na kuoa kwa kuchelewa sana! Ukiona hivyo fuatilia kwenye familia zao,utagundua tatizo hili lilikuwepo!
~Wengine wana Tabia za kuzalia nyumbani i.e,wanazaa hata kabla ya kuolewa( si wapagani si waliookoka).
~Kwa hizo ni Tabia ambazo huwa zinamfuatilia mtu,na tabia hizi huwa ni kifamilia zaidi.
~Hivyo,wewe unapookoka,usiishie hapo,haribu kila tabia za kifamilia zinazokuatilia! Nawe utakuwa salama! 
~Jikomboe kwa damu ya Yesu!!! Ndo maana kuna umuhimu wa kujikomboa!
~ungana nami katika haya maombi ya Siku 30.nawe utapata MPENYO!

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nami katk 0763 441172.
*Mungu akubariki*

KUVUNJA LAANA ZA FAMILIA AU UKOO.

*TOPIC: KUVUNJA LAANA ZA FAMILIA/UKOO.*(DAY 8).
SUB-TOPIC-01

*KUHARIBU MAGONJWA YA FAMILIA.*
NA *JOHN WEREMA*
~Lengo kubwa la haya Maombi ya mfungo wa siku 30 ni kutaka kupata MPENYO katika huduma,Familia,kiuchumi,n.k.
~Leo tutaanza Kuangalia laana ya Familia! Lakini tutaanza na Sub topic ya Magonjwa ya Familia/ukoo.
~Siku nilifundisha humu humu aina tatu za Magonjwa ambayo ni:-
1)Magonjwa ya Kurithi.

2)Magonjwa ya kutengeneza.

3) Magonjwa ya Mazingira!

(Kama huna hilo somo njoo inbox nikurushie,maana nilishafundisha)
~Leo nitazungumzia Magonjwa ya Kurithi tu!
*Kutoka 20:5b imeandikwa ” Kwa kuwa mimi,BWANA,Mungu wako,ni Mungu mwenye wivu;NAWAPATILIZA wana maovu ya baba zao,hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao*
~Hilo neno *NAWAPATILIZA*kwa Lugha nyingine linaweza kusomwa hivi *NINAWAHAMISHIA*
~tumeona kwamba kitu kikubwa ambacho kinamfanya Mungu aseme kwamba atabatiliza ni dhambi.

~Chanzo kikubwa cha Magonjwa huwa ni dhambi,maana yake; ukisamehewa Dhambi(uovu),unasamehewa na Magonjwa!

*Zaburi 103:3 imeandikwa “Akusamehe maovu yako yote,akuponya Magonjwa yako yote”*

~Ok,turudi kwenye msingi wetu; Kumbe Maovu yanaweza yakahamishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mtu mwingine ndani ya familia moja au ukoo mmoja!
~Kwa mfano, kwenye Biblia tunamuona mke wa Ibrahimu akikuwa tasa,Ule utasa ukaenda tena mpaka kwa Mke wa Isaka; haikuishia hapo ule utasa ulikwenda mpaka kwa mke wa mjukuu wa Ibrahimu,yaani Yakobo!!! Habari hizi utazikuta katika kitabu cha Mwanzo!!
~Kwa maana hiyo tunaona ule Utasa ulienda mpaka kizazi cha tatu cha Ibrahimu!!!
~Laana inapelekea maovu kuhamishwa kutoka kizazi hadi kizazi; na Kumcha Mungu kunafanya Baraka ihamishwe kutoka kizazi hadi kizazi!!!
~Ukitaka uamini haya ninayoyazungumza,hebu angalia baadhi ya familia Fulani; utakuta mtu ana Asthma, ukimuulizia vizuri utasikia kwamba bibi yake alikufa kwa Asthma!

~Au mwangalie Mtu mwenye Sickle cell,utakuta kuna sehemu kairithi either ndani ya Familia au ndani ya Ukoo! Magonjwa ya Kurithi ni mengi mfano Kifafa,n.k
~Chanzo cha yote hayo ni uovu ambao ulifanywa na mababu,sasa unakuta Watoto ndo wanarithi!
~Hivi uliwahi kujiuliza hili swali? Kwamba,kwenye familia ya watoto watano; ikatokea labda baba/mama anaumwa Asthma,lakini ile Asthma isiwapate hao watoto wote watano ikampata mmojawapo!?au ikampata mtoto wa mmojawapo wa hao Watoto watano?
~Jibu ni kwamba Asthma ni roho,na ili roho iingie ndani ya mtu lazima kuwe na maelewano baina ya hizo roho mbili!!!! Ndo maana imeandikwa hivi *Je watu wawili waweza kutembea pamoja wasipopatana?* (Amos 3:3)

~Maana yake unapoona umerithi ugonjwa aliokuwa anaumwa either bibi,shangazi,mjomba wako; tambua kabisa ile roho ya ugonjwa inaendana kabisa na wewe!
~Daima Magonjwa ya Kurithi huwa hayaponyeki kwa Dawa za Hospitalini bali huwa yanaponywa kwa Dawa inayoitwa *DAMU YA YESU*
~Ili uweze kupona,cha kwanza ni Lazima uhakikishe umejiengua kutoka katika ukoo wa Kibinadamu na kuingizwa katika ukoo wa Yesu Kristo!! Hii inatokea pale mtu anapookoka!(anaposamehewa dhambi)!!!!
*Kutoka 20:6 imeandikwa “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao,na kuzishika amri zangu*
~Maana yake,unapookoka unapewa hati ya kuwa mwana wa Mungu hivyo una uwezo wa kuyashambulia Magonjwa ya Kurithi nayo yakakuacha nawe ukawa huru kabisa! 
~Magonjwa haya ya Kurithi tunayashinda kwa kutumia Wagalatia 3:13 ambayo inasema hivi *”Kristo alitukomboa katika Laana ya Torati,kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu;maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti.*
~yawezakuwa ni Magonjwa ya kifamilia yanakusumbua,hebu leo chukua hatua kuyashambulia,nayo yatakukimbia nawe utakuwa huru!
N.B,anayeruhusiwa kufanya hivi ni yule aliyeokoka tu! Ukitaka kuomba haya Maombi kama bado haujaokoka,nakushauri okoka kwanza ndo uombe haya Maombi.
*Mungu akubariki*

KUFUNGUA MALANGO YALIYOFUNGWA.

SOMO: *KUFUNGUA MALANGO YALIYOFUNGWA*(DAY 7)
NA *JOHN WEREMA*
*Isaya 60:11 imeandikwa “MALANGO yako nayo yatakuwa wazi daima;Hayatafungwa Mchana wala usiku; ili watu wapate kukuletea utajiri wa Mataifa,na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.*
~Neno Malango limetokana na Neno Mlango.

~Na kazi ya Mlango ni kupitisha vitu viwe vibaya au vizuri wenyewe unapitisha tu.
~Ili Mtu aingie kwenye huduma,ni lazima mlango wa huduma uwe wazi,ili aingie kwenye Ndoa, Uzima,Utajiri,n.k no Lazima milango ya vitu hivyo iwe wazi.
*Ufunuo 21:25-26 imeandikwa” Milango yake haitafungwa kamwe mchana;kwa maana humo hamna usiku.Nao wataleta utukufu na heshima ya Mataifa ndani yake*
~Malango yako yakiwa wazi afya itaingia,malango yakiwa wazi utajiri utaingia,ndoa njema itakufuata,upako utaingia,n.k
~Yawezakuwa umekuwa unasumbuka muda mrefu,kumbe usijue labda milango ya kuingilia katika eneo fulani ilikuwa imefungwa!!!!
~katika haya Maombi ya Siku 30 hakikisha Ardhi imekombolewa na Malango yako yamefunguliwa! Hebu siku ya Leo inuka utumie angalau masaa mawili anza kufungua Malango YALIYOFUNGWA nayo uatafunguliwa katika jina la Yesu.

~Msitari wa kusimamia Mathayo 18:18.
*Mungu akubariki kama utafanya hivyo*

THAMANI YA MWANADAMU IMEKADIRIWA KUWA SAWA NA THAMANI YA DAMU YA YESU.

SOMO: *THAMANI YA MWANADAMU IMEKADIRIWA KUWA SAWA NA THAMANI YA DAMU YA YESU*(DAY 6)
NA *JOHN WEREMA*
✍🏻Kabla sijaendelea hebu angalia kwanza huu mfano ambao utakisaidia kulielewa hili somo!
*Kwa mfano*;Watu watatu walikuwa dukani,wakaiona simu inayouzwa *Tsh 140,000/-* na kila mmoja akawa na Shauku ya kuinunua simu hiyo! Mtu wa kwanza alikuwa na *Tsh 70,000/*tu mfukoni, na mtu wa pili alikuwa na *Tsh 100,000/*tu mfukoni,na mtu wa tatu alikuwa na *Tsh 180,000/-*tu mfukoni! na watu hao watatu kila mmoja anatamani kuichukua ile simu. 

*Swali* je kati hao watatu ni yupi atakayefanikiwa kuinunua ile simu???

(Bila shaka najua utaniambia kuwa ni yule mwenye *Tsh180,000/* na kiukweli hilo ndo jibu)
 Kwa maana hiyo simu haikombolewa/kuchukuliwa na yule aliyekuwa na *Tsh 70,000/* wala yule alikuwa na *Tsh 100,000/*bali simu ilichukuliwa na yule aliyekuwa na *Tsh 180,000/*
~Sasa tuendelee na somo letu.
*1 Petro 1:18-19 imeandikwa “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo,kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;bali kwa damu ya thamani,kama ya mwana-kondoo asiye na ila,asiye na waa,yaani, ya Kristo.*
~kwenye huo msitari 👆

UOTAJI WA MBEGU UNATEGEMEA ENEO ZILIPOPANDWA.

*SOMO:UOTAJI WA MBEGU,UNATEGEMEA ENEO ZILIPOPANDWA*(DAY 5)
NA *JOHN WEREMA*
*Luka 8:5-8 imeandikwa “Mpanzi alitoka kwenda kupanda Mbegu zake;naye alipokuwa akizipanda,Nyingine zilianguka karibu na njia,zikakanyagwa,ndege wa angani wakazila.Nyingine zikaanguka penye mwamba;zilipoanza kumea zikakauka kwa kukosa rutuba.Nyingine zikaanguka kati ya miiba,na miiba ikamea pamoja nazo ikazisonga.Nyingine zikaanguka penye udongo mzuri;zikamea,zikazaa moja kwa mia.Alipokuwa akinena hayo alipaza sauti akisema,Mwenye masikio ya kusikilia,na asikie.*
✍🏻Katika msitari huo 👆

FAIDA ZA KUJIUNGANISHA NA ARDHI ILIYOKOMBOLEWA.

*SOMO: FAIDA YA KUJIUNGANISHA NA ARDHI ILIYOKOMBOLEWA.*(DAY 4)
Part 3.
NA *JOHN WEREMA*
*Amos 3:3 imeandikwa ” Je watu wawili waweza kutembea pamoja,wasipokuwa wamepatana?*
~Mtu aliye kombolewa na Ardhi iliyokombolewa nia zao huwa ni moja! Chochote utakachotaka kujifanya, Ardhi itakuwa pamoja nawe kukusapoti.
*Ufunuo 12:15-16 imeandikwa “Nyoka akatoa katika kinywa chake,nyuma ya Yule huyo mwanamke,maji kama mto,amfanye kuchukuliwa na mto ule; Nchi ikamsaidia mwanamke;nchi ikafunua Kinywa chake,ikaumeza mto ule alioutoa yule Joka katika Kinywa chake.*
~Tumeona,Ardhi ilikuwa pamoja na yule mwanamke; Joka alipotoa mto ili umchukue Mwanamke yule,tunaona kabisa, Ardhi ilimsaidia katika kuumeza MTO ule.
~Ardhi uliyojipatanisha nawe inaweza kumeza mito ya mateso,mito yfa Magonjwa, mito ya kuharibu mimba,mito ya kukataliwa,mito ya kutokuolewa,mito ya Umaskini ambayo Shetani anaituma kuelekea kwako.
~Ndio maana Elisha Alipotambua kuwa ardhi haikuwa Upande wao,maana ilikuwa inawazalia mapooza ! Elisha akajipatanisha na Ardhi ile kwa *Kuweka chumvi ndani ya Chemichemi*tangu hapo Ardhi haikuzaa mapooza tena wala maji hayakutoa kufakufa!!!!(2 Wafalme 2:19-22)
~Kumbe solution ni kujipatanisha na Ardhi ili muwe kitu kimoja.
~Sikiliza,Kwa kuwa wewe ni mtumishi wa Ardhi,na Ardhi(Pacha mwenzio) uliyoikomboa na kujipatanisha nayo,nayo inakuwa ni mtumishi wa Mungu.
*Zaburi119:91b imeandikwa “Maana vitu vyote ni Watumishi wa Mungu*
~Kwa maana hiyo,kwa kuwa Ardhi ipo upande wako,maana yake utakachokikataa,na Ardhi nayo itakusapoti; ukisema Ardhi izae vizuri kila unachokipanda juu yake, itakuwa hivyo!!!! 
~Pia Mungu huwa anapenda kuzungumza na watu sana katika Ardhi iliyokombolewa! 
Kwa mfano,*Mungu hakuweza kuzungumza na Musa,hadi Musa alipojipatanisha na Ardhi ile; Vua viatu vyako maana mahali hapa ni Patakatifu.
~Tunaona tena Mungu anashindwa kuzungumza na Abramu kisa Ardhi aliyokuwepo Abramu;mpaka Mungu anaamua kuchukua hatua na kumwelekeza Abramu mahali pa Kwenda ili aweze kusema naye(Mwanzo 12:1)

~Kumbe Faida Mojawapo ya kujipatanisha na Ardhi iliyokombolewa ni kwamba,Mungu atazungumza na wewe!
~Tunaona Pia Kuna sehemu moja ilikuwa inaitwa *Nayothi* katika mji wa *Rama*;Aise Biblia inasema kila aliyefika mahali pale alijazwa Roho Mtakatifu na kuanza kutabiri; Mfano Mzuri ni Sauli aliyekuwa anamtafuta Daudi,alipoambiwa kwamba Daudi yupo Nayothi,Sauli akaamua aende Nayothi kumkamata Daudi,lakini cha kushangaza Sauli alipokanyaga tu Ardhi ya Nayothi alijazwa Roho Mtakatifu na kuanza kutabiri; maana yake,kilichompeleka hakukifanya bali alifanya kisichompeleka.
~Kumbe faida nyingine ya kujipatanisha na Ardhi iliyokombolewa ni kwamba mabaya yanapotumwa kwako,punde yanapofika katika Ardhi yako, pale pale yanakuwa baraka kwako.( Haleluyaaa).
Maana yake,ikitumwa mishale ili kuharibu ndoa yako, ama kazi yako,ama uchumba wako,ama huduma yako; punde mishale itakapofika kwenye ile Ardhi iliyokombolewa unayoiishi,utashangaa mishale baada ya kukuupinga inageuka kuwa baraka na msaada kwako! 
*hebu sasa itumie vizuri hii siku ya leo ili kujipatanisha na Ardhi ya mahali unapoishi,unapofanyia kazi,unapofanyia huduma,unapofanyia biashara n.k! Utaona MPENYO wa Ajabu sana!*
*Mungu akubariki*

NGUVU YA DAMU INAPOMWAGIKA KWENYE ARDHI.

*SOMO: NGUVU YA DAMU INAPOMWAGIKA KWENYE ARDHI* ( DAY 3)
Part 2.
NA *JOHN WEREMA*
✍🏻Damu inapomwagika juu ya Ardhi,huwa inafanya tabia mojawapo kati ya zifuatazo:-
*1) Damu inaweza kulia.*

~Damu inapolia,maana yake huwa inahitaji kisasi. 
*Mwanzo 4:10 imeandikwa “Akasema,Umefanya nini?SAUTI YA DAMU YA NDUGU YAKO INANILILIA KUTOKA KATIKA ARDHI.*
~Ahaaa,Kumbe Damu inapomwagika kwenye Ardhi ina uwezo wa kulia,na inapokuwa inalia maana yake huwa inataka ilipiziwe kisasi kwa yule aliyeimwaga.
~Damu inayolia,ni ile damu iliyomwaga pasipo hatia!!
Kwa mfano,tunamuona Kaini alivyoimwaga Damu ya ndugu yake kwa wivu tu,Damu ya Habili ikaanza kulalamika mbele za Mungu.
~Angalia Kilichompata Kaini baada ya damu ya Habili kumlilia Mungu 👇👇👇👇
*Mwanzo 4:11 imeandikwa” Basi sasa, umelaaniwa wewe katika Ardhi iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako.*
~Ahaa,kumbe kila aliyemwaga Damu isiyokuwa na hatia alilaaniwa!! Maana yake ukilaaniwa Hata ufanyeje kazi huwezi kufanikiwa!!!
~Yawezakuwa labda wewe ulipokuwa mdada ulifanya umalaya ukapata Ujauzito ukaamua utoe kisirisiri!! Maana yake ulipotoa Ujauzito ulimwaga damu isiyo na hatia, ambayo mpaka sasa inalia ikihitaji kisasi!!! 
~Au ni Ni mwanamme, umemuua mwenzako either kwa bahati mbaya au kimakusudi; damu ile ni lazima itake kisasi.
~Sasa yawezakuwa umeshindwa kupiga hatua kikazi,kimaombi,kibiashara,kihuduma nk,ni kwa sababu ya ile damu uliyoimwaga pasipo hatia,au yawezakuwa ulimwagiwa pasipo wewe kujua! Na Damu hiyo inalia usiku na Mchana ikihitaji kisasi!!
~Sasa ili uweze kupata MPENYO wa Mambo yako,ni lazima uinyamazishe damu inayolia na kulitaja jina lako. Hebu inyamazishe kwa kutumia Damu ya Yesu.
*2)Damu inaweza kunena(Kusema) inapomwagika kwenye Ardhi*
~Ili Damu iweze kusema au kunena ni Lazima imwagwe kwa kusudi maalum.
~Damu hii,huwa inanena kile ambacho imeambiwa ifanye wakati inamwagwa.
~Damu inaweza kunena mema au mabaya.
*WAEBRANIA 12:24 imeandikwa ” na Yesu mjumbe wa Agano jipya,na damu ya Kunyunyizwa,INENAYO MEMA kuliko ile ya Habili. “*
~Umeona sasa,Damu ya Yesu ilimwagika ili watu waokolewe,ili watu wafanikiwe,ili watu wasamehewe dhambi,ili watu waponywe n.k,Hivyo inapokuwa inanena huwa inasema hivi:-

” Waokolewe,wasamehewe,waponywe,wafaulu n.k!!!!
~Kumbuka,Damu ya Yesu ilimwagika kwenye Ardhi hii tunayoikanyaga!
~Kadharika,Mtu asiyekupenda naye anaweza akamwaga damu kwa ajili yako, halafu akainuizia Damu ile inene mabaya juu yako!
~Ndo maana hakuna mtu awezaye kwenda kwa mganga bila kuwa na kitu chenye damu.
~Adui yako anapopeleka either Ng’ombe,Mbuzi,kuku n.k kwa Mganga ili akutese; Mganga huwa anamuuliza,”Unataka fulani tumfanyeje, utasikia yeye anajibu labda *Asizae* ,sasa mganga anapokuwa anamchinja labda yule Jogoo,damu inapomwagika, huwa Mganga anaitamkia maneno! Kwa mfano *Aneth asizae* na kweli Aneth hawezi kuzaa mpaka ainyamazishe sauti ya ile damu.
~Tumia damu ya Yesu kunyamazisha damu inayonena Mabaya juu yako katika Ardhi.
*Mungu akubariki*

UKUTAKA KUMKOMBOA MWANADAMU KOMBOA ARDHI YAKE.

*SOMO,:UKITAKA KUMKOMBOA MWANADAMU,KOMBOA KWANZA ARDHI ANAYOISHI.*(DAY 2)     

Part 1.
NA *JOHN WEREMA*
*Mwanzo 3:17 imeandikwa ” Akamwambia Adamu,kwa kuwa umesikiliza sauti ya mke wako,ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza,nikisema usiyale;ARDHI IMELAANIWA KWA AJILI YAKO kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako.*
~Ukiangalia kwa makini kabisa msitari huo 👆

KUHUSU MAANDIKO YA KWENYE BIBLIA.

SOMO: KANUNI ZA USOMAJI MAKINI WA NENO LA MUNGU
Kwa nini unahitaji kujifunza somo hili?
Kutofuata kanuni za usomaji makini, kunasababisha matatizo makubwa yafuatayo:

1. Wasomaji wengi wa biblia kutoa tafsiri tofauti za Maandiko tena zinazokinzana na ukweli halisi. Hili ni tatizo kubwa ambalo limesababisha kuwa na uelewa unaokinzana juu ya mafundisho muhimu ya biblia. Hatimaye wengi watapotea na kuangamizwa kwa kukosa maarifa – Mathayo 22:29, Hosea 4:6.
2. Wasomaji wengi kushindwa kuzielewa baadhi ya aya na kudhani kuwa biblia inajipinga yenyewe wakati tatizo siyo biblia ila ni wao wenyewe. 
➡ Mwl J.K Nyerere alisema “Moja ya maadui wetu wakuu ni ujinga ..” Mtu akiwa na ufahamu wa kina wa jambo anakuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi yaliyo sahihi zaidi. Kukosa ujuzi wa mambo ni tatizo kubwa sana katika nyanja zote za maisha, ikiwa ni pamoja na ustawi wetu wa kiroho.
➡ Kwa sababu hizi, ni muhimu sana kufuata kanuni muhimu za kujifunza maandiko ili kuwa na ujuzi na uelewa wa kina juu ya maandiko ambayo tumeletewa na Mungu wetu ili yatuongoze. 
KANUNI MUHIMU ZA USOMAJI MAKINI
I. VIFAA MUHIMU KWA USOMAJI MAKINI WA MAANDIKO.
Ili kuwa na usomaji makini mtu anahitaji vifaa kadhaa ambavyo vitamsaidia kuelewa vizuri maandiko. Hapa nitataja na kuongelea vifaa vichache tu ambavyo ni vya msingi tu.
1. Biblia yenyewe

➡ Kanuni kuu ya usomaji makini wa maandiko ni kuwa Biblia inajitafsiri yenyewe. Msomaji makini wa maandiko anapaswa kufanya utafiti wa kina ndani ya biblia yenyewe kabla hajakwenda nje kutafuta ufafanuzi wa ziada. Maandiko yanasema “Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni, huku kidogo na huku kidogo” Isaya 28:10
➡ Ni muhimu kuwa na matoleo tafauti ya biblia, kwa mfano uwe na toleo la biblia la union, Kiswahili cha Kisasa n.k. Kama unajua Kiingereza ni muhimu pia kuwa na matoleo yake. Hii ni kwa sababu lugha za asili zilizotumika kuandika biblia siyo lugha zetu za sasa kama Kiswahili na Kiingereza. Agano la Kale liliandikwa kwa Kiebrania, na Agano Jipya liliandikwa kwa lugha za Kiaramu na Kiyunani, hivyo tafsiri za baadhi ya maneno zinaweza kuwa na utofauti kiasi fulani na ile lugha ya asili. Hii ni kawaida katika lugha. Kwa hiyo unaweza kuhitajika kulinganisha matoleo tofauti ili upate maana na ujumbe halisi wa aya husika.
2. Kamusi ya biblia. 

➡ Kamusi ya biblia inatoa maana ya maneno na uchambuzi wa kina wa majina (ya watu, miji na nchi) yaliyoandikwa katika biblia. Ufafanuzi huu unampa msomaji ufahamu wa kina juu ya mada, watu au mahali husika.
3. Bible commentaries – maelezo ya kitaaluma ya biblia.

➡ Vitabu hivi vinasaidia kupata ufafanuzi wa kiteolojia wa aya za biblia.
4. Itifaki ya biblia (Bible concordance)

➡ Itifaki inamwezesha msomaji kujua mafungu mengine ya biblia yanayofanana na yale anayosoma. 
4. Atlas (ramani).

➡ Ramani inamsaidia msomaji kujua mahali panapoongelewa katika maandiko. Kwa mfano Yohana 4:3-4 “aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya. Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria”. Ukiwa na atlas ya biblia itakuonyesha sehemu zote hizi na kukupa picha nzuri ya safari hii aliyofanya Yesu na mahali panapoongelewa.
II. MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOSOMA MAANDIKO

Unaposoma aya za Maandiko zingatia sana kuelewa yafuatayo:
➡1. Mlengwa alikuwa nani?

➡2. Muktadha: Mazingira na utamaduni wa mwandishi na waandikiwa.

➡3. Wakati kitabu au aya hiyo ilipoandikwa.

➡4. Soma aya nzima siyo fungu moja tu upate upana wa mada inayoongolewa.

➡5. Linganisha fungu moja na lingine, mwandishi mmoja na mwingine. Kumbuka kuwa biblia haijipingi, ukiona kama inajipinga jua kuwa ni wewe hujaelewa. 

➡6. Fahamu uelewa wa mambo wa wakati huo. Kwa mfano, mwandishi wa Ufunuo 5:11 anatumia maneno “hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu” kuelezea wingi wa watu aliwaona. Anatumia maneno haya kwa sababu wakati huo hawakuwa na ufahamu wa kuhesabu zaidi ya makumi elfu. Hawakuwa na neno kama vile, milioni, bilioni n.k. Hata sisi leo bado tuna kikomo cha kuhesabu.
7. Aina ya uandishi. 

➡ Je, ni Ushairi – Methali au ni kitendawili? Ni mfano – halisi au wa kufikirika? Je, ni unabii – yaani mafumbo ya unabii? au ni historia?

➡ Kumbuka kuwa vitabu vya Biblia havikupangwa kulingana na kwamba ni kipi kilianza kuandikwa bali kutokana na aina ya uandishi. Kwa mfano, vitabu vya Ezra, Nehemia na Esta viliandikwa baadaye sana baada ya nabii Isaya, Yeremia na Danieli lakini katika mtiririko vimewekwa kabla ya vitabu vya manabii hawa na hata kabla ya Zaburi na Mithali.
8. Elewa kauli. 

Je, aya hii ni amri, ushauri, agizo, au ni maelezo ya kihistoria tu, au ni unabii? 

➡ Watu wengi hawatofautishi kati ya vitu hivi. Kwa mfano kati ya amri na maelezo ya kihistoria, kati ya maagizo yaliyoishia kipindi fulani na amri za kudumu wakati wote. Haya ni makosa makubwa kabisa ya uelewa.
➡ Hili ni muhimu sana – msomaji makini anapaswa kutofautisha amri au unabii na maelezo ya kihistoria. Huu ni usomaji makini. Tunapaswa kuelewa haya.
9. Matumizi maishani (Application).

➡ Msomaji makini anapaswa kutafakari kwa kina juu ya aya anayoisoma. Je, ina ujumbe gani? Ni nini anachojifunza kutoka katika aya hiyo? Zaidi sana jifunze kuishi sawa sawa na neno hilo ulilojifunza.
HITIMISHO

➡ Kuna kanuni zinazoongoza usomaji makini wa Maandiko. Msomaji asipofuata kanuni hizi za msingi bila shaka atakuja na uelewa tofauti na hawezi kuwa na uelewa wa kina wa mada za maandiko. Mungu amewaahidi kuwapa Roho wake Mtakatifu ili awaongoze na kuwaelimisha wale wote wanaotumia muda wao kujifunza maandiko. Karibu sana ndugu yangu mpendwa katika mtiririko wa tafakari hizi ili sote tuendelee kujifunza mada muhimu toka katika maandiko kadri Mungu atakavyotupatia uzima huu.
➡ Pamoja kanuni zote hizo kutumika, msomaji anapaswa kuomba uongozi wa Roho Mtakatifu kabla ya kuanza usoma neno la Mungu.
MUNGU AKUBARIKI SANA UNAPOTAFAKARI SOMO HILI NA KUFANYA UAMUZI.

HONGERA KWA KUOKOKA.

*1⃣SEMINA YA NENO LA MUNGU UWANJA WA PEOPLES SINGIDA MJINI NA MWL MWAKASEGE*

*SOMO* MWONGOZO WA KIBIBLIA WA KUTAFSIRI NA KUOMBEA NDOTO*

*TAR 4 JULY 2017*

*SIKU YA KWANZA.*

KITABU CHA HONGERA KWA KUOKOKA  👇👇👇
https://drive.google.com/file/d/0BxdP6mgDJWByVERtampLTGZWRms/view?usp=drivesdk 

*MAOMBI*
Mungu wetu uliye hai tunakushukuru mno kwa nafasi uliyotupa siku ya leo ili tufanye kile ambacho unataka tufanye chini ya uongozi wako wa Roho wako Mtakatifu. Ahsante kwa ajili ya neema hii uliyonipa kusimama tena katikati ya kusanyiko la watu wako, na wateule wako na watoto wako. Unijalie ee Bwana katika neema hiyo kusema kile ninachotakiwa kusema, kufundisha kile ninachotakiwa kufundisha. Ufahamu na ufunuo kutoka kwako sawa sawa na makusudi yako ili katika neno hili ee Bwana Upate mavuno, matunda na watu wako wakakuone Wewe sawa sawa na neno lako. Heshima ni za kwako na watu wote tuseme Ameeen.

Bwana Yesu asifiwe! Kichwa cha somo tulichonacho katika semina hii kinasema.

*MWONGOZO WA KIBIBLIA WA KUTAFSIRI NA KUOMBEA  NDOTO*

LENGO KUBWA LA SOMO HILI NI
Kuimarisha uhusiano wako na Mungu katika Kristo Yesu.

Lengo la somo hili sio kukufundisha juu ya ndoto, ila ni kutumia mafundisho ya ndoto yaliyoko ndani ya Biblia kuimarisha uhusiano wako katika Kristo Yesu. Kumbuka hilo litakusaidia kadri tutakavyokua tunaendelea ili uweze kuona na kutathmini wewe mwenyewe kwamba kwa kadri semina inavyoendelea inaelekea jinsi Mungu anavyotaka kuona kama kila tunapojifunza kila siku kuna namna fulani yakusogea kwa Mungu  zaidi katika Kristo Yesu.  Pamoja na kwamba utajifunza mambo kadha wa kadha juu ya ndoto lakini bado Mungu alichokusudia ni zaidi ya hicho.

Bwana Yesu asifiwe! 
Na leo ni siku yetu ya kwanza na Mungu atatuongoza katika kile anachotaka tuangalie.

Fungua na mimi katika kitabu cha Mwanzo 41;1-8 “1 Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto; na tazama, amesimama kando ya mto. 

2 Na tazama, ng’ombe saba wazuri, wanono, walipanda kutoka mtoni, wakajilisha manyasini. 3 Na tazama, ng’ombe saba wengine wakapanda nyuma yao kutoka mtoni, wabaya, wamekonda, wakasimama karibu na wale ng’ombe wengine ukingoni mwa mto.4 Kisha hao ng’ombe wabaya waliokonda wakawala wale ng’ombe saba wazuri, wanono. Basi Farao akaamka. 5 Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema. 

6 Na tazama, masuke saba membamba, yamekaushwa na upepo wa mashariki, yakatokeza baada yao. 7 Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu. 8 Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo. 
Alafu nitasoma ule msitari wa 14 mpaka wa 16 alafu nitakupa maelezo  sawasawa na Roho Mtakatifu atavyoniongoza.
Msitari wa 14 unaendelea unasema

14 Ndipo Farao akapeleka watu, akamwita Yusufu, wakamleta upesi kutoka gerezani. Akanyoa, akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao. 15 Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri. 16 Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani. 
Kadri ninapopata nafasi ya kufundisha hili somo, ninashangaa kwamba bado hatumalizi kila kitu ambacho Mungu ameweka ndani yangu. Sijajua atakiachilia mpaka lini kwa staili hii, tumekuwa tukifundisha hili somo karibu kwa mfululizo karibu miaka miwili sasa, Sehemu hii tulikuwa hatujalifundisha kwa undani, lakini tumefundisha maeneo tofauti tofauti siku zingine siku nane na hatujamaliza na si kitu ambacho nilitegemea Mungu angenipa kukifundisha kwa sababu wakati Mungu alipokua anasema nami kwa njia ya ndoto  na kwa njia ya maono mbalimbali, alipokua ananiita kwenye utumishi na sikujua kitu cha kufanya na sikujua nitapata wapi tafsiri kama vile ilivyokua kwa farao na mimi nilitafuta waganga ambao wanaweza wakafasiri ndoto nikaenda nikatafuta wanieleze maana yake nao wakajaribu kueleza maana yake  baadae nilipokuja kupata maana ya hizo ndoto ndani ya Biblia nikaona kuna vitu vilikuwa vimepungua katika tafsiri yao na hawakutaka kukubali kwamba hawajui, afadhali hata wao waganga waliokuwa wanamzunguka farao walikua na ujasiri wa kukiri ya kwamba hawajui, lakini mimi niliokutana nao wakasema mimi ninajua.

Wakajaribu kunitafsiria na nikajaribu kutafuta vitabu vinavyotafsiri ndoto nilishangaa sana wakati ule sikuona kitabu cha kikristo kinachoweza kumsaidia mkristo akaweza akatizama ndoto kibiblia lakini  pia sikuona kitabu ambacho kinamsaidia mtu ambae  hata sio Mkristo kiweze kutafsiri ndoto kiusahihi kibiblia, Maana tafsiri ziko nyingi za ndoto na si zote zinatoka kwa Mungu kama tutakavyokua tunaendelea kuona.

Na ilinisumbua pia kuona kwamba hayo mafundisho hayakuwepo kanisani wakati ule, Sijajua kama kwenye kanisa lako mnapata mafundisho ya staili hiyo sijui. Lakini miaka ile ya 80 kule mwanzoni tulipokua tunaokoa na sehemu nilipokua ninasali na kuenda hata baada ya kukoka sikupata mafundisho ya kunisadia kwenda hata ndani ya Biblia ili niweze kujua Mungu anazungumza nini juu ya ndoto.
Na ilinichukua muda nilipoanza kumlilia Mungu kutaka kujua maana kuna vitu viko ndani ya zile ndoto ambazo zingenisaidia na sikuwa na mtu wa kunisaidia kuvitoa kule ndani niweze kupata na katika kukimbizana na Mungu usiku na mchana nikitaka kujua,
Na katika kusoma Biblia ghafla Mungu akaanza kunipa ufahamu kidogokidogo  juu ya ndoto ambazo zilinisadia kujua  vitu vingi sana ambavyo Mungu alikua ananisemesha juu ya wito ambao ametuitia na bado anaendelea kutufundisha mpaka leo, siwezi kukwambia najua kila kitu, 
Najua vitu vingi lakini sijui kila  kitu na katika hivyo vitu ambavyo Mungu amenipa kuvijua ameniruhusu kuanza kufundisha hivi karibuni miaka kadhaa kama miwili mitatu hivi na nitaenda nalo taratibu kadri Mungu anavyonipa niweze kulifundisha kwenye maeneo tofauti tofauti.

Bwana Yesu asifiwe.
Kwahiyo ninataka nikueleze hiyo kitu ili uweze kufahamu hiki kitu kilitokea wapi na Mungu anaporuhusu kidogo na kujifunza uweze kuelewa maana yake nini. Katika siku hii ya kwanza kwa kusoma hizi ndoto mbili za farao nataka kuzungumza na wewe kama vitu vinne tu vya utangulizi ambavyo ni …

*GHARAMA AMBAZO ZINAWEZA ZIKAMPATA MTU KWA KUTOKUJUA KUTAFSIRI NA KUIOMBEA NDOTO KIBIBLIA*

Kwahiyo kwa lugha  ya kawaida tungesema gharama ambazo zingeweza kumpata Farao haijalishi ni kiongozi, haijalishi ni mtu wa kawaida, mchukulie farao katika ngazi hizo mbili, Farao kama kiongozi Farao kama mtu wa kawaida kabisa kuna gamharama ambazo kama asungepata tafsiri sahihi hizo gharama zingekuja kwenye maisha yake,
Ziko nyingi lakini nimeona nikuwekee mtaji kidogo wa mahali Roho mtakatifu anataka  tuendelee.

Ya kwanza
1.KUTOKUJUA KILICHOKUSUDIWA KITOKEE KATIKA MAISHA YAKO.

Sasa tuna tizama picha ya farao lakini nataka uone huu ujumbe kama ni ujumbe wa kwako binafsi.

Mwanzo 41;28 na 32
Msitari wa28 unasema hivi

28 Ndivyo nilivyo mwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu. 

Mwanzo 41 :28

Angalia huo msitari vizuri
Huyu ni Yusufu anaongea, sasa angalia msitari wa 32
32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi. 

Mwanzo 41 :32

Kwahiyo kama unaota ndoto inajirudia ,.kuna sababu nyingi lakini sababu mojawapo ni hiyo hapo kwamba hicho kitu unachokiona kwenye ndoto kitatokea sasa  usipojua namna ya kuomba kisitokee hilo ni jambo lingine  tutalizungumza polepole,
Lakini ni njia moja wapo ya kukwambia ya kwamba kitatokea.

Angalia kile kitabu cha 
Ayubu 33:14 – 15

14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. 15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; 
Kwahiyo ndoto ni njia mojawapo ambayo Mungu anasema na mtu na usiposikia katika ndoto ya kwanza anakuletea ndoto mara ya pili, hiyo ni Ayubu sura ya 33 msitari wa 14 na 15, kwahiyo anakurudishia mara ya pili, saa nyingine hata mara ya tatu,
Saa nyingine hata mara ya nne.
Ndoto inajirudia, inaweza ikajirudia kwa kufanana inaweza ikajirudia kwa tofauti  kidogo kama vile ambavyo unaona ya farao ilivyojirudia unaona katika ndoto ya kwanza kuna ngombe na ndoto ya pili  kuna masuke, ukiitizama unaweza kufikiri ni ndoto mbili, 
Lakini hizo ndoto zina ujumbe unaofanana ukiendelea kujifunza namna ya kutafsiri ndoto ni rahisi sana  kuona kitu cha namna hiyo, saa nyingine wanaponiambia nimeota ndoto hii, nimeota ndoto hii saa nyingine inaweza jirudia usiku huohuo, anasema nikalaa alafu nikaota tena ndoto nyingine alafu nina mwambia hiyo ni ndoto moja, ina ujumbe unaofanana alafu namweleza ujumbe ulioko.

Saa nyingine mtu anaweza akaota usikiu huo akaota ndoto moja akakaa saa nyingine siku nyingine akaota au baada ya wiki mbili tatu akaota tena akiweza kunieleeza hizo zote mbili saa nyigine ninaona kabisa ndani yake, namwambia aanhaa hii ndoto inafanana na ile ya kwanza inamaanisha kuna kitu ambacho hukuona kwenye ile ya kwanza, 
Mungu anajaribu kukusemesha tena kwa sababu ndivyo Bilia inavyosema ya kwamba atakusemesha mara ya kwanza, mara ya pili hata kama hujali,

Huyu ndugu anaeitwa Farao alipoamka angalia kitu alichotoka nacho USIKU, Biblia  haitu ambii ni saa ngapi aliota ndoto, alipo ota ndoto akaamka akalala akaota tena ndivyo msitari wa tano unavyo tuambia

5 Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, 
Aka amka akalala akaota ndoto mara ya pili hiyo inahusu masuke, alipoamka Biblia inasemaje, alidharau akasema kumbe ndoto tu.
Na kama vile unavyoota ndoto alafu na wewe mwenyewe unasema afadhari kumbe ndoto  tu unaiacha hapo mpaka asubuhi alipoamka roho ikafadhaika ambayo nitakueleza maana yake nini baadae,lakini nilitaka uone ya kwamba kuna kitu ambacho Mungu alikua amekikusudia kwa ajiri ya eneo lile a dunia wakati ule, si tu kwa  ajiri ya misri, lakini pia  unaweza  uka fuatilia kwenye Biblia utagundua ya kwamba mpaka nchi za jirani zilipata shida ya namna hiyo, na kama  unasoma Biblia yako vizuri utagundua ya kwamba alipoota ndoto ilichukua miaka saba ndipo njaa ikaja, kwa sababu kwenye chakula kingi asingeshituka, 

Lakini ile njaa iliyokuja baada ya miaka saba ya shibe ile ndio iliomshtua , ile ndio kwahiyo miaka saba ya shibe si rahisi sana ukaona lakin Mungu alikua anajaribu kuzungumza nae vitu vita kavyokuja baadae, hata Yusufu ndicho alichonwambia anasema Mungu  anazungumza na farao atakayoyafanya hivi karibu sasa “ hivi karibu” ni miaka saba ijayo lakini unaona kabisa kipindi cha chakula kilianza mara moja.

Kwahiyo  kama Mungu anatumia ndoto kama ni mojawapo ya kukusemesha juu yakitu kinachokuja mbele yako na kama usipojua tafsiri yake, kama ni ndoto inayojua.moja kwa moja na tafsiri yake, kadri tutakavyokua tunaona kuna ndoto zingine zinakuja zina tafsirinmoja kwa moja huhitaji kufuatilia wala mahali pengine popote inazungumza moja kwa moja 

Angalia kile kitabu cha 

Mathayo 1: 18-24 18 Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 19 Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri
20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao. 
22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema, 23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi. 24 Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe; 
Nilitaka uone ya kwamba  hii ndoto haikuhiataji tafsiri ilikua na melekezo moja kwa moja, Haikua na mafumbo ndani haikua na fumbo lolote ndani ni maelekezo moja kwa moja,
Sasa ziko ndoto za namna hii lakini ziko zingine zina mafumbo yake na usipojua namna ya kufahamu utakosa kitu kikubwa sana k kilichoko mbele yako.

Gharama ya pili.
2. KUTOPATA MSAADA WA MUNGU KWA AJIRI YA KUJIANDAA JUU YA ULICHOOTA

kitabu cha 
Mwanzo 41: 31 na 3433 Basi, Farao na ajitafutie mtu wa akili na hekima amweke juu ya nchi ya Misri.Mstari wa 34a  Farao na afanye hivi

Nilitaka uone hilo “Farao na afanye hivi” akapewa maelekezo pale ya kitu cha kufanya, sasa cheki uelewe vizuri  hayo maelekezo hayakuwepo ndani ya ndoto  kwa kuota, yalikuweko ndani ya ndoto kama ujumbe , ujumbe utaupata tu saa wakati unatafsiri kama umefichwa.

Gharama ya tatu ni hii 
*3. KUNA UWEZEKANO MKUBWA KWA KUYUMBISHWA IMANI YAKO*.

Kumbukumbu la Torati 13:1-4 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda BWANA, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. Tembeeni kwa kumfuata BWANA, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye._

Sasa unaweza ukaendelea kusoma hapo. ila Ngoja turudi Mwanzo 41: 8 “Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo”.

Kwanini Farao aliwakimbilia waganga, ni kwa sababu walikuwa wamejihudhurisha mbele katika jamii kuwa wanaweza wakatafsiri ndoto. na kwa nini aliwafuata wenye hekima ni kwa sababu walijihudhurisha mbele ya jamii kuwa wanaweza wakatafsiri ndoto. Wakina Yusufu waliokuwepo lakini walikuwa gerezani  na yule ambaye alikuwa anajua habari za Yusufu yaani mnyweshaji wa mfalme  alipotafsiriwa ndoto yake akiwa jela na alipopata nafasi ya kurudi  akasahau. Ametoka jela na amerudishwa kwenye nafasi yake sawa sawa na alivyotafsiriwa na Yusufu akasahau.

Biblia inaanza kwenye Sura ya 41 Kitabu cha Mwanzo “ Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto”  ina maana katikati ya wale watu walioota wakiwa gerezani ili kuwajulisha ya kwamba kuna mwingine ana roho ya Mungu  anaweza akatafsiri kwa katika nchi ya kwenu .Ilipita miaka miwili na alinyamaza kimya.

Mpaka pale waganga na wachawi na wenye hekima waliposhindwa kutafsiri ndipo unamuona yule Mnyweshaji  alisema sasa nimefahamu kosa langu  na ndicho alichosema. Angalia ule mstari wa 9 Kitabu cha Mwanzo 41 “Basi mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu leo”. Lakini ilipita maika miwili.

Tatizo la kutafsiriwa ndoto na mtu wa imani nyingine  haiko kwenye tafsiri bali ilo kwenye ujumbe. Ngoja nijaribu kusema tena nasema hivi “Tatizo  la kutafsiriwa ndoto na mtu ambaye ni wa imani nyingine tatizo halipo kwenye tafisiri balo kwenye ujumbe.

Yalinipata mimi haya wakati Mungu alipokuwa ananisemesha Mwanzoni kabisa sitakuja sahau. Niliota ndoto niko ndani ya chumba,  akaja mtu akapita kwenye mlango na namtazama mimi nimekaa kwenye kiti na akaja kwangu moja kwa moja amevaa nguo nyeupe ndefu, saa hiyo sijaokoka aliponisogelea akatoa mkono wake na nilipotazama ulikuwa na jiwe jeupe alafu akaning’iniza ilikuwa na kamba , ilikaa kama yai lakini niliona kama ni jiwe. Akaleta moja kwa moja  kama vile anataka kunipa na kwa hiyo nilikunjua mikono yangu kama vile nataka kupokea. Akataremsha lile jiwe  karibu mpaka linanifikia akanyenyua juu alafu akanitazama  akasema “dhambi zimezidi duniani”. Akageuka  kueleka mlangoni nikaamka

Nilipoamka ile ndoto ilinifadhaisha, sasa cheki mahali nilipoenda nilikimbilia moja kwa moja kwa mganga na yule mganga alikuwa wa imani nyingine. Nilipofika nilimueleza  na alikuwa ni mtu Mzima kabisa nikamwambia mzee “Nimeota ndoto na ile ndoto imenisumbua sana” kwa hiyo nikamsimulia ile ndoto na akanitazama, akaniambia yule aliyekuja alikuwa ni malaika  na lile jiwe ni tuzo kwa ajili yako na hawezi kukupa si kwa sababu duniani dhambi zimezidi bali ni kwa sababu wewe  ndio umezisha dhambi.  Sasa nikamuuliza kuwa “sasa ndio nafanyaje”?.  Sasa sikia, hana namna ya kunielekeza kwa Yesu, sasa akaanza kunifundisha kutubu kwa dini yao. na ilikuwa ni shule kabisa alifundisha kutubu, na yale maneno siwezi kusema hapa na sijayasahau mpaka leo. Biblia inasema si kila mwotaji wa ndoto,hata yale mambo  aliyo yaota na yametukia. Usikimbilie kusema haa hii kitu ni sahihi. Biblia inasema cheki ujumbe unaokuja unakuleta karibu na Mungu katika Kristo Yesu au unakupeleka mbali?.  Kama unakuwa mbali biblia inasema usiyasikilize maono ya muotaji wa hiyo ndoto na hata kwako wewe mwenyewe.  Imenichukua muda mrefu sana nikihangaika sana nikaja nikaokoka baadae  na nikaanza kuomba Mungu anioneshe kwa kuwa alikuwa ananionesha kitu gani. Baadae nikaja nikakuta ndani ya biblia  iko “Yeye ashindaje nitampake jiwe jeupe” Kasome biblia yako. utaona iko kwa  Barua kwa kanisa la Peligramo andika ..na jina ambalo hakuna anayejua  na nitampa jina jipya

“Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea” Ufunuo wa Yohana 2:17
kwahiyo ina maanisha ningekuwa na mtu wa kunieleza kanisani nisingeenda kwa mganga. kama haya mambo ninayokueleza ningefundishwa kanisani  au Jumapili au kwenue bible study au mahali popote  ingenisaidia. Lakini sikuwa na huo msaada na msaada uliokuwepo ni waganga.  Na unaweza ukoona kabisa shida sio tafsiri bali shida ni ujumbe maana kulikuwa hamna namna anaweza kunileta kwenye toba  kwa Yesu. Hana namna ya kunileta kwenye toba kwa Yesu kwa hiyo hakunileta kwa Yesu  bali alinipeleka kwenye toba ya kwao. Ahsante Yesu kwa sababu neema ya Mungu ilinikamata na sikuzamia huko. Lakini watu wengi sana wanazamia huko na hiyo ndiyo inayowavuruga  katika sehemu mbali mbali na imani yao. Bwana Yesu asifiwee.

Okay, ninapoandika kwenye notes zangu na ninaposoma habari za Farao, na habari ya kuyumbishwa nimeiweka kwenye (mabano) kwa sababu Farao alikuwa na imani ja wachawi na waganga na miungu yao na Mungu akamletea ndoto. na Mungu hakumletea ndoto Yusufu bali alimletea Farao  kwa sababu ndoto ilimhusu Farao. Lakini sasa Mungu  hawezi akaruhusu huyo mganga awe na vyote viwili. Yaani kutafsiri na kutoa ujumbe. wakanyimwa vyote viwili yaani tafsiri na ujumbe.  Nia yake Mungu ni kitu gani alikuwa anatafuta ni kumuondoa Farao  kwenye imani yake kwa waganga  ili amtafute Mungu aliyehai. na kwa sababu hiyo ilibid lazima amlete mtu mwemye Roho wa Mungu.  Na Yusufu alijua ili asijeaweke imani yake kwa Yusufu  alipoambiwa kuwa nasikia wewe ukisimuliwa ndoto unaweza ukatafasiri kwa hiyo nimeona nikusimulie ndoto ili uweze kutafsiri. lakini Yusufu alijibu “Yusufu akamjibu Farao, akisema, *Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani” Mwanzo. 41:16.

Ili ajue ya kwamba yuko Mungu na ilibidi aelekezwe macho yake kwa Mungu  kitu gani kilitokea. ilipofika anaambiwa tafuta mtu mwenye akili atakaye simamia masuala haya na maelekezo haya. Farao alisema “Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake”Mwanzo. 41:38

Ina maanisha aligundua wale wachawi na waganga waliokuwa wamemzunguka  kuna vitu walivyokuwa wamepungukiwa.  na walijua kuwa watu wengine wana Roho wa Mungu  ambao wanaweza mumsaidia. inaweza ikawa ni ngazi  ya familia yako inategemea  umejizungushia watu gani wa kukusaidia. Unaweza ukaona nilikuwa nimezungushiwa watu gani wa kunisaidia na saa hiyo nilikuwa  chuo kikuu. na watu wengi sana wamepotea kwa sababu hiyo  kwa sababu hakuna msaada wa kibliblia wa Mungu   wa moja kwa moja unaosema kuwa haya masuala ni halisi na yanaweza yakavuruga imani za watu. Bwana Yesu asifiwe… Ngoja nikueleze jambo la nne.

Gharama ya nne.
4.KUTOKUJUA UOMBEJE AU UNAOMBAJE JUU YA KITU  KILICHOKUJA AU KITAKACHO KUJA NA NDOTO AMBACHO KINAWEZA KUGUSA ROHO, NAFSI AU MWILI WAKO.

Daniel 2  katika sura hii tunamuona Nebukadreza akiota ndoto na mbaya zaidi aliota ndoto  iliyomsumbua na alipoamka asubuh akawa amesahau. Na alipoamka  kama kawaida akawa ametafuta waganga na wachawi waliokuwepo  Babeli wakati ule. Katikati ya watu wenye hekima  wakina Daniel walikuwepo.  Bahati Mbaya sana wale waganga na wachawi walipoitwa mbele ya mfalme kwa ajili ya kutafsiri ndoto akina Daniel hawakuitwa. Walipofika pale Nebukadreza aliwaambia nimeota ndoto naomba tafsiri nao wakasema tueleze ndoto. Akasema nimesahau na akawaambia mnieleze ndoto niliyoota na tafsiri yake. wakamwambia hamna kitu cha namna hiyo. wakamwambia tueleze ndoto uliyoota na sisi tutakupa tafsiri yake.. akasema msifanye mchezo  nataka mnieleze ndoto niliyoota na tafsiri yake lasivyo ntawashughulikia ninyi na familia zenu. Ntawaua kabisa akasema lazima mniambie ndoto niliyoota na tafsiri yake , lakini wao walimwambia  hapana hii haiwezekani ni miungu peke yake ambayo haikaagi na wanadamu. Sisi tunachoweza ni kuwa tueleze ulichoota tutakutafsiria .Kasome biblia yako ilitolewa amri wauawe  . Ilipotolewa amri yule askari  wa Nebukadreza  aliyepewa amri ya kwenda kuwaua biblia haisemi ila kwa namna fulani alienda kwa Daniel. Kwanini  hakuanza mara moja na kuwaua, ila biblia haituambii  ila tunaona alienda kwa akina Daniel kuwambia kuwa na wao wako kwenye list ya kuuawa  kwa sababu walikuwa kwenye ngazi ya wenye hekima. Daniel aliuliza hii hasira kali ya mfalme namna hii imetoka wapi? tumekosea nini. Si ndio akaelezwa  baada  ya kuelezwa sasa.. soma hapo chini👇👇
Daniel 2:16-18 “Basi Danieli akaingia, akamwomba mfalme ampe muda, kisha yeye atamwonyesha mfalme tafsiri ile.  Ndipo Danieli akaenda nyumbani kwake, akawapasha habari kina Hanania, na Mishaeli, na Azaria wenzake; ili waombe rehema kwa Mungu wa mbinguni kwa habari ya siri hiyo, ili kwamba Danieli na wenzake wasiangamizwe pamoja na wenye hekima wa Babeli”
Ninachokataka nikuoneshe hapa ni kuwa akina Daniel waliijua siri ni kuomba na Katika kuomba kunahitaji muda kwa hiyo ni lazima utenge muda  wa kuombea ndoto unazoota. wengi sana wanazidharau ndoto  wanazoota na hawajajua kitu kilichoko ndani yake. Tunaona Daniel akiongea na wenzake akisema “tupe muda” na ukitaka kujua mkono wa Mungu ulikuwepo pale tunaona hasira yote ya mfalme ilitulia  maana angeweza kusema kama mmeshindwa kunitafsiria  na angemwambia yule askari wake  kuwa maliza hawa jamaa hawahitaji muda  ndio maana wana hekima, ndio maana ni waganga na ndio maana ni wachawi.  wauawe  lakini Daniel alienda akiwa amefunikwa na nguvu za Mungu  akamwambia mfalme naomba muda. Ulikiwa ni muda wa kufanya nini? ulikuwa ni muda wa kwenda kuombea ile ndoto. Hakumwambia kila mtu bali alitafuta wenzake wawili watatu ambao walikuwa na mzigo pamoja na yeye na wanaweza wakaomba. Na aliwashirikia ili waombe ukiendelea kusoma utaona biblia inasema “Mungu akawajibu kwa njia ya ndoto na Mungu alimwaotesha Daniel ndoto ile ile ambayo  Nebukadreza aliota lakini hakuishia hapo alimpa na tafsiri yake na ujumbe uliokuweko ndani yake.Bwana Yesu asifiwe.. haleluyaa haleluyaa.

Ni nidhamu ngumu kidogo  lakini ukiendelea nayo itakusaidia. unaona hii shida kwa Farao pia, Hakimbilii kuomba bali anakimbilia kutafuta tafsiri. Ni watu wengi mpaka leo wakiota ndoto hawakimbilii kuomba  bali wanakimbilia watafsiri  na si kila mtafsiri atakueleza sahihi, si kila mtafsiri atajua tafsiri na si kila tafisiri utapewa na ujumbe  saa hiyo hiyo zingine unapewa ujumbe saa hiyo hiyo mtu anakueleza na Mungu anakupa ufahamu saa hiyo hiyo. Lakini zingine inabid ung’ang’ane uombe  mara ya kwanza mara ya pili. Zingine zinanichukua  hata wiki nzima ninaomba juu ya hiyo ndoto kila siku baada ya wiki ghafla ninapata unaweza ukafikiri ni kama mtu fulani hivi kanishushia  kitu ndani na napata ufahamu kabisa  kuwa ni kitu gani kiko ndani.Lakini unahitaji nidhamu ya kibiblia.

wewe unafikiri ni kwa nini Farao alipoamka aladharau ndoto na alisema “Kumbe ndoto  tu”.Kitu gani kilitokea, kulipokucha asubuhi roho yake ikafadhaika. ile ni roho iliyokuja na ndoto  na ni ndoto ambayo imekuja na roho wa Mungu  uwe na uhakika roho Mtakatifu anaingia ndani  na haondoki mpaka au umepata au umekataa kwa hiyo ile kumfadhaisha  kuwa asiidharau hii ndoto imekuja kwa ajili yake. Hiki kilikuwa ni kiashiria kilichokuwa kinamsukuma  yeye kutafuta uso wa Mungu. sasa yeye kilipomjia alitafuta watu badala ya kutafuta uso wa Mungu. sasa *Najua si nidhamu ambayo watu wengi wanaipenda*  lakini nataka nikusidie maana unaweza ukaja ukakaa mahali ambapo hutakuwa na mtu wa kumuuliza  na  au utamwambia na atakuambia kuwa sijui. Sasa unaweza jikuta umepoteza ujumbe mkubwa sana kwa ajili yako, na kwa ajili ya familia yako na usijue kitu cha kufanya. 

Hata kama ndoto ibilisi kaipenyeza kama tunavyoona katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 13 :1-3 .Usije ukafikiri  kuwa ukienda mahali pengine penye msaada wa roho kipepo ambayo inatoa tafsiri usije ukafikiri kama ulivyoambiwa kwenye kitabu cha kumbu kumbu la Torati kuwa chunga ujumbe unaopewa. utabaniwa tu hapo na utaelezwa tafsiri yake na utabanwa kisawa sawa  ni Roho Mtakatifu peke yake ndiyo anaweza akakusaidia .Bwana Yesu asifiwe….

Kuna mtu mmoja aliponisikia nafundisha mahali aliniandika ndoto akisema “ Mwalimu  nimeota ndoto na nipo kwenye shehere na hiyo shehere ina chakula kingi sana kimefunikwa na kitambaa juu, juu ya kile kitambaa kulikuwa na fuvu la kichwa na kikafunuliwa kile chakula na watu waliokuwepo pale wakala kile chakula na yeye. Pamoja na kwamba kile chakula hakikuwa kitamu  mdomoni lakini nakumbuka tu nilikula. Lakini kile kitambaa kilichokuwa juu yake  kilichokuwa na picha ya fuvu la kichwa sijakisahau. basi akaamka kutoka ndotoni na hakuja kitu cha kufanya .Huyu mtu aliyeota ndoto  hakumaliza hata mwezi kiu yake ya kwenda kanisani iliisha, hamu ya kuomba ikaisha, Kiu ya kusoma biblia iliisha na hakujua kuwa ni matokeo ya ndoto  ile mpaka aliposikia nikifundisha somo hili la ndoto.  alafu akaniambia tena baada ya miezi kadhaa tena kupita akaota ndoto nyingine.

Sasa  amewezaje kuunganisha ndoto zingine na inamaanisha hapa katikati aliota tena ndoto nyingine  akaota mtu kaja na damu anataka kumnywesha kwenye ndoto  akakataa. na sasa aliniuliza Mwalimu sasa ndio naombaje sasa maana hizi ndoto zinanitesa.

Na niliposoma nilielewa mara moja maana yake nini na yote  hiyo ni kwa sababu nimesoma kwenye biblia na kujua maana yake nini. 

Kwa sababu kile chakula hakikuwa sherehe ya kawaida. Mungu alikuwa anamuonesha katika ulimwengu wa roho kitu kinachosukwa na adui kwa sababu si kila chakula unachokula kwenye ndoto ni kizuri. kuna chakula cha kipepo, kuna chakula ambacho kinaweza kikawa kinakuonesha juu ya agano  lililoko au mpango wa adui kukuingiza kwenye agano. Biblia inasema mtu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Bwana. kwa hiyo ina maanisha  ambacho unaweza ukapewa na kikavuruga imani yako. na Mungu anakuonesha  kuwa kuna kitu katika ulimwengu wa roho umepewa na ni kitu kinatokea.Bwana Yesu asifiwe.. 

Kilichomsaidia wakati wameona ameanza kukwepa  kwenda kanisani walijua amepoa kabisa  kwa hiyo walimtetea damu ili wamwingize kwenye agano  kwa sababu ile damu angekunywa ingemuingiza kwenye agano. unasema unapata wapi ipo kwenye biblia,  Yesu alisemaje  “Damu mnayo kunywa ipo kwenye  agano”.Ahsante Yesu alikataa, na zile ndoto zilimpitisha mahali pagumu kidogo  maana zile ndoto zilikuwa zinafanana.

nilienda mahali pengine mwingine aliniambia kuwa “Mwalimu nimeota ndoto na kuna chakula nimekula, sikutaka kula kile chakula na wamenilazimisha kula kile chakula  na nikamuuliza kimetokea kitu gani baada ya kuota hiyo ndoto.  alisema siwezi kuomba kanisani naenda na sielewi kile wanachofundisha kanisani. Nikamwambia weka mkono wako juu ya kinywa chako na nilipoachilia damu ya Yesu pepo likalipuka ndani yake saa hiyo hiyo nikakemea na akafunguka. lakini hakujua ya kwamba alipolishwa ndani ya ndoto  kuna kitu kilikuwa kinaingia pia.

Mwingine  aliota ndoto kaumwa na nyoka kwenye kidole cha pili cha mguu wake  na maumivu yalikuwa makli sana kwenye ndoto na azindika na alipozinduka  akakuta anasikia maumivu kwenye mguu, akatoa shuka yake  alafu akamulika na tochi. na aliona pale alipoumwa na nyoka panatoa damu.  na aliona halisi, na kesho yake alipoenda kansan kuombewa walikemea pepo la mauti likitoka ndani yake. lakini ni kitu kilichotokea kwenye ndoto. 

mwingine aliota ndoto yuko porini kakutana na mama mmoja na alipewa karatasi. alipoamka ana ile karatasi mkononi.  Lakini amepewa kwenye ndoto.  na usipojua kitu cha kufanya ni hatari sana.

Kila kimoja unachoota kwenye ndoto majibu yapo kwenye biblia  katika upana wake. Biblia inasema kusikia huja kwa neno la Kristo  kwa hiyo hakikisha unakuwa na neno la kutosha ndani yako. 

Mwingine aliota anakatwa na msumeno kwenye kidole gumba na makali ya msumeno ndiyo yanaanza kuingia akashtuka kwenye ndoto  akaweka mkono juu ya kile kidole na kuomba. Baada ya mwezi mmoja pale alipoota anakatwa kidole pamekuwa peusi  na akaniambia sasa Mwalimu ni kitu gani hiki. nilimwambia ulikemea na roho ilitoka ila kuna sumu iliingizwa. 

Nilienda mkoa mmoja na mtu mmoja aliniambia Mwalimu nimeota ndoto nimepigwa risasi kwenye ndoto  nikamwambia okay, nikamuuliza je risasi ilitoka huko kwenye ndoto akisema hapana. Nikamuuliza tena je ulipigwa upande upi?  na akaniambia mguu huu na nikamuuliza je ulipoamka ukijisikiaje akasema mpaka leo nina maumivu upande huu.

Naweza  nikakusumulia na kukusimulia.
Mwingine aliota ndoto usiku ni mdada kaibiwa pochi (wallet) si unajua akina mama wanakuwa na pochi mbili yaani ile ndogo na ile kubwa yake.  sasa aliibiwa ile pochi(wallet) ya ndani iliyokuwa na hela  sasa asubuh anafika ofisini anashangaa kanga’anywa nafasi yake ya kazi na kapewa mtu mwingine. yeye alipewa mahali ambapo kuna mshahara kidogo na hamna marupurupu. na aliniandikia hiyo ndoto ila shida yake ni nini ni kwa sababu hakuomba usiku saa ile ameota ile ndoto.  na Mungu alikuwa anamsemesha kuwa si halali wewe kunyang’anywa kipato chako yaani unaibiwa si halali kwako kunyang’anywa hiyo nafasi.  lakini hakujua na hamna mtu aliyemweleza tafsiri yake. kwa hiyo ililazimu tuanze kuomba kwa style nyingine kabisa. ili aweze kurudi kwenye nafasi yake. 

Sasa kuna mwingine alinisikia nae nikisimilia alisema  sasa ndio nimeelewa kuwa na mimi niliibiwa pochi (wallet) yangu iliyokuwà inapesa ndani na kufika ofisini nilibadilishiwa kazi. na alipewa kazi ambayo  haiko sawa na kitu alichosomea na mshahara wake ukaenda chini na hamna maelezo waliyompa  na kila akiuliza maswali wanakuwa wakali. Labda wangejua wanajua hizi siri mapema wangekua kitu cha kufanya. 

Ngoja niulize hapa wangapi ambao hapa  wameota ndoto wamekula chakula kwenye ndoto na hawajajua kitu cha kufanya nyosha mkono 

sasa si kila chakula unachokula kwenye ndoto ni kibaya. Biblia inasema hata Yesu alikuwa chakula pamoja na wanafunzi wake. kwa hiyo kuna chakula cha Bwana. na kuna chakula cha mashetani. pia ukienda kwenye biblia kuna kula chakula ambacho  ni kukuonesha kuwa siku zako za kuishi zimeisha au unaarifiwa na Mungu  kwamba ndugu yako ameamua kuondoka na ameomba Mungu akamtishie maisha yake. kwa hiyo utaona kama ni baba yako anakula chakula na unaona akikurushia sahani kamaliza kula. Kasome biblia yako Zaburi ya 91 “Nitakushibisha kwa wingi wa siku “ kwa hiyo anayesema nimeshiba sio yule anayetoa chakula bali anayekula hicho chakula.  kuna ndoto zingine hazina shida ila zingine zina shida.

Biblia inasema kwa wana wa Israel walipokuwa wametengeneza ndama walikula na kunywa na kucheza  hakikuwa chakula cha kawaida. ilikuwa ni meza ya mashetani.

sasa kama  umekula chakula usichokijua kwenye ndoto   ambacho kwa jinsi ya kawaida usingekula ujue kuwa kuna kitu kinapitishwa. sasa kamuulize Petro kwanini aliletewa maono ya wanyama na yeye alisema siwezi kula kitu najisi. katika ulimwengu wa roho  kuna kitu alikuwa analetewa na kama wasingetafsiri katika biblia ingekuwa ngumu sana kujua.

Wangapi hapa ambao wameumwa na Nyoka au wamefukuzwa na nyoka kwenye ndoto. 

Glory to God Glory to God.

Ngoja tufanye zoezi hapa, kama uliota ndoto unakula chakula na hujajua ni kitu gani  weka mkono wako kwenye kidevu chako. kama uliumwa na nyoka nyika mahali umeumwa.

Kuna mtu aliumwa na nyoka kwenye pete ya kidole chake cha ndoa na ndoa yake ilikufa baada ya mwezi. na hakujua mpaka aliposikia nafundisha. mwingine aliota nyoka kapita tumboni kwake na baada ya pale siku za mwezi zilivurugika kuanzia pale.

Kuna mwingine aliota nyoka kaingia kwenye mguu wake na kapotelea huko. Hakujua kitu cha kufanya hadi aliponisikia nikifundisha na alikuwa ananisikiliza kwa njia ya mtandao.  na nilipokuwa nakemea na mguu wake  ukaanza kutetemeka ndipo alikuja kuelewa kuwa kumbe haikuwa ndoto ya kawaida kuna kitu kimeingia ndani yake maana alikuwa anaishiwa nguvu upande wa kushoto kwa hiyo kama ni mkono au mguu shika. nataka tufanye zoezi ili tuone. Kama kuna nguvu za giza zilipita na pepo ambalo limekaa huko ndani kuna namna nitakavyoomba yataondoka tu mengine kwa kupiga kelele na mengine kimya kimya. Mungu atakusemesha baadae au sasa hii baada ya maombi haya  na utapata ufahamu wa kitu cha kufanya.

kwa sababu kitu cha msingi hapa kama utakuwa unaelewa hapa pole pole na tutaangalia kwemye lango la ndoto kuwa kuna mahali vitu vinapita. kama ni chakula ina maana imepita kwenye mdomo. Kama ni viungo kawaida au mguu

nilikuwa nasimuliwa na mtu mmoja nilikuwa nimeenda kufundisha habari za ndoto na nikawa nafundisha habari za kuombea lango la ndoto  na yeye akaanza kuombea lango la ndoto ya kwake.Ghafla usiku akaota ndoto. Ameenda mahali kwenye kijiwe anachokula na mtu anayeuza chakula pale siku hiyo baada ya kuona chakula anachouza  ghafla aliona madudu fulani. sasa anaona yeye tu  wengine wote hawaoni. na yeye akashtuka na akaanza kusema kumbe nakula chakula hapa kwenye ndoto kumbe si kizuri. Sasa anajaribu kuwaelesa wemzake kuwa msile kile chakula jamani hapo au hamuoni sasa wenzake wakawa hawaoni. Yule  anayeuza chakula akamfuata na akamwambia kuwa wewe kama umeona ondoka kimya kimya usiniharibie biashara hapa.  na akajua kuwa Mungu anamsehesha kuwa asiende tena kula chakula pale.

MAOMBI
Mungu katika jina la Yesu, Ahsante kwa sababu ya nafasi hii na asante kwa sababu ya neno lako ee Bwana wewe peke yako ndio ulifuatana na wanafunzi wako kila mahali wameenda kotekote biblia ndivyo inavyotuambia wakihubiri lile neno na wewe ukilithibitisha lile neno. kwa ishara zilizofuatana nao. Nami naomba ee Bwana sawa sawa na neno ulilonipa katikati ya watu wako na watoto wako nikiwa hapa singida  ee Bwana tunaomba mkono wako wenye nguvu upate kutusamehe na kuturehemu  sawa sawa na neno lako, mahali popote ambapo nguvu za giza zilipata mlango na kupitisha vitu vya kwake  tunajua lango la ndoto uliliumba wewe kwa ajili ya mwanadamu kwa ajili ya kusudi  lako. lakini Ee Bwana adui analitumia kwa ajili ya kupitisha  vitu vya kwake.  Ninaomba toba kwa ajili yangu na kwa ajili ya kila mmoja aliyeko mahali hapa anayeombewa na tunaomba mahali hapa Ee Bwana upate kuturehemu katika jina la Yesu Kristo. ninaomba toba ee Bwana kwa ajili ya maovu yote katika familia ambayo kuna maagano ambayo yanawafutailia  ambayo yalifanyika kwenye vyakula  au yalifanyika kwenye vinywaji ee Mungu katika jina la Yesu Kristo.  hizo nguvu za giza  zinajaribu kuzungumza na hawa watu na kuwaambia hawa ni wa agano hili na zinajaribu kuwaingiza katika agano hilo au wameingizwa kwenye agano na kwa sababu hiyo kuna mapepo ambayo yamepewa kufuatilia  kila eneo  ee Mungu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth  wewe uonae siri ninaomba rehema zako tunapoomba toba kwako na msahama kwa ajili ya  dhambi zetu na dhambi za kila mmoja  ninaomba ee Bwana toba kwa ajili ya uovu wa waliotutangulia  na kutuingiza katika maagano yanayotufuatilia katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth.  Tunaomba  toba kwa ajili ya jambo lolote ambalo lilitoa nafasi owa adui na akapita  kwa roho ya nyoka na kuingia katika miili ya watu ja kuwagonga na kuachilia sumu yake katika damu ya Yesu Kristo. na nyunyiza damu ya Yesu  kuanzia kwenye kinywa chake na damu ya Yesu Kristo katika kinywa chake ipite ee Bwana kwa mtu wa nje  na mtu wa ndani na kusafisha sasa inaondoa  dhambi na roho mbali mbali ndani ya watu ee Bwana katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth ×5  Nina nyunyiza damu ya Yesu  kwenye utumbo mkubwa na mdogo mahali ambapo giza zimebana kwa damu ya Yesu Kristo wa Nazareth.  Nanyunyiza damu ya Yesu katika Fikra mahali ambapo ibilisi amebana. nanyunyiza damu katika roho yake   ambapo nyoka amengonga huyu mtu katika ndoto  kwa damu ya Yesu Kristo ninaachilia moto wako  na kuondoa hiyo sumu  na kufuta kila uhalali wa adui kushambulia. katika jina la Yesu.. endelea kuomba..

Biblia inasema palipo na msahama pana kuwekwa huru. palipo na msahama pana ukombozi Ahsante Mungu wa sababu unasamehe. kwa mamlaka niliyopewa katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth  tunakwenda  kinyume kabisa na nguvu zote za mapepo na nguvu zote za za giza  zilizopita kwa njia ya hizo ndoto tulizozitaja.  Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth.  pepo majini na roho zote za uchawi zilizopita kwenye mwili wake toka kwa jina la Yesu × 3 endelea kuomba Toka jina la Yesu Kristo  kemea kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth..

Tukiwa tumefunika macho nauliza hili swali muhimu.  *Unajua hujaokoka Yesu si Bwana na mwokozi wa maisha yako au  ulikuwa umeokoka na ukarudi nyuma na hujapata nafasi ya kutengeneza. Nataka niombe kwa ajili yako jion ya leo mahali popote ulipo*. 

*Soma sala hii*.
Ee Mungu baba nimekuja mbele zako, ninaomba unipokee, ninatubu kwako dhambi zangu zote  nilizokukosea katika maisha yangu.Ninaomba toba kwako. Ninaomba unisamehe, ninaomba unirehemu, ninaomba unitakase  kwa damu ya Yesu iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu. Ee Bwana Yesu nimefungua moyo wangu, nakukaribisha sasa  ingia ndani yangu kwa uweza wa Roho wako uwe mwokozi, uwe kiongozi, uwe Bwana Kwangu. Kuanzia sasa na siku zote unisaidie nidumu ndani yako siku zote za maisha yangu. Shetani asinishinde, majaribu yasinishinde, dhambi isinishinde  katika jina la Yesu. Nikuishie wewe peke yako katika jina la Yesu. 

*FUATISHA MAOMBI HAYA  NA SOMA KWA IMANI*

Mungu katika jina la Yesu. Ninakushukuru kwa sababu ya uaminifu wako. Ahsante ee Bwana kwa ajili ya wale waliofanya sala hii kwa mara yao ya kwanza na wengine mara ya pili na wengine  mara ya tatu mara ya nne. Lakini kwa vyovyote  vile ee Bwana neema yako ya wokovu imefunuliwa juu yao ahsante kwa ajili ya kila mmoja  ahsante kwa ajili ya uzima wa milele ulioko ndani yao. Ahsante kwa majina yao kuandikwa ndani ya kitabu cha uzima. Ahsante ee Bwana kwa Yesu Kristo kuingia ndani yao upate kuishi na kuweka matunda na upate kujifunua . Hicho ndicho tunachoomba ee Bwana. Tembea  pamoja nao ukiwapa ushindi wa maisha ee Bwana katika jina la Yesu  tembea pamoja nao upate kujifunua wapate kukujua wewe na kukuishia wewe  katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth. Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth  tunakwenda kinyume kabisa  na nguvu zote za giza  na nguvu zote za mapepo na roho zote za majini  na maagano yote ya kipepo ambayo yatataka kuinuka ili kuzuia  nyendo zao hawa watu katika Kristo Yesu. Tunafuta maagano yote ya kipepo kwa damu ya Yesu  yafutike kabisa na nguvu za giza  tunakuamuru achia  hatua za watu hawa  achia roho zao, achia nafsi zao, achia miili yoa sasa, achia maisha yao, uchumi wao na viatu vyao sasa  katika jina la Yesu. Pepo tunakuamuru toooka. Hawa sio wa kwako tena kwa jina la Yesu. Tooka toka toka toka toka  kwa jina la Yesu. Achia tumbo lake achia kifua chake, pepo toka. Ee Bwana tunawakabidhi kwako watunze popote watakapokuwa katika jina la Yesu Kristo. Na kila mwemye pumzi aseme Ameeen.

Kama umefanya hii sala mara ya kwanza ndio umeokoa tayari. Kama ulikoka ukarudi nyuma basi Mungu amekusamehe na wewe jisamehe na akisamehe anasahau  kwa hiyo usijihukumu kabisa

Somo katibu cha *HONGERA KWA KUOKOKA NIMEKUWEKEA LINK PALE JUU.*

GLORY TO GOD. TUONANE TENA KIPINDI KIJACHO KATIKA MFULULULIZO WA SEMINA HII HAPA SINGIDA  NA WATUMIE NA WENGINE. 

=GLORY TO GOD GLORY TO GOD=

UMETIMIZA KUSUDI LA MUNGU?

KUNA JAMBO UNATAKIWA KUFANYA NDIO MAANA BADO UNAISHI.
Mwl Debora E. Lema✍✍
MATENDO 13:36
“Kwa maaan DAUDI akiisha kulitumikia shauri la MUNGU katika kizazi chake alilala ”
ALILALA BAADA YA KULITUMIKIA SHAURI LA BWANA. MUNGU hakuweki duniani bila sababu, kila kiumbe kilichopo chini ya jua kipo kwa sababu maalumu. Huwezi kupewa pumzi ya bure kwa HASARA, hivyo kwa muda ambao unaishi tafuta kujua MUNGU anahitaji nini kutoka kwako.
KUISHI NI KRISTO, NA KUFA NI FAIDA. FAIDA KWAKUA UMEISHI KWA UKAMILIFU WA KTISTO, KINYUME CHAKE ITAKUA NI KIFO CHA HASARA.
JITHAMINI, UMEBEBA KUSUDI LA MUNGU NDANI YAKO.🇮🇱🇹🇿

ZAB 78 UAMINIFU NA REHEMA ZA MUNGU PALE UOMBOLEZAPO.

Mlango 78
1 Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu,Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.

2 Na nifunue kinywa changu kwa mithali,Niyatamke mafumbo ya kale.

3 Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu,Ambayo baba zetu walituambia.

4 Hayo hatutawaficha wana wao,Huku tukiwaambia kizazi kingine,Sifa za BWANA, na nguvu zake,Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.

5 Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo,Na sheria aliiweka katika Israeli.Aliyowaamuru baba zetuWawajulishe wana wao,

6 Ili kizazi kingine wawe na habari,Ndio hao wana watakaozaliwa.Wasimame na kuwaambia wana wao

7 Wamwekee Mungu tumaini lao.Wala wasiyasahau matendo ya Mungu,Bali wazishike amri zake.

8 Naam, wasiwe kama baba zao,Kizazi cha ukaidi na uasi.Kizazi kisichojitengeneza moyo,Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.

9 Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde,Walirudi nyuma siku ya vita.

10 Hawakulishika agano la Mungu;Wakakataa kuenenda katika sheria yake;

11 Wakayasahau matendo yake,Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu,Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13 Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.

14 Akawaongoza kwa wingu mchana,Na usiku kucha kwa nuru ya moto.

15 Akapasua miamba jangwani;Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.

16 Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.

17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.

18 Wakamjaribu Mungu mioyoni mwaoKwa kutaka chakula kwa tamaa zao.

19 Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?

20 Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?

21 Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.

22 Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.

23 Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;

24 Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.

25 Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.

26 Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.

27 Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.

28 Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.

29 Wakala wakashiba sana;Maana aliwaletea walivyovitamani;

30 Hawakuachana na matakwa yao.Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao

31 Hasira ya Mungu ikapanda juu yao,Akawaua waliokuwa wanono;Akawaangusha chini vijana wa Israeli.

32 Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi,Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.

33 Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi,Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha.

34 Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta;Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii.

35 Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao,Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao.

36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,Wakamwambia uongo kwa ndimi zao.

37 Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake,Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.

38 Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema,Husamehe uovu wala haangamizi.Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake,Wala haiwashi hasira yake yote.

39 Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili,Upepo upitao wala haurudi.

40 Walimwasi jangwani mara ngapi?Na kumhuzunisha nyikani!

41 Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu;Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli.

42 Hawakuukumbuka mkono wake,Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.

43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri,Na miujiza yake katika konde la Soani.

44 Aligeuza damu mito yao,Na vijito wasipate kunywa.

45 Aliwapelekea mainzi wakawala,Na vyura wakawaharibu.

46 Akawapa tunutu mazao yao,Na nzige kazi yao.

47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe,Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu.

48 Akaacha ng?ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe,Na makundi yao kwa umeme.

49 Akawapelekea ukali wa hasira yake,Ghadhabu, na uchungu, na taabu,Kundi la malaika waletao mabaya.

50 Akiifanyizia njia hasira yake;Wala hakuziepusha roho zao na mauti,Bali aliiachia tauni uhai wao;

51 Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri,Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu.

52 Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo,Akawachunga kama kundi jangwani.

53 Hao akawachukua salama wala hawakuogopa,Bali bahari iliwafunikiza adui zao.

54 Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu,Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume.

55 Akawafukuza mataifa mbele yao,Akawapimia urithi kwa kamba,Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.

56 Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi,Wala hawakuzishika shuhuda zake.

57 Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;Wakaepea kama upinde usiofaa.

58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.

59 Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.

60 Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;

61 Akaziacha nguvu zake kutekwa,Na fahari yake mkononi mwa mtesi.

62 Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;Akaughadhibikia urithi wake.

63 Moto ukawala vijana wao,Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

64 Makuhani wao walianguka kwa upanga,Wala wajane wao hawakuomboleza.

65 Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi,Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;

66 Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma,Akawatia aibu ya milele.

67 Ila akaikataa hema ya Yusufu;Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.

68 Bali aliichagua kabila ya Yuda,Mlima Sayuni alioupenda.

69 Akajenga patakatifu pake kama vilele,Kama dunia aliyoiweka imara milele.

70 Akamchagua Daudi, mtumishi wake,Akamwondoa katika mazizi ya kondoo.

71 Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa,Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake.

72 Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake,Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.

PAMOJA NA KWA MUNGU AMEKUPA KILA ULILOOMBA USIBWETEKE NA KUJISAHAU BALI ZIDISHA IMANI NA UTII KWAKE KWA KYWA MUNGU NU MWAMBA IMARA NA WENYE NGUVU.

WEWE NI MJUMBE WA KRISTO DUNIANI.

TU WAJUMBE WA KRISTO DUNIANI.
Mwl Debora E. Lema✍✍
2 KORINTHO 5:20a
“Basi tu wajimbe kwa ajili ya KRISTO kana kwamba MUNGU anasihi kwa vinywa vyetu”
MJUMBE NI MWAKILISHI. Unapoamua kumkubali KRISTO moja kwa moja wewe ni mjumbe unayemwakilisha DUNIANI. Yote unayoyatenda yatamtukuza na kinyume chake utalitukanisha jina lake.Atasema na watu kupitia kinywa chake maana wewe ni mwakilishi wake, kwa matendo yako mema watamtukuza maana unadhihirisha uhalisia wake kupitia matendo yako.
MAANDIKO YANASEMA, WATAKATIFU WALIO DUNIANI HAO NDIO WALIO BORA, NA NDIO MUNGU ANAOPENDEZWA NAO. VINGINE VYOTE NI ZIADA NA UTAVIACHA DUNIANI.
🇹🇿🇮🇱

Tambua namna ADUI ANAVYOTUMI ARDHI AU ENEO UNALOISHI KUHARIBU MAISHA YAKO

*IJUE NAMNA AMBAVYO ADUI YAKO ANAVYOWEZA KUTUMIA ARDHI /NCHI UNAYOIKAA KUHARIBU MAISHA YAKO* 
ZEKARIA 18
18 Nami nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, pembe nne.
19 Nami nikamwuliza yule malaika aliyesema nami, Nini hizi? Naye akanijibu, Hizi ndizo pembe zilizowatawanya watu wa Yuda, na Israeli, na Yerusalemu.
20 Kisha BWANA akanionyesha wafua chuma wanne.
21 Ndipo nikauliza Hawa wanakuja kufanya nini? Akasema kwamba, Hizi ndizo pembe zilizowatawanya watu wa Yuda, hata ikawa hakuna mtu aliyeinua kichwa chake; lakini hawa wamekuja kuzifukuza, kuziangusha pembe za mataifa, walioinua pembe yao juu ya nchi ya Yuda, ili kuwatawanya watu wake.
Bwana Yesu asifiwe sana sana 
Nilikuwa moshi kwenye mji wa familia moja ivi na nilipokaa pale nikawa nafanya maombi kwa ajili ya ile familia katika yale maombi pepo likalipuka pale na likajielezea kuwa limechukua nafsi ya mtu ambaye alikuwa analitaka eneo ambalo wanalolikaa ambalo Baba yao alipewa na Babu yao lakini huyu mtu mmoja akawa analitaka lote liwe lake ,na hili kulipata ilibidi kwanza auwe Baba wa familia na akachukua damu na akaweka agano kwenye ardhi yao kwamba kiwepo na kiti kwenye hiyo Ardhi au nchi ambacho atakuwa anakitumia kuwafunga na kuwaharibu kupitia hiyo Ardhi yao na akafanya jambo lingine pia akaweka roho ya mafarakano na chuki na malumbano kati ya wanandugu ,akahakikisha anawatawanya wote pale kwenye ile ardhi na hata ule usiku ,kilichokuwa kinawafanya walumbane na kujisikia uchungu na kilio kwa Dada mmoja ndani ya ile familia usiku ule ni kwamba yule Aliyekuwa anataka kuvuruga ile familia alikuja usiku alimtuma mke wake ili aje awavuruge ule usiku wasielewane 
Na likaeleza kuwa damu ya marehemu yaan baba mwenye nyumba na hirizi aliyokuwa nayo ndio inayompa uhalali wa kukamata ile ardhi na kuwavuruga na kuwagombanisha na kuwatawanya ni Sawa Sawa na ile Zekaria 1:18-19 inaeleza juu ya nabii Zekaria alivyopewa macho ya rohoni ya kuona shida au tatizo lilikuwepo kwenye nchi au ardhi ya Yuda na Yerusalemu anasema kuwa kulikuwepo na pembe ambazo ziliwatawanya watu wa Yuda na Yerusalemu na zikahakikisha awafanikiwi kwenye ardhi hizo kabisa ,ile Zekaria 1:21 inaeleza kuwa zile pembe zilizowatawanya Watu wa Yuda na Yerusalemu zilikuwa na nguvu za kuwagawa na kuwatawanya kiasi ambacho hawakuweza kuinua kichwa hata kidogo yaani ziliwafanya wawe dhaifu sana mbele ya hizo pembe 
Kiukweli ni kwamba kama hautaweza kuzishughulikia ipasavyo utashangaa ardhi unayoikaa inakuwa moto ,huwezi kuendelea na saa ingine unalazimika kuikimbia nyumba yako au nyumba yenu kabisa 
Na kama adui amekusudia kukumaliza anaweza kutumia ardhi kabisa ya kwenu kukufarakanisha na kukuwekea mikosi na umaskini ,kutokuolewa wala kuoa 
Ukisoma Zekaria 1:21 utaona kuwa inatakiwa Mungu atume malaika zake kuwafungua ,na kuzifukuza na kuangusha chini vile vimewekwa kwenye hiyo ardhi hapo ili maisha yapate kurejea kwa upya 
Katika maelezo ya lile pepo lilidai kuwa limepewa haki ya kukamata ardhi ya familia ya yule Dada lilisema pia lilitumia maneno kukamata ardhi na maisha ya watu wa ile familia na hili jambo ukisoma Yeremia 30:3-4 utaliona wazi wazi kuwa katika ulimwengu wa kiroho wakitaka kukamata Ardhi na maisha ya wakazi wa hapo wanatumia maneno ya kuwafunga na kuwatawanya wakaao juu ya hiyo ardhi ,wakiisha tumia maneno ya kuwatamkia ya kimaagano na kuhachia roho ya umaskini ,njaa ,magonjwa ,mafarakano ,vifo basi wanakuwa wamemaliza kazi sasa kama ujajua kwenda kwa Mungu na kuomba toba na rehema basi hali inakuwa mbaya sana kwenye familia 

Watahachia vitu vibaya kwenye ardhi kwa maneno ya kimaagano yenye roho yenye nguvu nyuma yake ya kutawanya ,kufarakanisha ,umaskini na n.k na hili kukomboa hiyo ardhi lazima utumie pia maneno na ndio maana Yeremia 30:4-9 inaeleza wazi kuwa Mungu alipotaka kuwakomboa Yuda alianza kutuma kwanza neno kwao na kwa adui zao la ukombozi ,neno linaweza kutumika kukomboa shida ya familia iliyofungwa na roho za kipepo kwenye ardhi 
Neno la Mungu na damu ya Yesu na jina pia ni ufunguo wa kufungulia ardhi na wanayoikaa pia

JIFUNZE MAOMBI YA KUHARIBU NA KUWATEKETEZA MAAJENTI WA NGUVU ZA GIZA

MAOMBI YA KUHARIBU FARASI NA MPANDA FARASI WA KICHAWI.
Leo omba maombi ya kuharibu farasi na mpanda farasi wa kichawi.
Bwana YESU atukuzwe.

Ngoja nikupe maarifa kidogo tu ili uombe kwa siku moja hii na kushinda.

Inawezekana umeshawahi kuona farasi kwenye ndoto au maono.

Inawezekana unajua farasi anawakilisha nini katika ulimwengu wa roho.

Leo nasukumwa kukupa maarifa kidogo ya kukusaidia katika maombi.

Kwenye Ulimwengu wa roho farasi huwakilisha mambo yafuatayo.

1. Farasi huwakilisha safari yenye spidi.

Hivyo ukiota umepanda farasi wewe mwenyewe maana yake katika yale unayoyafanya mema kwa wakati huo unatakiwa uongeze spidi maana inahitajika spidi ili kuyakamilisha kwa wakati.

Maana yake kazi ya MUNGU unayoifanya inakupasa sana kuongeza spidi sana wakati huo maana jambo hilo liko ndani ya wakati maalumu.

Kama umeona watu wengine wamepanda farasi basi itategemea na mazingira uliyoona ndipo ujue watu hao na farasi hizo zinawakilisha nini.
2. Farasi huwakilisha mbio zenye spidi.

Katika Biblia farasi ametajwa sehemu nyingi sana.

Kuna farasi katika wema wa MUNGU na kuna farasi wa kipepo kwa kusdi la kishetani.

Kwenye ndoto inawezekana umewahi kuona farasi wa aina mbalimbali.

Naomba nikufafanulie ili kama ni farasi wa kipepo ujue sasa kulitumia jina la YESU KRISTO kuwashinda hao mawakala wa shetani.

1. Farasi mweupe huwakilisha ushindi na haki.

Lakini katika farasi mweupe inakupasa kumuomba MUNGU akujulishe aliyepanda juu ya farasi huyo ni nani na anawakilisha nini maana hata mpinga Kristo Biblia inamuonyesha kuwa atapanda farasi mweupe lakini cha ajabu mpinga Kristo kama roho ya kuzimu atakuwa na uta na mshale.

Ufunuo 6:2 ” Nikaona, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda ana uta, akapewa taji, naye akatoka, ali akishinda tena apate kushinda.”

Anayezungumzwa katika andiko hili ni mpiga Kristo lakini atakuwa amepanda farasi mweupe. Unajua maana yake?

Ni kwamba mpinga Kristo atakuja katika mfumo wa dini fulani iliyo kinyume na Wokovu wa Bwana YESU lakini huyo roho ya kuzimu atakuwa na uta yaani ana upindi na mshale, maana yake ni dini lakini dini hiyo kuua watu ni jambo la kawaida tu. Hilo tukio la mpinga Kristo ndilo tukio la kwanza kabisa la wapingaji wa Wokovu wa Bwana YESU.

Lakini tukirudi katika somo langu la leo.

Unadhani kwanini apande farasi na sio mnyama mwingine? Ni kwa sababu ya maana za kiroho za farasi. Kwahiyo mpinga Kristo ni mkusanyiko wa dini zote na na madhehebu yote ya dini ambazo zinakataa Kuokolewa na Bwana YESU na kumkataa ROHO MTAKATIFU na kukataa kuitii Biblia katika kusudi la MUNGU BABA.
2. Farasi mwekundu katika ulimwengu wa roho huwakilisha vita, mateso na kuondoa amani.

Ufunuo 6:4 ” Akatoka farasi mwingine, mwekundu sana, na yeye aliyempanda alipewa kuiondoa amani katika nchi, ili watu wauane, naye akapewa upanga mkubwa.”
Unaweza ukaona katika ndoto au maono mtu amepanda farasi mwekundu na anakushambulia au anafukuza kitu chako au mwana familia au familia. Tambua kwamba kutatokea vita hivyo yakupasa sana uwe muombaji ili kuharibu vita ya kipepo uliyoiona itakayoondoa amani kwako au katika ndoa yako au katika ukoo au jamii.
3. Farasi mweusi huwakilisha njaa.

Ufunuo 6:5 ” Na alipoifungua muhuri ya tatu, nikamsikia yule wa tatu mwenye uhai akisema, Njoo! Nikaona, na tazama, farasi mweusi, na yeye aliyempanda ana mizani mkononi mwake. ”

Kuna umasikini mwingine huwa una chanzo katika ulimwengu wa roho kutokana na mashambulizi ya kipepo.

Kuna ukata mwingine unaweza kukukumba kwa sababu tu huombi na adui anakuwa ameshakuwekea maroho ya kishetani ya kukufilisi.
4. Farasi wa kijivujivu huwakilisha roho ya mauti.

Ufunuo 6:8 ” Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda jina lake ni Mauti, na Kuzimu akafuatana naye. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi. ”

Wengi wanateswa sana na roho za mauti.

Nimewahi kufundisha somo kuhusu kuharibu roho za mauti(Unaweza uka-seach google utalipata na utafahamu kwa upana sana maana roho ya mauti ni katika maeneo mengi mno)
Katika maandiko hayo ya Kitabu cha Ufunuo 6 tunaona ni matukio ya siku za mwisho yaliyoamriwa na MUNGU kuelekea wakati wa kurudi kwa Bwana YESU, lakini kwanini nimekuwekea hapa maandiko hayo? Ni ili ujue maana ya farasi katika ulimwengu wa roho na sio ujue maana ya kitabu cha ufunuo, hivyo kujua kitabu cha ufunuo ni somo linge na hili.

Farasi hao aina nne wametajwa pia katika kitabu cha Zakaria 1:8-9 ” Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe.

Ndipo nikasema, Ee BWANA wangu, ni nini hawa? Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Nitakuonyesha ni nini hawa. ”
Farasi katika ulimwengu wa roho wanaweza wakatumika pia kama silaha za kipepo.

Kwanini leo tunaomba maombi ya kuharibu farasi na mpanda farasi wa kichawi?

Kutoka 15:1-3 ”Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni MUNGU wa baba yangu, nami nitamtukuza. BWANA ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.”
Nataka tujue yafuatayo kuhusu hili.

Baada ya MUNGU kuwaua farasi ya mpanda farasi wa kimisri ndipo hatuoni tena vita yeyote katika ya Farao na waisraeli.

Mwisho wa vita katika wa farao wateule wa MUNGU ni baada ya MUNGU huwaharibu farasi na mpanda farasi.

Kwenye maombi wewe uliokoka una mamlaka kuu sana.

Ni mara nyingi umesikia kuna wachawi wanatembea na ungo kwenda kuroga. Inawezekana kabisa wachawi wanaokusumbua wewe usiku huwa wanakuja na ungo kukuroga, huo ungo ndio farasi wa kichawi na aliyeanda ungo huo ndio mchawi. Ulishawahi kujiuliza ukiomba maombi ya kuteketeza kila ungo wa mchawi anayepanga kuja kukuroga, je mchawi huyo ataweza kusafiri? Jibu ni hapana.

Basi maombi ya kuharibu farasi na mpanda farasi wa kichawi yanaweza kumharibu mchawi na zana zake za kichawi. Maombi yako yanaweza kuharibu mchawi na vyombo vyake vya kusafiria kichawi, hivyo vyombo ndivyo farasi wa kichawi.

Mimi Peter tangu utotoni kule kwetu usukumani niliwahi sana kusimuliwa jinsi wachawi wanavyokwenda kuroga.

Siku moja usiku tukiwa kwenye moto katikati ya uwanja wa nyumbani tuliona moto mbugani kwa mbali na wakubwa wetu wakatuambia hao ni wachawi wamepanda fisi wakenda kuroga. Sasa kama iko hivyo basi ukiomba maombi ya kuharibu fisi wao wa kichawi hakika huyo mchawi hata kama anapanga kuja kukuroga hakika hatakuja maana ufasiri wake wa kipepo umeharibiwa kupitia maombi yako katika jina la YESU KRISTO.

Huo usafiri wa kichawi ndio farasi wa kichawi.

Leo usikubali farasi na mpanda farasi wa kichwai wakutese tena.

Omba maombi ya kuharibu mchawi na usafiri wake wa kichawi.

Fita itakoma tu kama utaharibu mchawi na vyombo vyake vya usafiri vya kichawi.

Ni ufunuo mzuri huu leo kwamba uombe maombi ya kuharibu farasi na mpanda farasi.

maombi haya ni muhimu sana na mara ya kwanza mimi nilisikia sauti nikiwa Kanisani kwamba niombe maombi ya kuharibu farasi na mpanda farasi wa kichawi, hakika nilishinda.

Baada ya maombi yale mimi naamini hakika hata kama mawakala wa shetani watataka kutuma maroho ya uharibifu basi hakika maroho hayo hayatasafiri maana usafiri wao wa kipepo nimeshauangamiza kwa damu ya YESU KRISTO.
Kuna farasi wengine kwenye ulimwengu wa roho sio farasi tu wa kawaida hivyo maombi yako katika jina la YESU KRISTO yatakuletea ushindi mkuu.

Ufunuo 9:17-21 ”17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti. Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao. Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo. Na wanadamu waliosalia, wasiouawa kwa mapigo hayo, hawakuzitubia zile kazi za mikono yao, hata wasiwasujudie mashetani, na sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, zisizoweza kuona wala kusikia wala kuenenda. Wala hawakuutubia uuaji wao, wala uchawi wao, wala uasherati wao, wala wivi wao.”
Ndugu omba na hakikisha unaishi maisha matakatifu ndipo hakika utakuwa na ushindi wa kudumu dhidi ya mawakala wa shetani.

Omba katika ROHO MTAKATIFU na omba kwa imani.

Jambo la Mwisho naomba uzingatie katika maombi ni kwamba kila unapopambana na maroho ya shetani tambua kwamba inakupasa upigane na maadui wanne ndipo utashinda kwa urahisi sana.

1. Adui wa kwanza ni hiyo roho ya kipepo iliyotumwa kwako.

2. Adui wa pili ni maroho yaliyowekwa kipepo ili kuisaidia hiyo roho unayopambana nayo ikitokea unataka kuishinda ili isitimize lengo la kishetani.

3. Adui wa tatu ni vyombo vya usafiri vya kichawi vilivyobeba hivyo unavyopambana navyo.

Vyombo hivyo vya usafiri wa kichawi ndivyo hivyo mimi nimeita farasi wa kichawi.

4. Adui wa nne ni yule aliyetuma maroho hayo ya kukutesa katika maisha yako.

Katika maombi yako hakikisha hubakizi hata adui mmoja ndipo utashinda vita ya kiroho vyema.

Maombi katika jina la YESU KRISTO ni silaha ya mwisho isiyoweza kushindwa na adui yeyote katika ulimwengu wa roho.

MUNGU akubariki na pia Ukipenda kunisapoti kwa sadaka yako ya hiari katika huduma yangu karibu sana na pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.

Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.

BWANA YESU Amekaribia Kurudi.

Je, Umejiandaaje?

Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?

Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.

Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.

Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.

Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.

Mkumbuke Mungu ili uuishi ULINZI WAKE

Mungu akupiganie NA AKULINDE WEWE MJA WAKE 
ZAB 70: Mlango 70
1 Ee Mungu, uniokoe,Ee BWANA, unisaidie hima.

2 Waaibike, wafedheheke,Wanaoitafuta nafsi yangu.Warudishwe nyuma, watahayarishwe,Wapendezwao na shari yangu.

3 Warudi nyuma, na iwe aibu yao,Wanaosema, Ewe! Ewe!

4 Washangilie, wakufurahie,Wote wakutafutao.Waupendao wokovu wakoWaseme daima, Atukuzwe Mungu.

5 Nami ni maskini na mhitaji,Ee Mungu, unijilie kwa haraka.Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,Ee BWANA, usikawie.

MUNGU NI MWAMINIFU NA FADHILU ZAKE NI ZA MILELE HAKIKA TUMFURAHIE NA KUMSHANGILIA HUKU TUKIMSHUKURU SANA.HALLELUJAH

KIROHO MWANAMKE ANA NGUVU KULIKO HATA YEYE AJUAVYO PALE AMTUMKIAPO MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI. YOH 4:20-26

WANAWAKE WANA NGUVU NA LAZIMA WAIOKOW JAMII KWA KUWAJIBIKA Zab 68: Mlango 68
1 Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika,Nao wamchukiao huukimbia uso wake.

2 Kama moshi upeperushwavyo,Ndivyo uwapeperushavyo wao;Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto,Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.

3 Bali wenye haki hufurahi,Na kuushangilia uso wa Mungu,Naam, hupiga kelele kwa furaha.

4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake,Mtengenezeeni njia ya barabara,Apitaye majangwani kama mpanda farasi;Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.

5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane,Mungu katika kao lake takatifu.

6 Mungu huwakalisha wapweke nyumbani;Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa;Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.

7 Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako,Ulipopita nyikani,

8 Nchi ilitetemekaNaam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu;Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.

9 Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema;Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.

10 Kabila yako ilifanya kao lake huko;Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.

11 Bwana analitoa neno lake;Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;

12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia;Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.

13 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua,Mbawa zake ziking?aa kama fedhaNa manyoya yake kama dhahabu?

14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko,Kulinyesha theluji katika Salmoni.

15 Ni mlima wa Mungu mlima Bashani,Ni mlima mrefu mlima Bashani.

16 Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivuMlima alioutamani Mungu akae juu yake?Naam, BWANA atakaa juu yake milele.

17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu;Bwana yumo kati yao kama katika Sinai,Katika patakatifu.

18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka,Umepewa vipawa katikati ya wanadamu;Naam, hata na wakaidi, BWANA Mungu akae nao.

19 Na ahimidiwe Bwana,Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu;Mungu ndiye wokovu wetu.

20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa;Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.

21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake,Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.

22 Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha,Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;

23 Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako,Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.

24 Ee Mungu, wameiona miendo yako;Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu

25 Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda,Kati ya wanawali wapiga matari.

26 Mhimidini Mungu katika mikutano,Bwana katika makusanyiko ya Israeli.

27 Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao;Wakuu wa Yuda, kundi lao;Wakuu wa Zabuloni;Wakuu wa Naftali.

28 Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.

29 Kwa ajili ya hekalu lako YerusalemuWafalme watakuletea hedaya.

30 Mkemee mnyama wa manyasini;Kundi la mafahali, na ndama za watu;Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha,Uwatawanye watu wapendao vita.

31 Masheki watakuja kutoka Misri,Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.

32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,Msifuni Bwana kwa nyimbo.

33 Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele;Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.

34 Mhesabieni Mungu nguvu;Enzi yake i juu ya Israeli;Na nguvu zake zi mawinguni.

35 Mungu ni mwenye kutishaKutoka patakatifu pako.Ndiye Mungu wa Israeli;Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo.Na ahimidiwe Mungu.

JIPE MOYO EWE MAMA NA DADA YANGU UTASHINDA …..TIMIZA WAJIBU WAKO

KUMSHUKURU MUNGU KWA DHABIHU.

DHABIHU NI SHUKRANI INAYOFUNGUA BARAKA NA KUONDOSHA VIFUNGO ALIVYOFUNGWA MTU ZAB 67: Mlango 67
1 Mungu na atufadhili na kutubariki,Na kutuangazia uso wake.

2 Njia yake ijulike duniani,Wokovu wake katikati ya mataifa yote.

3 Watu na wakushukuru, Ee Mungu,Watu wote na wakushukuru.

4 Mataifa na washangilie,Naam, waimbe kwa furaha,Maana kwa haki utawahukumu watu,Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.

5 Watu na wakushukuru, Ee Mungu,Watu wote na wakushukuru.

6 Nchi imetoa mazao yakeMUNGU, Mungu wetu, ametubariki.

7 Mungu atatubariki sisi;Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.

TUMSHUKURU MUNGU ILI TUBARIKIWE SOTE….MUNGU NI MWEMA SANA NA ATUBARIKI SOTE.

MTUMIKIE MUNGU KWA KUTUMIA AKILI TIMAMU KIROHO

ZAB 111:10 Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,Wote wafanyao hayo wana akili njema,Sifa zake zakaa milele.

MWIMBIENI BWANA MUNGU KWA AKILI

ELEWA NA PATA UTULIVU NA USIKIVU UMWIMBIAPO MUNGU KWA KUWA WAIMBAO KWA UMAKINI WA AKILI “HUPOKEA NA KUPATA MAJAWABU YAO TOKA KWA BABA MUNGU”

Zab 47 & 81 & 111:10

ZABURI 47:

1 Enyi watu wote, pigeni makofi,Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
2 Kwa kuwa BWANA Aliye juu, mwenye kuogofya,Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.
3 Atawatiisha watu wa nchi chini yetu,Na mataifa chini ya miguu yetu.
4 Atatuchagulia urithi wetu,Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,BWANA kwa sauti ya baragumu.
6 Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.
7 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,Imbeni kwa akili.
8 Mungu awamiliki mataifa,Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.
9 Wakuu wa watu wamekusanyika,Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu.Maana ngao za dunia zina Mungu,Ametukuka sana.
Zab 81 
1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha,Mshangilieni Mungu wa Yakobo.

2 Pazeni zaburi, pigeni matari,Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.

3 Pigeni panda mwandamo wa mwezi,Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu.

4 Kwa maana ni sheria kwa Israeli,Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.

5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.

6 Nimelitenga bega lake na mzigo,Mikono yake ikaachana na kikapu.

7 Katika shida uliniita nikakuokoa;Nalikuitikia katika sitara ya radi;Nalikujaribu penye maji ya Meriba.

8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;

9 Usiwe na mungu mgeni ndani yako;Wala usimsujudie mungu mwingine.

10 Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,Niliyekupandisha toka nchi ya Misri;Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.

11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,Wala Israeli hawakunitaka.

12 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,Waenende katika mashauri yao.

13 Laiti watu wangu wangenisikiliza,Na Israeli angeenenda katika njia zangu;

14 Ningewadhili adui zao kwa upesi,Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;

15 Wamchukiao BWANA wangenyenyekea mbele zake,Bali wakati wao ungedumu milele.

16 Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano,Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.
Kumcha Bwana ni  UKAMILIFU WA AKILI

SIO KWA SILAHA ZAKO …BALI NI KWA UWEZA WA MUNGU KUKUSHINDIA.

Si kwa UPINDE, PANGA AU SILAHA ULIZOSHIKA…BALI NI MUNGU AMEKUOKOA NA KUKUSHINDIA
ZABURI 44
1 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetuBaba zetu wametuambia,Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale.

2 Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa,Ukawakalisha wao.Wewe uliwatesa watu wa nchi,Ukawaeneza wao.

3 Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi,Wala si mkono wao uliowaokoa;Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako,Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.

4 Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu,Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo.

5 Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu;Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao.

6 Maana sitautumainia upinde wangu,Wala upanga wangu hautaniokoa.

7 Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu;Na watuchukiao umewaaibisha.

8 Tumejisifia Mungu mchana kutwa,Na jina lako tutalishukuru milele.

9 Lakini umetutupa, umetufedhehesha,Wala hutoki na majeshi yetu.

10 Waturudisha nyuma tukampa mtesi kisogo,Na watuchukiao wanajipatia mateka.

11 Umetutoa kama kondoo tuwe chakula,Na kututawanya kati ya mataifa.

12 Wawauza watu wako bila kupata mali,Wala hukupata faida kwa thamani yao.

13 Umetufanya kuwa lawama kwa jirani zetu,Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.

14 Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa,Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi.

15 Mchana kutwa fedheha yangu i mbele yangu,Na haya ya uso wangu imenifunika,

16 Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru,Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi.

17 Haya yote yametupata, bali hatukukusahau,Wala hatukulihalifu agano lako.

18 Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma,Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako.

19 Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu,Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.

20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu,Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu;

21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo?Maana ndiye azijuaye siri za moyo.

22 Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa.

23 Amka, Bwana, mbona umelala?Ondoka, usitutupe kabisa.

24 Mbona unatuficha uso wako,Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu?

25 Maana nafsi yetu imeinama mavumbini,Tumbo letu limegandamana na nchi.

26 Uondoke, uwe msaada wetu,Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.

Kustawi kutokana NA UWEZA WA MUNGU.

KUSTAWI KUTOKANA UWEPO WA ULINZI WA MUNGUZab 45
1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema,Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme;Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.

2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu;Neema imemiminiwa midomoni mwako,Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.

3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari,Utukufu ni wako na fahari ni yako.

4 Katika fahari yako usitawi uendeleeKwa ajili ya kweli na upole na hakiNa mkono wako wa kuumeUtakufundisha mambo ya kutisha.

5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako;Imo mioyoni mwa adui za mfalme.

6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele,Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

7 Umeipenda haki;Umeichukia dhuluma.Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta,Mafuta ya furaha kuliko wenzako.

8 Mavazi yako yote hunukia manemaneNa udi na mdalasini.Katika majumba ya pembeVinubi vimekufurahisha.

9 Binti za wafalme wamoMiongoni mwa akina bibi wako wastahiki.Mkono wako wa kuume amesimama malkiaAmevaa dhahabu ya Ofiri.

10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako,Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.

11 Naye mfalme atautamani uzuri wako,Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.

12 Na binti Tiro analeta kipawa chake,Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.

13 Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu,Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.

14 Atapelekwa kwa mfalmeNa mavazi yaliyofumwa kwa uzuri.Wanawali wenzake wanaomfuata,Watapelekwa kwako.

15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe,Na kuingia katika nyumba ya mfalme.

16 Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako,Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.

17 Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbuKatika vizazi vyote.Kwa hiyo mataifa watakushukuruMilele na milele.

ZAB 53 MWENYE AKILI TIMAMU  HUMTAFUTA MUNGU 

Mlango 53
1 Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;Wametenda uovu wa ufisadi na kuchukiza,Hakuna atendaye mema.

2 Toka mbinguni MUNGU aliwachungulia wanadamu,Aone kama yuko mtu mwenye akili,Amtafutaye Mungu.

3 Kila mtu amepotoka, wameoza wote pamoja,Hakuna atendaye mema,La! Hata mmoja.

4 Je! Wafanyao maovu hawajui?Walao watu wangu kama walavyo mkate,Hawakumwita MUNGU.

5 Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu,Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru.Umewatia aibu,Kwa sababu MUNGU amewadharau.

6 Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni!MUNGU awarudishapo wafungwa wa watu wake;Yakobo atashangilia,Israeli atafurahi.

KUTOMTAFUTA MUNGU NI UJEURI KAMA ULIVYO UJEURI MWINGINE NI BORA UKAJINYENYEKEZA KWANI HUJUI MUNGU AMEKUHIFADHIA AHADI KIASI GANI

ZAB 41 UWE NI MTU WA REHEMA KWA WENGINE ILI MUNGU AKUREHEMU WEWE.

KIZURI ZAIDI NI KUWAREHENU WENZETU…MUNGU NDIPO HUSHUGHULIKA NA HAJA ZAKO

Zab 41: 1 Heri amkumbukaye mnyonge;BWANA atamwokoa siku ya taabu.

2 BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,Naye atafanikiwa katika nchi;Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake.

3 BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.Katika ugonjwa wake umemtandikia.

4 Nami nalisema, BWANA, unifadhili,Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.

5 Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya,Atakufa lini, jina lake likapotea?

6 Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo,Moyo wake hujikusanyia maovu,Naye atokapo nje huyanena.

7 Wote wanaonichukia wananinong?ona,Wananiwazia mabaya.

8 Neno la kisirani limemgandama,Na iwapo amelala hatasimama tena.

9 Msiri wangu tena niliyemtumaini,Aliyekula chakula changu,Ameniinulia kisigino chake.

10 Lakini Wewe, BWANA, unifadhili,Uniinue nipate kuwalipa.

11 Kwa neno hili nimejua ya kuwa wapendezwa nami,Kwa kuwa adui yangu hasimangi kwa kunishinda.

12 Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza,Umeniweka mbele za uso wako milele.* * *

13 Na atukuzwe BWANA, Mungu wa Israeli,Tangu milele hata milele. Amina na Amina.
TUTAPONA IKIWA TUTAJIDHABIHU KWA AJILI YA WENGINE…MPENZI UWE NI FARAJA NA SULUHU KATIKA MATATIZO NA MAUMIVU YA WENGINE.

JENGA TABIA YA KUWABARIKI NAWE UTABARIKIWA 

ZAB 41 UWE NI MTU WA REHEMA KWA WENGINE

KIZURI ZAIDI NI KUWAREHENU WENZETU…MUNGU NDIPO HUSHUGHULIKA NA HAJA ZAKO

Zab 41: 1 Heri amkumbukaye mnyonge;BWANA atamwokoa siku ya taabu.

2 BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,Naye atafanikiwa katika nchi;Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake.

3 BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.Katika ugonjwa wake umemtandikia.

4 Nami nalisema, BWANA, unifadhili,Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.

5 Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya,Atakufa lini, jina lake likapotea?

6 Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo,Moyo wake hujikusanyia maovu,Naye atokapo nje huyanena.

7 Wote wanaonichukia wananinong?ona,Wananiwazia mabaya.

8 Neno la kisirani limemgandama,Na iwapo amelala hatasimama tena.

9 Msiri wangu tena niliyemtumaini,Aliyekula chakula changu,Ameniinulia kisigino chake.

10 Lakini Wewe, BWANA, unifadhili,Uniinue nipate kuwalipa.

11 Kwa neno hili nimejua ya kuwa wapendezwa nami,Kwa kuwa adui yangu hasimangi kwa kunishinda.

12 Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza,Umeniweka mbele za uso wako milele.* * *

13 Na atukuzwe BWANA, Mungu wa Israeli,Tangu milele hata milele. Amina na Amina.
TUTAPONA IKIWA TUTAJIDHABIHU KWA AJILI YA WENGINE…MPENZI UWE NI FARAJA NA SULUHU KATIKA MATATIZO NA MAUMIVU YA WENGINE.

JENGA TABIA YA KUWABARIKI NAWE UTABARIKIWA 

Shukrani ni dhabihu ya thamani kwa MUNGU WETU.

Zab 56:10 Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.Kwa msaada wa BWANA nitalisifu neno lake.

11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;Mwanadamu atanitenda nini?

12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu;Nitakutolea dhabihu za kushukuru.

13 Maana umeniponya nafsi yangu na mauti;Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke?Ili nienende mbele za MunguKatika nuru ya walio hai.

SHUKRANI NA DHABIHU TUJIFUNZE KATIKA ZABURI YA 24 & 50 & 54: 5-7
Dhabihu ni SHUKRANI INAYOKUSOGEZA KARIBU NA MUNGU.
Mshukuru Mungu kwa kila kiujazacho ulimwengu ni MALI YA BWANA 

Zab 56:

ZAB 50: Mlango 50
1 Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi,Toka maawio ya jua hata machweo yake.

2 Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri,Mungu amemulika.

3 Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza,Moto utakula mbele zake,na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.

4 Ataziita mbingu zilizo juu,Na nchi pia awahukumu watu wake.

5 Nikusanyieni wacha Mungu wanguWaliofanya agano nami kwa dhabihu.

6 Na mbingu zitatangaza haki yake,Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.

7 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena,Mimi nitakushuhudia, Israeli;Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.

8 Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,Na kafara zako ziko mbele zangu daima.

9 Sitatwaa ng?ombe katika nyumba yako,Wala beberu katika mazizi yako.

10 Maana kila hayawani ni wangu,Na makundi juu ya milima elfu.

11 Nawajua ndege wote wa milima,Na wanyama wote wa mashamba ni wangu

12 Kama ningekuwa na njaa singekuambia,Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.

13 Je! Nile nyama ya mafahali!Au ninywe damu ya mbuzi!

14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru;Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

15 Ukaniite siku ya mateso;Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.

16 Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia,Una nini wewe kuitangaza sheria yangu,Na kuliweka agano langu kinywani mwako?

17 Maana wewe umechukia maonyo,Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.

18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye,Ukashirikiana na wazinzi.

19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya,Na ulimi wako watunga hila.

20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako,Na mwana wa mama yako umemsingizia.

21 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza;Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe.Walakini nitakukemea;Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.

22 Yafahamuni hayo,Ninyi mnaomsahau Mungu,Nisije nikawararueni,Asipatikane mwenye kuwaponya.

23 Atoaye dhabihu za kushukuru,Ndiye anayenitukuza.Naye autengenezaye mwenendo wake,Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

MUNGU NI MWEMA

Mlango 24
1 Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya BWANA,Dunia na wote wakaao ndani yake.

2 Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari,Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.

3 Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA?Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili,Wala hakuapa kwa hila.

5 Atapokea baraka kwa BWANA,Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.

6 Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,Inukeni, enyi malango ya milele,Mfalme wa utukufu apate kuingia.

8 Ni nani Mfalme wa utukufu?BWANA mwenye nguvu, hodari,BWANA hodari wa vita.

9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,Naam, viinueni, enyi malango ya milele,Mfalme wa utukufu apate kuingia.

10 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?BWANA wa majeshi,Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

KIPAWA KILICHOMO NDANI YAKO KINAMTANGAZA YESU KRISTO?

*UJUE UMUHIMU WA KIPAWA CHAKE KRISTO KATIKA KUMTANGAZA YESU WAKO* 
MATENDO 28
7 Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya mkuu wa kisiwa, jina lake Publio; mtu huyu akatukaribisha kwa moyo wa urafiki, akatufanya wageni wake kwa muda wa siku tatu.
8 Ikawa babaake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, akaomba, akaweka mikono yake juu yake, na kumpoza.
9 Yalipokwisha kutendeka hayo wengine waliokuwa na magonjwa katika kisiwa wakaja wakapozwa;
10 nao wakatuheshimu kwa heshima nyingi; basi tulipoabiri wakatupakilia vitu vile tulivyokuwa na haja navyo.
Bwana Yesu asifiwe sana sana 
ukisoma Waefeso 4:1-11👉Utaona inaeleza wazi juu ya kupewa kipawa kwa kila mtu aliye ndani ya Kristo Yesu 
Hakuna mtu aliye ndani ya Yesu ambaye hana kipawa chake ,tofauti yetu tu ni kwamba tunapewa kwa kadri ya kipimo chake anayegawa ivyo vipawa ,uwa anagawa kwa kipimo anachokijua mwenyewe cha neema yake ndani ya mtu aliyemwamini na kukaa ndani yake 
Kuwa mtume ,nabii ,mwinjilisti ,Mwalimu ,mchungaji na n.k ni neema ya Kristo tu si kwa ujanja wala akili zako na hiyo neema ndani yake inapokuja kwako uwa inakuja na kipawa cha Kristo 
Kipawa cha Kristo Yesu ni zawadi ambayo unapopewa neema ya bure ndani ya Yesu unakikuta uko ndani ,haupangi wewe bali unakikuta tu ndani umo umo kwa Yesu 
KIPAWA 

Ni zawadi tunayopewa kupitia neema ya Yesu maishani mwetu na kipawa kinaweza kuwa cha kuhubiri ,kunena kwa lugha ,kuponya magonjwa ,unabii,kutafsiri lugha na n.k yaan n zawadi tu ambayo unaipokea kwa neema ya Mungu bila ya wewe kujua wala kutaka ,kwa sababu hiyo kipawa cha Mungu upangiwi na mwanadamu kuwa nacho bali ni Mungu binafsi ndie anayeamua akupe kipi na kipi asikupe 
1Wakorintho 12:9-11

Inaeleza juu ya kupewa karama za aina mbalimbali kama apendavyo Roho mtakatifu 
Karama za Mungu ni kile mtu amekirimiwa na Mungu kwa kipawa kilichopo ndani ya neema ya Yesu 
Kwa lugha ingine ni ivi Karama ni kitu ambacho umetunukiwa ndani ya zawadi ambayo Yesu uwa anagawa kwa kila amuaminie kwa kiwango cha nafasi ya upendeleo alichokikusudia kwa mtu aliyemuamini 
 Kwa hiyo sasa hii zawadi au kipawa cha Kristo kina umuhimu sana kwa mtu aliyemuamini Yesu ,kwa sababu ukiwa nacho kinakupa na kitu cha ukarimu wa Yesu ambacho ni karama na ukiwa na kipawa kinachofanya uwe na karama za Yesu kwa Roho mtakatifu kuna mambo uwa yanatokea kwa mtu aliye nacho Kipawa cha Kristo chenye karama za Mungu ndani yake na ukisoma Matendo 28:7-10 utaanza kuyaona moja baada ya lingine 
Kipawa cha Kristo chenye utendaji kazi kwa karama kwa Mtu wa Yesu uwa kinafanya yafuatayo 

1⃣Uwa kinaleta na kufunua msaada wa Mungu kwa wanadamu 👉Mat 28:8 ,Paulo aliyekuwa na kipawa cha utume ,alipewa ndani ya kipawa chake toka kwa Yesu karama ya uponyaji ,alikirimiwa nguvu ya kuponya baba yake na Publio ,ugonjwa wa kuhara damu na homa na pia ukisoma mstari wa 7 unaona wazi kuwa ukitaka karama za Mungu zifanye kazi vyema kwako hakikisha unakuwa na moyo wa upendo na wa ukarimu kwa watu ,Huyu mkuu wa kisiwa alijua amekaribisha wageni wa kawaida kumbe alikaribisha pia mtu mwenye kipawa cha Kristo chenye karama au utendaji wa nguvu za Mungu za uponyaji na kwa ule ukarimu wake akajikuta akaribisha sio wageni tu bali na karama ya Mungu ya uponyaji 
Ukiwa mchoyo sahau swala la kukutanishwa na karama za Mungu katikati ya matatizo si unajua kuwa Ibrahimu alipokea neno la muujiza wa kupata mtoto akiwa mzee kwa sababu ya kukaribisha kwake wageni ,akajikuta anamkaribisha Bwana Mungu na malaika na wakamkirimia mtoto wa kiume kwa miujiza 
2⃣Ufungua lango la kutatuliwa kwa matatizo ya watu yaliyoshindikana kwenye maisha yao 👉Mat 28:9 ,Baba yake na Publio mkuu wa kisiwa alipoponya kwa karama ya uponyaji ndani ya Paulo ,wengi waliona mwanga ,waliona langu la kupokea uzima na kutatuliwa shida zao ivyo wakaja wengi ,wanadamu wanayo matatizo mengi sana ,mengine wameyaficha na shida yao n kwamba uwa wanajiuliza n wapi pa kuyapeleka ,karama uwa inawapa ishara ya lango la Mungu lililowazi mahali na uwavuta kuliendea na wanapata msaada wakiisha kulijua kuwa liko mahali fulani 
3⃣Umpa yule aliyenacho heshima ambayo hakuwai kuiona kabla na pia umkirimia mahitaji yake 👉Mat 28:10
Kwa hiyo ni ngumu sana kutumika katika karama ya Mungu alafu Mungu asikuhudumie mahitaji yako ,wala hakuna haja ya kuwadai watu pesa ,kile kipawa chenyewe kitakupa karama na karama itakupa mahitaji yako yoote 
Amen amen yako mengi barikiwa kwa haya machacheKaribu Tujifunze kwa pamoja NA Mungu atakubariki. Hallelujah 

Mungu umwaniniyw umempa nafasi ya kutimiza HITAJI LAKO?

NI KWELI UNAMWAMINI MUNGU LAKINI UMEMPA NAFASI NYUMBANI MWAKO?
SHALOM…………………………
2 WAFALME 4:10.

Nakuomba,tumfanyie chumba kidogo ukutani ;Na ndani yake tumwekee kitanda,na Meza na kitanda na kiti,na kinara cha taa;Na itakuwa,atujiapo ataingia humo.
MUNGU Baba Nakutukuza wewe pekee yako,wewe ni mwema YESU kanifundisha kwamba u mwema Sana.MUNGU katika mwanao ninapata ukombozi na msamaha wa dhambi nakuomba unihurumie mimi bwana kwani ni mkosefu,Nisikie EE BWANA ni kwakuwa naitwa kwa jina lako.Nifundishe ROHO WA MUNGU kumtukuza Mungu kila siku.amina.
Imani yako ndiyo itakayokuwezesha ukutane na MUNGU kwa namna ya pekee kabisa na kwasababu imani haionekani kwa macho ila MUNGU tu ndiye aonaye kwahyo nikazie hapa tu kwamba imani yako inayokufanya mtumwa wa binadamu hiyo inakukokota kuelekea motoni.Imani lazima ilete madhara chanya kwenye matendo yako.Usije ukawa mwigizaji ukiwa huku unakuwa hivi Kule unakuwa vile.Somo hili linamtaka yule aliye na imani na MUNGU ndani yake,Avuke hatua ya juu kabisa ni kwamba imani yake ianze kuleta madhara katika maisha yake ya kiroho,Kwahyo sio kila asomaye hapa atachota kitu,Ni lazima uwe na imani dhabiti na si imani inayotegemea miujiza.Imani inayotegemea miujiza ni mfu kabisa kipindi tu miujiza inakuwa haipo.Na cha ajabu sana shetani naye anaweza kukuonesha ukajua ni MUNGU kumbe shetani.
Katika hii habari ya mama mshunami ambaye alimshurutisha Mtumishi wa MUNGU aingie nyumbani mwake ale.Na MUNGU alimpa kibali cha kumtambua Elisha kuwa ni Mtakatifu wa MUNGU ndipo anapomkaribisha na kumwandalia chumba akitoka huko Elisha apumzike,Lakini nyuma ya pazia MUNGU alikuwa anampa baraka ya mtoto kupitia huyu Mtumishi Elisha,Na Mara Elisha alipoona wema wa mama huyu kwa kumpa nafasi apumzike akasema ya kwamba atakuwa na mwana majira Yale Yale ile ni sauti ya MUNGU iliyokuwa ndani ya Elisha,Kwahyo mama alipotengeneza nafasi katika nyuma yake ndipo hapo MUNGU anatumia nafasi hiyo kumbarikia.Neno linasema kwamba aliona kuwa ni mtakatifu wa MUNGU manake hii kwamba Elisha hangepata kibali nje ya utumishi wake kwa MUNGU kwahyo huyu mama alimkaribisha MUNGU aliyekuwa ndani ya Moyo wa Elisha alitengeneza nafasi ya MUNGU katika nyumba yake.Na kwasababu aliwaza moyoni na kuamua kushirikisha na Kisha akamkaribisha basi ni kwamba nguvu ya MUNGU ndiyo iliyomvuta kwa imani yake.
Unamtumikia MUNGU ni kweli Kuna kitu kinaitwa nafasi ya MUNGU katika maisha yako,kama umetenga muda kidogo kwaajili ya MUNGU na mwingi kwaajili yako basi ndio maana kila wakati unakuwa mpweke na huo upweke utaondoka utakapofungua moyo Wako ujaze nafasi yako kwa kumpa MUNGU nafasi katika moyo Wako.MUNGU akutembelee Hata wewe.amina.
BY ZABURI 27:4…

ZAB 40 JINSI GANI MUNGU AKUJIBUPO UWAPO KATIKA UWEPO WA KUPOKEA MAJIBU 

ZAB 40
1 Nalimngoja BWANA kwa saburi,Akaniinamia akakisikia kilio changu.

2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu,Toka udongo wa utelezi;Akaisimamisha miguu yangu mwambani,Akaziimarisha hatua zangu.

3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu,Ndio sifa zake Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,Nao watamtumaini BWANA

4 Heri aliyemfanya BWANA kuwa tumaini lake,Wala hakuwaelekea wenye kiburi,Wala hao wanaogeukia uongo.

5 Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingiMiujiza yako na mawazo yako kwetu;Hakuna awezaye kufananishwa nawe;Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri,Ni mengi sana hayahesabiki.

6 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,Masikio yangu umeyazibua,Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.

7 Ndipo niliposema, Tazama nimekuja,(Katika gombo la chuo nimeandikiwa,)

8 Kuyafanya mapenzi yako,Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.

9 Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa.Sikuizuia midomo yangu; Ee BWANA, unajua.

10 Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.Sikuficha fadhili zako wala kweli yakoKatika kusanyiko kubwa.

11 Nawe, BWANA, usinizuilie rehema zako,Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima.

12 Kwa maana mabaya yasiyohesabikaYamenizunguka mimi.Maovu yangu yamenipata,Wala siwezi kuona.Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu,Na moyo wangu umeniacha.

13 Ee BWANA, uwe radhi kuniokoa,Ee BWANA, unisaidie hima.

14 Waaibike, wafedheheke pamoja,Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize.Warudishwe nyuma, watahayarishwe,Wapendezwao na shari yangu.

15 Wakae hali ya ukiwa, na iwe aibu yao,Wanaoniambia, Ewe! Ewe!

16 Washangilie, wakufurahie,Wote wakutafutao.Waupendao wokovu wakoWaseme daima, Atukuzwe BWANA.

17 Nami ni maskini na mhitaji,Bwana atanitunza.Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,Ee Mungu wangu, usikawie.

MUNGU WETU NI MWEMA NA JEMEDARI ASIYESHINDWA KUTUSIKIA KWA HUTUSIKIA HARAKA SANA HATA KABLA YA KUOMBA HUTUSAIDIA PALE TUNIAPO JAMBO YEYE BWANA WAMAJESHI HULIJIBU.

ZAB 40.     

Zab 38 MUNGU ATAKUPONYA MTUMAINI TU USIANGALIE UGONJWA BALI ANGALIA TUMAINI LA KUPONA

Mlango 38
1 Ee BWANA, usinilaumu katika ghadhabu yako,Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.

2 Kwa maana mishale yako imenichoma,Na mkono wako umenipata.

3 Hamna uzima katika mwili wanguKwa sababu ya ghadhabu yako.Wala hamna amani mifupani mwanguKwa sababu ya hatia zangu.

4 Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa,Kama mzigo mzito zimenilemea mno.

5 Jeraha zangu zinanuka, zimeoza,Kwa sababu ya upumbavu wangu.

6 Nimepindika na kuinama sana,Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.

7 Maana viuno vyangu vimejaa homa,Wala hamna uzima katika mwili wangu.

8 Nimedhoofika na kuchubuka sana,Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.

9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako,Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.

10 Moyo wangu unapwita-pwita,Nguvu zangu zimeniacha;Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.

11 Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu;Naam, karibu zangu wamesimama mbali.

12 Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego;Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya;Na kufikiri hila mchana kutwa.

13 Lakini kama kiziwi sisikii,Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.

14 Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,Ambaye hamna hoja kinywani mwake.

15 Kwa kuwa nakungoja Wewe, BWANA,Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.

16 Maana nalisema, Wasije wakanifurahia;Mguu wangu ukiteleza wajitukuza juu yangu.

17 Kwa maana mimi ni karibu na kusita,Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.

18 Kwa maana nitaungama uovu wangu,Na kusikitika kwa dhambi zangu.

19 Lakini adui zangu ni wazima wenye nguvu,Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi.

20 Naam, wakilipa mabaya kwa mema,Huwa adui zangu kwa kuwa nalifuata lililo jema.

21 Wewe, BWANA, usiniache,Mungu wangu, usijitenge nami.

22 Ufanye haraka kunisaidia,Ee Bwana, wokovu wangu.

JIPE MOYO RAFIKI YANGU MUNGU NI MWINGI WA REHEMA TUBU NA ULIKIRI JINA LAKE ILI UPONE. HOFUHUUA ROHO BALI UAMINIFU NA TUMAINI HUUISHA MOYO NA KUPONYA MARADHI YAKUSUMBUAYO.

TUNA UJASIRI KWA YESU KWA KUWA ALIFUFUKA.

TUNAUJASIRI WA KUSEMA HABARI ZAKE KWAKUWA ALIFUFUKA KATIKA WAFU.
Mwl Debora E. Lema✍✍
1 KORINTHO 15:14
“Tena kama KRISTO hakufufuka, basi kuhubiri kwetu ni bure, na imani yetu ni bure”
IMANI YETU si bure kwakua tunayesema habari zake hayupo katika wafu, alishinda kifo na mauti, hashindwi na lolote, hajawahi kushindwa na hata shindwa, waliomsema vibaya, wakamdhihaki, wakamtemea mate,baada ya siku tatu ALIPOFUFUKA KATIKA WAFU walikiri kwa ndimi zao kuwa YESU NI BWANA. 
HAYUPO KABURINI, UKIMWAMINI ATAFUFUA MAMBO YAKO YOTE YALIYOKUFA.
YEHOVA YU HAI.🇮🇱🇹🇿

ZAB 37 MWENYE HAKI HUCHANUA KWA KUWA ULINZI NA UTOSHELSVU WA MUNGU U JUU YAKE.

Mlango 37
1 Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya,Usiwahusudu wafanyao ubatili.

2 Maana kama majani watakatika mara,Kama miche mibichi watanyauka.

3 Umtumaini BWANA ukatende mema,Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.

4 Nawe utajifurahisha kwa BWANA,Naye atakupa haja za moyo wako.

5 Umkabidhi BWANA njia yako,Pia umtumaini, naye atafanya.

6 Ataitokeza haki yako kama nuru,Na hukumu yako kama adhuhuri.

7 Ukae kimya mbele za BWANA,Nawe umngojee kwa saburi;Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake,Wala mtu afanyaye hila.

8 Ukomeshe hasira, uache ghadhabu,Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.

9 Maana watenda mabaya wataharibiwa,Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi.

10 Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo,Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo.

11 Bali wenye upole watairithi nchi,Watajifurahisha kwa wingi wa amani.

12 Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki,Na kumsagia meno yake.

13 BWANA atamcheka,Maana ameona kwamba siku yake inakuja.

14 Wasio haki wamefuta upanga na kupinda uta,Wamwangushe chini maskini na mhitaji,Na kuwaua wenye mwenendo wa unyofu.

15 Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe,Na nyuta zao zitavunjika.

16 Kidogo alicho nacho mwenye haki ni boraKuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi.

17 Maana mikono ya wasio haki itavunjika,Bali BWANA huwategemeza wenye haki.

18 BWANA anazijua siku za wakamilifu,Na urithi wao utakuwa wa milele.

19 Hawataaibika wakati wa ubaya,Na siku za njaa watashiba.

20 Bali wasio haki watapotea,Nao wamchukiao BWANA watatoweka,Kama uzuri wa mashamba,Kama moshi watatoweka.

21 Asiye haki hukopa wala halipi,Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu.

22 Maana waliobarikiwa na yeye watairithi nchi,Nao waliolaaniwa na yeye wataharibiwa.

23 Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA,Naye aipenda njia yake.

24 Ajapojikwaa hataanguka chini,BWANA humshika mkono na kumtegemeza.

25 Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,Lakini sijamwona mwenye haki ameachwaWala mzao wake akiomba chakula.

26 Mchana kutwa hufadhili na kukopesha,Na mzao wake hubarikiwa.

27 Jiepue na uovu, utende mema,Na kukaa hata milele.

28 Kwa kuwa BWANA hupenda haki,Wala hawaachi watauwa wake.Wao hulindwa milele,Bali mzao wa wasio haki ataharibiwa.

29 Wenye haki watairithi nchi,Nao watakaa humo milele.

30 Kinywa chake mwenye haki hunena hekima,Na ulimi wake husema hukumu.

31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake.Hatua zake hazitelezi.

32 Mtu asiye haki humvizia mwenye haki,Na kutafuta jinsi ya kumfisha.

33 BWANA hatamwacha mkononi mwake,Wala hatamlaumu atakapohukumiwa.

34 Wewe umngoje BWANA,Uishike njia yake,Naye atakutukuza uirithi nchi,Wasio haki watakapoharibiwa utawaona.

35 Nimemwona mtu asiye haki mkali sana,Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni.

36 Nikapita na kumbe! Hayuko,Nikamtafuta wala hakuonekana.

37 Umwangalie sana mtu mkamilifu,Umtazame mtu mnyofu,Maana mwisho wake mtu huyo ni amani.

38 Wakosaji wataangamizwa pamoja,Wasio haki mwisho wao wataharibiwa.

39 Na wokovu wa wenye haki una BWANA;Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.

40 Naye BWANA huwasaidia na kuwaopoa;Huwaopoa na wasio haki na kuwaokoa;Kwa kuwa wamemtumaini Yeye.
 NALIKUWA KIJANA SASA SIJAWAHI ONA MWENYE HAKI AMEACHWA…. UMKABIDHI BWANA NJIAZAKO ….NAE ATATENDA. HALLELUJAH UBARIKIWE SANA KWA SOMO HILI

ZAB 33 UPONYWAJI NA MATUMAINI KWA WANGOJAO BWANA.

Mlango 33
1 Mpigieni BWANA vigelegele, enyi wenye haki,Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

2 Mshukuruni BWANA kwa kinubi,Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.

3 Mwimbieni wimbo mpya,Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.

4 Kwa kuwa neno la BWANA lina adili,Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu.

5 Huzipenda haki na hukumu,Nchi imejaa fadhili za BWANA.

6 Kwa neno la BWANA mbingu zilifanyika,Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake.

7 Hukusanya maji ya bahari chungu chungu,Huviweka vilindi katika ghala.

8 Nchi yote na imwogope BWANA,Wote wakaao duniani na wamche.

9 Maana Yeye alisema, ikawa;Na Yeye aliamuru, ikasimama.

10 BWANA huyabatilisha mashauri ya mataifa,Huyatangua makusudi ya watu.

11 Shauri la BWANA lasimama milele,Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.

12 Heri taifa ambalo BWANA ni Mungu wao,Watu aliowachagua kuwa urithi wake.

13 Toka mbinguni BWANA huchungulia,Huwatazama wanadamu wote pia.

14 Toka mahali pake aketipoHuwaangalia wote wakaao duniani.

15 yeye aiumbaye mioyo yao woteHuzifikiri kazi zao zote.

16 Hapana mfalme aokokaye kwa wingi wa uwezo,Wala shujaa haokoki kwa wingi wa nguvu.

17 Farasi hafai kitu kwa wokovu,Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake.

18 Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao,Wazingojeao fadhili zake.

19 Yeye huwaponya nafsi zao na mauti,Na kuwahuisha wakati wa njaa.

20 Nafsi zetu zinamngoja BWANA;Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu.

21 Maana mioyo yetu itamfurahia,Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.

22 Ee BWANA, fadhili zako zikae nasi,Kama vile tulivyokungoja Wewe.
MUNGU AISHIVYO NA UBARIKIWE KWA KUPATA NENO LA MUNGU LILILO ADILI. 

Endelea kuwa pamoja nami ili tumsifu Mungu wetu. Hallelujah

Huu ni MWAKA WA UTOSHELEVU KWAKO NA MUNGU AKUBARIKI.

TUMEANZA MWEZI WA SABA 
Namba saba ni namba ya UKAMILIFU NA

UTOSHELEVU.

Ninamuomba Mungu Akamilishe na kukupa

utosherevu katika mwezi huu wa 7

Katika tafsiri ya Ki-Ebrania ina maanisha kuwa

ni namba iliyo kamilika, inayojitosheleza.

Katika kitabu cha Ufunuo;

1. Kuna Makanisa SABA.

2. Kuna Matarumbeta SABA

3. Kuna vitasa SABA (Ufunuo 17:1)

4. Kuna watu SABA.

5. Kuna maangamizi SABA

6. Baada ya kukamilisha uumbaji Mungu

alipumzika katika siku ya SABA

(Mwz 2:2-3)

7. Kuna Malaika SABA wenye mapigo SABA

(Ufunuo 5:1)

8. Neno “Yesu” linapatikana mara SABA katika

Ufunuo.

9. Yusufu alitabiri juu ya miaka SABA ya

mavuno na miaka saba ya njaa.

10. (Mwanzo 41:1-57)

11. Namba ya Mungu katika kusamehe ni SABA

x SABA kwa siku (Mt 18:21).

12. Mungu alisema angewapiga Israel mara

SABA kwaajili ya dhambi zao.

(Walawi 26:24)

13. Mungu alisema mtu yeyote atakaye muua

Kaini atalipiziwa mara SABA

(Mwz 4:15)

14. Kuna mambo SABA ya thamani katika kitabu

cha Petero. (Petero 1:7,19, 2:4-7).

15. Naamani aliambiwa akaoge mara saba

katika mto Jordani ndipo atakasike. “Naye

Elisha akampelekea ujumbe, akisema, enenda

ukaoge katika Yorodani mara saba, na nyama ya

mwili wako itakurudia tena. Nawe utakuwa

safi.” (2Wafalme 5:10)

16. Miujiza SABA imerekodiwa katika injili ya

Yohana.

17. Neno “Wimbo Mpya” limetokea mara SABA

katika Agano la Kale

18. Neno “Yesu Akasema” limetajwa mara SABA

katika Injiri (Lu 23:34,43; Yoh 19:27; Mt 27:46;

Yoh 19:28,30; Lu 23:46)

19. Maombolezo kwaajili ya Yakobo yalikwisha

baada ya siku SABA (Mwz 50:10)

20. Pigo la maji kuwa damu kule Misri

lilimalizika baada ya siku SABA (Kutoka 7:25)

21. Israel walizunguka ukuta wa Yeriko kwa

muda wa siku SABA na siku ya SABA

walizunguka mara SABA (Jos 6:4)

22. Pasaka katika Agano la Kale ilidumu kwa

muda wa siku SABA (Kutoka 12:15)

23. Sauli alielekezwa na Samweli kukaa pale

Gilgali akisubiri amri ya Nabii kwa muda wa siku

SABA (1Samweli 10:8)

24. Karamu katika hema ya Musa ilidumu kwa

muda wa siku SABA (Wal 23:34,42)

25. Unajisi katika Agano la Kale ulidumu kwa

muda wa siku SABA (Wal 12:2; 13:4)

26. Mfalme Daudi alifunga akiomba kwaajili ya

mtoto wake kwa muda wa siku SABA (2Sam

12:16,18,22)

27. Mifugo katika Agano la kale ilipaswa

kubakia kwa mama zao kwa siku SABA ndipo

itolewe kwa Bwana. (Kutoka 22:30)

28. Njaa katika Kanani ilidumu kwa muda wa

miaka SABA (2Sam 24:13; 2Ki 8:1)

29. Maadui wakikujia kwa njia moja Bwana

atawatawanya kwa njia SABA

(Kumb 28:25)

• Kuna vitu 7 vilivyo funnuliwa

i. Hands, for benevolence (Kumb 15:8)

ii. Macho kwaajili ya maono (2Wafal 6:17)

iii. Masikio kwaajili ya kusikia (Zab 40:6)

iv. Midomo kwajili ya ushuhuda (Zab 51:15)

v. Madilisha kwaajili ya maombi (Dan 6:10)

vi. Moyo kwaajili ya ujumbe wa Mungu (Mdo

16:14)

vii. Milango kwaajili ya huduma (2Cor 2:12)

30. Yakobo alitumikia miaka SABA ndipo

ampate Raheri (Mwz 29:20)

31. Fedha ilisafishwa mara SABA (Zaburi 12:6)

32. Agano jipya imetaja tabia SABA za “heri”(Mt

5:3-9);

33. Neno “MIMI NI” lililosemwa na Yesu

limetajwa mara SABA katika Injili 

(Joh 6:35; 8:12; 10:7, 11; 11:25; 15:7, 1),
*Salamu za July*

Baraka NA MSAADA WA BWANA KATIKA SADAKA ZAB 20

Zab 20: Mlango 20

1 BWANA akujibu siku ya dhiki,Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.

2 Akupelekee msaada toka patakatifu pake,Na kukutegemeza toka Sayuni.

3 Azikumbuke sadaka zako zote,Na kuzitakabali dhabihu zako.

4 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako,Na kuyatimiza mashauri yako yote.

5 Na tuushangilie wokovu wako,Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu.BWANA akutimizie matakwa yako yote.

6 Sasa najua kuwa BWANA amwokoa masihi wake;Atamjibu toka mbingu zake takatifu,Kwa matendo makuu ya wokovuYa mkono wake wa kuume.

7 Hawa wanataja magari na hawa farasi,Bali sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.

8 Wao wameinama na kuanguka,Bali sisi tumeinuka na kusimama.

9 BWANA, umwokoe mfalme,Utuitikie siku tuitayo.

KILA UFANYALO KWA MOYO MUNGU HUUWEKA UAMINIFU WAKE KWA NA KUKUBARIKI.

TINGWA KULITAFUTA NENO LA MUNGU KAMA ULICHELEWA VILE HIVYO UNAFIDIA NAKUHAKIKISHIA MUNGU NI MWEMA SANA

Kibasa C.N

ZABURI YA 18:25-30 AHADI YA BWANA IMEHAKIKISHWA.

Mlango 18
1 Wewe, BWANA, nguvu zangu, nakupenda sana;

2 BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu,Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia,Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.

3 Nitamwita BWANA astahiliye kusifiwa,Hivyo nitaokoka na adui zangu.

4 Kamba za mauti zilinizunguka,Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.

5 Kamba za kuzimu zilinizunguka,Mitego ya mauti ikanikabili.

6 Katika shida yangu nalimwita BWANA,Na kumlalamikia Mungu wangu.Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake,Kilio changu kikaingia masikioni mwake.

7 Ndipo nchi iliyotikisika na kutetemeka,Misingi ya milima ikasuka-suka;Ikatikisika kwa sababu alikuwa na ghadhabu.

8 Kukapanda moshi kutoka puani mwake,Moto ukatoka kinywani mwake ukala,Makaa yakawashwa nao.

9 Aliziinamisha mbingu akashuka,Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.

10 Akapanda juu ya kerubi akaruka,Naam, aliruka upesi juu ya mabawa ya upepo.

11 Alifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha,Kuwa hema yake ya kumzunguka.Giza la maji na mawingu makuu ya mbinguni.

12 Toka mwangaza uliokuwa mbele zakeKukapita mawingu yake makuu.Mvua ya mawe na makaa ya moto.

13 BWANA alipiga radi mbinguni,Yeye Aliye juu akaitoa sauti yake,Mvua ya mawe na makaa ya moto.

14 Akaipiga mishale yake akawatawanya,Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.

15 Ndipo ilipoonekana mikondo ya maji,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Ee BWANA, kwa kukemea kwako,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwako.

16 Alipeleka kutoka juu akanishika,Na kunitoa katika maji mengi.

17 Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia,Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.

18 Walinikabili siku ya msiba wangu,Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.

19 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi,Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.

20 BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu,Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

21 Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

22 Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu,Wala amri zake sikujiepusha nazo.

23 Nami nalikuwa mkamilifu mbele zake,Nikajilinda na uovu wangu.

24 Mradi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu,Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

25 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili;Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

26 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.

27 Maana Wewe utawaokoa watu wanaoonewa,Na macho ya kiburi utayadhili.

28 Kwa kuwa Wewe unaiwasha taa yangu;BWANA Mungu wangu aniangazia giza langu.

29 Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi,Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.

30 Mungu, njia yake ni kamilifu,Ahadi ya BWANA imehakikishwa,Yeye ndiye ngao yao.Wote wanaomkimbilia.

31 Maana ni nani aliye Mungu ila BWANA?Ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?

32 Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu,Naye anaifanya kamilifu njia yangu.

33 Miguu yangu anaifanya kuwa ya kulungu,Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

34 Ananifundisha mikono yangu vita,Mikono yangu ikaupinda upinde wa shaba.

35 Nawe umenipa ngao ya wokovu wako,Mkono wako wa kuume umenitegemeza,Na unyenyekevu wako umenikuza.

36 Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Na miguu yangu haikuteleza.

37 Nitawafuatia adui zangu na kuwapata,Wala sitarudi nyuma hata wakomeshwe.

38 Nitawapiga-piga wasiweze kusimama,Wataanguka chini ya miguu yangu.

39 Nawe hunifunga mshipi wa nguvu kwa vita,Hunitiishia chini yangu walioniondokea.

40 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Nao walionichukia nimewakatilia mbali.

41 Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa,Walimwita BWANA lakini hakuwajibu,

42 Nikawaponda kama mavumbi mbele ya upepo,Nikawatupa nje kama matope ya njiani.

43 Umeniokoa na mashindano ya watu,Umenifanya niwe kichwa cha mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

44 Kwa kusikia tu habari zangu,Mara wakanitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.

45 Wageni nao walitepetea,Walitoka katika ngome zao wakitetemeka.

46 BWANA ndiye aliye hai;Na ahimidiwe mwamba wangu;Na atukuzwe Mungu wa wokovu wangu;

47 Ndiye Mungu anipatiaye kisasi;Na kuwatiisha watu chini yangu.

48 Huniponya na adui zangu;Naam, waniinua juu yao walioniinukia,Na kuniponya na mtu wa jeuri.

49 Basi, BWANA, nitakushukuru kati ya mataifa,Nami nitaliimbia jina lako.

50 Ampa mfalme wake wokovu mkuu,Amfanyia fadhili masihi wake,Daudi na mzao wake hata milele.

KUHUSU YESU KRISTO.

ASILI MBILI YA YESU KRISTO “MUNGU NA BINADAMU”
“DUAL NATURE OF JESUS CHRIST”
Tokea Dunia ianze, hapajawai toke Mtu yeyote alieishi kama Yesu Kristo. Yesu ni mtu wa maana sana ambaye ni Mwokozi, Mungu katika Mwili “Emanueli” (Isaya 9:6). Yesu sio Nusu Mungu na Nusu Binadamu kama watu na au imani nyingi zinavyo sema. Yesu yeye ni Mungu na ni Binadamu kwa wakati mmoja. Kwa maneno mengine, Yesu alikuwa na asili Mbili tofauti ambazo ni Mungu na Binadamu kwa wakati mmoja. “incarnation”
Biblia inasema kuwa, Yesu ni “Neno” ambaye ni Mungu na alikuwa kwa Mungu na akafanywa kuwa Mwili na kuishi nasi, soma Yohana 1:1 na 14. Hii inamaanisha kuwa, mtu huyu mmoja ambaye ni Yesu alikuwa ana asili mbili za Mungu na Binadamu.
Hii asili ya Mungu haikubadilika pale ambapo “NENO” lilipo kuwa Mwili (Yohana 1:1, 14). Badala yake, Neno liliunga ubinadamu (Wakolosai 2:9). Hivyo basi, Umungu wa Yesu Kristo haukuharibika na au badirika. Zaidi ya hapo, Yesu hakuwa mtu tu ambaye alikuwa na Mungu ndani yake au Mtu aliye fanya kazi ya Mungu pekee, la hasha, Yesu ni Mungu katika Mwili na ni sehemu ya Pili katika Utatu Mtakatifu. Biblia inatuambia katika Waebrania 1 aya ya 3 kuwa: Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi Yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno Lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko mbinguni. Hivyo basi, asilia hizi mbili za Yesu Kristo haziwezi kuchanganywa (Eutychianism), vile vile haziwezi kuwa pamoja na kuwa Mungu-Mtu (Monophysitism). Hizi asili mbili ni tofauti na zinajitemea na wakati huohuo ni moja katika Yesu (person of Jesus). Huu muungano unaitwa Hypostatic Union.
Jedwari lifuatalo litakusaidia uone hizi asili mbili za Yesu Kristo:
*******MUNGU-BINADAMU*******
1. Yesu anaabudiwa (Matayo. 2:2, 11; 14:33)

2. Yesu anamwabudu Mungu Baba (Yohana 17)
1. Yesu anaitwa Mungu (Yohana 20:28; Waebrania 1:8)

2. Yesu anaitwa Mtu/Binadamu (Marko 15:39; Yohana 19:5)
1. Yesu aliitwa Mwana wa Mungu (Marko 1:1)

2. Yesu aliitwa Mwana wa Adam (Yohana 9:35-37)
1. Anaombwa/prayed(Matendo ya Mitume7:59)

2. Anamwomba Mungu Baba (Yohona 17)
1. Yesu hana dhambi/sinless (1 Petro. 2:22; Waebrania 4:15)

2. Yesu alijaribiwa (Matayo. 4:1)
1. Yesu anafahamu kila kitu (Yohana 21:17)

2. Yesu alikuwa na Hekima (Luka 2:52)
1. Yesu anatoa uzima wa milele (Yohana 10:28)

2. Yesu Alikufa (Rom. 5:8)
1. Adhama zote za Mungu zipo ndani ya Yesu (Wakolosai 2:9)

2. Alikuwa na Mwili na Mifupa (Luka 24:39)
USHAHIDI ZAIDI WA ASILI MBILI YA YESU
Mafundisho ya muungano wa Hypostatic ni ya “communication idiomatum” (Ni maneno ya Kilatini “Communication of properties”). Haya ni mafundisho ya adhama mbili za Yesu Kristo za Mungu na Binadamu zote zipo ndani ya Yesu Mtu “person of Jesus”. Hii inamaanisha kuwa, binadamu Yesu alikuwa na haki ya kusema kuwa “Alikuwa na utukufu na Baba Mungu kabla ya dunia kuumbwa soma Yohana 17:5), vile ile kudai kuwa alitoka Mbinguni (Yohana 3:13), na kudai kuwa alikuwa kila mahalai “omnipresence (Matayo 28:20). Haya madai yote ya Yesu ni adhama za Mungu na kuwa yeye Yesu alikuwanayo.
Moja ya Makosa makubwa sana yanayo fanywa na wasio Wakristo ni kushindwa kwao kuelewa kuwa Yesu alikuwa na ASILIA MBILI. Kwa mfano, Mashahidi wa Yehova wao wanamwangali Yesu kama Binadamu na kupuuza adhama zake za Umungu. Mara zote wao hutumia zile aya ambazo zinakiri Ubinadamu wa Yesu na kuzipambanisha na aya ambazo zinasema kuwa Yesu ni Mungu. Kwa upande mwingine, Masayantisti wa Kikristo wao hufanya kinyume chake. Wao wana angalia zaidi upande wa Yesu ni Mungu na kusahau kuwa, Yesu alikuwa Binadamu vile vile.
Ili kumwelewa Yesu vyema, basi kila mafundisho ambayo yanamuhusisha Yesu, hayana budi kuzumgumzia Yesu kama Mungu na Yesu kama Binadamu. Hizo asilia Mbili ni zake. Kumbe ndio maana Yesu katika Luka 2:52 inasema: Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu. Na wakati huo huo alikuwa kila kitu “omniscient” Soma Yohana 21:17. Yesu ni Neno la Mungu aliye kuwa Mwili/Binadamu (Yohana 1:1, 14).
Zaidi ya hapo, Biblia inamhusu Yesu (Yohana 5:39. Mitume wote walimtabiri Yesu (Matendo ya Mitume 10:43). Mungu Baba anatoa ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 5:37; 8:18. Roho Mtakatifu naye anato Ushahidi kuhusu Yesu, Soma Yohana 15:26. Kazi zake Yesu nazo zinashuhudia kuhusu Yesu Soma Yohana 5:36; 10:25. Makundi ya watu nayo yanashuhudia kuhusu Yesu, Soma Yohana 12:17. NA YESU anajishuhudia mwenyewe Soma Yohana 14:6 ; 18:6.
Kuna aya nyingine nyingi ambazo zinamshuhudia Yesu kuwa ni Mungu nazo ni
Yohana 10:30-33; 20:28; Wakolosai. 2:9; Wafilipi. 2:5-8; 

Waebrania 1:6-8; na 2 Petro. 1:1.

1 Timoteo 2:5 inasema , ” Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani, mwanadamu Kristo Yesu, 6. aliyejitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wanadamu wote, jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ” Hivi sasa, kuna Mtu Mbinguni ambaye yupo katika kiti cha Enzi. Yeye ni Mpatanishi wetu kwa Mungu Baba (1 Yohana 2:1). Ni Mwokozi wetu (Tito 2:13). Ni Bwana wetu (Warumi 10:9-10) Huyo Mtu anaitwa YESU.
Hakika Yesu Ni Mungu.

Yote yanawezelana kwa MUNGU.

SIFA YA MUNGU WETU NI KUFANYA YALIYOSHINDIKANA KWA WANADAMU.
Mwl Debora E. Lema✍✍
LUKA 8:43-44
“Na mwanamke mmoja ambae ametokwa na damu miaka 12 aliyekuwa amegaramiwa Mali zake zote kwa waganga ASIPATE KUPONYWA NA MTU YEYOTE (44) Alikwenda nyuma yake akaugusa upindo wa vazi lake na Mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma”
MWANAMKE huyu alitaabika kutibiwa kwa waganga miaka 12 na alipoteza Mali zake, lakini hakupata msaada wowote. Lakini aliamini moyoni mwaka kuwa akigusa tuu upindo wa vazi la YESU atapona, alipotenda alichoamini KWELI AKAPONA. Haijalishi umepoteza wakati wako na Mali zako kuhusu tatizo lako kwa muda GANI, lakini umimwamini YESU Atafanya kwako hapo kwa hapo na utakuwa huru.
MUNGU NINAE MTUMIKIA HANA HISTORIA YA KUSHINDWA NA LOLOTE.
MKABIDHI MAMBO YAKO NAYE ATAFANYA.
YESU YUPO KWA AJILI YAKO.🇮🇱🇹🇿

DHANA YA Mwanamke KIBIBLIA

SEMINA YA WANAWAKE 01Jul17
Mwl Christopher Mwakasege
Kibiblia Mwanamke ni Nani?

Mungu, shetani, mwanamume, mume wako wanapokutazama wanakuonaje? Je wewe unapojitazama kwenye kioo unajionaje?
Mwz 1:27 

Mwanamke wa sura ya kwanza–alitwaliwa katika Neno. Mungu aliachilia uumbaji ktk Roho –ameachilia mbegu.
Mwz 2: 21-23

…23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
Mwanamke katika sura ya ya pili alitoka kwa mwanaume. 
Kwa kawaida tunamzungumzia mwanamke wa sura ya pili.
Mwanamke sura ya pili AMEONGEZEWA kitu na ALIMPUNGUZIA kitu mwanamume. 
Mwanamke wa sura ya kwanza ni yupi na wa sura ya pili ni yupi? Na wewe ni mwanamke yupi?
Mwz 3:15 “nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.”
..kumbuka, kiroho uzao ni wa mwanamke na kimwili uzao ni wa mwanamme. 
Mwz 17:15-16

15 Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara.
16 Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.
17 Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema moyoni…
Wafalme wanatoka kwa mwanamke.
Note tofauti ya Ismail na Ibrahim ilitoka kwa mwanamke. Kwa Sarah kuna vitu vya kumtengeneza mtoto.
…kabla hujatoka tumboni nalikutasa.
Gal 15…aliyenitenga toka tumboni mwa mama.
Yohana alijazwa RM toka tumboni
Zab 58:3

Mtoto hapotei baada ya kuzaliwa..bali ni tangu tumboni.
Tumbo lako la uzazi limesukwaje?
Esta 5:1-3

Note Esta wa sura ya 1, 2, 3, 4 na 5 wanatofautiana. 
Kuna kitu kilichotokea kwenye sura ya 4 kilichombadilisha Esta…na akaenda kama MFALME na siyo malkia.

kina mama wengi wana kitu cha Esta..Mungu hakukuwekea hicho kitu ili ucontrol. .ipo ndani kwa mwanamke kwa ajili ya kumsaidia mwanamume.
Mithali 18:22

Kuna vitu vingine Mungu HAWEZI kumfanyia mume wako mpaka ATAKAPO KUTAZAMA.
1 Petro 3:7

…wanamume kaeni na wake zenu KI AKILI…ili MAOMBI yenu YASIKILIZWE.
Mwanamke amepewa nguvu kubwa ya KUFIKIRI…hivyo shetani humpitia mwanamke kwenye fikra…mwanamke akitumia akili zake …anabomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe. 
Mwanamke wa kitabu cha Yeremia ana uwezo wa KULINDA!
Yer 31:22

Mwanamke ATAMLINDA mwanamume wake…
Yerusalemu hizi zinatofautiana
Eze 16:1-14
Ufu 21:9-10…Yerusalemu hii inatengenezwa mbinguni.
Mungu anapolitazama Kanisa, moja analitazama kwa sura ya mwanamke…Yerusalemu. .. imepambwa kama bibi harusi.
Ufu 7:1-6; 18; Ufu 12:1-17
Unapotokewa na picha ya mwanamke …ni ishara juu ya jambo fulani lililofichika….. 
OMBA: Mungu akarabati tumbo lako ili uzao wako ubarikiwe!
Luk 1:26-30
Esta 2:5-7; 15-17
Je umepata Neema kutoka kwa Mungu?
Tito 2:11-12
Je umepata Neema ya kujua sababu ya nafasi uliyopewa? Ni kuokoka tu? Neema inapokuja huwa loaded na vitu vingine.
Tafsiri ya neema ni pana, ni KIBALI cha Mungu toka kwa Mungu ili kukutumia KUTENGENEZA jambo analotaka kulitumia kwa AJILI ya WENGINE.
Neema hainunuliwi bali unapewa. …Rum 5:15-16
Neema ikija inabeba kitu kwa ajili yako.
Neema itakusaidia kuondoa wazo la kwanini umezaliwa. …litakupa nguvu ya kutafuta sababu ya kwanini Mungu amekulinda!
….inaondoa maswali ya vitu ambavyo hauna…bali unakwenda msalabani kwa ajili ya kuwajibika/kubebeshwa kitu fulani kwa ajili ya wengine..unahakikishiwa ya kwamba Bwana yu pamoja nawe. 
Esta alibeba neema ya Mungu/ kibali…ilimwezesha kuolewa na mfalme! Mungu alimpeleka hapo kwa ajili ya watu wengine. Neema ilikuwepo juu yake kwenye sura za mwanzo hadi sura ya tano ndipo kitu kingine kitokea kwenye ulimwengu wa Roho!
NEEMA SIKU zote hufanya kazi na IMANI.
Neema inapokuja juu yako Mungu anakupa kibali…shetani anachukia..anatengeneza ngome!
Lazima uombe kwa Mungu Neema inapokuja inakuwa Loaded kwa ajili ya wengine, jifunze/pata nafasi ya kumsikiliza Mungu a kufunguliwa

Ulichobeba na hatua ya tatu unapaswa kukipokea.

SHAUKU YA KUMWONA NA KUMPOKEA MUNGU.

TAMANI AU AZIMIA KUMWONA MUNGU.
Mwl Debora E. Lema✍✍
LUKA 19:3-5
“Huyu alikua akitafuta kumwona YESU ni mtu wa namna gani, asiweze kumwona kwa sababu ya umati wa watu maana ni mfupi wa kimo (4) Akatangulia mbio akapanda juu ya mkuyu apate kumwona (5) Na YESU alipofika mahali pale alitazama juu akamwambia Zakayo Shuka upesi kwa kuwa Leo imenipasa kushinda nyumbani nyimbani kwako”
ZAKAYO ALIAZIMIA MOYONI MWAKE KUMWONA LAZIMA AMWONE YESU, alipotambua udhaifu wake kuwa ni mfupi hawezi kumwona kwakua ni mfupi akakimbia mbio, na kwakua MUNGU ni mwaminifu YESU alipofika pale hakuna aliyemwambia atazame juu amwone ZAKAYO Lakini automatic akatazama juu.
UNAPOTAKA KUKUTANA NA MUNGU AY KUONA NGUVU ZAKE TIA BIDII, HATA KAMA KUNA MAMILIONI YA WATU ATAKUHUDUMIA.
FURAHI MAANA MUNGU ANAKUWAZIA MEMA.🇮🇱🇹🇿

KUJIKANA ILI KUMTUMIKIA MUNGU.

UNAFAIDA ULIYEACHA CHOCHOTE KWA AJILI YA KRISTO.
Mwl Debora E. Lema✍✍
LUKA 18:29-30
“Akawaambia, hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya UFALME wa MUNGU asiyepokea zaidi Mara nyingi katika zamani hizi na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”
Kuna watu wanaikana IMANI kwa ajili ya kupata kazi, mume, mke, mali, cheo, umaarufu nk.. Lakini YESU anasema ni heri aliyeacha vyote kwa ajili yake, atapata katika zamani hizi na hatimaye uzima wa milele.
USIOGOPE KUKOSA KAZI, AU KUTENGWA KWA AJILI YA KRISTO, KWANI YEYE ATAKUPA HATA VILE AMBAVYO HAVIPATIKANI KWA WANADAMU.
DAMU YA YESU IKUFUNIKE.🇮🇱🇹🇿

NGUVU YA MSAMAHA.

UMESHA MSAMEHE? 
Mpendwa:
(Mathayo 18:21-22″Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.)
Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mungu Mkuu anakwambia samehe saba mara sabini kwa siku. Cha ajabu watu wa siku hizi wamesha lisahau hili Neno la uzima tena lenye nguvu sana. Kama wewe ni Mkristo halisi, basi utakubaliana nami kuwa, NGUVU YA MSAMAHA ni kubwa kuliko HUKUMU unazo zitoa kwa wale walio kukosea au kosa. Haijalishi wamefanya nini, wewe kazi yako ni kusamehe kama ulivyo samehewa na Yesu.
Isaya 43:25 “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Umeona hapo kwenye Isaya? Yesu anafuta makosa yako si kwaajili yako bali kwa ajili yake yeye. Kwakuwa yeye ni Mtakatifu na mwenye huruma. Wewe huwezi fanya lolote lile liweze kukupa msamaha, ni kwa mapenzi yake tu, ndio maana umesamehewa. Lakini leo umeshahu na kuanza kuhumu yule aliye tenda dhambi, au yule aliye zini. Je, wewe hukuwai zini?
Waefeso 4:26-27′ Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.
Wengi wetu tunalala na vinyongo ndani yetu, huku tukijiita ni Wakristo, tena tulio Okoka. Neno linakwambia, “JUA LISICHWE” huku ukiwa na kinyongo ana au uchungu ndani yako. Huko ni kutenda dhambi. Ukifa na uchingu kwenye moyo wako, basi Jehannam inaweza kuwa yako. 
Mathayo 6:12″Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Basi usichoke kuwasamehe deni wadaiwa wako kama mabvyo Yesu ametusamehe.
Luka 17:4 “Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Umesha pewa formula ya kusamehe. Je, upo tayari kumsamehe yule aliye kukosea?

Utakuwa bora ukipata wokovu

“NITAKUFANYA KUWA BORA NA WA THAMANI KUBWA KULIKO FEDHA NA DHAHABU KWA WOKOVU WANGU”
1 Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,Na utukufu wa BWANA umekuzukia.
2 Maana, tazama, giza litaifunika dunia,Na giza kuu litazifunika kabila za watu;Bali BWANA atakuzukia wewe,Na utukufu wake utaonekana juu yako.
3 Na mataifa wataijilia nuru yako,Na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.
4 Inua macho yako, utazame pande zote;Wote wanakusanyana; wanakujia wewe;Wana wako watakuja kutoka mbali.Na binti zako watabebwa nyongani.
5 Ndipo utakapoona na kutiwa nuru,Na moyo wako utatetemeka na kukunjuka;Kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia,Utajiri wa mataifa utakuwasilia.
6 Wingi wa ngamia utakufunika,Ngamia vijana wa Midiani na Efa;Wote watakuja kutoka Sheba;Wataleta dhahabu na uvumba;Na kuzitangaza sifa za BWANA.
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako,Kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia;Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali,Nami nitaitukuza nyumba ya utukufu wangu.
Bwana Yesu apewe sifa sana sana 
Katika kufuatilia na kutafiti na kwa kulisoma neno la Mungu ,nmegundua kuwa katika siku za mwisho wokovu wa Mungu yaani nuru ya Mungu yenye mwangaza wa uzima na uponyaji kwa wanadamu utakuwa ni kitu cha thamani na bora sana kupita vyoote dunia na watu wa mataifa na wafalme wao watatafuta kuona wokovu wa Bwana na kila ambaye utaonekana kwake yaani juu yake atakuwa ni mtu bora na wa thamani kupita pesa na dhahabu kwa sababu katika Isaya 60:3 inaeleza wazi kabisa kuwa Mataifa wataijilia nuru yako na Wafalme wataujia mwanga wa kuzuka kwako  
Katika Isaya 60:3 yako mambo ma 2 pale yanaelezwa 
1⃣Anaeleza juu ya kujiliwa na mataifa kwa nuru yaani wokovu juu yako 
2⃣Anaelezea juu ya kuonekana kwa nuru ya Mungu juu yako ambayo itawafanya kwa mng’ao wake kuwamulika mpaka wafalme ,ambao kwa kweli watakaposikia na kuona wokovu wa Yesu kwako hakuna namna wataendelea kujizuia watakujia tu mahali ulipo na kuona kuwa unacho kitu bora na chenye thamani kupita fedha na dhahabu zao Ooh haleluya 
Nilikuwa kanisani siku moja ivi na katika ya ibada Mungu akaanza kunipa habari za mambo yatakayofanyika kupitia maisha yangu kwa mataifa na wafalme wao ,unajua niliinuka nikaanza kuwaambia kama kuna mtu bado hajaokoka afanye haraka kuna aina ya maisha nmeyaona ndani ya Yesu aisee n mazuri sana ,kumbe ndani ya Yesu kuna vitu bora ivi na vya thamani kubwa ivi ,maana nilijikuta nasikia mambo ya ajabu sana ,viko vitu ndani ya Yesu vimefichwa ukivijua ivyo umefaulu 
Waefeso 1:12-23 inaeleza juu ya kufanyika sifa ya utukufu wa Bwana juu yetu ambao ukikaa juu yetu ule utukufu wake wenyewe unatutambulisha juu ya falme na mamlaka za ulimwengu huu kabisa 
Kinachotakiwa ni kuendelea kumsii Mungu ayafungue macho yetu ya moyoni ili tuweze kujua na kufahamu kabisa uthamani na ubora wa wokovu wa Mungu ndani yetu ambao kwa ule utendaji kazi wake ndani yetu ,unatupa nguvu zilezile ambazo zilikuwa ndani ya Yesu na zikafanya kazi ya kumfufua na kumuweka juu sana kupita tawala na falme zoote za ulimwengu huu na sisi pia tunazo 😀😀 Oooh haleluya haleluya shetani lazima umeze wembe na kula misumari ya moto yenye damu ya Yesu ,lazima tukubomoe kikamilifu hatukuachi kwa siri hii 
Ubora na uthamani wa nguvu ile ile iliyofanya kazi kwa Yesu na kumfufua uko pia ndani yetu na tuondoke tukauangaze ulimwengu sasa Oooh haleluyaaaa

KUBOMOA MADHABAHU ZA SHETANI.

KUBOMOA MADHABAHU ZA SHETANI
Madhabahu ni nini?

Ni daraja la kuunganisha katika ya ulimwengu wa roho wa Mungu au shetani.

Kuna aina 2 za madhabahu, Madhabahu ya MUNGU (Nuru)na madhabahu ya shetani (giza)
***MADHABAHU YA MUNGU

Watu/watumishi wa Mungu katika Biblia walianza kwa kujenga madhabahu kabla ya kufanya chochote

NUHU – Mwanzo 8:20 “Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.”

MUSA – Kutoka 17:15 “Musa akajenga madhabahu, akaiita jina lake Yehova-nisi;”

YOSHUA – Yoshua 8:30 “Ndipo Yoshua alijenga madhabahu kwa Bwana, Mungu wa Israeli katika mlima Ebali.”

GIDEONI – Waamuzi 6:24 “Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri.”

SAMWELI – 1 Samweli 7:17 “Na kurudi kwake kulikuwa mpaka Rama; maana ndipo ilipokuwa nyumba yake; nako ndiko alikowaamua Israeli; na huko akamjengea Bwana madhabahu.”
***MADHABAHU YA SHETANI
shetani na watumishi wake wana madhabahu ambayo hutumia kupitisha mambo mabaya/maovu kutoka katika ulimwengu wa roho (giza) kuingia katika ulimwengu wa mwili.

Kutoka 34:11-13 “11 Liangalie neno hili ninalokuamuru leo; tazama, mbele yako namtoa Mwamori, na Mkanaani, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 12 Ujihadhari nafsi yako, usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi ile unayoiendea, lisiwe mtego katikati yako. 13 Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yao.”

Mungu anawaagiza wana wa Israeli wasifanye maagano na wenyeji bali wabomea madhabahu zao kwani matatizo ili yakupate lazima yatokee katika madhabahu ya shetani.

Kumb 12:2-3 “2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; 3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.”
MAMBO MUHIMU YANAYOUNDA MADHABAHU
Mungu wa madhabahu

Kuhani wa madhabahu

Washirika wa madhabahu

Kafara ya madhabahu

Nguvu ya madhabahu

MUNGU WA MADHABAHU

Neno “mungu” ni nafasi au cheo kama ilivyo kwa Rais. Kwa maana hiyo unapotaja jina la mungu inakubidi uainishe ni mungu yupi unayemtaja.

Kutoka 6:1-3 “1 Bwana akamwambia Musa, Sasa utaona nitakavyomtenda Farao; maana kwa mkono hodari atawapa ruhusa kwenda zao, na kwa mkono hodari atawafukuza katika nchi yake. 2 Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.”
**MUNGU WA MADHABAHU ZA KISHETANI

shetani ndiye mungu wa madhabahu za wachawi, waganga wa kienyeji, wasoma nyota na mawakala wote wa mauti.

2Kor 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.”

1Wafalme 16:32 “31 Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia. 32 Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.”
*****FANYA MAOMBI YA KUWAANGAMIZA MIUNGU WA MADHABAHU ZA KISHETANI*****

KUHANI WA MADHABAHU

Kuhani wa madhabahu ni mtu mwenye uwezo wa kuleta mambo kutoka ulimwengu wa roho kuingiza katika ulimwengu wa mwili.

Mwanzo 14:18 “Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.”
**KUHANI WA MADHABAHU ZA KISHETANI

1 Samweli 5:5 “Kwa hiyo makuhani wa Dagoni, na mtu awaye yote aingiaye nyumbani mwa Dagoni, hawakanyagi kizingiti cha nyumba ya Dagoni huko Ashdodi, hata leo.”

1Wafalme 18:25-26 “25 Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng’ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini. 26 Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya.”

**** FANYA MAOMBI YA KUWAANGAMIZA MAKUHANI WA MADHABAHU ZA KISHETANI

KAFARA YA MADHABAHU

Madhabahu haiwezi kukamilika kama hakuna kafara kwasababu kila mungu wa madhabahu huhitaji kafara.

Walawi 2:2 “kisha atauleta kwa wana wa Haruni, hao makuhani; naye atatwaa konzi moja katika huo unga mwembamba, na katika mafuta yake, na huo ubani wote; kisha kuhani atauteketeza kuwa ndio ukumbusho wake juu ya madhabahu, ni kafara ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana;”

Zaburi 40:6 “6 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.”

Zaburi 50:8 “Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako, Na kafara zako ziko mbele zangu daima.”

**KAFARA KWENYE MADHABAHU YA KISHETANI

Zaburi 106:36-38 “36 Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao. 37 Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani. 38 Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; Nchi ikatiwa unajisi kwa damu.”

Yeremia 32:35 “Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda.”

****MAOMBI YA KUANGAMIZA KAFARA ZA MADHABAHU ZA KISHETANI

WASHIRIKA WA MADHABAHU

Washirika wa madhabahu ni watu muhimu sana kwenye madhabahu. Kama vile wewe ulivyo ni mshirika wa kanisa Fulani vivyo hivyo kila madhabahu ya kishetani inayo washirika wake.

Eliya alifahamu umuhimu wa kuwa na washirika. 1Wafalme 19:9-10 “9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya? 10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.”

Mungu anamtoa Eliya hofu 1Wafalme 19:18 “Pamoja na hayo nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisichombusu.”

**WASHIRIKA WA MADHABAHU ZA KISHETANI

Hawa ni watu hatari sana, kwakuwa matatizo yote huanzia kwenye madhabahu za kishetani, wanao peleka jina lako/kazi yako/ndoa yako/elimu yako…… ni washirika wa madhabahu ili lijadiliwe kwa lengo la kuharibu maisha yako.

Washirika wa madhabahu ya kishetani mara zote ni watu wako wa karibu

Waamuzi 16:5 “Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.”

Mathayo 10:36 “na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.” Na Mika 7:5-6 “5 Msimwamini rafiki, msimwekee kiongozi tumaini; ilinde milango ya midomo ya kinywa chako ili mkeo alalaye kifuani mwako asijue habari. 6 Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na mavyaaye; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe.”

****MAOMBI YA KUWAANGAMIZA WASHIRIKA WA MADHABAHU ZA KISHETANI

NGUVU YA MADHABAHU

Nguvu ya madhabahu inategemea mambo yote yanayounda madhabahu yaani Mungu wa madhabahu, kuhani wa madhabahu, kafara ya madhabahu na washirika wa madhabahu.

Mashetani walio katika madhabahu wanao mfumo wa uongozi wa kifalme. Imeandikwa Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”

****FANYA MAOMBI YA KUHARIBU NGUVU YA MADHABAHU ZA KISHETANI

Isaya 47:9-12 “9 lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno. 10 Maana umeutumainia ubaya wako; umesema, Hapana anionaye; hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha, nawe umesema moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi. 11 Kwa sababu hiyo ubaya utakupata; wala hutajua kutopoa kwake; na msiba utakuangukia; hutaweza kuuondoa; na ukiwa utakupata kwa ghafula, usioujua. 12 Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.”

Ezekiel 13:17-22 “17 Na wewe, mwanadamu, kaza uso wako juu ya binti za watu wako, watabirio kwa akili zao wenyewe; ukatabiri juu yao, 18 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wanawake wale, washonao hirizi katika viungo vyote vya mikono, wawekao leso juu ya vichwa vya kila kimo, ili wawinde roho za watu; je! Mtaziwinda roho za watu wangu, na kuzihifadhi hai roho zenu wenyewe? 19 Nanyi mmeninajisi kati ya watu wangu, kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, ili kuziua roho za watu ambao haiwapasi kufa, na kuzihifadhi hai roho za watu ambao haikuwapasa kuwa hai, kwa kuwaambia uongo watu wangu wasikilizao uongo. 20 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni kinyume cha hirizi zenu, ambazo kwa hizo mnaziwinda roho za watu kama ndege, nami nitazitoa katika mikono yenu kwa nguvu; nami nitaziachilia roho zile mnazoziwinda kama ndege. 21 Na leso zenu nazo nitazirarua, na kuwaokoa watu wangu katika mikono yenu, wala hawatakuwa katika mikono yenu tena kuwindwa; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. 22 Kwa kuwa ninyi mmemhuzunisha moyo mwenye haki kwa uongo, ambaye mimi sikumhuzunisha; na kuitia nguvu mikono ya mtu mbaya, hata asigeuke, na kuiacha njia yake mbaya, na kuhifadhika; 23 basi, kwa sababu hiyo ninyi hamtaona tena ubatili, wala kutabiri mambo; nami nitawaokoa watu wangu katika mikono yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.”

JE WEWE NI SIMONI MKIRENE?

*JE! WEWE NI SIMONI MKIRENE, AU UNAMUHITAJI SIMONI MKIRENE?*
Bwana Yesu asifiwe sana, ninamshukuru sana Mungu aliyenipa nafasi hii ya kuandika ujumbe huu, 
Pia, nawashukuru sana wote mnaonitia Moyo, Mnaoniombea, mnaonishauri na kunitakia mema, kwenye huduma yangu!!.
Najua kichwa cha ujumbe kinakuvutia kutaka kujua nimeandika nini ndani, ya somo, 
Ninamwamini sana Roho Mtakatifu, kwamba atakuwezesha kuelewa, kile ninachaanisha!!. 
Tuanze kumuangalia MTU anayeitwa SIMONI MKIRENE, wa KWENYE BIBLIA. 
” *Wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simani Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo, ili auchukue msalaba wake*” MARKO 15:21
Ili unielewe ninachomaanisha kwenye ujumbe huu, unatakiwa kuelewa kwanza , 
1.Simoni Mkirene ni nani?

2. Simoni Mkirene Alifanya nini?

3.Alichokifanya Simoni Mkirene, Unatakiwa kukifanya, au kufanyiwa?
1.SIMONI MKIRENE NI NANI?
Hapa nataka nikueleze tu, huyu kwa kifupi, 
Simoni aliitwa Simoni Mkirene kwa sababu alizaliwa kwenye mji unaoitwa KIRENE (CYRENE), Nchini LIBYA. 
Sawa na Mtu tumuite, Mtanzania, Mtemeke, Mgeita, n.k
Kwa maana hiyo, Simoni hakua MYAHUDI, alikua M-AFRIKA, alizaliwa AFRIKA!. 
2.SIMONI MKIRENE ALIFANYA NINI?,
Wakati Yesu yupo kwenye wakati mgumu sana, alipobebeswa Msalaba, akielekea Goligotha, kwa ajili ya Mateso, 
Yesu alipokua kwenye hatua ambayo, kwa jinsi ya kibinadamu, asingependa apitie, 
SIMONI alikua anatoka zake Shamba, AKASHURUTISHWA KUBEBA MSALABA, 
“Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu”. LUKA 23:26
Alimsaidia Yesu kuubeba msalaba lakini kwa kulazimishwa!.

 

3.ALICHOKIFANYA SIMONI MKIRENE, UNATAKIWA KUKIFANYA AU KUFANYIWA?.
Hapa ndipo kwenye somo langu, 
Yesu alikua MYAHUDI, na Simoni, alikua MUAFRIKA, ukiacha masuala ya SIMONI KUSHURUTISHWA, lakini kwa Desturi, ni ngumu kwa WAYAHUDI KUCHANGAMANA NA WATU WA MATAIFA, 
Ingenoga zaidi, kama Yesu angesaidiwa na MYAHUDI MWENZAKE, 

Lakini alisaidiwa na MUAFRIKA, 
Maana yangu ni nini?, 
Ni hivi, 
Inawezekana kuna Mtu upo kwenye kipindi kigumu, kimaisha, kihuduma, kimahusiano, kijamii, kifamilia, kiuchumi, n.k,
Upo kipindi ambacho, kibinadamu, usingependa uupitie, kwa kifupi, unaelekea “goligotha yako”, 
Watu wa nyumbani/karibu/kanisani kwako yaani wayahudi wenzako, hakuna hata MMOJA anayejisumbua kukusaidia KUUBEBA MSALABA WAKO!, 
Unamuhitaji SIMONI MKIRENE WAKO WA KUJA KUKUSAIDIA!, 
Mtu ambaye inawezekana, SI WAKABILA YAKO, SI WA KANISA LAKO, SI WA KARIBU YAKO, aje kufanya huduma yake, ya kukusaidia kuubeba MSALABA!!

Ni Maombi yangu kwa MUNGU, Mtu huyo aje mwenyewe, sio lazima ASHURUTISHWE NA WATU, 
Na wewe unatakiwa kumsubiri, inawezekana YUPO SHAMBA BADO, atakuja, ataletwa na Mungu mwenyewe!. 
Upande wa pili, Inawezekana wew. Ndio Simoni Mkirene, kuna Mtu unatakiwa umsaidie kuubeba msalaba wake, yupo amechoka sana, 
Inawezekana bado upo shamba, hujatambua HUDUMA YAKO, 
Inawezekana una wazo la kusema, ‘atasaidiwa na ndugu zake’, au ‘watu wa kanisa lake’, nakwambia, usisubiri kushurutishwa, Nenda kafanya HUDUMA YAKO, 
Kuna Mambo makubwa yatatokea, baada ya kumsaidia huyo!!. 
Haijalishi anakufahamu, au hakufahamu, WEWE SIMAMA KWENYE NAFASI YA “SIMONI MKIRENE” 
…..Naamini kuna kitu umekiona, kupitia ujumbe huu!. 
MAMBO GANI YANAKWENDA KUONEKANA KWAKO, NA KWA FAMILIA YAKO, NA KWA ULIYEMSAIDIA??, 
KABLA HUJAYAJUA YALIYOTOKEA, JIJIBU SWALI HILI, *JE! WEWE NI SIMONI MKIRENE, AU UNAMUHITAJI SIMONI MKIRENE?*
Tukutane, kwenye sehemu ya Pili ya Somo hili……
 Naitwa Mwl Nick

0712265856

(WhatsApp#)

MTU MUNGU USIOGOPE.

USIOGOPE
Ipo sababu kubwa tunapo sema kuwa, Biblia ni Neno la Mungu. Biblia imekamilika na haina shaka ndani yake bali ni mwongozo thabiti kwa wanao taka kwenda kuishi na Mungu Mkuu, yaani Yesu Kristo.
Mwaka una siku 365 na katika kila siku, Yesu Mungu Mkuu (Tito 2:13) anakwambia usiogope, maana yupo pamoja nawe. 
Isaya Mlango 43: 1 Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, USIOGOPE, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. 
Yesu Mungu Mkuu yupo mahali pote na kwa wakati wote “omnipresent” na hii sifa ni ya Mungu pekee na si ya kibinadamu. ( Mathayo 18:20 ) “Kwa kuwa walipo wawili watatu, wamekusanyika kwa jina langu, mimi nipo papo hapo katikati yao”. Mwenye uwezo wa kukaa mahali pote ni Mungu.
Zaburi Mlango 23: 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 
Mathayo : Mlango 10: 28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Leo nawakumbusha tu kuwa, “USIOGOPE YESU MUNGU MKUU YUPO PAMOJA NAWE”
Pokea ulinzi wa Yesu na USIOGOPE TENA MAANA YESU YUPO PAMOJA NAWE.
Shalom,

KUUKOMBOA MUDA ULIOPOTEZA ILI KUVIPATA ULIVYOPOTEAZA.

By Henry Lameck

Bwana Yesu awe, neno lilotuongoza ni kutoka waefeso 5:15-17 _‘’Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; *MKIUKOMBOA WAKATI KWA MAANA ZAMANI HIZI NI ZA UOVU*. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana’’_~~Mistari hii tumekwenda nayo sana kwa siku ya siku zote nane na msisitizo ukiwa kwenye mstari wa 16*MKIUKOMBOA WAKATI KWA MAANA ZAMANI HIZI NI ZA UOVU*.  Katika bibliakuna wakati unatakiwa ukombolewe ambao ndio umebeba mapenzi ya Mungu na pia biblia imesema *zamani hizi* maana yake ni muda ambao umebeba uovu. Kwa hiyo ili tuweze tembea katika mapenzi ya Mungu inatakiwa tuwe na muda wa kwetu yaani tuukomboe muda na huo muda ukishakombolewa unatakiwa utumike katika kutembea katika zamani hizi.~~Katika kibabu cha Mwanzo 1;1 Biblia inasema hapo mwanzo Mungu aliumba ulimwengu. Na maana hapo bilia inaposema mwanzo maana yake ni kuwakuna lango la Muda lilifunguliwa kwa sababu Mungu aliikata hali ya umilele na akaweka muda. Mungu kaweka muda ili mwanadamu aweze kutembea kwayo. Na Yesu yeye ni alfa na omega maana yake ni mwanzo na mwisho. Katika hali ya kawaida Yesu anaishi kwenye umilele ila yeye kuwa alfa na omega ni ili tupate pa kwenda maana yeye anaishi kwenye umilele lakini katika kuishi kwenye umilele lakini bado yeye ndiye anayeucontrol muda maana yeye ni alfa na omega na yeye ndiye anatusaidia tuweze kutembea kwenye huo muda.~~Muda unafanya kazi na vitu vingi kama Fikra, sheria, muda wa kuabudu, muda wa kulelewa na ni maeneo mapana sana tumepita huko kama hukuwepo pata kanda sikiliza na kusikiliza na utapata kitu cha kukusaidia.*Lengo la semina hii kukuonesha kuwa muda wako umetekwa na unakatikwa kukombolewa kwa kuwa muda huo umebeba aina Fulani ya maisha*  . Na Kwa kuwa hutembei katika mapenzi ya Mungu na ina maana kuna vitu unakosa maana muda umebeba aina ya maisha ya mwanadamu. ~~Leo nataka tungalie kipengele kingine*MUDA WA TAIFA UNALOISHI NDANI YAKE*Leo nataka tuangalie kwa mtiririko wa mambo yafuatayo.*1* *Kila taifa limebeba kuishi kwa kufuata nyakati zilizopangwa juu yake kwa ajili yake**Matendo ya mitume 17:26-28*  _wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote. *Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao*; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu. Kwa maana ndani yakeyeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisisote tu wazao wake_~~Kila Taifa limeubwa kuwa liishi kwa kufuata nyakati, na ukisoma vizuri maandiko utaungana na mimi kuwa nyakati ziliumbwa kabla ya Taifa. Pia kilamuda uliumbwa kabla ya mwanadamu na hivyo muda kwa MUngu ni kitu cha muhimu sana.*2* *Siku ambayo Taifa linazaliwa ni lango la nyakati za aina ya maisha zilizoamriwa juu ya Taifa hilo*Isaya 66:8 Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya?*Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja?**Taifa laweza kuzaliwa mara?* Maana Sayuni, mara alipoona utungu, Alizaa watoto wake.~~Kuna Tofauti kati ya Taifa na Nchi. *Nchi ni ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki, hii ni kwa mujibu wa Biblia*. Na Taifa *ni  mkusanyiko wa watu waliokubaliana  na waishi kwa pamoja chini ya utawala Fulani* Taifa kuzaliwa niishara ya kuwa kuna lango linafunguliwa ,sasa kuna tofauti kati ya nchi kuzaliwa na taifa kuzaliwa.~~Biashara inapozaliwa ina maana kunalango Fulani la maisha linazaliwa ili kuingiza kwenye mfumo wa maisha yaliyoko kwenye biashara hiyo. Ndivyo ilivyo unapozaliwa mara ya pili ina maana unahamishwa kutoka kwenye ufalme wa giza na kuhamishiwa kwenye ufalme wa Mungu.~~Kuna tofauti kati ya Taifa kupata uhuru na nchi kuzaliwa. Tofauti kati ya kuzaliwa Israel na siku ya kuingia kwenyenchi yake. Na kuna wengine hawajui Taifa la Israel lilizaliwa lini. Ngoja nikuoneshe Kitabu cha *Mwanzo 49:1,28* _‘’ Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. *Hizo zote ndizo kabila za Israeli kumi na mbili*. Na hayo ndiyo aliyowaambia babayao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa mbaraka wake aliwabariki_~~Hapa tunaona kuwa familia ya mzee Yakobo iligeuka na kuwa taifa la Israel, na huu ndio muda ambapo Taifa lilizaliwa na kumbuka kuwa Taifa la Israel lilikuwa kati nchi ya Misri. *Kumbu kumbu ta Torati 4:34*  _Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia*taifa toka kati ya taifa lingine*, kwa majaribu, na kwa ishara, na kwa maajabu, na kwa vita, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa maogofya makuu, kama vile Bwana, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu?_~~Taifa la Israel lilikuwa ndani ya taifa lamisri lilipokuwa linazaliwa.  Na unapokuwa upo kuomba kwa ajili ya taifainatakiwa kuwa makini kidogo maana kuna umuhimu sana wa kujua kuwa taifa lilizaliwa lini. Lazima utofautishe kati ya kupata uhuru wa Tanganyika na kuzaliwakwa Tanzania. Kwa maana hii ya kupata uhuru ina maana hii nchi ilikuwepo bali ilikuwa chini ya utawala Fulani. Na Tanzania ilizaliwa  baada ya matokeo ya Muunganiko wa Tanganyika na Zanzibar. ~~Kwa hali ya kiroho taifa la Tanzania halijawahi kutawaliwa, maana Tanzania haijawahi kupata uhuru.~~ *Jana nilipokuwa nafanya maombi yakuombea Uchumi wa watu jana niliuliza kuwa watu wangapi wana Uchumi mbaya. Na pia niliuliza kuwa ni watu wangapi wameona watu katika eneo hilohilo wamefanikiwa na wao hawajafanikiwa. Sasa Kama jana hukunielewa leo tega sikio*~~Kama ni katika nchi hiyo hiyo kuna baadh ya watu wanafanikiwa lakini wewehufanikiwi ina maana hujajiconnect na Uchumi wa eneo wa nchi. Kwa sababu kila nchi inakwenda kwa hatua zake ina maana kuna tofauti kati ya hatua zako nahatua za Uchumi wa nchi.*3* *Ili maisha ya mtu yafanikiwe katika Taifa analoishi inabidi Nyakati zake ziendane pamoja na Nyakati za Taifa hilo**Zaburi 139:16* _Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; *Chuoni mwako ziliandikwa zote pia*, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado_  Mtu huyu siku zake ziliandikwa kwenye kutabu na ina maana mtu anapozaliwa ukurasa mpya unafunguka.  Sasa unganisha na*Matendo ya mitume 17:26* _ Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha *kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao*_~~Kwa hiyo inatakiwa kuwa kwa kila hatua anayoishi mtu yaani majira na nyakati inatakiwa yaendane na mazingiraya kiroho ya eneo nchi husika. Sasa zikiendana tofauti tofauti ina maana kunakuwa na shida Fulani na mtu atakayeishi katika taifa hilo hataweza kufaidi maendeleo ya uchumi ya nchi hiyo. Wageni wakijua mahali taifa linapita na wakajiconnect na Uchumi wa hilo eneo basi uwe na uhakika ya kuwa watafanikiwa kuliko wenyeji.~~ Mungu alituma mtu mbele yao  na alipewa nafasi ya kuwa kiongozi wa nchi na ona ndugu zake walipokuja FARAO aliwauliza kuwa je wanajua kazi gani  ili aweze kuwaconnect na muda wa Taifa hilo. Ghafla wakaanza kuwa watawala wa taifa hilo, Wamisri walipata shida na spidi ya kufanikiwa kwa wana wa Isreal maana walikuwa wanaenda kwa spidi kwa sababu ya  walijua namna ya kujiconnect na Uchumi wa eneo la Misri.~~Kaangalie habari za Isaka, Isaka alifanikiwa katika taifa lile la wafilisti na akapanda na akavuna japo wenyeji hawakuweza na alifunua na visima ambavyo vilikuwa vimefukiwa na baada ya mtu wakagombania. Baada ya kuendelea wenyeji waliona wivu kwa sababu ya maendele ya spidi ya Isaka.~~Uchaguzi wa jiji la London wa mayor wa jiji, alipatikana mhindi. Na iliwapa shida kidogo waingereza pale walipoonamhindi anakuwa mayor. Na Tunajua kabisa wahindi ni wageni uingereza. Na kama ni wageni ina maana kuwa wazazi wake walikuwa wamemuandaa na aliweza kujua namna ya kujiconnect na nyakati za taifa hilo. Sasa jiulize Yusufu aliwezaje, na Daniel alitokea wapi, hawa watu walijua namna ya kuingi akwenye majira na Nyakati za eneo.*4* *Ombea Mipaka ya Taifa kieneo kwa maana hali ya mipaka inaamua hali ya muda wa kiroho ya taifa**Kutoka 19:12* ‘’ _Nawe utawawekea mipaka watu hawa pande zote, ukisema, Jihadharini, msipande mlima huu, wala msiuguse, hata mapambizo yake; kila mtu atakayeugusa mlima huu, bila shaka atauawa_~~Mpaka unaowekwa kwa jinsi ya mwili ni mipika ya kiroho kwanza unaotenganisha aina ya maisha kati ya hao watu/baina ya pande mbili kati ya hali ya kiroho. Katika kitabu cha kutoka tunaona ya kuwa watu hawa walikuwa naMungu yule yule lakini upande wa Musa alikuwa na aina Fulani ya maisha kwa sababu ya eneo alikuwa amekaa na nje ya mipaka ya lile eneo nako walikuwa na maisha tofauti kwa sababu ya Matendo ya Mitume 17:26 ‘’ *Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao*~~Mipaka ya nchi au Taifa Fulani ni mipaka inayoamua hali (maisha) ya kiroho ya sehemu hata ya kiuchumi kwa sababu imepewa majira na nyakati na miapaka yake~~Mipaka ya taifa inaashiria mipaka ya muda wa aifa na kazi yake moja wapo ni kuunganisha muda wa watu husika na muda wa taifa hilo ambalo watu wanaishi. Nchi nyingi sana zinaishi kwenye sheria na kutokea kwenye sheria mama yaani katiba lengo lake ni kuweka kuishi kwenye mfumo Fulani wa maisha.~~Mpinga kristo anapotaka kuleta vitu vyake kwanza lazima atabadilisha majirana sheria  ili kuweza kuwabana watu watakao kuwepo wakati huo waweze kuwa na mfumo Fulani wa maisha . Na ndio maana biblia inasema pasipo maono watu huacha kujizuia maana ana heri mtu anayetii sheria. Na kazi moja wapo ya sheria ni kukufanya uweze kuishi kwenye maono Fulani na kuweza kukufanya uweze kujua matumizi ya muda ambao ndio umebeba maisha.~~Biblia inasema njozi hii ni kwa wakati uliomriwa na ijapokawia biblia inasema ingojee. Watu wengi wanaona tabu sana kutii sheria na kwa kuwa hawana waono na hata kama wanayo hawajui kuwa yanawapeleka wapi. *Isaya 10:13* * Kwa maana amesema, Kwa nguvu za mkono wangu nimetenda jambo hili, na kwa hekima yangu; maana mimi nina busara; nami nimeiondoa mipaka ya watu, nikaziteka akiba zao, nikawaangusha waketio juu ya viti vya enzi kama afanyavyo shujaa.*~~Maana yake ni hali ya mipaka inaamua hali ya kichumi  ya eneo na biblia imetumia akiba na akiba maana yake ni Uchumi wa baade unaotegemea sasa. Kwa hiyo mipaka inashikilia muda na muda  na muda unapitisha maisha na inakuwa na sauti juu ya hali ya maisha yawatu waliochini ya mipaka hiyo.~~Kwa mfano hapa kwetu Tanzania hapa. Na tuanze na huu mpaka kati ya Tanzania na Kenya wakati Fulani ulipata shida kidogo na kilichotokea kuna vitu tuligawana na mpaka leo shirika letu na halijainuka mpaka leo na linasua sua pia angalia na reli iliyokuwepo pale nayo ilikufa afu cheki na Wafanyakazi waliokuwa wa EAC zamani zile wengine hawana kazi hadi leo na hata wale wastaafu hawajaweza kulipwa mpaka leo. Shida ni iko kwenye mpaka na hapo ndipo tulipobanwa na tokea mpaka huo umepata shida hata maisha ya watu na nchi yaliyotegema mpaka huo yalivurugika kabisa. Haya na mambo ya rohoni usigombane na serikali bali omba Mungu kuhusu hili eneo.~~Pia endelea kuombea mpaka wa mashariki mwa nchi yetu ili ukae sawa na uweze kupitisha maisha ambayo Mungu kayakusudia.  Cheki pia mpaka wa Uganda na Tanzania kipindi kile cha Idd Amini na kwa kweli angekuwa anasoma biblia asingegusa kabisa ule mpaka maana kuna vitu vilitakiwa kuwa ule mpaka upishe na ambavyo ulivurugwa ukaraibu kabisa maeno ya eneo lile na nchi yao kwao na ya kwetu ilipata shida maana kuna aina Fulani ya maisha yanayoamriwa na mpaka yakakosekana.~~Pia angalia mpaka wa Msumbiji na Tanzania kipindi kile Taifa na Msumbiji iko chini ya ukoloni, na ona ilivuraga kabisa ule mpaka wa kusini na isababisha maisha ya ile mikoa ya kusini kuwa nyuma ya wakati na fananisha na leo kwa kweli iko nyuma. Na sababu kuu ni mipaka ilipoguswa ilivurugwa na kamaBiblia ianvyosema Isaya 10:13 “ *nami nimeiondoa mipaka ya watu, nikaziteka akiba zao* maana yake Uchumi wa maeno ulivurugwa na *Uchumi* hapa limefichwa kwenye neo *akiba*~~Pia kumbuka kuombea mpaka kati ya Tanzania na Malawi, maana nao unatakakuleta shida kwa sababu nao una sauti ya maisha ya watu wa kusini wanaoutegemea huo mpaka. Haya mambo ni ya ndani sana na ni neema tu ya Mungu ameamua kuyateremsha kwa staili hili.~~Mfano wa Jumuia ya ulaya  na kujitoa kwa uingereza. Uingereza umejitoa Umoja wa ulaya alafu inataka kutumia mpaka kwa ya Umoja wa ulaya na Umojawa ulaya inajaribu kweka mashart kwa uingereza kuwa uingereza inataka kutumia mipaka ya Umoja wa ulaya kupisha tu Uchumi na sio watu. Kwa maana hiyo inakuwa ni ngumu sana kuchagua kitu gani mpaka upitishe maana mpaka huo unaopitisha Uchumi ndio huo unapitisha  na watu sasa uingereza inapokuwa inataka kuchagua kupitisha tu aina Fulani ya maisha inakuwa ni taabu kidogo. Sasa hapa ndipo hekima inahitajika sana kwa nchi zote ambazo zitakuwa zinategema mipaka ya uingereza na mipaka ya Umoja wa ulaya kibishara maana zisipojua cha kufanya Uchumi utayumba,kwa mujibu wa Isaya 10:13.*5* *Muda wa taifa unaweza kukwamisha kwa watu wa taifa hilo kutokuandaliwa kwa ujio wa mabadiliko ya nyakati ya mbele yao**Mwanzo 15:13-16*  _Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa*miaka mia nne*. Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi. Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema. Nakizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado_*Kutoka 2:23-25*  _Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa. Mungu akasikia kuugua kwao, *Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya na Ibrahimu na Isaka na Yakobo*. Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu akawaangalia_*Kutoka 12:1-2, 37-42*  _Bwana akanena na Musa na Haruni katika nchi ya Misri, akawaambia, Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu. Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi, walipata hesabu yao kama watu sita mia elfu watu waume waliokwenda kwa miguu, bila kuhesabu watoto. Na kundi kubwa lawatu waliochangamana mno wakakwea pamoja nao; na kondoo na ng’ombe, wanyama wengi sana. Nao wakaoka mikate isiyochachwa ya ule unga waliouchukua walipotoka Misri, maana, haukutiwa chachu, kwa sababu walitolewa watoke Misri, wasiweze kukawia, nao walikuwa hawajajifanyia tayari chakula__Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa ni miaka mia nne na thelathini. Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri. Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za Bwana kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa Bwana, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao_~~Ukiangalia kitabu cha Mwanzo ukaona kuwa muda wa agano wa kukaa Misri ulikuwa ni miaka 400 ‘’ . _nao watateswa muda wa *miaka mia nne*_ una unakuta muda wa mateso ulikuwa umeisha na ndio maana walipoanza kulia haikutakiwa tena waendelea kulia pale  na ndio maana Mungu alilikumbukaagano. _*Mungu akakumbuka agano lakealilolifanya na Ibrahimu na Isaka na Yakobo*_  . na ndio maana Mungu alianza mapema kumuandaa Musa kwa ajili ya kuja kuwaokoa wana wa Israel ili waweze kuondoka katika taifa Misri.~~Muda wa taifa unaweza ukatekwa na ukakwamisha kabisa watu na wana wa Israel walipolia kwa Bwana, Mungu alilikumbuka agano lake alilolifanya na Ibrahimu. Wana wa Israel walipokuwa wanaomba walikuwa wanaomba maisha yao yabadilishwe maana hawakuwa wanaomba ili waweze kuondolewa katika taifa hilo. Lakini agano linasema kuwa baada ya miaka 400 wanakuwa hawana uhalali tena wa kuweza kuishi chini ya Utawala wa Farao na ilitakiwa waweze kuondoka.~~Na maana ya agano lilokuwepo lilikuwa linasema hibi  baada ya miaka 400 Mungu alikuwa hahusiki tena na waowakiwa Misri na ndio maana Mungu alimbebesha Musa majira na nyakati ili aweze kulitoa taifa lileMisri, na una mpaka wakakubali iliwachukua miaka 30,walipokuwa wanajadiliana namna ya kutoka huko Misri.  Na ina maana kila kitu kilistop kwa muda wa miaka 30 walipokuwa wanavutana.~~Baada ya kukubali kuondoka tena iliwachukua miaka 40 kuweza kuingia katika nchi ambayo Mungu waliwaambia kwa sababu ya kubishana tena njiani. Na ukijumlisha jumla ni miaka 70 yaani ile 30 wakati wanabishana kutoka misri na miaka 40 wakati wakiwa safarini.  Na kwa maana hiyo muda wa agano wao wakukaa katika nchi ya kwao ulikuwa nyuma kwa miaka 70. Umewahi fikiria kwa muda wote huo ni mambo mangapi yalistop.  Sasa jumlisha na ule muda waliokaa Misri yaani miaka 400 yote na jumla na hii ni 470 ina maana yote ilistopkabisa.~~Angalia *Kutoka 23: 23,28-30* _ Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwenye Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawakatilia mbali. Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.*Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja* nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua.*Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, hata utakapoongezeka wewe, na kuirithi hiyo nchi*_~~Anazungumzia kipindi kipi, ni kipindi wanapojiandaa kwenda Kanani. Na walipovuka Jordan walianza kupamba nakitu kingine na spidi ya kuwatoa ilikuwa inategemea sana maandalizi waliyokuwawanayafanya  maana halikuwa suala la lakuwatoa wale watu waliokuwa wanatakiwa kuondolewa bali ni suala la wao kujiandaa.~~Hata baada ya wao kuweza kujiandaana kuingia ile nchi na Joshua aliwowarithisha watu wote wakasema sisi na nyumba zetu tutamtumikia Bwana. Na kizazi chao wote waliweza kumtumikia Bwana kwa muda wao hadi kizazi chao kilipoisha.  Na ndipo kiliinukakizazi kingine kisichomjua Bwana na hiki ni kipindi cha Waamuzi.*Na leo nataka nikupe agenda za maombi ya kuombea ili taifa letu liweze vuka hapa mahali**1*  *Omba Mungu awasaidie viongozi wanapotaka kuleta mabadiliko kwenye taifa, familia, siasa, kanisani au eneo lolote lile ambalo Mungu anataka mabadiliko*.~~Musa alipewa upako lakini kuweza kuleta mabadiliko  lakini ilimchukua miaka 30 na kama tungesema ni vipindi vya siasa tungesema ni awamu tatu maana ni miaka 10 bado tu mabadiliko hayajafikia na pia ongeza na miaka mingie 40 yaani bado wanabishana tu. *2* *Mungu ainue watu kuwahimiza na kuwalinda watu ambao Mungu kawaandaa kwa ajili ya kubeba muda wa kiroho ili kuwasaidia watu kubeba muda wa taifa wa kiroho ili kuwasaidia watu kuishi muda huo*~~ *Musa* alizaliwa ili aweze kubeba majira na nyakati za kulibadilisha taifa naIsrael ili litoke Misri na linekee Kanani. Na alishindwa kufika kwa sababu ya kushindwa kuchukuliana na watu wale. Katika wakolosai 4:5 biblia inasema enendeni kwa hekima na watu walio nje. Omba Mungu atoe hekima hii kama alivyotoka kwa sulemani ya kujua namnaya kuwaongoza watu.~~Naongea na watu kama akina*Joshua* ambao Mungu anawatafuta kwa ajili ya kuwarithisha watu wake urithiambao Mungu kakukusudia~~Naongea na wana wa *Isakari wanaojua Nyakati na mambo yanayotakiwa kufanyika katika nyakati hizo*~~Naongea na watu kama  *Esta* wa kulikomboa taifa lote, watu kama*Daudi* wenye kuleta uchaji na ufalme wa Mungu katika nchi. Maana Daudi ndiye aliyeleta kiti cha enzi cha Bwana na sanduku la Bwana.~~Watu kama *Samweli* maana samweli alipitisha watu wawili mikononi mwake Daudi na Sauli. Na omba Mungu awafanye hawa watu washike zamu zao na hata kama walikuwa wamejificha wapi Munguatawafuata hata kwa vichaka vya moto ili walifanye kusudi la Bwana.*3* *Mungu awape kuelewana watu waliopewa muda wa kitaifa kwa kufanana na ili kwamba katika hali hiyo ya kila mtu kuwa na majukumu tofauti lakini waweze kuelewana*~~Musa na Haruni walikuwa na majukumu tofauti na Haruni ndiyo alikuwa anaisema ndoa ya Musa na Mungu akamkasirikia sana Haruni na isingekuwa Musa kuomba Mungu akifanya kitu kibaya sana. Omba watu  hawa waelewane ili kusitokee ufa, maana Taifa la Israel lilisimama kwa siku7  ili kutatua huu mgogoro.~~Yusufu  na Faro waweze kuelewana ilikazi ya Bwana iweze kufanyika. Na kisiwepo izuizi~~Daudi na wana wa Isakari ili waweze kutumia muda vizuri sawa sawa na kusudi na Bwana.~~Samweli na Sauli waweze mtii Bwana na kulifanya taifa lilipie kipindi kizuri na isitokee tena Ikabodi maana yake utukufu kwa Bwana kuondoka katika Taifa.~~Elia na Ahabu waweze elewana na taifa liache kuabudu miungu mingine na limrudie Bwana.~~Esta na Ahusero ili kuweza kulisaidia taifa. Modekai walikuwa anamuambia Esta kuwa yupo kwenye muda wake lakini walikuwa hawambebi kwenye maombi ili ndoa yake ikae vizuri maana ndiyo ilibeba maisha ya kwao. Na iliwagharimu siku tatau kufunga na kuomba ili kuerejesha suala hili mahali pake baada ya kuharibika.~~Daniel na watawala wa Babeli ili nchi ikae vizuri.*4* *Mungu awape kuelewana kati ya aliyebeshwa muda wa kiroho wa taifa na watu wake*~~Joshua na wana wa Isarel, japo walimzoe sana Musa lakini Mungu alitaka pia Joshua amtumikie na akamilishe kusudi lake maana muda wa Musa ulikuwa tayari umeisha.  Na wawe na kibali machoni pa watu wote wa Bwana.~~Elia na Ahabu, maana Elia alikuwa ameibuka tu na watu kama hawa wapo tukiomba Mungu anawaleta na atawaibua, japo Elia alibeba majira na Nyakati za taifa. Japo Elia alikuwa na mamlaka juu ya muda ila japo alisimamisha muda bado lakini na yeye alipata shida maana miaka 3 ya ukame alilishwa na kunguru.~~Mikoani ninakopita huwa naona watu kiu waliyonayo na naomba Mungu sana ili Mungu ainue waalimu wa kuweza kutusaidia taifa hili liweze pata neno la Bwana maana hatuwezi tumika sisi wenyewe katika taifa zima la Tanzania lakini watu wana kiu sana ya neno la Mungu. Na ukiona kiu ya neno la Bwana inaongezeka basi ujue kuwa ni Mungu anataka kuwapa melekezo watu wake kwa ajili ya kutembea katika majira yake na nyakati zake.*HIZI NI AJENDA ZA MAOMBI NA OMBEA SANA MAANA KUPONA KWA TAIFA NI KUPONA KWAKO*

USIKATE TAMAA NDUGU MUNGU NI MWEMA.

2017/06/30
*SEHEMU YA 2.*
Tunaendelea pale tulipoishia Jana
Andiko la Msingi lilikuwa ni 1Samweli 30:1-20
*Kwa nini usikate tamaa?*
Ukweli zipo sababu nyingi ndani ya Biblia lakini kwa mtazamo wangu sababu kubwa inayozibeba zote ni hii *”Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda,KWA SABABU YEYE ALIYE NDANI YENU NI MKUU KULIKO YEYE ALIYE KATIKA DUNIA” (1 Yohana 4:4).*
Haleluya, ukiijua kweli hii na maadam unaenenda kwa uaminifu mbele za Mungu HAKUNA sababu ya kukata tamaa kwa sababu aliye NDANI yako ambaye ni Mkuu (mweza wa yote) anasema;
“Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako;nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu” (Isaya 41:10)
“Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto,hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza” (Isaya 43:2).
“Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana” (Isaya 54:17).
“Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili;je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza?” (Yeremia 32:27)
Mfalme Daudi naye kwa kuthibitisha kweli hii anatuambia *”nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maanaWewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji” (Zaburi 23:4).*
Mtume PAULO anakazia kwa kusema *”Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu (Wafilipi 4:13).”*
Tena zaidi ya yote BWANA Wetu Yesu anasema‘…

*MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI’.*
Naam tukirejea kwenye andiko letu la somo, tunaona kwamba Mfalme Daudi licha ya kukatishwa tamaa si tu na adui zake bali hata askari na rafiki zake hakukubali kukata tamaa, bali BWANA ambaye Daudi alimtegemea, alimtia nguvu mpya hata maandiko yanasema *‘Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia.Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote’(1 Samweli 30:17&19).*
Mpenzi msomaji wangu naamini ujumbe huu umekuongezea imani ndani yako,NAAM USIKATE TAMAA MTETEZI WETU YU HAI,NI MUNGU MWENYE NGUVU TENA MSHAURI WA AJABU, mpe leo nafasi akusaidie.
*NA NIKUTAKIE MAISHA MEMA*

SAA ya wokovu ni SASA.

SAA YA WOKOVU NI SASA!NINI MAANA YA KUOKOKA?

KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya;

Kunusurika, kusalimika, kupona, kukombolewa, kufunguliwa au kutoka katika janga au hatari fulani.Ambavyo jamii yetu maneno haya tunayatumia sana,
NINI MAANA YA WOKOVU?  

Watu wengi neno hili wamelitafsiri vile wa pendavyo au waonavyo sasa Swali hili acha lijibiwe na maandiko matakatifu, na maneno haya yasibadilishwe kwamba ni wakati gani wa kuokoka kitendo kikishamalizika cha kukiri kifuatacho ni uwokovu kwa mjibu wa neno, fuatilia hapa chini,

“Kwasababu ukimkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa mtu hukiri hata KUPATA WOKOVU”. (Rum 10:9-10.)
Baada ya kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako, ni muhimu sana kupata mafundisho ya awali, yatakayokusaidia kujua kwa hakika, maana ya KUOKOKA au WOKOVU; “ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.” (Efe 4:14)

 

Lini unatakiwa ufanye uamuzi huu muhimu?

Hebu MUNGU na aseme nawe kupitia maneno yake ambayo ni amina na kweli anasema:

Warumi 13:11 

Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
2Wakorintho 6:2 

“Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa”
Biblia inaonya kuwa “tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa” yaani wakati huu unaposoma hapa ndio wakati wako wa kutubu na kumgeukia Mungu kwa njia ya kristo kama bado haujafanya hivyo kwani huu ni uamuzi ambao kila mwanadamu lazima aufanye.Mungu ana kalenda yenye miaka mingi lakini kwenye swala la kuukiri wokovu wa kristo wakati ni sasa..Ninakuomba umpe kristo maisha yako,ili hata kama ukifa muda wowote akupokee na uishi naye milele.
WOKOVU SIO DINI

MAANA HALISI YA WOKOVU

Wokovu ni mpango wa Mungu mwenyewe wakumtafuta na kumkomboa Mwanadamu.
Baada ya Adam na Hawa wanadamu wa kwanza kutenda dhambi na kuvunja uhusiano wa Mungu na Mwanadamu , bado Mungu aliendelea kumpenda mwanadamu na kutafuta ni kwa namna gani na kwa njia ipi ya kurudisha uhusiano wake na mwanadamu aliyemuumba.
“kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu,hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele, Yohana 3:16”
“Kila mtu amwaminiye” hii ina maana kwamba wokovu ni kwa wale tu watakao mwamini mwana pekee wa Mungu ambaye ni Yesu Kristo na ambao hawajamwamini hawajaokolewa hivyo wamepotea na hawana uzima wa milele. Wokovu ni njia pekee aliyoichagua Mungu ili kurudisha uhusiano wake na Mwanadamu kwa Kumwamini Yesu Kristo.
Usidanganyike wala mtu yeyote asikudanganye Wokovu unatoka kwa Mungu mwenyewe kwa njia ya Kristo Yesu. “Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakaseni na uchafu wenu wote na vinyago vyenu vyote. Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu nami nitawapa moyo wa nyama. Nami nitatia Roho yangu ndani yenu na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu na kuzitenda, Ezekiel 36:25-27”
“Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao , Nao watakuwa watu wangu, kwa sababu nitawasamehe maovu yao na dhambi zao sitazikumbuka tena, Waebrania 8:10,12” “Naye atazaa Mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao, Mathayo 1:21” Hivyo mtu aliyepokea wokovu halisi wa Mungu hatendi dhambi yoyote kwani anaongozwa na Mungu mwenyewe kwa njia ya Roho Mtakatifu na amri za Mungu kwake sio nzito (Yohana 14:26). Anaishi maisha ya utakatifu, yanayompendeza Mungu ( Zaburi 16:3)
MAANA HALISI YA DINI

Dini ni mpango wa wanadamu wenyewe wa kumtafuta Mungu. Na Mungu ameukataa mpango huu Kwani haufikii viwango anavyohitaji. “mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzuia tamaa za mwili, Wakolosai 2:23”

“Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami, nao huniabudu bure, wakifundisha maf- undisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Mathayo 15:8-9”
Hivyo dini haiwezi kumusaidia mtu kushinda dhambi kwani anakua hana msaada wowote wa Mungu atajitahidi kujizuia kwa ukali lakini atashindwa. Na kwa mtu anayeshiklia dini kwake amri za Mungu ni nzito.Mtu yey- ote anaweza kuanzisha dini na kupata wafuasi wengi laki- ni sio wokovu kwani unatoka kwa Mungu mwenyewe.
WOKOVU NI HAPA DUNIANI

Usikubali uongo wowote wokovu ni hapa duniani na baada ya kufa ni hukumu na hukumu hii itategemea uliishije hapa duniani.” Na Kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, baada ya kufa hukumu, Waebrania 9:27”
“Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo Watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliofanya mabaya kwa ufufuo wa hukumu Yohana 5:28-29”
Kwa hiyo maisha yetu ya hapa duniani ndiyo yatakayoamua hukumu yetu itakavyokuwa.

Mungu amezibitisha mwenyewe kuwa kuna Watakatifu Duniani.”Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, Nao ndio nliopendezwa nao, Zaburi 16:3”

Kataa uongo wowote tunaokoka hapa duniani na tunaishi Maisha ya utakatifu yanayompendeza Mungu.
SALA YA TOBA

Inawezekana kabisa ya kuwa wewe unayesoma ujumbe huu hujaokoka – yaani hujampokea Yesu Kristo ndani ya moyo wako kama Bwana na Mwokozi wako. Lakini sasa umeona umuhimu wa kumpokea Yesu Kristo katika maisha yako.
Naamini Roho Mtakatifu ameweka fursa hii mikononi mwako kwa mpango maalum wa Mungu ili ufike mahali pa kutubu na kuokoka. Inawezekana kabisa, pia ya kuwa hujawahi kuambiwa juu ya umuhimu wa wewe kuokoka. Lakini napenda kukuambia ya kuwa ni mpango wa Mungu uokoke. Soma Wakolosai 1:13,14 na Yohana 1:12-14 na 1 Timotheo 2:3-6 na Warumi 1:16,17 na Yohana 3:7. Ni vigumu kuona baraka za Damu ya Yesu bila ya kuokoka.
Kwa hiyo kama unataka kuokoka – tafuta mahali palipo na utulivu, na usome kwa sauti sala ifuatayo: (ukiweza unaweza kupiga magoti unapoomba sala hii)

“Ee Mungu wangu ulie Mtakatifu. Ninakuja mbele zako. Mimi ni mwenye dhambi. Naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizokukosea katika maisha yangu. Ninatubu kweli. Naomba damu ya Yesu Kristo iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho wako – uwe Bwana na Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Ahsante kwa kunisamehe na kwa kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina.
Ikiwa umesoma sala hii kwa kukusudia kabisa na kwa imani, basi wewe umeokoka na dhambi zako zimesamehewa na kusahauliwa na Mungu sawasawa na alivyoandika katika neno lake. Damu ya Yesu iko juu yako sasa.
Baada ya kuokoka

Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:
1.Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7)

2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11)

3.Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17)

4.Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6)

5.Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25)
Ukipenda unaweza kuniandikia kwa anwani hii hapa chini juu ya uamuzi uliofikia leo wa kuokoka, ili tumshukuru Mungu pamoja, na tuzidi kukuombea; na pia, tukutumie maandiko mengine ya kukusaidia

MTHIBITISHE MUNGU ULIYENAYE KATIKATI YA MATAIFA

MTHIBITISHE MUNGU ULIENAE KATIKATI YA MATAIFA.
Mwl Debora E. Lema✍✍
SEHEMU YA NNE. (HITIMISHO)
BAADA YA MUNGU KUKUSHINDIA UTUKUFU UTARUDI KWAKE, NA WEWE UTAHESHIMISHWA.
DANIELI 3:28a, 30
“Nebukadreza akanena akasema, na ahimidiwe MUNGU wa Shedraka, na Meshaki, na Abednego, aliyewatuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini.(30) Kisha mfalme AKAWAKUZA Shedraka, Meshaki na Abednego katika wilaya ya Babeli”
IKIWA UNA MUNGU WA KWELI NDANI YAKO hawezi shindwa na lolote, vita vijapoinuka pale UNAPOSIMAMA katika kweli yake ATAJITHIBITISHA mwenyewe wala ww hutatumia nguvu wala akili kumthibitisha, kikubwa wewe dumu katika kuisimamia kweli hata kama mazingira hayakupi tumaini, wakati ambao hamna tumaini ndipo MUNGU hujidhihirisha kwamba yeye ndie MUNGU asiyeshindwa na lolote.
MAANDIKO YANASEMA, YEYE MUNGU AMEAHIDI KUWA NASI TANGU SASA MPAKA UKAMILIFU WA DAHARI.
TENDEA KAZI ULICHOJIFUNZA.
 UBARIKIWE🇮🇱🇹🇿

ONDOA KABISA MSONGO WA MAWAZO.

NJIA NZURI ZA KUONDOA MSONGO WA MAWAZO. 
Jifunze baadhi ya njia nzuri ambazo unaweza kuzitumia kukabilina na msongo wa mawazo. Kwa sababu kila mmoja wetu yupo tofauti na vitu vinavyoleta msongo wa mawazo ni tofauti, hakuna njia moja sahihi ya kuleta mabdailiko kwako. 

Zifuatazo ni njia za kutumia:
1: Kukwepa Vyanzo Vya Msongo Wa Mawazo: Si rahisi kukwepa kila chanzo cha msongo wa mawazo na ni vibaya kukwepa chanzo cha msongo wa mawazo ambacho inabidi ukikabili. Jifunze kusema hapana: 
 Wakwepe watu wanaoksababishia msongo: Kama kuna mtu anakusababishia msongo wa mawazo kila wakati, punguza muda wa kukutana naye au vunja kabisa mahusiano naye.
 Dhibiti mazingira mabovu: Kama habari za jioni za kwenye TV zinakukera, zimisha hiyoTV na kama msongamano wa magari kwako ni kero, chukua njia nyingine isiyo na msongamano hata kama ni ndefu zaidi.
 Kwepa mada zinazokupa maudhi: Kama mada za dini au siasa hukupa maudhi, acha kushiriki kwenye mada hizo. Kama kila siku unalumbana na watu fulani kuhusu mada fulani, acha kuanzisha mada hizo au tafuta kisingizio cha kuondoka mada hizo zinapoanzishwa.
 Chunguza ratiba yako: Itazame kwa kina ratiba yako, majukumu yako na kazi ulizojipangia kwa siku. Kama mambo ni mengi mno, yagawanye kwenye makundi ya yale ambayo ni lazima yafanywe na yale ambayo ni muhimu kufanyika. 
2. Badili Mazingira ya chanzo:Kama inashindikana kukwepa chanzo cha msongo wa mawazo, badilisha mazingira yake. Jaribu kufikiria ni nini cha kufanya ili chanzo hicho kisijitokeze tena hapo baadaye.
 Onyesha hisia zako: Kama kuna kitu au mtu anakukera, mweleze wazi kabisa kwa njia ya kistaarabu. Kama husemi, unajenga chuki na kuiacha hali ikibaki pale pale.
 Usilee matatizo: Usilikalie lile linalokukera, liseme wazi na chukua hatua mara moja ya
3. Badilika Kuendana Na Chanzo: Kama huwezi kukibadili chanzo cha msongo wa mawazo, wewe badili mtazamo wako kuhusu chanzo hicho:
• Rekebisha viwango vyako: Moja ya sababu ya kujipa msongo wa mawazo ni kutaka kila kitu kiende sawa kwa kiwango cha hali ya juu. Usijiweke kwenye mtego wa kushindwa kwa kujiwekea viwango vya juu kiufanisi. Jiwekee viwango vinavyowezekana kwako na kwa wenzako na jifunze kukubali matokeo ambayo hayakufika kiwango lakini siyo mabaya.
• Yakumbuke mazuri yako: Msongo wa mawazo ukikunyemelea, chukua muda kidogo kushukuru kwa yale yaliyo mazuri katika maisha yako, ikiwa ni pamoja na vipawa nyako vizuri na vyenye nguvu. Hili litakusaidia kukupa mtazamo tofauti wa mambo yaliyo mbele yako.
4. Kubaliana Na Yale Ambayo Huwezi Kuyakabili: Vyanzo vingine vya msongo wa mawazo huwezi kuvibadili wala kuvizuia. Huwezi kukizuia kifo cha mtu wa karibu yako, wala ugonjwa mkubwa, au mporomoko wa uchumi wa nchi. Hapa inafaa kukubaliana na hali ingawa ni vigumu.
 Usijaribu kudhibiti kisichowezekana: Vitu vingi sana katika maisha yetu vipo nje ya uwezo wetu – hasa tabia za watu wengine. Kuliko kung’anga’nia na kugombana nao wabadili tabia, fikiria zaidi namna unavyoweza kuepukana na matatizo yao.
 Tazama upande wa pili: Unapokumbana na vikwazo vikubwa, chukulia kuwa ni nafasi ya kujifunza na kukomaa. Kama ni maamuzi yako mwenyewe ndiyo yaliyokusababishia matatizo, chukua nafasi hiyo kutafakari na kujifunza kwa maamuzi yako ya baadaye.
 Jifunze kusamehe: Lazima ukubali kuwa tunaishi katika ulimwengu wenye mapungufu mengi na kwamba binadamu kufanya makosa ni kawaida. Usiwe na hasira na chuki, jifunze kusamehe na kuendelea na mambo mengine.
5. Pumzisha Na Burudisha Mwili Wako Mwili wako utapata uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na msongo wa mawazo endapo utaulea kwa kupata muda wa kuupumzisha na kuuburudisha. Katika kuulea mwili wako unaweza kufanya yafuatayo:
• Fanya matembezi, Pumzika kwenye bustani au sehemu zenye mazingira ya asili
• Mkaribishe rafik nyumbani na kupiga stori za kwaida zisiwe za jambo linalookupa msongo wa mawazo
• Soma kitabu kizuri, Sikiliza muziki, Angalia vichekesho.

 

• Jichanganye na marafiki wenye mawazo mazuri, hao watakusaidia kuondokana na madhara yanayotokana na kuwa na msongo wa mawazo. Jaribu kuwa ni mtu wa kufurahisha na kufurahia mambo kwani kicheko ni dawa ya kuondoa msongo wa mawazo kwa njia nyingi.
• Mazoezi Na Chakula Kizuri Unaweza kuongeza uwezo wako wa kukabiliana na msongo wa mawazo kwa kujenga afya ya mwili wako.
• Punguza matumizi ya kahawa na sukari. 
• Acha sigara, pombe na kushiriki Ngono kama sehemu ya kuondoa msongo wa mawazooo
*******************Njia mbaya za kuondoa msongo wa mawazo**************

Hebu tazama njia ambazo baadhi ya watu hutumia, njia ambazo hupunguza tatizo kwa muda mfupi na kulifanya tatizo kuwa kubwa zaidi baadaye:
 Kuvuta sigara, Kunywa pombe sana

 Kula sana au kula kidogo

 Kukaa kwenye TV au kompyuta, saa nyingi sana

 Kujitenga na marafiki, familia na shughuli.

 Kutumia vidonge

 Kulala sana

 Kuahirisha mambo

 Kujishughulisha saa zote kuepuka matatizo

 Kuwatulia wengine msongo wao (kubwatuka, kufoka, kupigana)

UMEJITAYARISHAJE KIROHO KUUONA UKOMO WA MAISHA YAKO DUNIANI?

1⃣ *WALIVYO KUFA WATUMISHI WA MUNGU NA MABABU WA AGANO LA KALE !!!*
“`MWL BARNABAS MUZUSA, +243994138550.

BUKAVU D.R CONGO.“`
Shabaa: KUANDAA KIFO CHAKO VIZURI,MAANA SHERTI UTAKUFA.
Watu wengi, tukiongelea kifo, hujisikia vibaya. Lakini jua kwamba kifo,lazima itatupata sote kesho. Jambo kubwa siyo kuogopa kifo,ila nijiweka tayari kwa ajili yake.
A. IBRAHIMU
Mwanzo 25:8

*Ibrahimu* akafariki, naye akafa katika uzee mwema, mzee sana, ameshiba siku, akakusanyika kwa watu wake.
ELEWA HII KUHUSU IBRAHIMU.

i. *Alikufa na uzee mwema, yaani siyo uzee usio wa usumbufu.*

ii. Mzee sana; yaani hakufa kijana.

iii. *Ameshiba siku; nikusema aliishi siku nyingi,hadi akayakinayi maisha.*
B. ISAKA
Mwanzo 35:28-29

[28]Siku za *Isaka* zilikuwa miaka mia na themanini.

[29]Naye Isaka akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake, ni mzee, ameshiba siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika

ISAKA PIA:

i. *Alishiba siku; nikusema alifikia hatua yakushiba maisha ya hapa duniani na kuanza kutarajia maisha ingine tofauti na haya,yaani ya mbinguni.*

ii. Yakobo na Esau walimuzika; yaani hakuacha matengano katika jamaa lake,ingawa ilikuwa wakati alikuwa anaishi,lakini kushirikiana kwa watoto wake kumuzika,ilionyesha umoja. Wazazi,lazima tukesheye umoja wa watoto wetu tunapoishi.
C. YAKOBO
Mwanzo 49:33

[33]Basi Yakobo alipokwisha kuwaagiza wanawe, akakunja miguu yake kitandani, akafa, akakusanywa pamoja na watu wake.
ELEWA HII AJILI YA YAKOBO.

i. *Kabla yakufa aliwahusiya wanawe; kila mzazi anastahili kuwaachiya wanawe,maagizo ya mwisho (testament) kabla ya kufa,zaidi sana,sawasawa na mapenzi ya MUNGU.*

ii. Alipokuwa naongea akakunja miguu na kukata roho; hakufa kifo cha kubabaika kama,wanavyo kufa wengi leo.
D. YUSUFU
Mwanzo 50:22-26

[22]Akakaa Yusufu katika Misri, yeye na nyumba ya babaye. Akaishi Yusufu miaka mia na kumi.

[23] *Yusufu akaona wana wa Efraimu hata kizazi cha tatu;* na wana wa Makiri, mwana wa Manase, *walizaliwa magotini mwa Yusufu.*

[24]Yusufu akawaambia nduguze, Mimi ninakufa, *lakini Mungu atawajia ninyi bila shaka, atawapandisha toka nchi hii,* mpaka nchi aliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.

[25]Yusufu akawaapisha wana wa Israeli, akasema, Bila shaka Mungu atawajia ninyi, *nanyi mtaipandisha huko mifupa yangu.*

[26]Basi Yusufu akafa, mwenye miaka mia na kumi; wakampaka dawa, wakamtia katika sanduku, huko Misri.

JIFUNZE KWA YUSUFU HAYA:

i. *Aliona wana na wana wa wanawe hâta kijazi cha tatu; huu ni mtu aliye ishi na kuona baraka za kizazi chake.*

ii. Wana wa wanawe walizaliwa magotini mwake; huyu alikuwa ni baba muzuri wa familia (hakuwa irresponsable).

iii. *Alikufa na matumaini katika ahadi ya MUNGU,kutoa Israéli misri na kuwaingiza kaanani.* 

iv. Alicha agizo la imani,hata miaka ilipita hakupoteza tumaini.
E. MUSA
Kumbukumbu la Torati 34:7

[7]Musa alikuwa mtu wa miaka mia na ishirini alipokufa; jicho lake halikupofuka, wala nguvu za mwili wake hazikupunguka.
i. *Jicho la Musa halikupofuka kwa miaka 120 alipokufa; hakuna jinsi MUNGU hawezi tenda kwako,kama anamakusudi na wewe. Musa,alichungwa hivyo sababu,MUNGU alikuwa na kazi macho kusoma na kuandika sheria.*

ii. Nguvu za mwili wake hazikupunguka; hii ni miongoni mwa baraka za kumutumikia MUNGU,kwamba miili yetu hurejeshewa nguvu kila leo.
F. YOSHUA
Yoshua 24:29

[29]Ikawa, baada ya hayo, Yoshua, mwana wa Nuni, mtumishi wa BWANA, akafa, mwenye umri wa miaka mia na kumi.

*Sikia, ikawa baada ya hayo; nikusema Yoshua alikufa baada ya kufanya kazi, mbalimbali,hakutoka duniani bila kuacha ushuhuda nyuma yake.*
G. DAUDI
1 Mambo ya Nyakati 29:28

]Akafa mwenye umri mwema, ameshiba siku, na mali, na heshima; naye Sulemani mwanawe akamiliki badala yake.

JIFUNZE HILI, DAUDI ALIISHI MIAKA MINGI,ALIPOKUFA AMESHIBA:

i. Siku,

ii. Mali, 

iii. Heshima,

( *IKIWA DAUDI ALISHIBA HIVI VYOTE KWA NINI SISI LEO HATUSHIBI ???*)

iv. Nyuma yake aliacha murithi, na wewe ukifa leo ni nani anaweza endelesha yale, unayo yataabikia???
*MUNGU AZIDI KUWABARIKI*
SOMO LITAENDELEA…KARIBU KWA MAONI YAKO.

Mthibitishe MUNGU ULIYENAE KATIKATI YA MATAIFA

MTHIBITISHE MUNGU ULIENAE KATIKATI YA MATAIFA.
Mwl Debora E. Lema✍✍
SEHEMU YA 3.
VITA VINAPOINUKA, MUNGU ANASIMAMA KUPIGANA MWENYEWE.
DANIELI 3:25
“Akajibu akasema, tazama, Mimi ninaona watu 4, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara, na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu”
WANAPOINUA vita juu yako wanategemea watakukuta katika hali ile ile waliyokuacha nayo, wengine walikuchonganisha na ndugu au rafiki zako wao wakaondoka wakirudi watakuta mkifurahi pamoja, wengine walichonganisha makazini wakafukuzwa kazi, wachonganishi wanaporudi watakuta umerudi kazini na cheo umepandishwa. Hayo yote ni kwa sababu mwanaume wa wanaume ameingilia kati.
MUNGU AKIINGILIA KATI, HAKUNA WAKUSIMAMA KINYUME NA WEWE. 
SOMO LINAENDELEA…..🇮🇱🇹🇿

USIKATE TAMAA NDUGU MUNGU NI MWEMA

SOMOShalom, katika kufundisha ujumbe huu andiko letu kuu la somo ni *1Samweli 30:1-20.* Hii ni habari ya Daudi ambayo inaeleza namna ambavyo Daudi akiwa ameenda vitani, adui zake walikuja wakateka familia na mali zao walizoziacha na kuondoka navyo. Hivyo Daudi aliporejea kutoka vitani na askari wake mia sita ndipo akakuta mji wao umechomwa moto na familia zao wote wametekwa.Licha ya wanaume hao kulia hadi kuishiwa nguvu, Biblia inasema hivi *‘‘Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika Bwana, Mungu wake’ (1 Samweli 30:6).*
Hadi leo Shetani hutumia roho ya kukatisha tamaa kuwafanya waamini wengi kushindwa kufikia tamati ambayo Mungu ameikusudia kwenye kila eneo la maisha yao. Kumbuka roho ya kukata tamaa inafanya kazi kwa karibu na roho ya hofu. Roho ya hofu na kukatisha tamaa huelekezwa kwa mtu ambaye anatia bidii au amedhamiria kufanya na kufikia hatua hatua kubwa mbeleni.
Katika kuachilia roho ya kukata tamaa zipo njia nyingi ambazo adui hutumia, mojawapo ikiwa ni kutumia maneno ambao ndio mkakati wake mkubwa. Sambamba na maneno, adui hutumia na vitendo pia kuhakikisha anatimiza dhamira yake. Kumbuka lengo la Shetani kuleta roho ya kukatisha tamaa si tu kukufanya ushindwe kufikia malengo bali zaidi ni kukufarakanisha na Mungu ili uone kwamba ahadi zake si za kweli na wala si mwaminifu.
Katika kitabu cha 2 Samweli 17:1-2 Biblia inasema *”Zaidi ya hayo Ahithofeli akamwambia Absalomu, Niache nichague watu kumi na mbili elfu, nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu; nami nitamshambulia wakati atakaokuwa amechoka, na mikono yake imekuwa dhaifu, NAMI NITAMTIA HOFU; na watu wote walio pamoja naye watakimbia; nami nitampiga mfalme peke yake’.*
Mpenzi msomaji, hivi ndivyo adui anavyowaza hata leo juu ya watoto wa Mungu katika kuhakikisha anawakatisha tamaa na kuwavunja mioyo yao, naam unapaswa kuwa makini na silaha hii ya giza ya maneno.
Hebu tuone mifano kadhaa ndani ya Biblia;
1. Kukatishwa tamaa kwa Jairo wakati anamuomba Yesu amponye mwananwe mgonjwa(Rejea Marko 5:22-23, 35-36). Mstari wa 35 na 36 inasema *‘Hata alipokuwa katika kunena, wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema,Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu?Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi,Usiogope, amini tu’.*
2. Kukatishwa tamaa kwa Nehemia wakati ameamua kuujenga ukuta uliobomoka(Rejea Nehemia 2:19, 4:1-3, 7-8). Kwenye ile Nehemia 4:1-3 imeandikwa *‘Lakini ikawa, Sanbalati aliposikia ya kwamba tulikuwa tukiujenga ukuta, akaghadhibika, akaingiwa na uchungu sana,akawadhihaki Akanena mbele ya nduguze na mbele ya jeshi la Samaria, akisema, Wayahudi hawa wanyonge wanafanyaje? Je! Watajifanyizia boma? Watatoa dhabihu? Au watamaliza katika siku moja? Je! Watayafufua mawe katika chungu hizi za kifusi, nayo yameteketezwa kwa moto? Basi Tobia, Mwamoni, alikuwa karibu naye, akasema,Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe’.*
Je unaona nguvu ya maneno katika kukatisha tamaa. Naam kila unapopiga hatua ya kutaka kufanikiwa na kufikia hatua nyingine, Shetani naye anaandaa jeshi la kukukatisha tamaa usifikie malengo yaliyokusudiwa. Hata sasa Shetani yuko kazini akitumia roho ya hofu kukatisha watu wengi tamaa wasipige hatua. Ndiyo maana ujumbe huu unakuja kwako kukuhakikishia kwamba huna sababu ya kukata tamaa.

MUNGU AKUBARIKI SANA
*SOMO LITAENDELEA……..*

Jifunze kusema no.

*JIFUNZE KUSEMA NO*       *CHUKUA HII POINT ITAKUSAIDIA*

Sio kila anachokifanya mtu maarufu (star) au mkubwa wako au kiongozi wako ni sahihi na kinafaa kufanywa.. Noo Kuna vingine sio sahihi..ndo maana wewe unakichwa chako na yeye anacho cha kwake..   

*fikicha_akili💉💉💉*

*📌Usifate kufanya uovu ili tu kumpendezesha mwanadamu .🔨🔨* Kumbuka yeye naye ni mwanadamu.. Wala hajajiumba yeye. Tena isitoshe anamiguu miwili kama yako.. Kichwa kimoja na macho mawili alafu hana mbingu ya kukupeleka.😂 
*Mathyo 10:28*
“Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”.
*Jifunze kwa kina Daniel walikubali kutupwa kwenye tanuru la moto lakini hawakukubali kutii sheria ya mfalme ya wao kuabudu sanamu..*

Unajua mwenyewe msemo huuu

Ukubwa wa Pua si wingi wa…….😍 
*Mungu amekupa utashi..* Kakutofautisha na viumbe vingine jifunze kuchanganua jema na baya.. 

Akaaaaa. *Sina maana uache kuwasikiliza wakubwa zako..* No wasilikilize *lakini jifunze kuyapima* wanayoyasema.. Sio kila jambo hata lililo ovu unakubali.. 

*Jifunze kusema No*

Maisha Ndoani 

*Funzo kwa wenye michepuko
* 👇👇
Kabla mahusiano yao hayajakolea 

jamaa akamkalisha chini huyu mdada na kumpa misimamo yake.
“Mpaka tumekuwa kwenye mahusiano maana yake nimekupenda

Nilikwambia tangu awali nina mke na watoto.

Nampenda mke wangu ndio maana nilifunga nae ndoa…..
Sitamani hata siku moja aje kuumia eti kwasababu yako
Sina malengo yoyote na wewe hususani ya kindoa maana tayari niko na ndoa…..nakuheshimu pia kwa nafasi yako lakini kuwa na nidhamu kwenye ndoa yangu……kukupenda wewe haina maana kwamba mke wangu simpendi no,ni udhaifu wa wanaume tulionao 
Sitaki uwasiliane na mke wangu hata mara moja

Sitaki ajue nina hawara nje,mke wangu anasali anamuomba Mungu.
Hata mahusiano yetu najua ataonyeshwa kwenye ndoto tu!

Ni afadhari akawa ana hisia tu lakini sio ajue.
Aisha akajibu ” ina maana huna malengo kabisa na Mimi

Ko una mpango wa kunichezea tu? 
“Kwani ulitaka nini ziada kutoka kwangu?jamaa akamuuliza.

Nataka unizalie watoto namimi nataka ndoa hata mke wa pili
Haa eti nini!?kama ni hivyo tuishie hapa ,dini yetu hairuhusu kawatafute wakina mzee Yusufu sihitaji stress ndio maana nimekwambia mapema misimamo yangu kama utaiweza,huiwezi tuishie hapa….
Haya nimekuelewa ntafuata huu utaratibu kwasababu nakupenda.alijibu dada…..poa una amani lakini?aliuliza jamaa 

Yes usijari……
Naomba ninapokuwa nyumbani usinitext wala nisiione call yako ni mpaka iwe ninapokuwa kazini tu…..
He sasa si uweke password kama hutaki mkeo asione simu yako?

Hapana sitaki kuonekana kutokuaminiwa na wife…na usichati na Mimi kwa msg za kawaida au Whatsap wala messenger,tutumiane email tu.
Aisha akajibu “sawa”
Uhusiano wao uliendelea lakini Aisha hakuwahi kuwa na amani kwa mapenzi yenye mashart kama yale ,ilikuwa inamuuma akikumbuka maneno ya jamaa na vile anavyo mheshimu mkewe na si yeye…..alivumilia tu kwakuwa jamaa ana hela,chochote alichotaka alipewa.
Alitumia kila mbinu ili kumvutia jamaa,alijaribu kumuuliza kitu anachokipenda huyo buana ili amfanyie mfano chakula anachopenda,lakini jamaa hakuwa muwazi Sana kwake.
Alitamani sana kumjua huyo mke wa jamaa lakini hakuweza

Alijaribu kutafuta hakufanikiwa,ila mara kadhaa alimskia jamaa akiongea nae kwenye simu anamuita Magdalena…..au mama Francisco.
Siku moja akiwa saluni kwake aliyofunguliwa na jamaa akiwa na msichana wake wa kazi

Akaanza kupitia Facebook akaingia kwenye profile ya jamaa aone marafiki zake ,
Akasearch jina la Magdalene akalipata,akafungua profile yake akakuta ni kweli ni mkewe jamaa,kwanza alimuweka mumewe Picha yake ya wasifu.
Akamuomba urafiki,muda huo huo mag akaacept……akamshukuru kwa kumkubalia urafiki mag akamwambia “karibu my”

Akajibu asante….
Wakachat sana siku ile…..huyu Aisha akajisemesha “nimemmaliza tayari…..usiku ule hakulala usingizi akimtafakari yule mwanamke….amfanyie nini maana ndio kikwazo kikubwa chake.
Kulipokucha mchana akiwa nyumbani kwake akamtext msichana wake 

” nimeongea na huyu mshamba nimemkaribisha saluni nimemwambia tunampa ofa aje,sasa naomba akija hapo wewe endelea kumfumua hizo nywere zake Mimi nitamnunulia soda ntamuwekea na pilipili atajuta kunifahamu”!
Dada pilipili!!?aliuliza huyo binti 

Wewe nawe baki na hilo ilo ,namaanisha sumu!alijibu Aisha 

Anhaà hapo sawa,ko nisimuwahishe niende nae taratibu?
No wewe Fanya kawaida Mimi dakika chache ntakuwa hapo…alijibu aisha
Mag dakika 20 akawa amefika na gari yake 

Akamjulisha Aisha akampa maelekezo msichana wake akawa amemwona akampokea…..wakaanza kazi
Dakika 10 mbele Aisha akawa amefika ,story zikaendelea

Magdalene hamjui Aisha, Aisha anamjua Magdalena.
Baada ya kumsuka nywere akiwa karibu na kumaliza Aisha akamwambia ngoja nikununulie na soda japo ukanywe hata nyumbani,soda gani vile?
“Yoyote nichukulie my dear nashkur sana”alijibu mag
Aisha akazuga kama anaenda dukani lkn alikuwa kazunguka nyuma ya saluni yake akatoa chupa ya take away kwenye pochi yake, na akapita dukani akaagiza zingine mbili za kwao na binti yake.
Akampa Magdalena soda aina ya pepsi,akashukuru akawasha gari akaondoka…..akionyesha kufurahishwa na Huduma zao na upendo au ukarimu wao asijue mtego wa muwindaji.
Huku nyuma walianza kupongezana wakiamini zoezi lao limefanikiwa walijua kwa vyovyote vile angekunywa njiani

Na iwapo angekunywa tu asingefika mbali kutokana na ujazo wa paketi aliyomimina kwenye chupa……
“sikutaka kumpa mapema halafu afie hapa sitaki mizoga ya watu hapa akafie mbele huko pumbavu kabisa” alijisemesha Aisha.
Kumbe Magdalena ile soda hakunywa kwenye gari.
Akawa amefika nayo mpka home…..
na kwasababu ilikuwa imepoa akaingia nayo ndani akaiweka kwenye friji akazichanganya na zingine.
Ikawa imelala kwenye friji.
Mchana wa kesho yake jamaa akarudi nyumbani kula chakula 

Alipokuwa anaondoka kurudi ofisini,akamwomba mkewe ampe soda,na soda yake kubwa ni pepsi akampa ile ya kina Aisha pasipo kujua .
Patamu hapo……
Akiwa anaondoka akaona kuna email imeingia ,kucheki anakutana na text ya Aisha “uko wapi my?”
Natoka nyumbani naenda ofisini, OK basi nipitie saluni Nina shida kidogo……….
Anataka amuulize maendeleo ya familia yake ,ana wasiwasi je soda ilinyweka?au ile sio sumu kadanganywa?
Jamaa alipofika Aisha akaingia kwenye gari akamkiss jamaa 

Wakaondoka wote kuelekea ofisini kwa jamaa.
Aisha akalalamika njaa ikabidi ampitishe mahali akala akamsubiri.

 walipokuwa wakiondoka akiwa kwenye gari akaona soda akamwomba anywe,jamaa bila ajizi yoyote akampa….kumbe ni ile yenye pilipili!
Na kwakuwa alikuwa kakaukiwa akaanza nayo hapo hapo!

akakata kama nusu hivi
Huku wakipiga story…….. 
Dakika tano peke zilikuwa ni nyingi akaanza kuskia maumivu makali hamna mfano,moja kwa moja akajua ni ile soda…..ha! Akajishika tumbo akatoa macho akamuuliza “hii umeitoa wapi?jamaa akajibu” nyumbani kwenye friji langu”
Ooooooh my god mkeo ameniua jamani! Mkeo ameniua niwahishe hospital plz!
Mke wangu amekuua?

kivipi hebu niambie!!!
Dah!Kweli mkeo anasali…….

Aisha anaongea huku akilia kwa uchungu mkubwa akatamka neno la mwisho akasema

“Nakufa kwa upumbavu wangu mwenyewe, niwahishe hospital labda ntapona mimi!
Jamaa dakika 15 akawa amefanikiwa kufika hospital akaingia nae ,jopo la madaktari wakiwa wanamhangaikia yeye akawa amewasha gari akatoroka kukwepa msala…….huku nyuma Aisha ikawa ndio kwa heri bye bye!
Kuchunguzwa ikaonekana amekufa kwa kula chakula au kinywaji chenye sumu.
Kumtafuta aliyemleta hospital wakashangaa hawamwoni.na bahati nzuri simu ya marehemu akawa ameondoka nayo.
Taarifa ikafika police.
Na ilipotangazwa iwapo angetokea ndugu wa marehemu ,wa kwanza akawa ni binti wa saluni.
Police ilibidi waanze nae yeye kuchunguza simu yake,Bahati nzuri au mbaya kwake,zile Meseji walizochati na dada hakuzifuta………
binti akawa ni mtuhumiwa namba moja ilionekana kuna MTU walimpa sumu na marehemu lakini ninani?na mbona Aisha ndiyo amekufa tena?wakaenda kuirenew ile line ya marehemu.
Upelelezi ulipokuwa ukiendelea tayari yule binti akabanwa mpaka akakiri kuhusu mpango waliousuka na marehemu dhidi ya mke wa jamaa aitwaye japhert….. Walipomtafuta akaja japhert pamoja na mkewe.
Magdalena akahojiwa kama anamfahamu Aisha akaeleza vile walivyojuana kupitia Facebook kama wiki tatu tu.
Akaeleza vile walivyompa na ofa ya kwenda kusuka na 

“huyu binti ndiye aliyenisuka na wakaninunulia soda” lakini ile soda sikuinywa nikaenda nayo nyumbani…………………akasimulia kama hapo juu.
Mume akawa anashangaa anaona ni kama move baadae mahakama ikamtia hatiani yule binti.
Walipofika nyumbani Magdalena ilibidi ambane mumewe
“Vipi Mume wangu marehemu kumbe alikuwa hawara wako?”

Ilibidi mumewe awe muwazi tu kwake,akamweleza Kisa kizima

huku akilia kwa uchungu mkubwa…….
Ni kweli Mimi ndio nilitaka kukuua kwa upumbavu wangu,naomba unisamehe,sijui kwanini wanaume haturidhiki na hatutosheki?hakuna chochote ninachokikosa kwako lakini tamaa tu!
Usimwache Mungu unayemtumikia mke wangu,ningefanyaje Mimi kukupoteza wewe!?
ningefanyaje na watoto hawa?

Mama akamfuata mkewe akamkumbatia miguu huku akilia 

Jamaa akawa ameishiwa maneno ya kuongea zaidi ya “nisamehe”…….wakaangua kilio cha kumshukuru Mungu.
Mwishoni mama Francisco akiwa amemkumbatia mmewe,anasema mwili wote ulikuwa kama unachemka,akasema nyamaza nimshukuru Mungu:
“EEH MWENYEZI MUNGU,BABA WA REHEMA,MUNGU UTULINDAYE,

BIBLIA IMESEMA WEWE USIPOULINDA MJI WAULINDAO WAKESHA BURE…….
USIPOILINDA NDOA,HATUWEZI KUFANYA CHOCHOTE……. 
ASANTE KWA UAMINIFU WAKO KWANGU,

ULINIAHIDI IWAPO NIGEKUWA MWAMINIFU KWAKO,USINGENIACHA WALA KUNIPUNGUKIA HATA SEKUNDE TANO!
NA KWAMBA MAADUI ZANGU WANGEKUWA ADUI ZAKO.

NA UMESHATIKIZA AHADI YAKO KWANGU.
ASANTE KWA KUHAKIKISHA NAZIDI KUWA SALAMA.

UMETULINDA MIMI NA MUME WANGU NA WATOTO.
ILE SODA PAMOJA NA KWAMBA IMEINGIA MPAKA NDANI KWANGU,LAKINI HAKUNA ALIYEKUNYWA NAJUA NI UWEZA WAKO LAKINI HATA MMOJA WETU ANGEKUNYWA ASINGEDHURIKA MAANA UMESEMA ” TUKILA VYA KUFISHA HAVITATUDHURU…………TULINDE TUTUNZE ZAIDI KWA UTUKUFU WA JINA LAKO AMENI.
Baba Francisco yupo ametulia na mkewe sasa hivi na ameshika sana mambo ya imani,anasali balaa.
Anajuta kwanini alijiingiza kwenye matatizo eti kwasababu ya hawara…….hataki kabisa kuisikia michepuko.
Nasema hivi tenda wema UTAVUNA mema

Ukitenda kwa hila UTAVUNA hila

MTHIBITISHE MUNGU ULIENAE KATIKATI YA MATAIFA

MTHIBITISHE MUNGU ULIENAE KATIKATI YA MATAIFA. 
Mwl Debora E. Lema✍✍
UTANGULIZI.
Unapokua na uhakika na MUNGU wako huna sababu ya kutahayari wala kuogopa, maana huwa anapigana vita vyake mwenyewe wewe huna uwezo wakupigana.
DANIELI 3:17
“Kama ni hivyo, MUNGU wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru iwakayo moto, naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme”
UKIJUA MUNGU ulienae anauwezo gani, hutaogopa kukiri UWEZA wake mbele za watu, bila kujali mazingira wala ugumu unaopitia. DANIELI alisema kwa ujasiri mbele ya mfalme Nebukadreza kamwe hawawezi kuisujudia sanamu ya dhahabu aliyoiweka mfalme, ni kwa kuwa walitambua MUNGU wao peke yake ndie anayestahili kuabudiwa.
JITAIDI KUJIONYESHA KUWA UMEKUBALIWA NA MUNGU, NA NGUVU ZA KIUNGU ZIKO NDANI YAKO.
SOMO LINAENDELEA……..

Fungua vifungo vya ROHONI

“EFATHA”
SHALOM…………………………
MARKO 7:33-35.

AKAMTENGA NA MAKUTANO FARAGHANI,AKATIA VIDOLE VYAKE MASIKIONI,MWAKE,AKATEMA MATE,AKAMGUSA ULIMI.AKATAZAMA JUU MBINGUNI,AKAUGUA,AKAMWAMBIA ,”EFATHA” MANAKE FUNGUKA! MARA MASIKIO YAKE YAKAFUNGUKA,KIFUNGO CHA ULIMI WAKE KIKALEGEA,AKASEMA VIZURI.
KATIKA BWANA NAFSI YANGU ITAJISIFU,WANYENYEKEVU WASIKIE,UKUU WAKO EE YESU MPENDA WATU,YESU HATA SASA NIPO KIFUNGONI,NAHITAJI EFATHA JUU YA MILANGO MITANO YA UFAHAMU WANGU NATAKA NISIKIE UKINIITA,NATAKA KUONA UKUU WAKO,NATAKA NIHISI MGUSO WA NENO LAKO,NATAKA NIHISI HALAFU NJEMA YA AMANI,NATAKA NIONJE ILIVYO NJEMA KUISHI NDANI YAKO KATIKA UMOJA WA MUNGU BABA ROHO MTAKATIFU MUNGU MILELE NA MILELE,YESU UKINISAMEHE NAWEZA.AHSANTE YESU KWA KUNIPOKEA.
Wapo ambao wapo magerezani wakati huu,na pengine hata wewe umetika gerezani kama si wewe basi ndugu au jirani yako ameingia magerezani ilivyo halali au kwa kuonewa tu.Yawezekana pia wakati huu Kuna mtu anaingizwa gerezani,Na pengine walau hata umekaa walau mahabusu au lock up.Haya ni magereza ya kimwili nimekuleta huku ili angalau ujue maana ya kukaa gerezani.kukaa gerezani manak ni kunyimwa mambo Fulani au nikisema kwamba nikuishi kwa kuangalia anachofikiria mwingine kwa wakati huo,au niseme ni Kule kunyimwa kabisa uhuru wa kufanya jambo na hata kama utapewa ruhusa ya kufanya hivyo basi lazima uwe chini ya masharti Fulani,usivuke mpaka.
YESU anamponya Leo kipofu na bubu kwa wakati mmoja.Sisemi aliponya hapana sioni haja ya kusema aliponya sababu YESU anaponya hata sasa kwa yule anayeamini YESU anapomponya huyu mtu tunaona akipitia hatua mbalimbali na nyingi kidogo tofauti na tulivyozoea.Katika MATHAYO SURA YA NANE.1-13.YESU anaonesha utofauti kidogo anatema mate na anaugua huku akitazama juu mbinguni halafu,kinachoshtua hapa ni pale YESU anaposema Efatha manake funguka ni pale anaposema funguka hapa tu,ni kwamba huyu mtu alikuwa amefungwa tu,YESU anaenda kuvunja gereza linalomkabili,Sababu YESU angesema Imani yako imekuponya,au nataka takasika,au beba godoro lako,uende au umesamehewa dhambi zako usirudie tena,ila hapa YESU anasema kwamba funguka.
Nimesukumwa tupite Kwa kina katika mistari hii ili ujue utofauti wa maombi,hasa kwa kile unachotakiwa upokee binafsi.Bathromayo naye alikuwa kipofu na hata wa huyu naye ni kipofu ila namna ya kuwaponya hawa ni tofauti kabisa.Kwa namna hii gereza ambalo wewe umefungwa linalingana kabisa na kosa ulilo fanya hata muda wa kuishi ndani ya gereza utategemea umefanya kosa gani.Nikwambie tu ndugu yangu usiige namna ya kuomba kwa mtu,Mwige YESU alivyosali kila wakati usiseme nataka niombe kama yule hapana omba kama YESU mwenyewe Sababu yeye ndiye anayejua ugumu wa kigungo chako.Usijisemee mimi ni kipofu tu sioni,Mara bubu na maneno mengine mengi Sana sema kwa habari kuingia kufunguliwa.Kuna wakati inakupasa uombe ufunguliwe sababu unakuuwa umefungwa kwenye jera ya kishetani unakuwa si huru tena unakuwa ni mfungwa kabisa.huwezi toka humo hadi nguvu ya YESU iwe juu yako.Unapoomba mtu Fulani aokolewe ni lazima,uombe gereza lake lifunguke kwa Jina la YESU KRISTO.
BY ZABURI 27:4…

Ubatizo

[290617] *Rev:- Odrick Bryson*: 
*SOMO:-*

*ULAZIMA WA KUBATIZWA*  
            *KWENYE* 
         *MAJI MENGI* 
*KWA MKRISTO ALIYEOOKOKA !*
💒💒💒💒💒💒💒💒💒

Mstari muhimu wa kukumbuka 
*MATHAYO 3:13-16:-*
*13* Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. 
*14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?*
*15 Yesu akajibu akamwambia, kubali hivi sasa (kunibatiza kwa haya maji mengi); KWA KUWA NDIVYO ITUPASAVYO KUITIMIZA HAKI YOTE. Basi akamkubali.* 
*16* Naye Yesu alipokwisha kubatizwa *AKAPANDA KUTOKA MAJINI*; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake “.
📖📖📖📖📖📖📖📖📖📖

BWANA WETU YESU KRISTO ambaye anatajwa katika *Waebrania 2:10:-” Kwa kuwa ilimpasa yeye, ambaye kwa ajili yake na kwa njia yake vitu vyote vimekuwapo, akileta wana wengi waufukilie utukufu, kumkamilisha KIONGOZI MKUU WA WOKOVU WAO kwa njia ya mateso “*.

 

Yesu kristo anatajwa yeye kuwa ndiye kiongozi mkuu wa wokovu wetu . 
Na kama yeye ndiye *KIONGOZI MKUU* wa wokovu wetu. Maana yake yeye ametuonyesha kivitendo sisi wanafunzi wake njia gani ya kufuata kuhusu Ubatizo , *hatuna haja ya kuhangaika kuuliza uliza watu ubatizo wa maji mengi au machache upi ni sahihi?* Imetupasa kumwangalia na kumfuata Yesu tu na wala sio mtu mwingine awaye yote ambaye anakuja kutuhalalishia kubatizwa kwenye maji machache ya kikombe , kwamba sio tatizo. Mmmmh! HUO UBATIZO WA KIKOMBE WA KUNYUNYUZIWA MAJI USONI. *Huo ni ubatizo wa namna nyingine na wa kigeni, ambao tunapaswa kujiepusha nao kabisaa*. Biblia inasema katika WARUMI 16:17-18:-“Ndugu zangu, nawasihi, waangalieni wale wafanyao fitina na mambo ya kukwaza *KINYUME CHA MAFUNDISHO MLIYOJIFUNZA; mkajiepushe nao* . Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Yesu Kristo, bali matumbo yao; na *kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu”.*

*WAEBRANIA 13:8-9:-” Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele. Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine, na ya kigeni…… “*
Hao wanaohubiri na kutetea ubatizo wa maji machache ya kikombe, kwamba unaweza kubatizwa tu wala hamna tatizo lolote na mbinguni utakwenda . *Huku Biblia haituoneshi wala kutufundisha hivyo kabisa juu ya ubatizo huo*. Watu kama hao na waalimu kama hao ni wadanganyaji wakubwa wenye maneno laini na ya kujipendekeza tu kwa watu huku wakiidanganya na kuipotosha mioyo ya watu wanyofu. 
*Neno lenyewe ubatizo linatokana na neno la kiyunani “Baptizo` “* . Maana yake *”Kuzamisha”*. 
Sasa hivi wewe tokea Mwanzo mpaka Ufunuo. *UBATIZO WA KUNYUNYUZIWA MAJI YA KIKOMBE USONI UMEUONA WAPI KWENYE BIBLIA?* Halafu bado watu tumebakia tunafarijiana tu kwa kudanganyana danganyana tu. Halafu tunadai eti na sisi tunakwenda mbinguni?! Sijui hiyo mbingu ipi ?! Endelea kuung’ang’ania uongo wako huo, uone kama mwisho wa siku kuna mbingu utakayoiona !! Biblia inasema katika *ZABURI 119:29, 118:-” Uniondolee njia ya uongo, unineemeshe kwa sheria yako. UMEWAKATAA WOTE wazikosao amri zako, kwa maana hila zao ni uongo “*. Ubatizo wa kweli wa ki-biblia ni wa maji mengi tu. Sasa wewe mtu *mbishi usiyeambilika* wewe endelea kung’ang’ania huo ubatizo wako wa uongo wa maji machache ya kikombe. Hujielewi tu kwamba mpaka hapo Mungu amishakukataa tayari . Na jehanamu ya moto utakwenda Mpendwa kwa sababu ya kiburi cha moyo wako wa kutokulitii neno hili usomalo [ ISAYA 66:2 ].
*KIONGOZI MKUU* wa wokovu wetu, Yesu Kristo yeye hakutufundisha hivyo wa hakubatizwa hivyo. Yesu Kristo ndio kioo chetu sisi , tena yeye ndiye Dira yetu ya imani yetu ya wokovu. *Yeye alituonyesha sisi wafuasi wake njia ya kufuata ni kubatizwa kwenye maji mengiiiii tu.* Nawala sio vinginevyo. Hilo tu. Full stop *[1YOHANA 2:6]*.
Hao watu wanaotuletea ndani ya kanisa la Mungu *mafundisho ya namna nyingine, na ya kigeni* kinyume na kweli ya Biblia ilivyo . . Ndugu zangu tuwatazame kwa macho ya tahadhari sana watu kama hao . Na kujiepusha nao!
 

*KUNA MKRISTO MMOJA ALINIAMBIA HIVI :-*

 “Ubatizo ni ishara tu ya kuuunga mkono UKRISTU haijalishi ni wa maji, mafuta, ulanzi na wala uwingi wa kimiminika kitumikacho cha msingi ni wewe kumjua Mungu na kutenda yaliyo mema na kumwamini Yesu Kristo kwa kushika kikamilifu amri yake kuu aliyotuamuru yaani amri ya UPENDO hivyo vingine vyote ni mbwembwe na nakshi tu za makanisa na madhehebu”.

*MAJIBU YA UFAFANUZI*
Wengi wanapouuza *kubatizwa kwenye maji mengi*, wanakuwa wanamtazamo potofu kama wa huyo ndugu kwamba suala la ubatizo kwao hawaoni kama ni jambo lenye ulazima mkubwa. 
Ni muhimu kufaham vizuri kushika mengine yote katika Neno la Mungu, lakini UKAKOSA JUU YA NENO MOJA TU, umekosa juu ya yote . Biblia inasema waziwazi katika *ZABURI 119:6:-“Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako YOTE “*. Na tena neno la Mungu linaendelea kusema katika *YAKOBO 2:8-10:-“Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, Mwatenda vema*. Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji. *Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja tu, amekosa juu ya yote”*.
Unaweza kuona mpaka hapo. Pamoja na kudai kwako kwamba eti kikubwa ni kumwamini Yesu na kushika amri kuu ya upendo. Ni vyema. Lakini Hupaswi kuishia hapo tu, ukadhani basi kwa hilo imetosha ; huku mengine umeacha kuyafanya, utakuwa umedanganyika sana mpendwa . *Lakini ni muhimu uelewe vile vile kama USIPOTII AGIZO LA KUBATIZWA KWENYE MAJI MENGI KAMA YESU ALIVYOBATIZWA* . Utakuwa umekosa juu ya yoote, tena mbele za Mungu wewe utakuwa ni mkosaji utakayehukumiwa kutupwa Jehanamu ya moto. Mungu hataki utii neno lake nusu nusu, bali anataka utii maagizo yake *”YOOTE”* aliyokuamuru katika Neno lake kuyatenda . Bwana Yesu alisema, *”Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu ; na kuwafundisha KUYASHIKA YOOTE niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari “* [ EZEKIELI 3:10; KUMBUKUMBU 1:35-36; MATHAYO 28:19-20].
*UBATIZO NI SUALA LA LAZIMA KAMA KWELI UNATAKA KWENDA MBINGUNI*. Ni lazima kwa sababu, kwanza, Yesu Kristo mwenyewe kiongozi mkuu wa wokovu wetu alibatizwa na tena akasema *…..” Kubali hivi sasa ; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote”…….* (Mathayo 3:15). Neno hilo ” itupasavyo au imetupasa “, maana yake “Ni suala lazima kubatizwa”. Na hapo ubatizo alioutamka Yesu ulikuwa ni wa maji mengi. Na sababu ya pili ni lazima kubatizwa kwa sababu *Injili ya ubatizo ni agizo kuu la Yesu Kristo* kwa kila mtu aaaminiye *[ MARKO 16:15-16; MATHAYO 28:19-20]*. Kwa maana hiyo usilichukulie suala la ubatizo kanakwamba sio suala lenye umuhimu au ulazima sana kiivyo unavyofikiri . Ukienenda hivyo ndugu yangu utakuwa umepotea sana kwenda gizani mbali na kweli ya Neno la Mungu [YOHANA 17:17] 

 

Lakin Ndugu yangu panapokuwapo na mawazo mawili yanayokinzana juu ya jambo fulani ubatizo upi ni sahihi wa maji mengi au machache , Moja kwa Moja miongoni mwa hayo mawazo mawili kuna moja ni kosa na kuna wazo moja lingine ni sahihi. *Mpaka hapo tumishaona ubatizo wa maji mengi ndio ubatizo ulio wa kweli ki-biblia* [Soma YOHANA 3:23]
Umezungumzia kuhusu ubatizo, kuwa haijalishi vyovyote ulivyobatizwa ni sawasawa tu Kwa kuwa haushuudii mbinguni. *Jibu :- Siyo kweli*. Hatuwezi kujiamulia sisi kubatizwa vyovyote tu tutakavyo sisi wenyewe , la asha! Ni lazima tubatizwe kama neno la Mungu Biblia inavyotuonyesha na kusema tubatizwe, huko ndiko kutembea katika *njia za Bwana zilizonyoooka* [ ZABURI 119:9, 105; HOSEA 14:9 ] 

*UMUHIMU MKUBWA WA UBATIZO KWA MKRISTO*
Yafuatayo ni mambo manne muhimu tunayojifunza kuhusu umuhimu mkubwa wa kubatizwa kwenye maji mengi 
 *(1) UBATIZO NI UFUNGUO WA WOKOVU WETU* 

 

Biblia inasema katika 1 PETRO 3:20-21

 inasema “MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI (si kuwekea mbali uchafu Wa mwili bali jibu la dhamili safi mbele za Mungu)

 

Ubatizo si kitu cha kupuuzwa na MTU kujifanyia anavyotaka maana huo ni ufunguo wa Wokovu. 
*UHUSIANO WA UBATIZO WA MAJI MENGI NA UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU*
Roho Mtakatifu aanatajwa kuwa ni *mito ya maji yaliyo hai*. Unaweza kuona [YOHANA 7:37-39]. Sasa basi kama vile tunavyobatizwa kwa maji mengi , vivyo hivyo tunapobatizwa kwa Roho Mtakatifu tunazamishwa ndani kabisa ya Roho Mtakatifu , na huyo Roho anatufurikia pande zote ndani na nje yetu kotekote [YOHANA 14:16-17; MATENDO 1:8].  

    

Kuna wakristo wengine wanafikiri ukishabatizwa kwa Roho Mtakatifu basi ubatizo wa maji hauna maana tena ubatizwe. Jambo hilo siyo sahihi kabisa. 
Ni muhimu kufaham unapobatizwa kwenye maji unatimiza sehemu ya haki yote, na hapo unafungua mlango wa wewe kupokea ujazo wa Roho mtakatifu.
Pia unaweza mpokea Roho Mtakatifu kabla ya kubatizwa, lakini Mara umpatapo *ATAKURUDISHA KWENYE UBATIZO WA MAJI Ili kutimiza haki yote*. Kama alivyofanya kwa watu wa nyumbani mwa kornelio, walipokea ubatizo wa Roho. Petro akaamuru warudi majini maana ni sehemu ya haki yote.

*[ MATENDO 10:44-48]*

*(2) UBATIZO UNATUPA ONDOLEO LA DHAMBI ZETU*.
Biblia inasema katika *MATENDO 22:16:-“Basi sasa unakawilia nini? Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako, ukiliitia jina lake”*
Mwili huu uliobeba laana ya dhambi: nuksi, balaa na mikosi ya kila aina juu yake, tunapobatizwa kwa kujazamishwa kwenye maji mengi , yote hayo kiroho yanazikwa ; tunainuliwa kutoka majini tukiwa tumepokea mwili mpya uliotakaswa, uliobeba baraka za Mungu na kumfanya Roho Mtakatifu akae ndani ya mwili huo. Ndiomaana ubatizo wa maji uliambatana sambamba na kumpokea Roho Mtakatifu [1KORINTO 6:19; 1KORINTO 3:16-17]
UBATIZO ni msingi wa wokovu wetu ndiyo maana Paulo katika *Matendo 19:1-6* anauliza wanafunzi kama wamempokea Roho Mtakatifu, nao kwa sababu ni wanyofu wakasema hawana, Ndipo Paulo kwa sababu anaamini kuwa ili umpate Roho Mtakatifu sharti ubatizwe *akarudi kuwauliza usahihi Wa ubatizo wao*.

Ndipo akawarudisha kwenye msingi Wa kumpokea Roho Mtakatifu. Akilejea katika *MATENDO 2:38-39* Inasema *”Tubuni mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Bwana Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”*
Kama hujatubu na kubatizwa ule ujazo Wa Roho Mtakatifu huwezi pata na ukiiupata kabla ya kubatizwa utakurudisha tena kubatizwa kwenye maji . Maana ubatizo unatupatia ondoleo la dhambi zetu na kumkaribisha Roho Mtakatifu afanye makao ndani ya miili yetu.

*(3) UBATIZO UNATUUNGANISHA PAMOJA NA KRISTO*
Biblia inasema katika *WARUMI 6:3-5:-“Hamfaham ya kuwa sisi sote TULIOBATIZWA KATIKA KRISTO YESU tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba , vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima . Kwa maana MLIVYOUNGANIKA NAYE katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake”*  
Waliobatizwa katika Kristo Yesu ni watu wale ambao wamebatizwa kwa mfano ule ule wa wa ubatizo aliobatizwa nao Yesu , yaani wa maji mengi. Hao tu ndio waliobatizwa katika Kristo Yesu. *USIPOBATIZWA KWA MAJI MENGI UNAKUWA HAUJAUNGANISHWA PAMOJA NA KRISTO kwa mfano wa mauti yake* . Na kwa sababu hiyo hautakuwa miongoni mwa watu wale ambao watafufuliwa siku ile ya mwisho *katika awamu ya kwanza ya ufufuo wa uzima*, watakaofufuliwa na kunyakuliwa kumlaki Yesu mawinguni . Lakini *watu wale wote wasiobatizwa kwenye maji mengi na tena hawakuwa watakatifu vilevile* , wao wataendelea kubakia makaburini na kukongojea ufufuo wa hukumu *[YOHANA 5:24-29; 1THESALONIKE 4:13-18]* . Huu ndio ukweli ninaokwambia Mpendwa . Ninakuhurumia wewe tu ambaye *unajifariji bure kwamba umebatizwa tangu utotoni*, na umekuwa ni mtu mbishi na mkaidi wa kutokukubali kuamua kwako *KUBATIZWA UPYA KWENYE MAJI MENGI* kwa ubatizo ulio wa ki-biblia . Mbinguni hutoingia kamwe mpendwa. Kubali kulipokea neno hili lenye maonyo kwako , utaiponyesha roho yako [MITHALI 5:11-13, 23; ISAYA 50:4-9]              
 

*(4) UBATIZO NI ISHARA YA KUFA, KUZIKWA NA KUFUFUKA PAMOJA NA KRISTO*.
Biblia inasema katika *WAKOLOSAI 2:12 na Efeso 2:6:-” Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho , katika Kristo Yesu “*.  
Soma pia WARUMI 6:3-4  
Kitu tunapokizika maana yake tunakichimbia shimo, tunakitupia humo ndani na kukifunikiza kabisa na udongo pande zote. Hapo tumekizika kitu hicho . 

   

Na kwa msingi huo Ubatizo ni mfano wa shimo la *kaburi la kiroho* . Tunapokuwa tumebatizwa kwa kuzamishwa kwenye maji mengi, ndio hasa tunakuwa tumezikwa pamoja na Kristo. Na tunapokuwa tumeinuliwa kutoka ndani ya maji, tunakuwa tumefufuliwa pamoja na Kristo. *Ndiyomaana ubatizo lazima uwe ni wa maji mengi ili kukamilisha maana nzima ya kiroho ya tendo la ubatizo wenyewe*.      

 Mtu ambaye hajabatizwa kwa ubatizo wa maji mengi, maana yake mtu huyo hajafa, hajazika wala hajafufuliwa pamoja na Kristo katika ulimwengu wa roho. Na wala mtu huyo anakuwa hajapata nafasi ya kuketishwa pamoja na Yesu katika ulimwengu wa roho. *Na hivyo mtu kama huyo kuiona kwake mbingu ni ngumu mnooo, nusra kutokuwezekana kabisaa*. Labda itokee tu kama bahati nasibu mtu uingie mbinguni kama yule muhalifu msalabani ambaye aliookoka tu dakika za mwishoni akafa, na hivyo kwake isingepatikana nafasi yoyote ya kubatizwa [ LUKA 23:39-43]. Lakini tofauti na mazingira hayo, wewe ambaye una nafasi ya kubatizwa upya kwenye maji mengi na hutaki kufanya hivyo ; kuingia kwako mbinguni mpendwa, *hilo sahau kabisa*.    

     

TUKISHAJUA HUO UMHIMU MKUBWA WA UBATIZO ndiyo tunarudi sasa kujiuliza huu UBATIZO unafanywaje!?
Je, ni kwa maji meng Au Maji machache!? *(YOHANA 3:23 inayo majibu)*
Je, unabatizwa ukiwa mkubwa au Mtoto!?
*Jibu :- Mtoto mdogo/mchanga hajui chochote kile hawezi akalisikia Neno la Mungu akaamini na kutubu dhambi zake , hivyo hawezi kuwa na sifa yoyote ya kubatizwa (Marko 16:15-16; MATENDO 2:37-41)*

*NOTE*

Huwezi kuubeza ubatizo kuwa si chochote wala si lolote. Ubatizo ni msingi Wa kuuendea wokovu.
Kama tulivyoona hapo juu kwenye kipengele namba moja kwamba *UBATIZO NI UFUNGUO WA WOKOVU WETU*.
 Biblia inasema katika *1 PETRO 3:20:-*” Watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa ; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, *WALIOKOKA KWA MAJI*. 
Mstari huo katika Biblia ya kingereza ya *Bible in Basic English*, unasomeka hivi :-” Who in the days of Noah, went against God’s orders; but God in his mercy kept back the punishment, while the Noah got ready the ark, in which small number, that is to say eight person, *got salvation through water* 
Katika tafsiri ya Biblia ya kingereza ya *King James Version*. mstari huo pia unasomeka hivi :-” Which sometimes were disobedient, when once the longsuffering of God waited in the days of Noah, while the ark was a preparing, wherein few, that is, *eight souls were saved by water*”.

*1 PETRO 3:20-21*:-” Watu wasiotii hapo zamani uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja siku za Nuhu, Safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane , *waliokoka kwa maji. MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo”*.
Neno la Mungu limetuambia hapo Mtu wa Mungu Nuhu pamoja na familia yake na jamaa zake, *waliookolewa kwa maji, waliupata wokovu wao kutoka katika maji*. Na maji yaliyotumika hapo kimsingi yalikuwa ni maji mengi mfano wa gharika [MWANZO 7:17-20 ]. Na tendo hilo linahusianishwa leo na *UBATIZO UNAOTUOKOA PIA SIKU HIZI*, yaani ubatizo wa maji mengi. 
Wakati wa Nuhu aliambiwa achonge safina , kwa maana hukumu ya Mungu ya Gharika itashuka upesi juu ya uso wa dunia. Na wanadamu wote waovu watakufa pamoja na viumbe vingine vyote vilivyo juu yake [MWANZO 6:17-19]. Kumbuka *Maji* hayo ndiyo yaliyomfanya Nuhu aingie ndani ya safina . Wakati wanadamu wengine huku wanaangamia wanakufa kwa kutapatapa ndani ya maji. Kwa upande wa pili wa Nuhu, *maji* hayo tena ndiyo yaliyompaisha Nuhu aliyekuwa ndani ya Safina, kwenda juu juu juu zaidi. Wakati wengine wanaangamia ndani ya maji, yeye anazidi kupaishwa juu zaidi. Biblia inatuambia mfano wa mambo hayo ni *ubatizo unaotuokoa pia siku hizi*. Nini maana yake hasa ? 
Safina ya Nuhu ilimwakilisha Yesu atakayekuja . Leo Safina tuliyenaye sisi ni Yesu [YOHANA 10:9]. Na Ubatizo wa maji mengi leo ndio unaotufanya sisi tuingizwe ndani ya Yesu *[WAGALATIA 3:27]*. Sasa basi hivi karibuni muda sio mrefu ujao, maagamizo ya hukumu ya Mungu yatashuka upesi tena juu ya uso wa dunia wakati wa *Dhiki kubwa*; na wanadamu wengi mno pamoja na viumbe vingine wataangamia sana vibaya kama utitiri *[SEFANIA 1:2-3, 14-18]*. Wakati hayo yanaendelea kutokea , tayari sisi tulio ndani ya Yesu wetu (Safina) tutakuwa tumenyakuliwa kupaishwa juu zaidi kwenda kumlaki Bwana hewani wakati wa parapanda ya mwisho. Na wakati sisi tulio ndani ya Yesu tumenyakuliwa kwenda juu, wakati huo hapa chini duniani tutakuwa tumewaacha wenye dhambi wote wakiteremshiwa maangamizi mazito sana *[MATHAYO 24:19-21; 1WAKORINTO 15:50-53; 1THESALONIKE 4:13-18]*.
Kwa maana hiyo wewe kama ni mkristo ambaye *hujaokoka na tena hujabatizwa kwenye maji mengi pia*; maana yake ni kwamba wewe bado unakuwa haupo ndani ya Yesu [WAGALATIA 3:27]. Na hivyo hautakuwa na sehemu yoyote miongoni mwa wale watu watakaonyakuliwa kupaishwa juu mbinguni. Utabakia hapa chini duniani ukiangamizwa pamoja na watu waovu. 
Mpendwa, 
*MPENDWA KUBALI KUITIMIZA HAKI YOTE* yaani :- *(1) Uokoke kweli kweli* na *(2) ubatizwe kwenye maji mengi kama Yesu*, *(3)*kisha uishi maisha matakatifu yanayompendeza Mungu mpaka mwisho. Ukiyazingatia hayo yote matatu kwa ukamilifu. Ni hakika Utakuwa miongoni mwa wale watakaonyakuliwa kumlaki Bwana Yesu mawinguni *[WAEFESO 5:25-27; UFUNUO 3:1-6]*

MUNGU AWABARIKI WOTE kwa kila asomaye ujumbe wa neno hili na kuutendea kazi.  

🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺
Mtumishi wa Mungu aliye hai 
*MWL, EV, REV:-ODRICK BRYSON*
*( 0759 386 988; 0717 591 466*)
Whatsapp group. 
*”KWELI YOTE YA NENO LA MUNGU ISIYOGOSHIWA”*
   [ 2 WAKORINTO 2:17].
🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺

USISHUPAZE SHINGO KWA MUNGU.

UNAPOSHUPAZA SHINGO MUNGU ANAKUACHA.
Mwl Debora E. Lema✍✍
WARUMI 1:28
“Na kama walivyokataa kuwa na MUNGU katika fahamu zao, MUNGU aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanya yasiyowapasa”

MUNGU anakupa chaguo ya kuifuata iliyo njema, wakati mwingine unaweza ona kama MUNGU anakosea kukupitisha katika njia mbalimbali au magumu unayopitia bila kumuulza MUNGU kwanini unapitia, ukatumia akili yako kwa ufaham wako. Mwisho wake ni kuangukia majuto, na kupata hasara utakayokugarimu maisha yako.
YESU AKIWA NDANI YAKO, NAWE NDANI YAKE, UTAOMBA LOLOTE KWA JINA LAKE NAE ATAFANYA, NDIVYO MAANDIKO YANAVYOSEMA.
DAMU YA YESU IKANENE UZIMA NDANI YAKO, SASA NA HATA MILELE.
🇮🇱🇹🇿

UKUU WA MUNGU.

UKUU WA MUNGU HUWA UNAJIDHIHIRISHA KATIKA MAMBO MADHAIFU.
Mwl Debora E. Lema✍✍
 1 SAMWELI 17:49
“Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga mfilisti katika kipaji cha uso, jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi”
1 SAMWELI 17:40a
“Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe LAINI matano katika kijito cha maji…..”
UTENDAJI KAZI WA MUNGU ni tofauti kabisa na utendaji kazi wa mwanadamu, mwanadamu hutumia vitu vyenye nguvu kujipatia ushindi, Lakini MUNGU hutumia vionekanavyo dhaifu na kuachilia nguvu ya kiungu ndani yake iletayo ushindi, MUNGU hababaishwi na hali, mazingira, jinsia yako, anauwezo wa kufanya makubwa kwa udhaifu huo huo ulionao.
KUMBUKA, ALILISHA MAELFU kwa mikate mitano na samaki wawili, kibinadamu si rahisi lakini alitenda. Anauwezo wa kubariki kidogo ulichonacho kikabadili mfumo mzima wa maisha yako.
YASIYOWEZEKANA KWA WANADAMU KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA.
🇮🇱🇹🇿

Ikimbie Ibada ya Sanamu.

IKIMBIE IBADA YA SANAMU.
Mwl Debora E. Lema✍✍
1 korintho 10:14
“Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu”
1 Yohana 5:21
” Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu”
IBADA YA SANAMU si mpaka kuamudu mizimu au mashetani, chochote unachokipa NAFASI ya kwanza katika maisha yako tofauti na MUNGU hicho kimesimama mbele yako kama ibada ya sanamu kwako. 
MPE MUNGU NAFASI YA KWANZA, POPOTE UENDAPO NAFASI YA MUNGU HAINA KAIMU.
NEEMA YA KRISTO IKUFUNIKE DHIDI YA MADHAIFU YAKO.
🇮🇱🇹🇿

NURU YAKO NA IANGAZE

Bwana Wetu Yesu Kristo atukuzwe wapendwa Katika Kristo ; habari za uzima. 
Karibu sana tujifunze NENO la BWANA ambacho ni chakula cha uzima wetu wapendwa. 
     SOMO : NURU YAKO IANGAZE 

                  ====================
Ni maombi yangu wapendwa Roho Mtakatifu aseme na kila mmoja wetu katika somo hili ; Roho Mtakatifu amfundishe Kila mmoja sawasawa na mapenzi yake kwetu. 
 Basi Tuanze somo letu kwa kusoma:
      Tusome MATHAYO 5:13-16
13 Ninyi ni chumvi ya dunia ; lakini chumvi Ikiwa imearibika itatiwa nini hata ikolee ? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa n’a watu. 
14 Ninyi ni nuru ya Ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. 
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango ; nayo yawaangaza wote waliomo Nyumbani. 
16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.  
Baada ya usomi wa andiko hilo, tuyaone maneno Haya :
NURU

………Ni mwangaza wenye mng’ao.

         Ni mwangaza unaong’ara. 

Lengo na kusudi la nuru au la mwangaza huu ni kuwamulika watu waliomo gizani wapate kuiona nuru.
ANGAZA 

……………. Ni kufanya sehemu au Mahali iwe na mwanga. 

-Ni Kumulika sehemu, Mahali au kitu Kwa kutumia tochi, taa, Mshumaa, mwenge au umeme…! 
√ Ndugu zangu katika Kristo ; kama tulivyoona ni kwamba Mahali ambapo hakuna nuru siku zote panakuwa na giza kwasababu mwangaza haupo Mahali hapo ; na hapo huwezi kitu chochote Maana Hakuna nuru Wapendwa .

-Kama tulivyosoma hapo juu kwamba Taa Inawashwa ndani ya nyumba Kwa ajili ya kuwamulika wale watu waliomo mle ndani wapate kuonana. 

-Ndivyo ilivyo nuru wapendwa, inakuja kuwamulika watu waliomo gizani. 
Wapendwa Na ndugu zangu watumishi wa Mungu ; hii nuru ninayoizungumzia hapa kwanza :

-Ni Yesu Kristo Bwana na mwokozi wa maisha yetu sote tumwaminio. 
         Tusome YOHANA 12:46
√ Mimi nimekuja ulimwenguni ili niwe nuru ya Ulimwengu ; ili Mtu kila aniaminiye mimi asikae gizani. √
-Huyu sio mwingine wapendwa bali ni Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai asemaye kwamba Amekuja ulimwenguni ili kila mtu, hapa Hakuna ubaguzi wa rangi, Kabila,jinsia….bali ni kwa kila mtu, yeyote Yule atakayemwamini Yesu Kristo moyoni mwake huyo Mtu atatoka gizani na kuja nuruni Maana Yesu Kristo ndiye Nuru hiyo. 

-Hivyo ili mpendwa upate kuwa nuruni ni Lazima umwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako yote mpendwa wangu. 
             Soma Pia YOHANA 9:5
√ Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya Ulimwengu. √ 
Hallelujah Hallelujah wapendwa, jina la Bwana lihimidiwe daima. 

-Tunaona pia Bwana Yesu Kristo Anasema kwamba Muda yumo ulimwenguni yeye ndiye nuru ya huu ulimwengu.

-Yesu Kristo yuko popote pale mpendwa, popote pale utakapokwenda Yesu Kristo yupo na nuru yake inaaangaza mpendwa wangu. 

-Mwanadamu alipomtenda Mungu dhambi, alijitenga na uso wa Mungu, hivyo mwanadamu akatoka Katika nuru akawa dhambini Yaani akawa mpotevu mbele za Mungu. 

-Lakini Mungu akaona si Vema mwanadamu aliyemfanya Kwa sura na Mfano wake apotee, akamtuma Mwanaye wa pekee ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele upatikanao ndani yake Yesu Kristo. 

-Ndio maana tunaona Bwana Yesu Kristo anasema amekuja ulimwenguni ili kila mtu amwaminiye awe nuruni ; ina maana kwamba Mtu yeyote atakayemwamini Yesu Kristo atatoka Kule dhambini na kuingia Katika nuru.

-Hivyo mpendwa wangu sauti hii inakuita Leo Kwa Huruma zake Mungu ya kwamba kama bado hujamwamini Yesu Kristo ; mpendwa mwamini Yesu Kristo leo upate kuwa nuruni mpendwa. 
√ Lakini pia wapendwa wangu Nuru ninayoizungumzia hapa Ni MATENDO YAKO WEWE MKRISTO. 

-Kumbuka kwamba Wote waliompokea Yesu Kristo walipata uwezo wa kufanyika wana wa Mungu ; Ndio wale waliaminio jina lake ; YOHANA 1:12
-Inamaana unapomwamini Yesu Kristo unakuwa na uwezo Wa kufanyika Mtoto wa Mungu. Na Yeyote yule amwaminiye Yesu Kristo ni Lazima matendo yake, Matendo yako, matendo yangu yanapashwa kupendana na utoto wa Mungu. 

-Hivyo matendo yako yawe Mema mpendwa utavuna kwa kulingana na matendo yako. 
√ Ndio maana tunaona kwamba tunaambiwa Katika MATHAYO 5:14

ya kwamba Sisi Yaani mimi na wewe tuliaminio jina la Yesu Kristo ni nuru ya Ulimwengu huu. 

-Simaanishi kwamba utembee na tochi mitaani, Wala sikuambii utembee na umeme, wala eti utembee na taa mitaani mpendwa ; bali Nataka nikuambie kwamba Matendo yako wewe ndio yatawafanya wale waliomo gizani wapate kumtukuza Mungu wetu aliye mbinguni. 

-Matendo yetu Wakristo Yaani wana wa Mungu yawaangaza wale ambao bado wao gizani, wamjie Mungu.

-Sio kupitia wewe jina La BWANA Linatukanwa mpendwa. 

Bali kupitia matendo yako jina la Yesu Kristo aliye hai litukuzwe na mataifa Yote.. 
√ Wapendwa MATENDO yetu yawe ladha kama vile ladha Ya chumvi ndani ya chakula ndugu zangu ; Yaani matendo yetu sisi wakristo yawe ladha nzuri Kwa mataifa Yote wanaotutazama. 

-Matusi, Uongo, Masengenyo, Fitina, Chuki wapendwa visipatikane kwetu wapendwa.

-Nuru yetu wapendwa iwalete watu kwa Yesu Kristo ; wewe na mimi ni mawakili wa Mungu, hivyo kupitia mini Na wewe watu Mjue Mungu wayatukuze matendo yake. 
√ Ndugu zangu Naomba nikuambie kwamba Kila tuendako wapendwa tumwakilishe Yesu Kristo ; Yaani matendo yetu yamwakilishe Yesu Kristo mbele ya mataifa Yote. 

-Ni kweli unayo imani Sawa, lakini kumbuka Imani yako bila matendo imekufa mpendwa. 

-Hivyo ambatanisha imani yako na matendo mema mpendwa wangu. 

Nakusii sana mpendwa wangu popote pale ulipo jifunze kutenda mema, Usiseme tu unayo imani Huku matendo yako yamo gizani itakuwa ole sana kwako. 
-Usiseme unayo imani Huku unavaa nusu uchi, Unatembea na kuacha maumbile yako wazi mbele ya watu. 

-Usiseme unayo imani Huku kinywa chako kimejaa uongo na matusi. 

-Usiseme unayo imani Huku umejaa umbea, uchonganishi Katika ya ndugu, Huku umejaa masengenyo mpendwa. 

Nuru yako Yaani matendo yako yaendane na imani yako Kila Uendako. 

-Kila tuendako wapendwa tumwakilishe Bwana Yesu Kristo ; matendo yetu yamwakilishe Yesu Kristo.
√ Mpendwa wangu Nuru yako iangaze mbele ya watu wengine ; Yaani matendo yako yawaangaze watu walio gizani wamjie Bwana Yesu Kristo ; wapate kuokolewa na hatimaye kuupata uzima wa milele upatikanao ndani yake Yesu Kristo.

ENDELEA KUMUOMBA MUNGU….USIACHE 

……………USIACHE KUMLILIA MUNGU………………Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. – Zaburi 50:15.
Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba. – Kumbukumbu la Torati 28:7 
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia. – Isaya 41:10 – 15.
USIACHE KUOMBA (Zungumza Na MUNGU) 

Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? – Luka 18:1-8
Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya. – 1Petro 3:12 
SOMA NENO KILA SIKU (Chakula Cha Roho)

Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. – Mathayo 4:4 
Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. – Joshua 1:8
Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu. – Zaburi 119:105.
SIKIA NA KUTII SAUTI YA MUNGU (Neno Lake)

Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiliza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimilizia agano na rehema aliyowaapia baba zako; naye atakupenda na kukubarikia na kukuongeza tena ataubarikia uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, nafaka zako na divai yako, na mafuta yako, maongeo ya ng’ombe zako, na wadogo wa kondoo zako, katika nchi aliyowaapia baba zako kuwa atakupa. Utabarikiwa kuliko mataifa yote; hakutakuwa na mtu mume wala mke aliye tasa kati yenu; wala kati ya wanyama wenu wa mifugo. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao. – Kumbukumbu la Torati 7:12-15
Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. – 2Petro 3:9 
Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina. – Wafilipi 4:19-20.